Jaguar: Wakenya kuwaondoa kwa kipigo Watanzania, Wachina, Waganda na Wapakistani nchini mwao

Mihemko ya muda mfumo tu atatulia maana hajatumwa na mamlaka
 
 
Majirani zetu Wakenya..ndo mmefikia huku ?
 
Hehehe! Mbona Watanzania mumebabaika hivi, mara nyingi huwa mnasema hamhitaji chochote Kenya, ila ukiangalia takwimu za uhamiaji, mpo mnakuja huku kwa maelfu sio mchezo, hili lisiwababaishe wala kuwapa wasiwasi, ni kauli za mwanasiasa aliyeishiwa sera, hana lolote la maana tangu aingie kwenye uongozi, huyu jamaa sijaona chochote alichokifanya, hapo anajaribu kutafuta pa kutokea.
Raia wa Afrika mashariki wako huku wanajituma kuliko maelezo na tunafaidi sana kiuchumi, rais wetu mwenyewe alishasema mwana Afrika mashariki yeyote ajihisi kama Mkenya, anahitaji tu kitambulisho basi.
 


Sio kubabaika tatizo hatukulitegemea hili kutoka kwa jirani yetu wa toka nitoke...and infact tunafaham hamna uwezo huo wa kututoa kimabavu namna hiyo
 
Sioni ulichoandika
 
Xenophobia katika ubora wake
Alafu cha ajabu ni wao ndo wamejazana kwenye nchi za watu [emoji23][emoji23][emoji23]anzeni muone mtajua hamjui
 
Kama nakumbuka vizuri baada ya Jiwe kuapishwa kama rais alianza kwa kuwafurusha wakenya huko Tz. Siungi mkono tamko la Jaguar, kwa maoni yangu, wale ambao sio waafrika ndio tunafaa kuwafurusha. Omba omba wa kitanzania wametapakaa kwenye miji ya Kenya. Machangudoa na wachuuzi pia kutoka Tz wapo wengi sana Kenya ila wakenya huwa hawana bifu nao.
 
Wewe ndiye nonsense in the present run n long run too. Kaisome UN Charter chapter 6 na 7 inasemaje utaelewa. Kuna wakati Cohersion and Excessive Power is needed to resolve some stupid problems
 
Kama kawaida yenu kujitetea
 
Una akili nyingi saana

Yaan kwakifupi kuliko kuvunja jumuiya nzima kwa sababu ya nchi moja ni bora Kenya ivuliwe uanachama wa jumuiya ya afrika ya mashiriki kwani technically watakaobaki ni wale wanaotumia bandari yetu na tunaelewana sana
 
Huyo ni muhuni tu, mamlaka za Kenya hazita fumbia macho upunguani kama huo.
 
Tumieni sheria na taratibu za nchi menu kuwatoa nchini kama wanaishi na kufanyakazi kinyume na sheria, ndivyo alivyofanya Magufuli, kinyume cha hapo ni ukiukwaji wa sheria, hatutovumilia.
 
Yaan kwakifupi kuliko kuvunja jumuiya nzima kwa sababu ya nchi moja ni bora Kenya ivuliwe uanachama wa jumuiya ya afrika ya mashiriki kwani technically watakaobaki ni wale wanaotumia bandari yetu na tunaelewana sana

Wewe hapo kwa kuvimbiwa makande una ubavu gani wa kuvua uanachama wa Kenya kwenye huu muungano, ifahamike asilimia 40% ya uchumi wa EAC umemilikiwa na Kenya, hivyo nchi hii ndio baba ukanda huu, hamna anayeweza kumfukuza baba nyumbani.
Narudia tena, hizo ni kauli za mwanasiasa ambaye ameishiwa, anafahamu uchaguzi unakaribia, ndio anatafuta jinsi ya kutibua apate kiki, haya mataifa tunategemeana na hakuna mwenye ubavu wa kumfurusha mwenzie, rais wetu alishalitambua hilo na akaamrisha wana EAC wote waje na kujihisi Wakenya, wamiliki biashara na kila watakachoweza, hapa kwangu mtaani getini duka la kwanza ni la Mtanzania, familia yangu inategemea duka lake kwa bidhaa nyingi tu na haijawahi tokea sku hata moja tukawaza Utanzania wake, cha msingi ukiwa na hela, nenda dukani kwake, nunua ulichkifuata piga stori, sepa zako kafanye mengine.
Pembeni hapa kuna jengo lenye vyumba vya kupanga, yaani apartments, mali ya Mchagga fulani raia wa Tanzania, hapo amewekeza na anategemewa kwa njia moja au nyingine.

Hivyo muendelee kuropokwa na kutokwa povu ni ruksa, lakini mwisho wa siku kila mmoja wetu ataishia kitandani usiku na kukoroma, lakini uhusiano baina ya haya mataifa upo pale pale, raia tunahusiana na kufanya biashara.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…