Jaji Elinaza Luvanda ajiondoa kuendesha kesi ya Mbowe na wenzake baada ya washtakiwa kudai hawana imani naye

Kibatala miaka yote mbinu zake ni hizo hizo tu kutafuta kumaliza kesi kwa short cut badala ya kuwekeza katika kupangua mashitaka kwa hoja za kisheria
Alifanya kwa sugu akashindwa,akafanya kwa mdude akajitoa
Kutokua na imani na jaji hakumpunguzii mteja ukali na ugumu wa mashitaka
 
Hujaelewa na wala hujajifunza kitu! Unaweza kumkataa hakimu kwa kutokua na imani naye, lakini haimaanishi unachagua jaji au hakimu unaye mtaka! Ukitaka kujifunza au kuelewa, subiri mchakato wa hii kesi utakavyo endelea!
nimejifunza kuwa ukifika Mahakamani kama unaona Jaji au Hakimu hasomeki basi unatamka tu kuwa sina imani na Jaji/Hakimu kisha Jaji au Hakimu anajitoa kwenye kesi yangu.
vivyo hivyo ikitokea tena mwengine haeleweki nasema sina imani naye kisha anajitoa, na mwengine na mwengine.........Kumbe huo ndio utaratibu mpaka niridhile na Jaji ama Hakimu ninaye mtaka mimi.
duh! Mahakama zetu zimeendelea sana.
 

Hapana huna uwezo huo, wala hakuna alie na uwezo huo.

Pamoja na hayo, unaweza kuonyesha (na unaruhusiwa) kutokuridhika na Jaji au hakimu na unaweza kutoa hoja zako kutokana na kutoridhika kwako na kuomba Jaji au hakimu ajitoe kwenye kesi yako. Jaji au hakimu naye ana uhuru wa kukubali kujitoa au kutojitoa. Kama una kumbu kumbu utakumbuka kuna kesi nyingine mahakamu ya kisutu Mbowe aliomba Hakimu ajitoe na hakimu alikataa na akaendelea.

Hata huyu angeweza kukataa, naamini ilikuwa busara kwake kujitoa.

Hapa chini ni maneno ya Jaji akikubali kujitoa kama alivyonukuliwa na gazeti la Mwananchi :

"Nimesikiliza ombi la mshtakiwa wanne katika kesi hii( Mbowe) na mawakili wa upande wa mashtaka niseme tu ombi la Mbowe ni la msingi na lina maslahi mapana kwa umma licha ya kuwa malalamiko yake ni ya kudhani..hivyo nichukue fursa hii kukaa pembeni ili nimpishe Jaji mwingine aje achukue nafasi ya kuendelea na shauri hili, niwashukuru wote kwa ushirikiano na nawatakia kila la heri Insha'Allah," amesema Jaji Luvanda.
 
Kesi itaanzaje bila hati ya mashitaka au kwa mashitaka batili?
 
Unasema sio swala la kisiasa halafu unaongea siasa tupu !

Unaonyesha Jaji inabidi aangalie "interest" za Jamhuri badala ya kusimamia haki.

By the way kama Jaji anawaonea huruma hao watu kukaa mahabusu alitakiwa atumie muda wake kufanyia kazi pingamizi la shitaka la ugaidi kwani kama angekamilisha like na ku-drop charge za ugaidi wangekuwa huru na mashitaka mengine yangeendelea. Lakini alichofanya ni kutolitolea maamuzi na kusema atatoa maamuzi siku nyingine isiyo na jina...

Siasa tupu !
 
Jaji Luvanda ni mmoja wa wasiojulikana waliopachikwa huko mahakamaniili kuipendelea Serikali. Bipi kuhusu msajili wa mahakama,Mr.Simba ambaye naye ni miongoni mwa hao wasiojulikana?Si atampanga asiyejulikana mwenzake ili kuzidi kudidimiza haki kama ilivyo kawaida yake?
 
Nimefanya field mahakamani hakuna unachokiandika hapa nisichokifahamu, hizi zote ulizoweka hapa (hoja zako) ni hisia tu, hauna uthibitisho, unamsemea jaji usiemjua "his motive behind".

Kama majaji/hakimu wengine huamua kuwaachia watuhumiwa halafu baadae wakamatwe tena, kwanini Luvanda ameshindwa?

Hili linatokea wakati ambapo kuna malalamiko ya muda mrefu mahakama zetu zinatumiwa na CCM kwa manufaa yake kisiasa, ndio maana hili suala linachukuliwa kisiasa tofauti na wewe unavyotaka iwe kitaaluma, majaji na mahakimu wetu ikija kesi yenye merits kwa CCM mara nyingi huziweka taaluma zao pembeni.

Hapa sioni sababu ya kuleta nadharia, muhimu tuangalie situation kama hii inapotokea kwenye kesi nyingine majaji/mahakimu hufanya nini? sheria inasemaje? na sio jaji anafikiria nini.

Na endapo washtakiwa wangeachiwa huru halafu wakamatwe tena public ikilalamika wangeeleweshwa hivyo ndivyo sheria inavyotaka, lakini sio kumsemea jaji ambaye hujui amepokea maelezo gani toka kwa wakuu wake wa kazi, hasa ukizingatia na jaji ni muajiriwa wa TISS.
 
Wapambe wake Mbowe wanasukumwa na hisia kuliko mashtaka dhidi yake ambayo ni mazito kiasi cha kuvuta wawakilishi wa Balozi za nje.

Kama zilivyo hoja zako, Mawakili wa utetezi hawamtendei haki mteja wao. Kwa kuwa hati ya mashtaka ilikuwa na mapungufu wangeendelea na kesi ili watumie mapungufu hayo kujenga hoja za kumnusuru mteja wao. Kitachotokea yataandaliwa mashtaka mazito ambayo watakuwa na kazi kuyapangua
 
Masikini Mbowe anafungwa hivi hivi kutokana na ujinga wa Watanzania, kuwapigania watu wasiojielewa ni kazi sana.
Mlevi wa Konyagi anajipigania mwenyewe wacha kutusingizia. Atavuna alichopanda ''Chaga Gangsters.''
 
Ucjiongopee mwenyw
 
Hujaelewa chochote, ila kumbuka kuna Mtu aliyangulia kukuambia kwamba akili kama hizi ni kwa sababu ya aina ya kilevi unachotumia! Najua huwezi kuelewa kwa sababu ya biaseness inayo kutawala! Siyo kosa lako, hapa ndipo tulipo fikishwa na shule zetu za kata na utawala wa ‘kichawi’ wa ccm!
 
Unajiona ulivyo mtupu kumkichwa???
 
Mbona huyo mumeo jaji ameshajitoa wewe unabwekabweka tu hapa. Mwambie abadilishe mawazo basi kama anaweza.
 
Hakuna cha mashitaka mazito wala nini! Kesi ya Mbowe ni nyepesi tu, sema uzito unaouona Wewe ni mapenzi yako kwenye uongozi wa dhuluma, uvunjaji wa katiba na ubambikiaji kesi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…