Jaji M.C. Othman Jaji Mkuu mpya wa Tanzania

Jaji M.C. Othman Jaji Mkuu mpya wa Tanzania

Ili kusave muda naomba utuambie mtoa mada amedanganya wapi Je hawa jamaa sio ndugu??????
Sijakataa kwamba ni ndugu. lakini undugu wao hauhusiani na kazi watakazofanya. na wala hakuna ushahidi uliowekwa hapa kwamba eti Othmani wa TISS ndiye aliyechagiza kuteuliwa kwa huyu Ndg yake New CJ. kama unao ushahidi weka hapa
 
Tusaidie tafsiri yake basi ili na sisi tukawachemshe wengine
"(Naanza)......... Kwa jina la Mwenyezi Mungu, mwenye kuneemesha neema kubwa kubwa na mwenye kuneemesha neema ndogo ndogo"
" Amani ya Mwenyezi Mungu na iwe juu yenu wote !"
 
Sijakataa kwamba ni ndugu. lakini undugu wao hauhusiani na kazi watakazofanya. na wala hakuna ushahidi uliowekwa hapa kwamba eti Othmani wa TISS ndiye aliyechagiza kuteuliwa kwa huyu Ndg yake New CJ. kama unao ushahidi weka hapa

Hivi hili suala la conflict of interests wewe halikutishi???????
 
Maandalizi ya Mahakama za Kadhi na OIC na hatimaye kuifanya Tanzania kuwa kama Sudan, Nigeria au hata Somalia!
 
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116539
E-mail: press@ikulu.go.tz
Website: www.mawasilianoikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425




PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais Jakaya Mrisho Kikwete, amemteua Jaji Mohamed Chande Othman kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania, kuanzia tarehe 28 DIsemba, 2010.

Jaji Othman anachukua nafasi ya Jaji Augustino Ramadhani anayestaafu kwa mujibu wa sheria tarehe 27 DIsemba, 2010.

Kwa sasa Jaji Othman ni Jaji wa Mahakama ya Rufaa na pia ni mtaalamu binafsi juu ya hali ya Haki za Binadamu huko Kusini mwa Sudan, hadi mwezi Agosti 2011.
Jaji Othman alizaliwa tarehe 1 Januari, 1952, ana shahada ya kwanza ya Sheria (LLB) ya Chuo Kikuu cha Dar-Es-Salaam na Shahada ya Uzamili (MA) kutoka katika Chuo Kikuu cha Webster, Geneva-Uswisi.

Amewahi kuwa Makamu wa Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Rwanda huko Arusha na amewahi kushika nafasi sawa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali huko Timor Mashariki.

Jaji Othman pia, amewahi kufanya kazi ndani na nje ya nchi katika Mashirika mbalimbali ya Kitaifa na Kimataifa kama vile Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDP) na Shirika la Msalaba Mwekundu.

Jaji Othman ataapishwa kesho tarehe 27 Disemba, 2010 katika viwanja vya Ikulu saa 4:00 asubuhi.

Imetolewa na Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais Msaidizi
Ikulu
Dar es Salaam
26 Disemba, 2010

Hivi cheo cha Primi Kabanga ni sahihi hapo kweli(blu) au angetakiwa awe Mwandishi Msaidizi
wa Habari wa Rais
maana yake hapo kwenye blue ni kama vile yeye ni mwandishi wa habari wa msaidizi wa Rais (makamu wa Rais?) wataalamu wa lugha karibuni
 
Sijakataa kwamba ni ndugu. lakini undugu wao hauhusiani na kazi watakazofanya. na wala hakuna ushahidi uliowekwa hapa kwamba eti Othmani wa TISS ndiye aliyechagiza kuteuliwa kwa huyu Ndg yake New CJ. kama unao ushahidi weka hapa
Ni mtu mwenye akili zenye kuenea kwenye kizibo cha soda tu ndie anaweza asione walakini kwenye huu uteuzi!
Kwa suala la udini kwangu sidhani kama lipo ILA ni wehu wa hali ya juu kuwapa ndugu wawili (kama kweli ni ndugu kama inavyosemwa) nyadhifa sensitive kama hizi. i.e. Directore wa Usalama wa taifa na jaji mkuu. Inabidi bunge liingilie kati mapema sana kabla mambo hayajaharibika!!
 
Nasikia harufu ya mahakama ya kadhi
 
Oic ,kadhi, zimenukia .dah udini utaiangamiza nchi .mahakama ,bunge kwisha kazi.
 
Hivi cheo cha Primi Kabanga ni sahihi hapo kweli(blu) au angetakiwa awe Mwandishi Msaidizi
wa Habari wa Rais
maana yake hapo kwenye blue ni kama vile yeye ni mwandishi wa habari wa msaidizi wa Rais (makamu wa Rais?) wataalamu wa lugha karibuni

mkuu naona wewe upo sahihi kuliko huyo jamaa wa ikulu.... sina uhakika ana cheo nyadhifa gani kwani hayo maandishi yenye blue hayaeleweki...
 
CJ Chande, hongera, tunakutegemea usimamie suala la katiba mpya kwa umakini!
 
Sijakataa kwamba ni ndugu. lakini undugu wao hauhusiani na kazi watakazofanya. na wala hakuna ushahidi uliowekwa hapa kwamba eti Othmani wa TISS ndiye aliyechagiza kuteuliwa kwa huyu Ndg yake New CJ. kama unao ushahidi weka hapa

Ndugu yangu, hakuna mjadala kuwa Chief Justice kama vyeo vingine kama mawaziri, wakurugenzi wa mashirika ya umma, etc, lazima wafanyiwe vetting na usalama wa taifa, TISS. Vijana wa TISS wanafanya vetting, wanampelekea mkuu wa TISS then anampelekea Rais. Mwenye final input kwenye file za vetting za watu kabla haijaenda kwa Rais ni mkuu wa TISS. Sasa kwenye issue hii Othman wa TISS ilikuwa ni wazi kuwa ana conflict of interest kwa kuwa mdogo wake pia yupo kwenye majina haya. Mkuu wa TISS anaweza kuandika file zuri kwa mtu mmoja na kuwachafua wengine hivyo ku-influence uteuzi wa Rais moja kwa moja.
 
Mkwere mdini na atuendleza forever

Udini ni upi?.Aliyemaliza ni Augustino hukuona tatizo,lakini kwa vile aliyechaguliwa ni Othman unaona ni udini.Tatizo la wadini wa kikristo linajitokeza hapa,kwamba kila mara wanataka wasikie majina ya kwao tu.
Hayo maeneo aliyowahi kupelekwa jaji Othman kufanya kazi zake na kwa ufanisi nahisi ana sifa ya kazi yake zaidi lakini mwenyewe yawezekana hata dini yake haifahamu vizuri ni mfano wa Salim Ahmed Salim namuonea huruma.
Kawahi kufanya kazi zilizopelekea wakristo kujitenga na taifa kuu la kiislamu la Indonesia huko Timor.Amefanyia kazi msalaba mwekundu na sasa anajitahidi kufanikisha kulimega tena taifa la kiislamu la Sudan.Hivyo kwa taifa lisilokuwa na dini kama Tanzania huyu anaweza asione nongwa kurejeshwa mahakama ya kadhi.
 

Attachments

  • CHANDE.jpg
    CHANDE.jpg
    16.6 KB · Views: 75
These Chandes.Tusije sasa tukawa tunakabidhiwa kwa freemasons moja kwa moja.Mm,kazi kweli.Naomba mtu mwenye habari kamili kuhusu Chande huyu atupe taarifa.Asije akawa mtoto wa Andy Chande,Grand Master wa Freemasons Lodge ya Africa ya Mashariki.Kama ndiye uteuzi wake ni muafaka kwa freemasons maana atasimamia uingizwaji wa ushenzi wao kwenye katiba mpya na mchakato mzima wa uanzishwaji wa mahakama ya kadhi.Well done freemasons,mna akili nyingi, lakini hekima hamna!
 
Lets wait and see hakuna haja ya kuwa na speculation za udini. Utendaji wake ndio utatupa fact labda kama kuna mtu anajua style za utendaji wake.
 
Ndugu yangu, hakuna mjadala kuwa Chief Justice kama vyeo vingine kama mawaziri, wakurugenzi wa mashirika ya umma, etc, lazima wafanyiwe vetting na usalama wa taifa, TISS. Vijana wa TISS wanafanya vetting, wanampelekea mkuu wa TISS then anampelekea Rais. Mwenye final input kwenye file za vetting za watu kabla haijaenda kwa Rais ni mkuu wa TISS. Sasa kwenye issue hii Othman wa TISS ilikuwa ni wazi kuwa ana conflict of interest kwa kuwa mdogo wake pia yupo kwenye majina haya. Mkuu wa TISS anaweza kuandika file zuri kwa mtu mmoja na kuwachafua wengine hivyo ku-influence uteuzi wa Rais moja kwa moja.
Ndg Upo sawa, well and good. lakini kwa mujibu wa Ibara ya 36 ya Katiba hii tunayotaka ibadilishwe, hayo uliyoyasema kuhusu Vetting hayapo, so bado Rais ndiye anayefanya maamuzi ya mwisho nani amteue kulingana na LABDA na maslahi yake yeye mwenyewe kama Mkulu, ndio kama wachangiaji wengine wanasema labda kateuliwa kwa sababu za kuianzisha Mahakama ya Kadhi, OIC....etc. bado nasisitiza sidhani kwamba DG wa TISS ndio kachagiza uteuzi wa New CJ
 
Achanini na dini angalieni vigezo muhimu, kama ifuatavyo

Mara east Timor, Mara south Sudan, mara mahakama ya wanyamulenge arusha. Mmemshtukia mkwere anakukusudia uongozi wake utupelekeee?

Msijesema sikiwaambia mapema!
 
Back
Top Bottom