Jaji Eliezer Mbuki Feleshi anafaa kuwa AG

Jaji Eliezer Mbuki Feleshi anafaa kuwa AG

Tunkamanini

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2014
Posts
377
Reaction score
93
Kutokana na kujiuzulu kwa aliyekuwa mwanasheria mkuu wa serikali Jaji Werema ni wazi sasa nafasi hiyo inabaki wazi.

Kwa walio wadau wa tasnia hii ya sheria nadhani wataungana nami pasina shaka lolote kuwa kutokana na nafasi hiyo kuwa nyeti kwa ustawi wa Taifa lolote lile duniani, inahitaji kushikiliwa na mtu mwenye nidhamu, weredi na mwenye uadilifu wa hali ya juu.

Kwa wasomi na wanataaluma wa sheria nchini wenye sifa hitajika ni adimu sasa kwa taifa letu hili kwa sasa, binafsi namfahamu vyema Mhe. Jaji Feleshi licha ya kufanya nae kazi kwa muda wa miaka michache lakini ni mtu ambaye ukimweka na viongozi waandamizi wenye hadhi yake ni kama mtu aliyeshushwa toka peponi.

Hakuna mtu wa kada yeyote anaeza ongea swala la hongo kwa Mhe. Jaji Feleshi, kwa kipindi chote nlichofanya kazi pale Sukari sijawahi ona mfanyakazi wa kawaida akimtangulia kufika ofisini na alikuwa wa mwisho kutoka ofisini, sikuelewa nia ya Mhe Rais kumtoa kwenye uDPP lakini huenda alikuwa akiandaliwa kushika nyazifa za juu katika muhimili huo muhimu ili kuusuka upya lakini kutokana na ombwe hili katika nafasi ya AG bado sijaona mtu mbadala.
 
Nimrod Mkono anafaa sana kuwa mwanasheria mkuu wa serikali
 
Naunga mkono hoja, nafasi hii inahita mtu mwenye kaliba ya Dr. Feleshi, huwa naskitika sana pale watu wasiomfahamu vizuri huyu jamaa wakimbedha, hakuna mwanasheria muadilifu na mchapa kazi kama huyu jamaa.
 
Change + feleshi. = ghorofa mwanza, DPP

,.....................network error
 
laki si pesa kwako kila jambo huwa ni midhaha tu, watu wa aina yako siku zenu zinahesabika humu Tanzaniani.
 
Last edited by a moderator:
Hapa tulipofika kama ingeliwezekana tungeliomba ashushwe mmoja toka juu mbinguni au tumkodishe Patrick Lumumba PL toka Kenya kama expert.
 
Mwacheni Rais afanyanye kazi yake acheni kumwekea maneno mdomoni anajua kazi yake
 
Naona wafaidika wa Escrow bado mnaendeleza mtandao wa ulinzi; ebu tujikumbushe malalamiko ya bosi wa TAKUKURU (kama tulivyojulishwa katika wikiliks) juu ya rushwa kubwa kubwa kwamba DPP wa wakati huo wa EPA and co alifanya nini juu ya mashitaka ya watuhumiwa?
 
NCH hii bado ina mijitu miPUMBAVU haijawahi kutokea yaani nch hii hakuna watu wengine icpokuwa wale walivurunda sehem moja wanapelekwa sehem nyingine yaani hata hii kumuwaza huyo ndg nikudhihirisha ukiAZI wa mtu
 
Mwacheni Rais afanyanye kazi yake acheni kumwekea maneno mdomoni anajua kazi yake

Una uhakika anajua kazi yake kweli? angekuwa anajua kazi yake angeshindwa vipi kuchukulia hatua za kinidhamu wateule wake badala yake ni mpaka kapata shinikizo la nje?

Mtu kajiuzulu kutokana na matumizi mabovu ya ofisi na yenye harufu ya kijinai then Raisi anampongeza na kumpamba eti uongozi wake ulitukuka na ulisheheni uadilifu!!? Shame, shame shame...only in Tanzania.
 
Naona wafaidika wa Escrow bado mnaendeleza mtandao wa ulinzi; ebu tujikumbushe malalamiko ya bosi wa TAKUKURU (kama tulivyojulishwa katika wikiliks) juu ya rushwa kubwa kubwa kwamba DPP wa wakati huo wa EPA and co alifanya nini juu ya mashitaka ya watuhumiwa?

Jambo usilolijua ni kama usiku wa giza, nadhani hata huyo Hossea mwenyewe humfahamu, Dr. Feleshi alipoomba mdahalo na Hossea aelezee ni mafaili gani ameyahold Hossea alijibu nini?

Kesi ni ushahidi, narudia tena kesi yoyote ile mahakamani ni ushahidi, hakuna water tight evidence unapelekaje kesi mahakamani wakati unatambua wazi kwamba utashindwa?
 
Jambo usilolijua ni kama usiku wa giza, nadhani hata huyo Hossea mwenyewe humfahamu, Dr. Feleshi alipoomba mdahalo na Hossea aelezee ni mafaili gani ameyahold Hossea alijibu nini?

Kesi ni ushahidi, narudia tena kesi yoyote ile mahakamani ni ushahidi, hakuna water tight evidence unapelekaje kesi mahakamani wakati unatambua wazi kwamba utashindwa?

Kwahiyo tulidanganywa pesa za EPA zilirudishwa?

kama zilirudishwa hiyo siyo water tight evidence siyo?
When the right does not read the left it is so difficult to lie!
 
Kwahiyo tulidanganywa pesa za EPA zilirudishwa?

kama zilirudishwa hiyo siyo water tight evidence siyo?
When the right does not read the left it is so difficult to lie!

Kwani umesahau Rais aliahidi nini? mbona nashindwa kukushangaa?
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Naunga mkono hoja, nafasi hii inahita mtu mwenye kaliba ya Dr. Feleshi, huwa naskitika sana pale watu wasiomfahamu vizuri huyu jamaa wakimbedha, hakuna mwanasheria muadilifu na mchapa kazi kama huyu jamaa.
Hebu tuanzie na alipokuwa DPP mazuri yake. "outstanding perfomance" hiyo unayoizungumzia tuiangazie wapi??!!!
 
Jambo usilolijua ni kama usiku wa giza, nadhani hata huyo Hossea mwenyewe humfahamu, Dr. Feleshi alipoomba mdahalo na Hossea aelezee ni mafaili gani ameyahold Hossea alijibu nini?

Kesi ni ushahidi, narudia tena kesi yoyote ile mahakamani ni ushahidi, hakuna water tight evidence unapelekaje kesi mahakamani wakati unatambua wazi kwamba utashindwa?

Watu wanashindwa kuelewa kuwa ile ilikuwa ni kampeni tu ya kuitenga PCCB na DPP, huyo Hossea mnaemwamini mmuulize kwa nini aling'ang'ania ushahidi wa UDA ili kuwalinda akina Kisena kitu kilichopelekea Feleshi aiondoe kesi mahakamani.
 
Kwani umesahau Rais aliahidi nini? mbona nashindwa kukushangaa?

Kwahiyo Rais ndiye anayetakiws kuandaa mashitaka siyo? Endelea kushangaa ila hakatizi mtu nyumba ya ufisadi misingi imebomolewa tupo katika mkakati wa kulijenga taifa lenye kujiheshimu na kujisimamia!
 
Back
Top Bottom