Uchaguzi 2020 James Mbatia: Chama chetu cha NCCR Mageuzi kinakwenda kuwa chama kikuu cha upinzani nchini

Lord Diplock MR

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2015
Posts
1,393
Reaction score
3,237
Mwenyekiti wa chama cha NCCR Mageuzi Mheshimiwa Sana James Mbatia amesema chama chake kinakwenda kuchukua nafasi yake na kuwa chama kikuu cha upinzani nchini. Mbatia amesema baada ya uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi nchini Tanzania mwaka 1995 NCCR Mageuzi kilikuwa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania.

Mbatia amesema kuwa chama chake kimefanya utafiti na kugundua sababu zilizokifanya chama chake kuwa na wabunge wachache.

Chama cha NCCR- Mageuzi kinaelekea kurudi kwenye nafasi yake ya kuwa chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania, kama ilivyokuwa baada ya uchaguzi mkuu wa kwanza ndani ya mfumo vwa vyama vingi uliofanyika mwaka 1995" James Mabatia, Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi Taifa

 
MWEMBESI ONE,

Huyu Mbatia wamecheza dili na CCM anapewa wabunge kati ya kumi au 20 alafu wanakuwa wachama chake wanaiuwa chadema.

NCCR Mageuzi wakiwa wana wabunge itaonesha kuwa uchaguzi ulikuwa bomba huru na wa haki ili wahisani wasitunyime misaada.

Wakibaki peke yao tutapigwa dola ndio maana NCCR Mageuzi kwa sasa ni CCM B

Sent using Jamii Forums mobile app
 
October wataijua vizuri CCM.

Bunge lijalo kutakuwa na wabunge watatu tu wa upinzani Mrema, Shibuda na Cheyo!
 
Tutakao katwa CCM tutapelekwa NCCR kujaribu bahati zetu kutokea huko.. Huenda!
 
Ana mtaji wa chama tawala. Anamegewa punje ndogo kulingana na thamani ya utu wake.
 
Wamefanyia kazi mapungufu ya Chadema
Wao hawatukani, hawatumiki na Mabeberu ni Wazalendo nk
 
Ameshahakikishiwa mbeleko na meko ndo mana anajiamini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…