Jamaa anamuoa mchumba wa rafiki yake kama mke wa pili

Jamaa anamuoa mchumba wa rafiki yake kama mke wa pili

Nitumie namba ya huyo dogo inbox nimshauri direct maana asije akaaga dunia please mkuu Kama ishu iko serious
Ingekua vema USHAUR Hapa Hapa tu mkuu[emoji120]

USHAUR wako Unaweza wasaidia hata wengine pia[emoji120]
 
Ashukru Mungu kwa yaliyotokea,Wala Haina haja ya kulazimisha amtangulize Mungu mbele ,afanye maisha yake mengine Kuna kitu kikubwa sn Mungu kamiepusha nacho
Kweli mkuu,
Huwez jua mungu kaepusha nini
 
Kiumbe mwanamke kumuelewa ni ngumu sana na ukiona unaanza kumuelewa mwanamke ujue siku zako za kuishi zimeisha hapa duniani
 
Na yalianza muda mrefu. Haiwezekani ndani ya kipindi kifupi waoane.
Ukitaka kuishi kwa amani na mwanamke usimuone wivu, mpe mahitaji yake ila usimuoneshe km unamhitaji sana.
Usemalo Lina ukweli kabisa, Hawa hawakuanza hivi karibun..

Huenda kulkua namahusiano ya Siri yanaendlea hapa katkat
 
Mpuuzi mpuuzi TU,
sijajua uko kwenye uke wenza kafuata nini.

Na sijui Ni Nani alimshaur kua uke wenza atafurahia maisha
Yaani hapo kwenye uke wenza sijamuelewa kabisa huyo dada, kumuacha kaka wa watu kwenda kuolewa mke wa pili mmh. Si kwa wivu huu nilionao mke wa pili ni big no bora kubaki single tu. Ila siku atalia machozi ya damu , malipo soon tu
 
Mambo mazito haya.Mapenzi!

Ngoja kwanza niangalie The expendables,nitarudi
 
Dah! Jamaa huwez Amin alkua anamgharamia Yule mwanamke utadhan mke wake wa Ndoa.

Jamaa yangu Ni form four, ila alipambana kumlipia Ada mpaka binti uyu kamaliza chuo kikuu.

Kibaya Zaid ata hapo sheli anakofanya kazi uyu binti, jamaa ndo kamuunganisha na ndo mdhamini wake.

Binti kapangiwa nyumba nzima, anaishi kwa Raha Sana.

Jamaa alkua analipa kila kitu khs mahitaj yake yote ya nyumbani mpaka dharula za familia yake.

Gari anayotembelea kamnunulia uyu jamaa,
(Tena nilishiriki ipasavyo kwenye mchakato mzima wa kuiagiza mpak kuitia mkononi)

mafuta juzi juzi TU tunatoka gym alipitia she'll kumuwekea ya 350,000 kwa ajili ya mizunguko yake.nikishuhudia mwenyewe.

Mshahara anaolipwa sidhan hata Kama uwa anaugusa kabisa.

Kwakweli,
alichomfanyia jamaa Ni zaidi ya unyama[emoji26]
Mimi hata sioni kama huyo binti anampenda huyo jamaa kiukweli naona alikuwa anapenda tu pesa zake.
Hivi mtu aliyekufanyia hayo yote na unajua kinachoendelea kwenye familia yako unashindwaje kumwambia yanayojiri ili mkae mjue mnafanyaje ili kumpa nafasi ya kurekebisha pale alipopwaya angalau kumpa muda akishindwa ndio uchukue maamuzi mengine ila tayari ulimshirikisha ashindwe tu mwenyew kutetea penzi kama kweli alikuwa serious ila hata huko mbele kusiwe na wakulaumiwa.
Huyo bidada alikuwa na mahusiaono ya siri muda mrefu tu ila kwa huyo mchumba alikuwa anazuga mana huduma anapata.
Huwezi nambia process zote kuanzia barua,mahari mpaka ndoa inakaribia anashindwa kumweleza mpenzi wake kama kweli anampenda.
Mwambie huyo dogo akimbie tena asigeuke nyuma hapo hakuna mwanamke mana unaanzaje kumchukua huku unajua kabisa amekusaliti.
Atafute mwanamke kwingine wapendane huyo mchumba tayari ni mke wa mtu aachane nae atamsumbua tu yeye na familia yake.
Kuna familia zinatia aibu sana mana misaada na hela za watu wamekula sana ila wakaona binti yao aolewe na kwingine wao kama wazazi walishindwa nini kumuita huyo kijana kumuuliza ana mpango gani mana inaonekana wanamjua fika.
Aachane nao kwanza kuna familia ukioa unaenda kubebe matatizo na stress mfano mzuri ni hiyo.
Sorry nimeandika kwa hasira kama vile namjua huyo dogo.
 
Dah! Jamaa huwez Amin alkua anamgharamia Yule mwanamke utadhan mke wake wa Ndoa.

Jamaa yangu Ni form four, ila alipambana kumlipia Ada mpaka binti uyu kamaliza chuo kikuu.

Kibaya Zaid ata hapo sheli anakofanya kazi uyu binti, jamaa ndo kamuunganisha na ndo mdhamini wake.

Binti kapangiwa nyumba nzima, anaishi kwa Raha Sana.

Jamaa alkua analipa kila kitu khs mahitaj yake yote ya nyumbani mpaka dharula za familia yake.

Gari anayotembelea kamnunulia uyu jamaa,
(Tena nilishiriki ipasavyo kwenye mchakato mzima wa kuiagiza mpak kuitia mkononi)

mafuta juzi juzi TU tunatoka gym alipitia she'll kumuwekea ya 350,000 kwa ajili ya mizunguko yake.nikishuhudia mwenyewe.

Mshahara anaolipwa sidhan hata Kama uwa anaugusa kabisa.

Kwakweli,
alichomfanyia jamaa Ni zaidi ya unyama[emoji26]
Kwenye miti hapana wajenzi

Halafu bado binti anajitetea eti hamuelewi jamaa!

Ndomana watu wengine wanaamua kuroga

Jamaa achukulie changamoto hii in positive way japo inauma sana na itamchukua muda kua sawa lakini ajitahidi kumove on

Amshukuru Mungu hata kwahilo maana kila kitu kitokeacho hua kuna sababu nyuma yake. Hivo hajui Mungu kamuepushia nini ama kamuandalia nini kizuri mbele

Mi naamini wakati mwingine mpaka uje umpate yule perfect match huna budi kupitia changamoto hizi za kuumizwa ili utakapompata yule sahihi ujue namna ya kumthamini

Wakati huu ninyi kama marafiki zake wa karibu ndo muda wa kua nae bega kwa bega katika kumtia moyo mwenzenu ikibidi kumpeleka kwa mwanasaikolojia ama kwenye nyumba za ibada
 
Afu wanawake Sijui huwa mnawaza Nini,

Najaribu kuwaza huyu binti kafata nini kwa jamaa maana hata kiuchumi dogo alimpita mbali brother.

Afu ukizingatia jamaa tayar alkua na MKE wake na watoto watano wakubwa kabisa.

Afu anamuacha jamaa Alie single, anaenda kuingilia Ndoa ya Watu na kwenda kuolewa kama MKE wa pili kwa jamaa mwenye MKE na watoto watano.

Natafakari sana Sipati majibu.[emoji848]
Unaweza kukuta anaridhishwa kwenye ile sekta nyeti Mana kuna watu wazima sio haba wanajua anatakiwa afanye nini plus maexperience kibao kampagawisha bidada.
Labda dogo alikuwa anagusa gusa tu akaona anazingua.
 
Update....
Ni kwamba mwanamke alinyang'anywa simu ya awali alokua anatumia na kapewa simu mpya yenye line mpya ya Airtel.

Nmefanikiwa kuipata hio namba na nmempigia na kuongea mwanamke mwenyewe.

Anasema,
"Shem mi sio kwamba simpendi rafiki ako, nampenda sana na nilitamani awe mme wangu. Sema rafiki ako hakua serious na Mimi. Miaka 4 yote tangu ameleta barua hamna kinachoendelea. Familia inanisumbua Sana afu nikimwambia hataki kunielewa anadai mpaka amalizie nyumba yake. Nyumba imeisha anadai finishing bado. Hivi kweli shemej nyumbA inaweza mzuia mtu wasifunge Ndoa? Hivi kweli anachonifanyia mwenzako unaona Ni sahii."

Nikamjibu,
"Kwaiyo meji ukaona Njia rahisi Ni kuolewa TU na rafki yake, hujui itamuumiza Kias gani?"

Akasema,
"Shemej nikwambie TU ukweli, uyu B tangu mwanzoni ashaonesha ananipenda Sana. Afu tangu zaman keshaonesha Nia ya kunioa MDA mrefu. Sema Mimi TU ndo nilikua kikwazo, afu kingine uyu B anakubalika Sana uku nyumban.

Shemej presha kwa familia yangu kuhusu B Ni kubwa Sana, Baba na mama na dada zangu wote wanataka niolewe na B. Imefkia mpaka mama ananambia uyu alonichumbia Ni mhuni TU miaka 4 Ni uchumba sugu huo. Imefkia mpaka baba haniongeleshi kisa sitak kuolewa na B. Na wote washanambia nisipoolewa B Mimi sitokua mwanao Tena na watanifuta kwenye ukoo.

Shemej yang mi mwenywe Niko Njia panda apa, moyoni mwangu B hayupo kabisa ila nalazimishwa TU na familia yangu. Uto rafiki yako hawamtaki kabisa ata kumskia uku nyumbani."

Nikamwambia,
"Kwaiyo shemej uko serious kabisa umelazimishwa Hii ndoa?"

Akasema
"Ndio Shem, yaan naomba TU uniombee msamaha TU kwa rafk yako. Mi bado nampenda Sana."

Nikamwambia,
"Bas Shem naomba ufanye jion tuonane ata kwa jamaa tujue tunaliwekaje hili"

Akasema,
"Sawa, ila Mimi kwa jamaa siwez kuja tena.italeta balaa. Labda yeye ata aje kwako niwakute apo kwako"

Nikasema,
"Sawa"

Ninachowaza Sasa,
Kama ni kweli uyu mwanamke kalazimishwa. Na kweli ANAMPENDA jamaa.

Nawaza kumshauri rafiki yangu, ashirikiane na uyu mwanamke.
Kisha binti atoroshwe akawekwe mafichoni kwa sikU kadhaa Hadi ile harusi ilopangwa itakapopita.

Uyu B atakapomtafuta akakosa Basi Iyo Ndoa ya kulazimisha itakua imeota manyoya.

Afu Sasa uyo B aje kwetu kulalamika kwetu katoroshewa MKE, na sisi tuje tumuoneshe kua upumbavu hatutaki.

SIJUI KAMA NIKO SAHII AU LAH[emoji848]

ushauri wenu tafadhali
Haupo sahihi! Acheni aolewe na huyo jamaa aliyetoa helaa. Hilo mnalotaka kufanya sio njia sahihi, na si dawa ya hilo tatizo.
 
Basi sawa upo sahihi.

Ila huyo uncle naye awe na msimamo kama wako, azisome haraka alama zako za nyakati aelewe kwamba unampenda!

Maana wewe ulivyoandika umeonekana mjanja, unajali mahusiano na utamfaa.

Iwe pingamizi kwake tu uncle sasa, ukichukulia maisha ya ujana ni mafupi sana hayazidi miaka20.

Huko mbele ya safari ni ubibi na ubabu na furaha zenu zinageukia kutaniana na kucheza na wajukuu, hamjazeeka hapo?

Uncle afanye maamuzi magumu, wakati wenu ni sasa.
Uncle ni mkubwa kwangu sana tu....hatuna malengo makubwa zaidi ya kupeana raha
 
Kwani michepuko hawafanyiwagi hayo?

Lakini naona harufu ya chumvi kidogo.

Umpangishie nyumba, umnunulie na gari, halafu usioe kisa unasubiri nyumba iishe....thubutuuu

Na hakuna binti wa hivyo akubali kuolewa mke wa pili, kisa ndoa tu?
Nina mashaka.
Nakaziaaaaaaa

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Sijawahi kuandika nyuzi za ovyo mkuu,
Nnapokwambia alkua mchumba wake miaka minne namaanisha minne kweli.

Dogo tayar alkua na mtoto nje, alimzaa akisoma shule na ndo sababu ya dogo kuishia form 4 maana alikimbia miaka 30 jela ndo akaingia uko Kwenye kubangaiza.

Uyu mchumba wake amempata akiwa chuo mwaka wa 1.
Miaka 2 yote ya uchumba wao binti alkua anasoma chuo mkoa mwingine kabisa.

Mwaka 1 wote binti aliajiliwa Kama mtendaji wa tarafa mkoani uko vijijini,

Jamaa ndo kamtoa uko na kamuunganisha na kazi ya sheli kwa rafiki yake mmoja hapa mjini

Mwaka 1 tu ndo wamekua wote hapa mjini, yaani namaanisha mwaka huu 2021 unaoishia. (Yaani tangu mwezi octoba mwaka Jana mpaka leo Hii)

Na jamaa alompangia maksudi na hakutaka kuishi na kwake kwa maana jamaa yeye bado anaishi kwao (nyumba ya familia)

Ndo alipanga akishamaliza ujenzi wakahamie Kwenye nyumba yake anojenga sahvi.
Sema pamoja na kumpa pole jamaa etu,lkn na yeye alizidi mbwembwe nadhan hadi bint akawa na waswas nae,yaan umpangie dem nyumba nzima alaf usiishi nae kweli???

Unaeza kukuta hata huyo broo hajamchezea dem ila n swaga tuu,kumbuka demu anafanya kazi sheli means anakutana na jamaa mara kibao,

Muhimu n kumuelekeza dogo uhalisia baada ya hilo asonge mbele kama ambulance

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Kuna haja ya kuangalia yumba(familia) unayo enda kuposa au kuanzisha mahusiano nayo.

Angalau iwe na hofu ya Mungu ata kido au iwe familia ye heshima kidogo, utaepuka mambo mengi.

Jamaa anaoneka ni mtu mstaarabu kwa mujibu wa maelezo yako. Hivyo basi Mungu amemuepusha na hiyo familia ya kikora. Kwamaana imeandikwa "Bwana atakupa msaidizi wa kufanana wewe" kwaiyo huyo muhuni mwacheni aolewe na muhuni mwenzake.

Jamaa awe na subira miaka 39 bado hajachelewa sana wala hajawai. Amuombe Mungu ampe anayemfaa, mstaarabu kama yeye.

Tokea juzi uzi ulipo anza nilijua kabisa uyo dada anadanganya kuwa kalazimishwa na asingetokea hiyo jioni. Lakini shukuruni hakutokea kwa sababu kuna uwezekano mkubwa kama angepata mualiko huo wa kuonana na nyie, siku tatu kabla au mbili, angewapangia tukio la ajabu kama siyo criminal basis la udhalilishaji.

Hampendi uyo dogo na inawezekana hajawai kumpenda. Kama angekuwa anampenda angemwambia tokea yeye mwenyewe kwa mdomo wake, kuwa rafiki anamtongoza, haiingii akilini adi anafikia hatua ya kuposwa. Huyo dogo ana habari. Alafu anadai kalazimishwa na nyie bado mna muamini na kutaka kuonana naye.

Sheria zipo kulingana na Sheria za ndoa "Marriage Act" dogo anaweza kudai malizake na gharama alizo tumia kipindi cha uchumba wao, ikiwa ni pamoja na zawadi na gharama nyingine kama vielelezo vipo. Ila kwa upande wa kiroho tunashauri aachane navyo na asemehe yaani asibebe manung'uniko moyoni "akomboe nafsi yake" hii njia ya kiroho ndiyo nzuri zaidi. Maana unaweza kutumia sheria ukarudishiwa mali zako lakini ukabaki unateseka moyoni miaka yote.

Mwisho kabisa Nina swali. Yule binti aliye zaa nae utotoni hadi wakaacha shule,hakufaa kuwa mke wake?. Mtoto aliye zaliwa anamtunza kama inavyo stahili?.
 
Back
Top Bottom