Jambo ambalo lilikushangaza na hutolisahau baada ya kujiunga na elimu ya sekondari form 1


Du nimeipenda hiyo familia nzima inampeleka New comer
sasa sijui ni yupi mmiliki wa huo msanduku?
 
mi kuna siku mwalimu wa math alitufundisha asubuhi kusolve swali fln la linear programing.......akasema jioni atakuja kutuuliza kama tunakumbuka au lah......sasa nikashinda siku nzima na meza ile calculation....mpka nikajiamini kabisa kwamba "sasa kitu kimekaa""

Sasa mwalimu alipokuja tu darasani akaniita "" we hapo konani njoo utukumbushe hesabu ya asubuhi""

Nikajisemea kimoyomoyo ""Leo mbuzi kaja kufia kwangu mimi muuza supu,, lazma ntang'oa hata demu leo kwa jinsi ntakavoshusha mambo pale ubaoni"".

Basi bhana nikajichomoa taratibu huku natembea mwendo ule wa wataalam wa math kama mnaufaham.......

Basi kufika pale ubaoni mwalimu kwanza akaanza nisifia jinsi nnavojiamini na watu wakapiga na makofi kabisa nkaona "" mambo si hayo sasa"......Basi mwalimu akaandika swali pale kama la asubuh tu lkn cha ajabu alibadilisha zile data zoote na kakiingereza ka ajabu ajabu akakaongeza pale na kunikabidhi chaki pale.

Hahahaaaaa sitaki kukumbuka nilivoaibika siku ile jamani[emoji23][emoji23]
Nilijikanyaga pale mikononi jasho jingi kila pozi linagoma.....dooooohh

Akaona sio mbaya akinitembezea mboko nne za nguvu za kumpotezea mda wake
 
Heee namuonaga dogo ana mavitabu makubwa sijui abort,nelkon,Lambert, university physics, BS, huku mimi kaka yake nina kibanga kampiga mkoloni,juma na uledi,[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
ulivota taja tu hvo vitabu inaonesha wazi unamchora mwenzio[emoji849]
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] nimecheka sana...umefanya nimekumbuka hesabu za log na kusoma fofiga,zilinitesa hizi hesabu jaman duh
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] nimecheka sana...umefanya nimekumbuka hesabu za log na kusoma fofiga,zilinitesa hizi hesabu jaman duh
aaah waalimu wa math siku zote wanafanana tabia dunia nzima..........wanapenda sana tunavoumbuka ubaoni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…