Uchaguzi 2020 James Mbatia: Chama chetu cha NCCR Mageuzi kinakwenda kuwa chama kikuu cha upinzani nchini

Ukimuukiza leo atakuambia alinukuliwa vibaya..
 
C.kimei vunju,nccr mageuzi kwesha habari yake
Ungajuhudi
 
Hata ubunge hapati vunjo CCM wamemuweka kimei hachomoi, mzikeni akaendeleze tabia za kishoga
 
Mbatia alibaki yeye tu kama m/kiti na mbunge pekee wa NCCR mageuzi, aliposoma alama za nyakati kuhusu uchaguzi ujao aliamua kuunga mkono juhudi kupitia mlango wa nyuma ili kukwepa wajumbe. Lakini amesahau kilichotokea kwa Lipumba wakati yeye Mbatia akiwa ndani ya ukawa.

Katika kila jambo ikiwemo siasa kuna kupanda na kushuka.
Kwa mfano Uingereza chama kilichokuwa kinapinga/kuchelewesha kujitoa katika umoja wa ulaya kilipoteza viti vingi nakupelekea chama kingine kupata ushindi na kuharakisha kujitoa katika baadhi ya mambo waliyoona hayana faida kwao.

Kule nchini Uholanzi chama kikuu cha upinzani katika uchaguzi ulio pita kilibaki na wabunge 9 kutoka 36 na kuamua kuungana na chama kingine ili kujenga upya nguvu na mikakati yakurudi ulingoni.

Ni kweli NCCR kilikuwa chama kikubwa cha upinzani na kikashuka. Lakini mbatia kwa kukubali kucheza ngoma ya ccm hasitegemee kukirudisha chama cha NCCR kuwa chama kikuu cha upinzani.

Ngoma ya ccm ni ngoma ya kichawi, hujui wanakuchezesha ngoma kusherehekea kafara waliyotoa ama wanakuchezesha ngoma ili wewe ndio uwe kafara.
 
James Mbatia, hiyo ni ndoto ya mchana.
 
Mpeni pole.
 
Kwahiyo mgombea wenu wa urais hawezi kushinda mnagombea kwa nin Sasa vyama vingine bwana utafikir akili zao ziko tumboni
 
Mwenyekiti wa NCCR mageuzi alitamka wazi na haikuwa siri katika moja ya vikao kwa wale ambao tulimsikiliza kwa umakini sana, alisema NCCR mageuzi imejipanga kuwa chama kikuu cha upinzani na kina baraka zote. Waliwavuna wanachama wengi na waliokuwa wabunge wa Upinzani kujiunga nao.

Niwaulizeni tu ndugu zangu hivi mikutano yao inadhihirisha hivyo na kuna dalili zozote za wao kuwa chama kikuu cha upinzani Tanzania.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…