Jaji Elinaza Luvanda ajiondoa kuendesha kesi ya Mbowe na wenzake baada ya washtakiwa kudai hawana imani naye

ucwe mwehu ww,mshatakiwa anayo haki hyo ucwe poyoyo
 
Kwa maana hiyo unasema katika kesi ya jinai jaji kamwe hawezi kufuta hati ya mashitaka na kufuta kesi? bali anatoa amri wa jamhuri kurekebisha hati ya mashitaka?
 
Mahakama inaweza kugundua kosa yenyewe (suo moto) au kwa kushtuliwa na upande wowote kwenye kesi. Pia hata kama mahakama ikishtuliwa na upande wowote, tuseme upande wa utetezi. Mahakama inanguvu ya kisheria kutoa amri kwa upande ulioleta hiyo hati(hapa ni serikali tuseme) kurekebisha na kesi iendelee, na hichi ndicho alichokifanya jaji. He is perfectly correct under the law.
 
Hapa nachoona unachotaka kufanya ni kuficha udhaifu wa jaji, hizo sababu ulizoorodhesha za kimazingira na nyinginezo sioni kwanini uzipe kipaumbele wakati inajulikana wazi hati ya mashtaka ikikosewa nini kinafuata, jaji sio kocha ni refarii, anatakiwa awe kati, asijigeuze mwalimu wa upande mwingine wa kesi, hilo naamini hata mtoto mdogo atakubaliana nami, na ndio sababu Mbowe na wenzake wanaamini jaji anatumiwa na mamlaka zake za uteuzi, he is simply under pressure avunje sheria ili kuwalinda jamhuri kwenye hii kesi feki.
 
Ameshakubali kujitoa,ata kusoma pia hujui au?
 
Kuna mazingira tofauti Mkuu, ila Jaji/Hakimu anaweza kufuta mashtaka kama Jamhuri ikishindwa kuonesha kuwa una kosa la kujibu, yaani wakiwa na stori tu alafu bado usionekane uhalifu wako.

wakati meingine ni pale hakuna ushahidi wowote/wakutosha hii sana sana ndio kubwa, hapa utaweka na pale ambapo Jamhuri inasema tu upelelezi haujakamilika kila mara Mkuu.

Kwa haraka ni mazingira haya sana sana, ila sasa unaweza ukatoka mahakamani wakakukamata tena na tena na tena.
 
Kama kweli huyo jaji amewekwa kimkakati kupindisha sheria, basi atagoma kujitoa kama ilivyokuwa kwa Sugu kule Mbeya..
Jaji keshajitoa muwe mnasoma between the lines,ata kusoma tu ni shida!
 
Hii inazidi kudhihirisha tu udhaifu wa mahakama zetu katika kutoa haki. Jaji anajua kwamba akitenda haki katika kesi kama hii na yeye atakuwa anajitafutia matatizo, hivyo bora kukaa pembeni. Bila shaka ulishuhudia mahakama ilivyopigwa butwaa pale Mbowe alipotoa hoja ya kumkataa Jaji. Jaji alionekana kama vile kautua mzigo mzito aliotwishwa na ulioonekana wazi kabisa kumwelemea.
 
Kwa maana hiyo unasema katika kesi ya jinai jaji kamwe hawezi kufuta hati ya mashitaka na kufuta kesi? bali anatoa amri wa jamhuri kurekebisha hati ya mashitaka?
Hati ya mshitaka ni mali ya jamhuri sio mahakama . Mahakama haina nguvu yoyote ya kisheria kufuta hati ya mashitaka ila kufuta kesi pale tu inapojiridhisha kuwa jamhuri wameshindwa kuthibitisha madai yao yaliyowekwa kwenye hati ya mshitaka. Hivyo ni jukumu la jamhuri kuomba kufuta hati ya mashitaka na sio kufuta kimsingi ni kuiondoa hiyo hati mahakamani na kesi kufutwa. Tofautisha kati ya kesi na hati ya mashitaka. Hivi ni vitu viwili tofauti.
 
Msomi udhaifu uko wapi wakati tuna mahakama zinazofata sheria.
 
Tuhuma alizozitoa Mbowe dhidi ya Jaji Luvanda sio tu zinamchafua yeye bali zinawachafua Majaji wote na Muhimili wa Mahakama.
Hivyo Mbowe na Mawikili wake walipaswa wathibitishe tuhuma hizo nzito.
Mbwa wabwekeao Lori hawana uwezo wa kulikatisha safari yake! Unajionyesha utupu wako uliokujaa kichwani juu ya taratibu za kimahakama! Kazitafute ujitunze ili ujisaidie badala ya kubweka humu! Kama jaji kakiri kuwa hati ya mashtaka kukosewa kimsingi kesi inajifuta automatically kwani ni kupoteza muda na rasilimali pesa kusikiliza kesi isiyokuwepo! Unaelewa Sasa wewe bush lawyer?
 
Hii paragraph yako ya mwisho hasa mstari wa mwisho ndio ingeweza kuelezea hoja zako vizuri, kwanza jamhuri ishindwe kesi kwa kukosea hati ya mashtaka, pili Mbowe aachiwe huru, then akitoka nje tu, wamkamate tena wamfungulie mashtaka upya, lakini sio jaji kuwaambia jamhuri warekebishe hati ya mashtaka, hii kitu sijawahi kuiona popote.
 
Kwa wakili yeyote Jaji ni mwalimu ndio maana tunasoma kesi tofauti tofauti kupata mamlaka yakusema jambo.

Mkuu kuna jambo bado haujaweza kulifahamu vizuri, nitakupa mifano hapa, tuseme haya Jaji angeamua kumuachia huru Mbowe, alafu akatoka tu akakamatwa tena. Unadhani public ingechukuliaje hiyo hali? (Sasa kuna Majaji wanaitwa Grand Judges) hawa ni wazee wakuangalia public sana, pengine Hon. Luvanda ni miongoni mwao. (Sio kosa wala)

Sasa turudi kwenye hili jambo, kwanini sasa kaamua kutolifuta?, kuna mambo mengi miongoni ni

1. Kuitafuta haki kwa pande zote mbili
Hapa haimaanishi kuwa umeona kuna mapungufu na yanaweza kurekebishika basi ukaamua kama Jaji/Hakimu kufuta kesi kwa kuangalia 'teknikaliti'

2. Kuwarahisishia muda wao watuhumiwa
Kumbuka Mh. Mbowe na wenzake wapo ndani bila dhamana, sasa ni vipi kawarahisisgia muda na kuondoa usumbufu?, Akifuta hati watakuwa huru dakika chache wakitoka tu nje pale wakamatwe tena, kesi ianze upya pengine ikachukua muda mrefu zaidi kosa halina dhamana, sasa kwanini Mahakama ipoteze muda kiasi hicho?.

Kumbuka moja ya malengo ya Mahakama Kuu Tz ni kuendesha kesi kwa muda mfupi ziishe.

Unaweza ukasema angejuaje kama angekamatwa tena?, Ipo wazi tu sababu bado Jamhuri ina 'interest' na kesi angekamatwa tu na wangerudi pale pale sasa maana yakr ni nini kwanini asiwaambie warekebishe wailete ikiwa sawa ili hali zipo kesi zinamruhusu kufanya hivyo.

Mkuu hili swala ni lakitaaluma sio kisiasa, tuliangalie kwa jicho la taaluma.
 
Hujaelewa na wala hujajifunza kitu! Unaweza kumkataa hakimu kwa kutokua na imani naye, lakini haimaanishi unachagua jaji au hakimu unaye mtaka! Ukitaka kujifunza au kuelewa, subiri mchakato wa hii kesi utakavyo endelea!
 
Kesi iendelee. Mawakili wa mbowe wanasumbua mahakama ili kupiga hela ya wafadhili kwamba wanamtetea mteja wao kibaraka wa wazungu.
Unazijua taratibu za mahakama? Jaji kakiri mwenyewe kuwa hati za mashtaka zimekosewa na kashindwa kuitupa kesi yenyewe! Hata mimi ningemkataa Kwa kushindwa kufanya maamuzi kwani hakutakiwa kuwa biased Kwa kiasi kile! Mbowe anakwenda kuwa huru kwani jaji atakayepangiwa anakwenda kuifuta kesi bila masharti ili jamhuri ijifunze kuandaa hati za mashtaka ya kubumba!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…