Jamani hawa watoto wananiona mimi kama kikatuni fulani

Jamani hawa watoto wananiona mimi kama kikatuni fulani

Duu!! Hata mimi nikafikiri nimepatwa na Deja vu, kumbe ishaletwaga maana na hisi kama habari hii nshaiona mahali .

Jamaa anasema hii imetokea juzi juzi eti

Lakini ni hii hii bahati mbaya kafunga profile yake ningeenda kumletea uzi wake
 
Jamaa anasema hii imetokea juzi juzi eti

Lakini ni hii hii bahati mbaya kafunga profile yake ningeenda kumletea uzi wake
Umenifanya niangalie profile yake ni kweli aliuleta ila upo tofauti kidogo ingawa unaelezea hayo hayo kupendwa na watoto.

Duuh mkuu una kumbu kumbu thread ya jan 25 unaikumbuka hadi leo?
 
Ubaguzi ni kitu kibaya sana,
Ubaguzi wa aina yoyote ile siyo mzuri: Iko hivi, majuzi nimeenda kwenye Super Market kununua baadhi ya mahitaji sasa wing niliyokuwepo mimi nikakutana na familia fulani hivi ya Waarabu wanananua vitu vyao, hivyo wala hatukusalimiana kwasababu hatufahamiani.

Sasa muda wa kulipa umefika tukakutana nao tena, wenyewe wakiwa wamebeba katoto kadogo kakike kama kama miezi 8 hivi. Nikaweka baada ya vitu vyangu pale nikawa nasubiri nifanyiwe mahesabu niondoke zangu. Katika kupepese macho huku na kule nikakuta kale katoto kananingalia sana usoni, mimi nikatabasamu tu wacha kaanze kucheka kwa nguvu.

Wale waarabu wakaanza kushangaa nao, wakawa wanatania kwamba wewe unamfahamu huyu. wakaamua kukaweka chini. Kakawa kanapiga miguu kama kanataka kuruka huku kananinyooshea mikono nikabebe.

Nikakabeba tu, kakafurahi kweli hako, sasa ile naanza kukaepeleka kwa baba yake hicho kilio chake kalichokishusha ova mtu mzima. Nikabaki tu nacheka maana wiki lilipita nimekutana na matatu kama haya na vitoto vidogo.
We ni le mutuz ?
 
Umenifanya niangalie profile yake ni kweli aliuleta ila upo tofauti kidogo ingawa unaelezea hayo hayo kupendwa na watoto.

Duuh mkuu una kumbu kumbu thread ya jan 25 unaikumbuka hadi leo?
Why go through all that trouble aisee ???
Tatizo ni lipi hapa, mimi kusema nachekwa na vitoto au kuanzisha uzi wa pili ???
Kaaaazi kwelikweli.......................
 
Umenifanya niangalie profile yake ni kweli aliuleta ila upo tofauti kidogo ingawa unaelezea hayo hayo kupendwa na watoto.

Duuh mkuu una kumbu kumbu thread ya jan 25 unaikumbuka hadi leo?

Hata uzi wa mwaka 2013 naukumbuka kama niliusoma

Ile nikipitia tu content ndani nakumbuka otherwise niwe sikuusoma nafikiri kila mmoja anaweza kukumbuka au sio
 
Nakuheshimu sana mkuu

Narudia tena nakuheshimu sana

Nisamehe kama nimevuka mipaka

Nilihisi ni mjadala wa kawaida tu

Hahahhaa,
Mkuu Jimmy bwana,
Sasa unaomba msamaha wakati hujanikosea ???
Mimi niko amani zote, yale maneno nilikuwa nayasema tu mzee!
Tuko pamoja na mimi ninakuheshimu sana mkuu, narudia tena nakuheshimu sana!
 
Mkuu ushawahi kuliliwa na mtoto mpaka baba yake anaona wivu anadhani mkewe alichepuka ukizingatia mtoto anafanana na mother ake 🙂🙂🙂
 
Mbona hakuna ubaguzi hapo wewe umeichukulia ndivyo sivyo kama angelia baada ya kukuona na kujificha hapo sawa lakini kukulilia na wazazi wake kukubali umbebe mtoto wao na bado akawa hataki kurudi kwa wazazi wake basi hiyo ni baraka kubwa sana mshukuru Mola wako kwa hilo pia endelea kuwapenda watoto.
 
Kupendwa na watoto ni jambo jema sana. Huwa ni malaika wanaona mioyo. Ni bahati hiyo. Nami huwa ninapendwa mno na watoto hata niwe mkali lakini wapi. Hata nikiwa hospital tu watoto watanifuata in a way nacheka tu.
 
Back
Top Bottom