Jaji M.C. Othman Jaji Mkuu mpya wa Tanzania

Jaji M.C. Othman Jaji Mkuu mpya wa Tanzania

Hivi sasa tunataka ateuliwe Pagan ndiyo tuone anafaa? Alipoteuliwa Jaji Ramadhani na huyo huyo JK mbona hapakuwa na maneno? Hivi kuna mtu anaweza ku-punch holes juu ya uwezo wa Jaji Chande ukiondoa "dhambi" yake ya kuwa Muislam. Na kwa hiyo mnachosema ni kwamba kwa vile kaka yake yuko TISS basi yeye aadhibiwe kwa kutopewa haki yake ya kutumikia taifa hili kwa sifa zinazomstahili. Mimi sioni kama hiyo ni issue maana kuna wakati nchi hii Bomani mmoja alikuwa waziri wakati Bomani mwingine akiwa ni Attorney General na wala hakuna aliyekosa usingizi.

Ni jambo la kusikitisha kwamba kuna watu wana phobia mbaya dhidi ya dini za wenzao (namaanisha wote wakristo na waislamu) na utashangaa wenyewe uumini wao unaishia kwenye majina yao tu halafu ndo wako busy kuharibu sifa nzuri za wengine. kwa wanaomfahamu Jaji Chande wanajua kwamba ana elimu nzuri sana ya kutosha, ana uwezo mkubwa sana wa kikazi na ushahidi ni hukumu na maamuzi mbalimbali aliyoyatoa. Uzoefu wake kitaifa na kimataifa hauna ubishi na sidhani kama kuna yeyote kati ya hao washindani wake wanamfikia kwa yote hayo. Kwa taarifa yenu hata ndani ya Judiciary, wengi wa Majaji waandamizi (tena wakristo) walikuwa wanaomba ateuliwe yeye ili alete mageuzi kwenye Judiciary hii yenye changamoto luluki, ikiwemo maslahi duni ya watumishi wake na rushwa iliyokita mizizi. Wafanyakazi hawana ari ya kufanya kazi na wanahitaji mtu atakayetupia jicho na Jaji Chande ni mmoja wa wale wachache wenye uwezo huo. Tukumbuke kauli ya Mwalimu kwamba hatateuliwa au kukataliwa mtu kwa sifa ya dini au kabila lake. Hatuchagui Mufti au Askofu hapa. Hii ni kazi ya kitaaluma na ifikie wakati Rais akifanya uteuzi mahiri na maridhawa apewe sifa zake!
 
Kama TISS wanashirikishwa kwenye uteuzi Wa Jaji mkuu na je Judicial Service Commission wabafanya kazi gani??
 
Kama TISS wanashirikishwa kwenye uteuzi Wa Jaji mkuu na je Judicial Service Commission wabafanya kazi gani??
Haya maswali yote yanakuja baada ya kuteuliwa muislam. Mbona walipoteuliwa majaji wakuu waliomtangulia hamkuuliza? Huyu ni jaji mkuu wa tano ndio mnauliza. Tumewachoka na chuki zenu kwa waislamu na tena wengi wenu nyie ni wapenzi wa CHADEMA, mnaboa sana. Kila kitu udini udini udini tu.
 
Hivi kuna mtu anaweza ku-punch holes juu ya uwezo wa Jaji Chande
most of his judicial experience is not local

na hata huko alikokuwa hakupata courtroom experience yeyote, unless mtuambie aliruhusiwa kuingia mahakama za nchi nyingine, jambo ambalo litaibua maswali ya uraia
 
Ifike mahala tuache kutia nyongo kila jambo linalofanywa na watawala. Nimesoma kwa makini wasifu wa Jaji Mkuu mpya Othman Chande. Inajitokeza waziwazi kwamba huyu ni mtu mwenye wasifu na sifa za juu kabisa katika maswala ya sheria na mahakama. Ana uzoefu wa hali ya juu kitaifa na kimataifa. Mamlaka ya uteuzi wangekuwa ni wajinga kama wangemuacha kwa sababu tu kaka yake ni Mkurugenzi Mkuu wa TISS. Tony Blair na Gordon Brown waliwahi kuwateua mtu na mdogo wake kuwa katika baraza la mawaziri. Juzijuzi Chama cha Labour kiliwapitisha mtu na kakake kugombea nafasi ya Kiongozi wa labour.

Ni ujuha na ujinga kumteua mtu kwa sababu ya dini, udugu, ukabila, n.k. Vilevile ni ujuha na ujinga wa kutisha kuacha kumteua mtu kwa sababu tu ndugu yake alishatangulia huko serikalini hata kama ana sifa. Haya mambo ya ku-balance kidini, kikabila, kidugu, kikanda na kimokoa ndiyo yanaletekeza mijitu mingine kuteuliwa kuwa mawaziri hata kama haina sifa ili wateuzi waonekane walizingatia mgawanyo wa kimkoa, kidini, kikabila, n.k. Kama mtu ana sifa basi ateuliwa, na kama hakuna mtu mwenye sifa kwa nafasi husika kutoka hiyo dini au kabila au mkoa basi na iwe hivyo. Si lazima kila dini au mkoa uwakilishwe katika nafasi za uteuzi.

Othman Chande, chapa kazi. Una nafasi ya kujitengenezea legacy ya pekee kwa kutoa msukumo muhimu ili hatimaye nchi yetu iwe na Katiba Mpya yenye kuzingatia misingi ya demokrasia na haki za binadamu.


Lazima tukemee pale tunapoona udini unachukua kasi.
Alishaahidi kila nafasi ikitokea lazima amchague m-kadhi na angalia nafasi zake nyingi za uteuzi.
 
hahahahahah, ili kukata mzizi wa fitini ilibidi awe Nyamburusi Shumbushu Mwakitwange

Au hata wangemteua Ng'wanambogolo kuepuka hisia za udini na kupendeleana.

duh hii nchi jamani!?
 
Ifike mahala tuache kutia nyongo kila jambo linalofanywa na watawala. Nimesoma kwa makini wasifu wa Jaji Mkuu mpya Othman Chande. Inajitokeza waziwazi kwamba huyu ni mtu mwenye wasifu na sifa za juu kabisa katika maswala ya sheria na mahakama. Ana uzoefu wa hali ya juu kitaifa na kimataifa. Mamlaka ya uteuzi wangekuwa ni wajinga kama wangemuacha kwa sababu tu kaka yake ni Mkurugenzi Mkuu wa TISS. Tony Blair na Gordon Brown waliwahi kuwateua mtu na mdogo wake kuwa katika baraza la mawaziri. Juzijuzi Chama cha Labour kiliwapitisha mtu na kakake kugombea nafasi ya Kiongozi wa labour.

Ni ujuha na ujinga kumteua mtu kwa sababu ya dini, udugu, ukabila, n.k. Vilevile ni ujuha na ujinga wa kutisha kuacha kumteua mtu kwa sababu tu ndugu yake alishatangulia huko serikalini hata kama ana sifa. Haya mambo ya ku-balance kidini, kikabila, kidugu, kikanda na kimokoa ndiyo yanaletekeza mijitu mingine kuteuliwa kuwa mawaziri hata kama haina sifa ili wateuzi waonekane walizingatia mgawanyo wa kimkoa, kidini, kikabila, n.k. Kama mtu ana sifa basi ateuliwa, na kama hakuna mtu mwenye sifa kwa nafasi husika kutoka hiyo dini au kabila au mkoa basi na iwe hivyo. Si lazima kila dini au mkoa uwakilishwe katika nafasi za uteuzi.

Othman Chande, chapa kazi. Una nafasi ya kujitengenezea legacy ya pekee kwa kutoa msukumo muhimu ili hatimaye nchi yetu iwe na Katiba Mpya yenye kuzingatia misingi ya demokrasia na haki za binadamu.

Samahani kidogo, hapo nilipopigia mstari panaendana kabisa na u-consultant ulioufanya kwa chadema kwenye ubunge wa viti maalum. Ukaamua kujaza watu wa koo fulani fulani na mikoa fulani fulani ili tu kukidhi mahitaji na matakwa ya wachache. Nchi hii watu wanaijua jinsi inavyoendeshwa kiubabaishaji, teuzi nyingi zinafanyika kiundugu, kidini, kikabila halafu hamtaki watu wa-question nia zenu mnapofanya kazi za umma.
 
We huna karatasi ndo mana huwez kurudi,ila sijaona sbb ya kututusi namna iyo aise,ingawa kwel tuna judge mambo kwa kuangalia vitu visivyo kua na maana ila huwez kututusi ivyo,we endelea kubeba box huko si tunajenga nchi huku

Sorry Madcheda, pamoja na kuona kwamba jamaa amekutusi, in practice ni kweli alichosema. Ukweli ni kwamba kuwa muislamu/mkristo maybe hakusaidii chochote kwa jamii za watu hao, na ni ukweli kwamba watanzania ni waongeaji mno kwa kila jambo hata lisilohitaji maelezo mengi kama hili-Badala ya wanaJF kutoa mapungufu kwa CJ aliyepita ili kumpa changamoto CJ huyu na hatimaye matarajio ya watz at-least kufikiwa kupitia mhimili huu, watu wamejikita kwenye muislamu-mdogo wa TISS and the like! ambavyo havimsaidii CJ huyu kushughulikia vitu ambavyo katika uhalisia Taifa linahitaji..
 
Tatizo hapa watu hwaelewi wanachobishana, MC Othman, ana sifa nzuri za kuwa CJ hata zaidi ya sifa alizonazo Kikwete kuwa rais, ana sifa bora zaidi ya kiongozi yeyote yule mwingine wakuteuliwa na rais; however, kuwa na ndugu wawili kwenye jopo la maamuzi inaweza kuraise "conflict of interest". Tunachoitaji ni mtu au taasisi inayatambua kazi za CJ na kazi za TISS (director's order) hatuandikie hapa, then tutajudge na kujua kama JK alikosea au la, siamini kama hakuna mtu mwingine (hata kama muislam) ambaya ana sifa kama zake (othamn) au pengine zaidi yake, na ikumbukwe watu wana doubt si kwa ajili ya uwezo wake bali kuweka ndugu wawili kwenye decisive points siyo vizuri...pengine labda Kikwete angepindisha sheria kidogo apeleke jina lake bungeni lijadiliwe like how they do in the US (senate wanamconfirm):Biography of John G. Roberts
 
Udini udini tu kati ya waisilamu na wakiristu mbona sisi wapagani hatulalamiki na tuko wengi hapa nchini na hatuna waziri hata mmoja!!!!!!
 
Duh, huyu Chief Justice mpya ni mdogo wake mkuu wa usalama wa taifa, yaani director general of the Tanzania Intelligence and Security Services (TISS), Rashid Othman. Katika vetting ya Chief Justice huwa mkuu wa TISS anahusishwa kwa karibu kupitisha majina.

Hii ina maana kuwa Othman wa TISS kampigia chapuo mdogo wake kuwa Chief Justice mpya! It's very possible candidates wengine wa post hii walichafuliwa makusudi ili dogo apite.

Tutarajie nini kuhusu maamuzi sensitive ya mahakama kuhusu katiba mpya, mgombea binafsi, na mengine ambayo yatawagusa watawala kwa karibu. It's obvious kuwa usalama wa taifa ndiyo itakuwa inaiendesha mahakama ya Tanzania. Othman wa TISS atakuwa anatoa maagizo tu kwa dogo wake Othman Chief Justice.

"Dogo hiyo kazi ya Chief Justice si nimekupigia chapuo mimi, sasa nimeshauriana na Rais na uamuzi wa mahakama ya rufaa kwenye kesi hii uwe hivi...."

Kazi ipo hapa... TISS itakuwa inaiendesha mahakama ya Tanzania mpaka mwaka 2017 ambapo Othman atakuwa amefikia umri wa kisheria wa kustaafu.
Sikubaliani, hata kama ni ndugu haiwezekani wakafanyakazi kwa misingi uliyoandika, wakifanya hivyo waishia kuwa very unpopular katika jamii hii, kitu ambacho sidhani kama wanakihitaji ,
 
Chande ni jaji wa ccm na ndio maana kesi zote za uchaguzi dhidi ya makada maarufu wa chama hicho alizisikiliza yeye na kuwapa ushindi kama vile ile kesi ya uchaguzi dhidi ya Chrisant Majiyatanga Mzindakaya kule sumbawanga!! He is not a judge at par with distingished judges lile the late Mwalusanya and Lugakingira or even Kisanga for that matter!! Kesi zote za ccm watapeta na ndio maana Mkwere alikimbilia kuteua majaji wengi wasiostahili professionally lakini wa------- yake!!
 
Nakumbuka wakati niko sekondari nilikuwa na special interest with African American history na literature. Nadhani hii ilichangiwa zaidi na kwenda kwangu pale USIS (maelezo sasa hivi) baadae ilipohamia kule PUGEOT HOUSE. Katika kusoma kwangu among my favorites alikewa Malcolm X ambaye quote yake ni ninayoipenda ni aliposema kuwa TOMORROW BELONGS TO THOSE WHO PREPARE FOR IT TODAY lakini pia bila kumsahau WEB DU BOIS lakini nilisoma kitabu kilichoandikwa na FREDRICK DOUGLASS ambaye alisema..."TO UNDERSTAND, A MAN MUST STAND UNDER." Kwa maneno mengine ni kuwa only by considering all the hardships a man has overcome in life, hivi ndivyo Douglass alivyokuwa anaamini, so can the rest of us judge him fairly. ivyo jaji Othman hana tofauuti katika hili.

Mimi ninamfahamu Jaji Othman and i fail to understand kwa nini uteuzi wake uwe issue nzito tena katika ukumbi huu wa the so called EXPERTS and GREAT THINKERS


Anyone who knows Judge Othman should by now realize that reputation was everything to him the work of art he had sculpted, the summit he had climbed, the treasure he had stored up from years of public service. Jaji Othman ninavyomjua mimi has often spoke of his life and reputation as one and the same. It really concerns me kuwa hakuna aliyekuja na any constructive criticism of his intellectual work as the learned au mtu aliyebobea kwenye fani yake.



Huyu Jaji wetu mpya, like most who rise to power, he had toiled for years in anonymity serving others of higher station. I just wanna tell you one thing, endeleeni kumtukana na kumkejeli as much as you want lakini mkae mkijua kuwa huyu jaji mkuumpya is not for turning. Ndio ni Muislam na kama kuna mtu hapendi then he hilo ni shairi lake. Lakini kwenye Tanzania iliyojaa maskini ya leo hii na pia Tanzania ambayo its common waislam kuambwa kuwa HAWAJASOMA lets just say kuwa hizi baseless accusations if anything zitamsaidia in an important way, by underscoring the fact that he carried along with him the aspirations of the 'under-educated' Muslims in Tanzania.


Hapa once again JK na team yake imeweza kuwathinitishia kuwa you dont have to be born into privilege ndio utafanikiwa. Hii pia ni kkuwaonyesha wanaolalamika kuwa its possible for a MSWAHILI na MUSILAM kuwa Jaji Mkuu Tanzania ni possible tena Jaji ambaye miaka ypte yake ya utumishi amekuwa akitoa huduma bila kujali MKRISTO au dini nyingine yoyote ile. As a nation we should be proud kuwa we are moving on from petty politics na kuangalia mbele. If anything appointment ya Jaji Othman ni culmination of his life and his struggles.
Your a great thinker
 
Jamani tusiangalie majina ya watu na dini zao. tukienda hivi na wasilamu naowakiliza ni lini jaji mkuu alikuwa muislamu kabal ya huyu mutawajibuje. Hivi ni nani aliyemteua Jaji Augustino Ramadhani kuwa jaiji Mkuu kumbkumbu zangu ni JK mbona hamkubeba mabango mtaani kumpinga?

Juzi mulimsangilia JK alipomchagua Magufuli na mwakyembe inakuwaje leo munamuona mdini. hembu kuweni neutral alafu muangalie qualification na experience za candidates wote.
Haya munayazungumza lakini mwisho wake ni mbaya itafika wakati tutayakataa majina yetu ya kiarabu na kizungu tubakie na kiasili. tubamie na majina kama Mizengo Pinda na yale ya kati kama Peter tutayakataa ili tuchaguliwe.

soma gazeti la CITIZEN wasifu wakila mtu umewekwa analyse alfu ndiyo uje kutuambia hoja zako.
infact katika watatu hawa wanakaribiana au kulingana experinece yao angalia hata umri unakaribiana inaonyesha muda walikuwa kwenye profession ni sawa laba Othmani ana internation experience zaid ya wenzake.
 
Wakristu badala ya kupiga kelele you better brace for impact! OIC na Kadhi hazikwepeki kwa vyovyote vile. Anzeni kuzoea. Ila kinachouma zaidi ni kuwa Top four za Tanzania (Bila kugusa Zanzibar) yupo mtu mmoja mkristu anayeweza kukaimu urais (speaker ana makinda). Usalama wa Taifa (Muislam), Wizara ya mambo ya ndani (usalam ni Mwislam), Mahakama (Mwislam), Urais (Mwislam). Kwa nini JK hana imani na Wakristu kwenye mambo ya Usalama?
we nawe acha uongo wako,angekua hana imani na wagalatia angemteua mkuu wa majeshi kutoka upande huo?mbona mnapenda kupotosha mambo na kuyakuza bila sababu za msingi.DCI Manumba anaswali msikiti gani?
 
Haya maswali yote yanakuja baada ya kuteuliwa muislam. Mbona walipoteuliwa majaji wakuu waliomtangulia hamkuuliza? Huyu ni jaji mkuu wa tano ndio mnauliza. Tumewachoka na chuki zenu kwa waislamu na tena wengi wenu nyie ni wapenzi wa CHADEMA, mnaboa sana. Kila kitu udini udini udini tu.

Mi nakuunga mkono ndugu yangu, kuwa chadema sio kupinga tuu kila jambo hata lenye maana. kila kitu udini udini sasa hembu onyesheni mapungufu ya Jaji Othmani ili tuyaone na tulinganishe na mapungufu ya cadidates wengine alafu ndiyo museme museme Othmani hafai.

Kama tutabaki na udini udini kila kitu hata CHADEMA yenyewe tutahama na kurudi zetu CCM

Inashanaza watu kujadili udini ooh mdogo wa nani alfu wanajiita GREAT THINKERS waapi. hembu semeni kama tukiamua asichaguliwe muislamu au mkiristo nani sasa atachaguliwa
 
Siamini sana katika udini..kwasababu nauona kama agenda tu inayomwagwa na wakubwa kwa wananchi wa kawaida..sisi wananchi hatuna udini,na ndio maana wengine tumekuwa darasani kwa zaidi ya miaka 4 bila kufahamu nani ni wa dini gani haswa au wa kabila gani..labda kwa ku-guess tu tukisikia jina lake.
Katika hili la Jaji Mkuu mpya, napata shida kidogo na 'profile yake' aliyeteuliwa..kwamba siioni kama ni ya kuweza kuleta mabadiliko kivile..labda katika hicho alichojipatia ndio ajenge 'profile'.
Kila la kheri Jaji Mkuu mpya..nakubaliana na aliyesema ni kama JK wakati huu anatimiza wajibu tu..lakini si kwa moyo wa 'kuwiwa, na kuumia'!
 
Back
Top Bottom