Jamaa yangu ana Pass degree ila kapata kazi kwenye multinational company bila connection

Jamaa yangu ana Pass degree ila kapata kazi kwenye multinational company bila connection

kyagata

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2016
Posts
10,406
Reaction score
19,892
Sio kwamba nimesimuliwa hapana.

Huyu jamaa yangu alihitimu bcom in accounting kutoka pale udbs miaka kadhaa iliyopita.

Basi majuzi kati tuko nae ghetto tunapiga mvinyo tukaona tangazo kutoka kwenye kampuni kubwa mafuta lenye makao makuu yake huko Uingereza wakihitaji mhasibu kigezo ni uwe na degree ya uhasibu na uzoefu wa miaka minne wa kufanya kazi za kihasibu.

Mshikaji chap akaingia kwenye portal ya hiyo kampuni husika akajaza taarifa zake kisha akaapply ile kazi. Basi bana baada ya siku chache akapokea email kutoka kwa wahusika ikimpa maelekezo ya lini interview itafanyika na wapi.

Siku ya interview kaenda zake na Mungu wake tu, kafika pale anasema akakuta wadau wengine kama 10 hivi na katika kudadis akagundua baadhi yao walikua na cpa akati yeye hata cpa hana.

Basi interview ikaenda vyema tu na akawa anajua hawezi kupata ile kazi sababu ya cv za baadhi ya washindani wake kuwa nzuri kuliko yake pia wenzie walikua na matokeo mazuri ya shule.

Ila Mungu huyu ni wa ajabu jamaa jana akiwa zake kwa mhindi wake anachapa kazi akapokea simu akijulishwa kuwa kafaulu ule usahili na tayari amepokea offer letter ambayo nimebahatika kuiona. Salary yao sio haba kabisa ni salary inayokuweza kuishi vizuri tu kwa maisha yetu ya kitanzania.

Nilichojifunza kutoka kwa huyu msela wangu ni kuwa na ujasiri na kumtanguliza Mungu. Kuna watu kumbe wana matokeo mazuri ya shule ila interview zinawatoa knock-out na kuna watu wenye matokeo mabovu kama huyu jamaa angu ila ni wajanja wa kujibu vyema maswali ya usaili.
 
Experience haujaongelea labda jamaa ako alikuwa nayo
 
What we don't know us as human beings we're incapable of controlling outcome,but only process.
We try to force things to happen Ila Mara nyingi havitokii. Kumbuka hata demu ukitongoza halafu ukimuacha anakuja mwenyewe.
When it's your set ups,your right time,your patience is being rewarded. Hauoni hata predator anakaa anasubiria like mamba,tiger,American cougar aka puma. When a deer is set up Ana pull the trigger na sio lazima apate,akikosa hawajutii wanasubiria wakati mwingine.
But human being anataka kuonyesha Ile kitu inaitwa sense of mattering, grandiosity,sense of adequacy analazimisha vitu vitokee due to our ego.
sense of worth, our sense of adequacy, our sense
of importance, our sense mattering, we love to be macho.
Tunataka kufanya vitu vitokee ili tutoke mbele ya dunia tujipige kifua tuseme kuwa sie ndio tumefanya haya angalia nilivyo mwerevu ili kutafuta external validation.
Pia we don't accept that nothing is certainty. Everything comes with some degree of certainty with probability ranging from greater than zero and less than one. Kwa namna nyingine Ina range from 0. 00000000000000000000000001% to 99.999999999999999999999999%. Nothing is sure in this world. Anything has got some probability or percentage of to be true or false nothing is false and true but to some degree.
We love yes or no but between is the biological threat to our to survive or psychology discomfort.
Human beings love to be right hate to be wrong. And our brains hate uncertainties since its implications is the same like biological threat.
We hate uncertainties we love to know the future while God don't love us to know our future. Hapa ndio waganga wetu wapiga ramli ndipo wanapopigia hela na wachungaji wanaoishi kwenye nyumba ya zaidi 50M na huku muumini wake anaishi kwenye nyumba ya makuti anashindwa kuhawana naye alichojaliwa na Muumbaji.
 
What we don't know us as human beings we're incapable of controlling outcome,but only process.
We try to force things to happen Ila Mara nyingi havitokii. Kumbuka hata demu ukitongoza halafu ukimuacha anakuja mwenyewe.
When it's your set ups,your right time,your patience is being rewarded. Hauoni hata predator anakaa anasubiria like mamba,tiger,American cougar aka puma. When a deer is set up Ana pull the trigger na sio lazima apate,akikosa hawajutii wanasubiria wakati mwingine.
But human being anataka kuonyesha Ile kitu inaitwa sense of mattering, grandiosity,sense of adequacy analazimisha vitu vitokee due to our ego.
sense of worth, our sense of adequacy, our sense
of importance, our sense mattering, we love to be macho.
Tunataka kufanya vitu vitokee ili tutoke mbele ya dunia tujipige kifua tuseme kuwa sie ndio tumefanya haya angalia nilivyo mwerevu ili kutafuta external validation.
Pia we don't accept that nothing is certainty. Everything comes with some degree of certainty with probability ranging from greater than zero and less than one. Kwa namna nyingine Ina range from 0. 00000000000000000000000001% to 99.999999999999999999999999%. Nothing is sure in this world. Anything has got some probability or percentage of to be true or false nothing is false and true but to some degree.
We love yes or no but between is the biological threat to our to survive or psychology discomfort.
Human beings love to be right hate to be wrong. And our brains hate uncertainties since its implications is the same like biological threat.
We hate uncertainties we love to know the future while God don't love us to know our future. Hapa ndio waganga wetu wapiga ramli ndipo wanapopigia hela na wachungaji wanaoishi kwenye nyumba ya zaidi 50M na huku muumini wake anaishi kwenye nyumba ya makuti anashindwa kuhawana naye alichojaliwa na Muumbaji.
Umemaliza Kila kitu.
 
Mungu ndio anatoa rizki kwa kila mmoja fanya unachoweza mengine tumuachie Mungu. Mimi nimeshafanya kazi ofisi zina maboss vilaza lakini still ni maboss na wanaongoza institution na zinaenda hazifeli.
Akili inayokuza taasisi ni akili ya biashara sio ile ya IAS, CPA sijui. Hizo ni ziada tu kupunguza idadi ya wanaoomba kutumikia taasisi na watendaji.
 
Kujiamini kwenye 'interview' pamoja na 'body language' ndio imempa kazi
 
Back
Top Bottom