Jaguar: Wakenya kuwaondoa kwa kipigo Watanzania, Wachina, Waganda na Wapakistani nchini mwao

Jaguar: Wakenya kuwaondoa kwa kipigo Watanzania, Wachina, Waganda na Wapakistani nchini mwao

Mbunge wa Jimbo la Starehe Charles Njagua maarufu kwa jina la kisanii Jaguar amesema hawataki wafanyabiashara kutoka Tanzania na Uganda kwenye jimbo lake na ameahidi waondoke la sivyo atawapiga.
.
"Watanzania na Wachina wanaofanya biashara Kenya, hatuwataki, tunawapa masaa 24 waondoke, wasipoondoka tutawapiga na hatuogopi mtu."
#Tv1updates #kwesesports #kweseiflix #kwese #kfs #Kitaakimetuamin
Mihemko ya muda mfumo tu atatulia maana hajatumwa na mamlaka
 
Ndio solution ya jino kwa jino?

Labda muwaadhibu kwenye sera zenu kama nchi kuwabagua wao na sio kuchinja mzee!

Kuchinjana hakuna tofuti na nyote kua manyani wa mwituni!

Ndio maana SA waliua Waafrika wenzao ila sio kuwaua wao kama lipizo!
Wao kila siku wanalalama tz ndio inachelewesha federation at the same time wanatuogopa that bomboclot man usitafute aman wakati wa vita utaanza kufa wakat wakati wa aman dumisha amani wakati wa vita tafuta ushindi tu mzee baba

Retaliation kwa discriminative sera na sheria against them kwenye nchi yenu ni sawa....kuuana kama kisasi ni uhayawani wenyewe!
 
Hehehe! Mbona Watanzania mumebabaika hivi, mara nyingi huwa mnasema hamhitaji chochote Kenya, ila ukiangalia takwimu za uhamiaji, mpo mnakuja huku kwa maelfu sio mchezo, hili lisiwababaishe wala kuwapa wasiwasi, ni kauli za mwanasiasa aliyeishiwa sera, hana lolote la maana tangu aingie kwenye uongozi, huyu jamaa sijaona chochote alichokifanya, hapo anajaribu kutafuta pa kutokea.
Raia wa Afrika mashariki wako huku wanajituma kuliko maelezo na tunafaidi sana kiuchumi, rais wetu mwenyewe alishasema mwana Afrika mashariki yeyote ajihisi kama Mkenya, anahitaji tu kitambulisho basi.
 
Hehehe! Mbona Watanzania mumebabaika hivi, mara nyingi huwa mnasema hamhitaji chochote Kenya, ila ukiangalia takwimu za uhamiaji, mpo mnakuja huku kwa maelfu sio mchezo, hili lisiwababaishe wala kuwapa wasiwasi, ni kauli za mwanasiasa aliyeishiwa sera, hana lolote la maana tangu aingie kwenye uongozi, huyu jamaa sijaona chochote alichokifanya, hapo anajaribu kutafuta pa kutokea.
Raia wa Afrika mashariki wako huku wanajituma kuliko maelezo na tunafaidi sana kiuchumi, rais wetu mwenyewe alishasema mwana Afrika mashariki yeyote ajihisi kama Mkenya, anahitaji tu kitambulisho basi.


Sio kubabaika tatizo hatukulitegemea hili kutoka kwa jirani yetu wa toka nitoke...and infact tunafaham hamna uwezo huo wa kututoa kimabavu namna hiyo
 
Hehehe! Mbona Watanzania mumebabaika hivi, mara nyingi huwa mnasema hamhitaji chochote Kenya, ila ukiangalia takwimu za uhamiaji, mpo mnakuja huku kwa maelfu sio mchezo, hili lisiwababaishe wala kuwapa wasiwasi, ni kauli za mwanasiasa aliyeishiwa sera, hana lolote la maana tangu aingie kwenye uongozi, huyu jamaa sijaona chochote alichokifanya, hapo anajaribu kutafuta pa kutokea.
Raia wa Afrika mashariki wako huku wanajituma kuliko maelezo na tunafaidi sana kiuchumi, rais wetu mwenyewe alishasema mwana Afrika mashariki yeyote ajihisi kama Mkenya, anahitaji tu kitambulisho basi.
Sioni ulichoandika
 
Xenophobia katika ubora wake
Alafu cha ajabu ni wao ndo wamejazana kwenye nchi za watu [emoji23][emoji23][emoji23]anzeni muone mtajua hamjui
 
Kama nakumbuka vizuri baada ya Jiwe kuapishwa kama rais alianza kwa kuwafurusha wakenya huko Tz. Siungi mkono tamko la Jaguar, kwa maoni yangu, wale ambao sio waafrika ndio tunafaa kuwafurusha. Omba omba wa kitanzania wametapakaa kwenye miji ya Kenya. Machangudoa na wachuuzi pia kutoka Tz wapo wengi sana Kenya ila wakenya huwa hawana bifu nao.
 
Hili tatizo sio rahisi kama unavyolisemea hapa....

Unawacheka Wakenya wakati Kariakoo kuna Wachina walishachinjwa sometimes ago...

Issue hapa sio eti tuwafanyie nini au tuwachukulie hatua gani maana ninaona ni solution ya jino kwa jino which is nonsense in a long run!

Nadhani ni suala la kuelimisha wanasiasa na wananchi wetu mpaka waelewe...

Naona ni ignorance on both sides...wananchi bado hawajajua maana ya soko huria na maana ya competition!

Ni elimu tu hapa!

Sio kwamba Tanzania au UG au RW ni bora sana katika kuruhusu biashara huria,nao ni wabovu vilevile...ni kuelimisha EA yote mpaka kila mtu aelewe!
Wewe ndiye nonsense in the present run n long run too. Kaisome UN Charter chapter 6 na 7 inasemaje utaelewa. Kuna wakati Cohersion and Excessive Power is needed to resolve some stupid problems
 
Kama nakumbuka vizuri baada ya Jiwe kuapishwa kama rais alianza kwa kuwafurusha wakenya huko Tz. Siungi mkono tamko la Jaguar, kwa maoni yangu, wale ambao sio waafrika ndio tunafaa kuwafurusha. Omba omba wa kitanzania wametapakaa kwenye miji ya Kenya. Machangudoa na wachuuzi pia kutoka Tz wapo wengi sana Kenya ila wakenya huwa hawana bifu nao.
Kama kawaida yenu kujitetea
 
Una akili nyingi saana

Yaan kwakifupi kuliko kuvunja jumuiya nzima kwa sababu ya nchi moja ni bora Kenya ivuliwe uanachama wa jumuiya ya afrika ya mashiriki kwani technically watakaobaki ni wale wanaotumia bandari yetu na tunaelewana sana
 
Huyo ni muhuni tu, mamlaka za Kenya hazita fumbia macho upunguani kama huo.
 
Kama nakumbuka vizuri baada ya Jiwe kuapishwa kama rais alianza kwa kuwafurusha wakenya huko Tz. Siungi mkono tamko la Jaguar, kwa maoni yangu, wale ambao sio waafrika ndio tunafaa kuwafurusha. Omba omba wa kitanzania wametapakaa kwenye miji ya Kenya. Machangudoa na wachuuzi pia kutoka Tz wapo wengi sana Kenya ila wakenya huwa hawana bifu nao.
Tumieni sheria na taratibu za nchi menu kuwatoa nchini kama wanaishi na kufanyakazi kinyume na sheria, ndivyo alivyofanya Magufuli, kinyume cha hapo ni ukiukwaji wa sheria, hatutovumilia.
 
Yaan kwakifupi kuliko kuvunja jumuiya nzima kwa sababu ya nchi moja ni bora Kenya ivuliwe uanachama wa jumuiya ya afrika ya mashiriki kwani technically watakaobaki ni wale wanaotumia bandari yetu na tunaelewana sana

Wewe hapo kwa kuvimbiwa makande una ubavu gani wa kuvua uanachama wa Kenya kwenye huu muungano, ifahamike asilimia 40% ya uchumi wa EAC umemilikiwa na Kenya, hivyo nchi hii ndio baba ukanda huu, hamna anayeweza kumfukuza baba nyumbani.
Narudia tena, hizo ni kauli za mwanasiasa ambaye ameishiwa, anafahamu uchaguzi unakaribia, ndio anatafuta jinsi ya kutibua apate kiki, haya mataifa tunategemeana na hakuna mwenye ubavu wa kumfurusha mwenzie, rais wetu alishalitambua hilo na akaamrisha wana EAC wote waje na kujihisi Wakenya, wamiliki biashara na kila watakachoweza, hapa kwangu mtaani getini duka la kwanza ni la Mtanzania, familia yangu inategemea duka lake kwa bidhaa nyingi tu na haijawahi tokea sku hata moja tukawaza Utanzania wake, cha msingi ukiwa na hela, nenda dukani kwake, nunua ulichkifuata piga stori, sepa zako kafanye mengine.
Pembeni hapa kuna jengo lenye vyumba vya kupanga, yaani apartments, mali ya Mchagga fulani raia wa Tanzania, hapo amewekeza na anategemewa kwa njia moja au nyingine.

Hivyo muendelee kuropokwa na kutokwa povu ni ruksa, lakini mwisho wa siku kila mmoja wetu ataishia kitandani usiku na kukoroma, lakini uhusiano baina ya haya mataifa upo pale pale, raia tunahusiana na kufanya biashara.
 
Back
Top Bottom