Jamhuri ya Kiislam ya Iran

Jamhuri ya Kiislam ya Iran

Hivi kiongozi, Nina swali ....

Mtume Mohammad alikuwa thehebu gani ndani ya uislamu...?
Mtume hakuwa nadhehebu sababu zama zake kulikuwa hakuna haja jambo hilo kwani ilikuwa jambo likiwatatiza maswahaba wanapata majibu moja kwa moja kutoka kwake.

Ulitakiwa kabla ya kuniuliza swali hilo ujiulize ni ipi historia ya kutokea kwa haya madhehebu. Halafu ukisema madhehebu haya ni ike namna ya ufahamu wa wanazuoni katika kuzielewa nususi za Qur'an na Sunna ili kupata hukumu ya jambo fulani.

Madhehebu hayahusiani na itikadi,maimamu wa madhehebu zote nne za kifiqihi katika uislamu walikuwa wana itikadi moja bali walitofautiana katika mambo hukumu za kiislamu,zikiwemo miamalati,ibada na mfano wa hayo.

Kwa maana nyingine madhehebu sio mapote na madhehebu hayajishughulishi na itikadi.

Shia ni pote ambalo linaingia katika sifa ya dini. Ukiambiwa kundi fulani au pote fulani ujue lina itikadi zake na mienendo yake tofauti na wengine au asili.
 
Write your reply...si utaje hapahapa huo ubaya wa washia?,na huyo mwandishi we fanya kupaste hapa paragraph chache kama amechemka ama anasema kweli tuone,kwanini ufanye siri?
Itikadi yao ya 5

YA NNE:
Kauli yao kuwa Qur-aan imebadilishwa:
Itikadi ya Kishia ni kuwa Qur-aan imebadilishwa, au bora tuseme mafundiho ya madhehebu ya Kishia yanaitakidi kuwa Qur-aan imebadilishwa.
Anasema Ibni Hazm kuwa:
‘Mashia Imamiyah wote wa zamani na wa sasa wanaamini kuwa Qur-aan imebadilishwa na kuongezwa yasiyokuwemo na kupunguzwa ndani yake mengi pamoja na kubadilishwa mengi. ‘
Haya ni maneno ya Ibni Hazm
Anasema Ni’imatullah al-Jazairiy:
‘Habari ni nyingi sana bali ni nyingi kupita kiasi (mutawaatir) zinazotuthibitishia kuwa Qur-aan imebadilishwa maneno yake, mada zake, na irabu yake.’
Al-Anwaar an-Nu’umaniyyah – Juzuu ya 2 ukurasa 357
Kauli hizi zimesemwa na wingi miongoni mwa maulamaa wa Kishia akiwemo Al-Huuru Al-’Aamiliy anayejulikana kuwa ni miongoni mwa maulamaa wakubwa.
Hebu tusikilize maulamaa wa Kishia wanasema nini juu ya Al-Huuru Al-’Aamiliy.
Anasema Al Khunsariy:
‘Al-Huuru Al-’Aamiliy alikuwa katika maulamaa wetu wakubwa sana waliotangulia na waliokuja baadaye na alikuwa bahari ya elimu’.
Ama Annuriy yeye anasema juu yake:
‘Al-Aamiliy alikuwa mfanya tahakiki, mwenye kuielewa vizuri elimu ya hadithi na mcha Mungu sana.’
Sasa hebu tumsikilize Al-Huuru Al-’Aamiliy mwenyewe anasema nini juu ya Qur-aan tukufu. Anasema Al-Huuru Al-’Aamiliy:
‘Juwa kuwa ukweli usio na shaka ndani yake kutokana na habari nyingi sana zilizotufikia ni kuwa hii Qur-aan tuliyonayo mikononi mwetu imebadilishwa kidogo baada ya kufa kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), na wale walioikusanya baada yake wakapunguza mengi kati ya maneno yake na aya zake.’
Maneno kama haya yalitamkwa pia na Al Qumy na Al-Kulayniy na wengi miongoni mwa maulamaa wa Kishia akiwemo Ahmed bin Abi Twaalib Al Tubrusiy.
Anaendelea kusema Al-Aamiliy:
‘Na itikadi hii kuwa Qur-aan imepunguzwa ni katika mambo ya lazima kuamini kila mwenye kufuata madhehebu ya Kishia.’
Yote haya yamo ndani ya kitabu cha ‘Mira-atul Anwar’ ukurasa wa 36, Na maana yake ni kuwa Al-Aamiliy anaitakidi kuwa kila mwenye kufuata madhehebu ya kishia lazima aamini kuwa baada ya kufa kwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), Qur-aan imepunguzwa na kuongezwa yale yasiyokuwemo.
Anasema Yusuf Al Baharani:
‘Kutokana na wingi wa riwaya hizi, inawezekana hata kuzitilia shaka sheria zote za dini kwani habari zote hizi zimepokelewa kupitia njia hiyo hiyo moja, mashekhe na wapokeaji wote ndiyo hao hao. Ikiwa watu hawa wameweza kufanya khiana kubwa, basi vipi watashindwa kuifanya khiyana hii ndogo?’
Unakusudiwa hapa uimamu wa ‘Aliy bin Abi Twaalib (Radhiya Allaahu ‘anhu) kuwa amana hiyo ni kubwa zaidi kupita dini yenyewe.
Durar al Najafiyah – ukurasa 294
Ama Adnan al Baharani yeye anasema :
‘Habari hizi (za kubadilishwa Qur-aan) ni nyingi sana hata haina haja ya kuziandika baada ya kuwa na uhakika kuwa pande zote mbili wamebadilisha kwa kuongeza na kupunguza (anakusudia na wao Mashia pia wamebadilisha), na kwa vile hata Masahaba na Tabiina wanayajuwa hayo vizuri, bali ijmai ya kundi lenye haki linayakubali hayo.’
Anakusudia kuwa Shia ndilo kundi lenye haki na kwamba ni wajibu kwao kuwa na itikadi hiyo.
Shumus ad-Duriyah – 126
Anasema ‘Aliy bin Ahmad al-Kufiy:
‘Maulamaa wote wa riwaya na athar wamekubaliana kuwa Qur-aan hii iliyo mikononi mwa watu si kamili.’
Maneno haya haya yamesemwa na An-Nuur at-Twabrasiy katika kitabu chake maarufu sana kiitwacho ‘Faswlul Khitwaab’ – Ukurasa 27
Anasema An-Nuur at-Twabrasiy katika kitabu chake hicho maarufu kiitwacho ‘Faswlul Khitwaab fiy Tahriyfi Kitaab Rabbil Arbaab:
‘Miongoni mwa dalili kuwa Qur-aan imebadilishwa ni ule ufasaha wake mwingi katika baadhi ya aya na upuuzi ulio ndani ya baadhi ya aya.”
Katika kitabu chake hicho An-Nuur at-Twabrasiy ameziandika sura nyingi sana pamoja na aya anazodai kuwa zimeachwa au kubadilishwa, na hapa nitaandika baadhi chache ya sura na aya hizo:
Nitaanza na Sura maarufu waliyoipa jina la ‘Suratul wilayah’: anasema Attubrusiy kuwa sura hiyo ni kama ifuatavyo:
“ ﻳﺄﻳﻬﺎ ﺍﻟﺬﻳﻦ ﺁﻣﻨﻮﺍ ﺁﻣﻨﻮﺍ ﺑﺎﻟﻨﻮﺭﻳﻦ ﺃﻧﺰﻟﻨﺎﻫﻤﺎ ﻳﺘﻠﻮﺍﻧﻲ ﻋﻠﻴﻜﻢ ﺁﻳﺎﺗﻲ ﻭﻳﺤﺬﺭﺍﻧﻜﻢ ﻋﺬﺍﺏ ﻳﻮﻡ ﻋﻈﻴﻢ ﻧﻮﺭﺍ ﻓﻲ ﺑﻌﻀﻬﻤﺎ ﻣﻦ ﺑﻌﺾ ﻭﺃﻧﺎ ﺍﻟﺴﻤﻴﻊ ﺍﻟﻌﻠﻴﻢ ، ﺇﻥ ﺍﻟﺬﻳﻦ ﻳﻮﻓﻮﻥ ﺑﻌﻬﺪ ﺍﻟﻠﻪ ﻭﺭﺳﻮﻟﻪ ﻓﻲ ﺁﻳﺎﺕ ﻟﻬﻢ ﺟﻨﺎﺕ ﺍﻟﻨﻌﻴﻢ ﻭﺍﻟﺬﻳﻦ ﻛﻔﺮﻭﺍ ﻣﻦ ﺑﻌﺪ ﻣﺎ ﺁﻣﻨﻮﺍ ﺑﻨﻘﻀﻬﻢ ﻣﻴﺜﺎﻗﻬﻢ ﻭﻣﺎ ﻋﺎﻫﺪﻫﻢ ﺍﻟﺮﺳﻮﻝ ﻋﻠﻴﻪ ﻳﻘﺬﻓﻮﻥ ﻓﻲ ﺍﻟﺠﺤﻴﻢ ﻇﻠﻤﻮﺍ ﺃﻧﻔﺴﻬﻢ ﻭﻋﺼﻮﺍ ﻭﺻﻴﺔ ﺍﻟﺮﺳﻮﻝ ﺃﻭﻟﺌﻚ ﻳﺴﻘﻮﻥ ﻣﻦ ﺣﻤﻴﻢ”
’Yaa ayuha lladhiyna amanu aaminu binnurayni anzalnahuma yatluwaani ‘alaykum ayaatiy wa yuhadhiraanikum ‘adhaabi yawmin ‘adhiym nuuran fiy ba’adhihima min baadhin wa anaa ssamiy’ul ‘aliym. Inna lladhiyna yuwafuwna bi’ahdi Llaahi wa rasuwlihi fiy ayatin lahum jannatun na’iym walladhiyna kafaruw mim ba’adi ma aamanuw binaqdhihim miythaqhim wama ‘aahad-hum arrasuwlu ‘alayhi yuqdhafuwna fil jahiym. Dhalamuw anfusahum wa ‘asaw wasiyat rrasuwl ulaaika yusqawna min hamiym.’
Haya yamo ndani ya vitabu vyao mashuhuri kama hicho nilichotangulia kukitaja cha Nuri Al Tubrusi, na pia mwanachuoni wao mwengine aitwae Abi Shahar Ashub na wengi miongoni mwa maulamaa wa Kishia wameandika hayo.
Imepokelewa kuwa ‘Aliy bin ‘Abdillaah alipoisoma aya isemayo:
‘Kuntum khayra ummatin ukhrijat linnas.’ Na maana yake ni: ‘Nyinyi ni umma bora mliodhihirishiwa watu.’
Akasema Ja’afar Asw-Swaadiq: ‘Umma bora wanamuuwa Amiril muuminin na Al-Hasan na Al-Husayn alayhimu ssalaam?’
Na alipoulizwa: ‘Vipi niisome?’
Akajibu:
‘Isome hivi: ‘Kuntum khayra aimmatin’ . Na maana yake: Nyinyi ni maimamu bora.’
Hata suratul Inshiraah wanasema imeteremshwa kama ifutavyo:
‘Alam nashrah laka swadrak – wawadhaana ‘anka wizrak – alladhiy anqadha dhwaharak - warafaana laka dhikrak - bi ‘Aliyyin suhrak.”
Hizi ni baadhi chache sana ya aya na sura wanazoitakidi kuwa zimebadilishwa. Na Nuri Attubrusi huyu katika kitabu chake ameandika faharasi ya Qur-aan yote kuanzia Suratul Baqarah mpaka Suratul Ikhlas huku akizichambua aya anazosema kuwa zimebadilishwa.
Kilichobaki ni kumjuwa: nani huyu Nuri Attubrusiy aliyeandika kitabu akidai kuwa Qur-aan hii tuliyonayo imebadilishwa?
Anasema Abbas Al Qumiy mwandishi wa kitabu kiitwacho: ‘Alkuniya wal laqab:
‘An-Nuur at-Twabrasiyy ndiye Shekhe wa Waislamu – mwenye elimu ya Manabii na Mitume – mwenye kuaminika – aalim aliyekamilika.’
Ama Agha Barzak Al Taharani katika kumsifia An-Nuur at-Twabrasiy anasema:
‘Imamu wa maimamu wa elimu ya hadithi na ni katika maulamaa wakubwa wa kishia katika karne za mwisho na mkuu wa mashekhe wa kiislamu katika karne hii.’
Hivi ndivyo anavyosifiwa huyu aliyeandika kitabu akakiita: ‘Fasli l khitab fiy ithbat taharif kitab rabbi l arbab.
Na maana yake ni:
Kauli ya uamuzi juu ya kubadilishwa kwa kitabu cha Allaah.
 
huruma wapi wewe?
unaonekana mbinafsi.. et "Nimeingia na huruma ya ki elimu"

halafu ulivyokuwa hujuh UMESHINDWA tambua kuwa ndani ya uislamu kuna madhehebu as ukristo ulivyo na madhehebu yake eg.roman Lutheran etc
hao shia wapo ndani ya uislamu.
na itikadi zao zpo different sana na Hawa wa kawaida...ambao ni madhehebu mengine.
na ndiyo sababu kuu ya kuwa against na wenzao..mbona hapa bongo kuna wale wa shia aka wasuni.wao Wana taratibu zao ma ufika mbali ZAIDI hata kuipinga bakwata na Wana umoja wao na Sheria zao..but haijabadilisha wao kuwa waislamu...
kuna propaganda nyingi zinasemwa dhidi ya iran lakini ki uhalisia c za kweli..

ni kama Roman walivyo na itikadi tofauti na walokole na kufikia hatua ya kupingana but haibadilishi maana ya kuwa walkristo...
Nikusahihishe. Sunni au answar sunni historia ina trace back to Yemen. Hivyo sunni ni tofauti na shia. Shia ni kama wale wahindi wa Upanga ambao wamekua wakiadhimisha sherehe za kumtukuza Imam Hussein (A.S). Hivyo shia ni tofauti na sunni. Ila pia sunni wanakua tofauti kwa masuala kadhaa na waislam wengine wanaomfuata Imam Shafi
 
Nikusahihishe. Sunni au answar sunni historia ina trace back to Yemen. Hivyo sunni ni tofauti na shia. Shia ni kama wale wahindi wa Upanga ambao wamekua wakiadhimisha sherehe za kumtukuza Imam Hussein (A.S). Hivyo shia ni tofauti na sunni. Ila pia sunni wanakua tofauti kwa masuala kadhaa na waislam wengine wanaomfuata Imam Shafi
SAHIHI KIONGOZI.
Nililengaaa hivyo bt nikawa nashindwa ng'amua majinaa
 
Naipenda JAMHURI YA KIISLAMU YA WATU WA IRANI sababu msimamo wao wa kutoteteleka na U.S na anasonga mbele maisha yanaenda.
You Tube,Facebook, Instagram, WhatsApp, YouTube nakadhalika kule hakuna.
NAIPENDA NA NIMEIPENDA NA NITAIPENDA JAMHURI YA KIISLAMU YA WATU WA IRANI.Na sisi Muslims wote tuwaige wairani kwa umoja wao bila kutengana.
Bahati mbaya wewe kapuku usiyejua lolote ndio unayeinga mkono ila wenzio watawala mashariki ya kati hawaungi mkono
 
Saudi Arabia ndio kijana wa Sunni na Iran ndiye kinara na promoter wa Shia duniani. Iran inatumia pesa nyingi sana kuhakikisha ushia unaenea duniani na hasa kuwabadili wasunni kuwa washia imefikia hatua kwa ufadhili wa Iran misikiti ya mashia inajengwa na kunakuwa na mgao wa pesa kwa watu wote wanaosali hapo kila baada ya swala ya ijumaa. Jambo hili linaukosesha usingizi wasunni na hasa Saudi Arabia ambaye ni mnufaika mkuu( kiuchumi) wa uislamu kupitia utalii, hija, umrah nk. Kwaiyo ni vita ya kiuchumi iliyobeba taswira ya vita ya kidwini.
Hata sasa Saudia anatamani Israel/usa waivamie Iran na kuiteketeza kabisa.
 
Mtume hakuwa nadhehebu sababu zama zake kulikuwa hakuna haja jambo hilo kwani ilikuwa jambo likiwatatiza maswahaba wanapata majibu moja kwa moja kutoka kwake.

Ulitakiwa kabla ya kuniuliza swali hilo ujiulize ni ipi historia ya kutokea kwa haya madhehebu. Halafu ukisema madhehebu haya ni ike namna ya ufahamu wa wanazuoni katika kuzielewa nususi za Qur'an na Sunna ili kupata hukumu ya jambo fulani.

Madhehebu hayahusiani na itikadi,maimamu wa madhehebu zote nne za kifiqihi katika uislamu walikuwa wana itikadi moja bali walitofautiana katika mambo hukumu za kiislamu,zikiwemo miamalati,ibada na mfano wa hayo.

Kwa maana nyingine madhehebu sio mapote na madhehebu hayajishughulishi na itikadi.

Shia ni pote ambalo linaingia katika sifa ya dini. Ukiambiwa kundi fulani au pote fulani ujue lina itikadi zake na mienendo yake tofauti na wengine au asili.
Kwa hiyo Shia wana Msahafu wao tofauti na Sunn?
Tofauti iko wapi?
 
Write your reply...hivi kwani tunafuata maulamaa au tunafuata quran?,kwamfano mimi sijui hata ulamaa mmoja sasa ukileta habari kuwa shia ni makafiri kwakuwa ulamaa fulani kasema hivi ntakushangaa tu,maana mimi hakuna ulamaa naemjua na hawana maana yeyote kati yao na mahusiano baina yangu mimi na Mungu
 
Write your reply...hivi kwani tunafuata maulamaa au tunafuata quran?,kwamfano mimi sijui hata ulamaa mmoja sasa ukileta habari kuwa shia ni makafiri kwakuwa ulamaa fulani kasema hivi ntakushangaa tu,maana mimi hakuna ulamaa naemjua na hawana maana yeyote kati yao na mahusiano baina yangu mimi na Mungu
Unapoelezea kitu jaribu kutoa dalili ya unachokisema sio unabisha bila sababu na jaribu kujifunza usifunge fahamu ya ubongo wako kisa tu unaweza kubishana
 
Mtume ni muhasisi wa WASHIA dogo. Ndo maana familia yake ilifanyiwa unyama na wachache kwa manufaa yao.
Wataje walio ifanyia unyama familia ya mtume kama si wajiitao mashia wa Ali ?

Na ni wapi mtume ameasisi USHIA ?

Kwanza unamjua Ibn Sabai Myahudi ?

Bro kama umekaririshwa kuhusu USHIA sio mimi.

Nasubiri majibu ya maswali yangu.
 
Wataje walio ifanyia unyama familia ya mtume kama si wajiitao mashia wa Ali ?

Na ni wapi mtume ameasisi USHIA ?

Kwanza unamjua Ibn Sabai Myahudi ?

Bro kama umekaririshwa kuhusu USHIA sio mimi.

Nasubiri majibu ya maswali yangu.
Shekh wangu akikujibu nitag maana hawa hawaja kaa wakafatilia mambo ila wanackia ckia tu
 
Write your reply...hivi kwani tunafuata maulamaa au tunafuata quran?,kwamfano mimi sijui hata ulamaa mmoja sasa ukileta habari kuwa shia ni makafiri kwakuwa ulamaa fulani kasema hivi ntakushangaa tu,maana mimi hakuna ulamaa naemjua na hawana maana yeyote kati yao na mahusiano baina yangu mimi na Mungu
Hii hapa dalili ya kuwa sikiliza na kuwaheshimu maulamab

KWA NINI YATUPASA KUWAHESHIMU MAULAMAA WETU?.
Kutoka kwa Abu Muhamad 'as' amesema, amesema Imamu Ally Bin Muhamad 'as':
ﻋَﻦْ ﺃَﺑِﯽ ﻣُﺤَﻤَّﺪٍ ﻋﻠﯿﻪ ﺍﻟﺴﻼﻡ ﻗَﺎﻝَ ﻗَﺎﻝَ ﻋَﻠِﯽُّ ﺑْﻦُ ﻣُﺤَﻤَّﺪٍ ﻋﻠﯿﻬﻤﺎ ﺍﻟﺴﻼﻡ ﻟَﻮْ ﻟَﺎ ﻣَﻦْ ﯾَﺒْﻘَﯽ ﺑَﻌْﺪَ ﻏَﯿْﺒَﺔِ ﻗَﺎﺋِﻤِﻨَﺎ ﻋﻠﯿﻪ ﺍﻟﺴﻼﻡ ﻣِﻦَ ﺍﻟْﻌُﻠَﻤَﺎﺀِ ﺍﻟﺪَّﺍﻋِﯿﻦَ ﺇِﻟَﯿْﻪِ ﻭَ ﺍﻟﺪَّﺍﻟِّﯿﻦَ ﻋَﻠَﯿْﻪِ ﻭَ ﺍﻟﺬَّﺍﺑِّﯿﻦَ ﻋَﻦْ ﺩِﯾﻨِﻪِ ﺑِﺤُﺠَﺞِ ﺍﻟﻠَّﻪِ ﻭَ ﺍﻟْﻤُﻨْﻘِﺬِﯾﻦَ ﻟِﻀُﻌَﻔَﺎﺀِ ﻋِﺒَﺎﺩِ ﺍﻟﻠَّﻪِ ﻣِﻦْ ﺷِﺒَﺎﮎِ ﺇِﺑْﻠِﯿﺲَ ﻭَ ﻣَﺮَﺩَﺗِﻪِ ﻭَ ﻣِﻦْ ﻓِﺨَﺎﺥِ ﺍﻟﻨَّﻮَﺍﺻِﺐِ ﻟَﻤَﺎ ﺑَﻘِﯽَ ﺃَﺣَﺪٌ ﺇِﻟَّﺎ ﺍﺭْﺗَﺪَّ ﻋَﻦْ ﺩِﯾﻦِ ﺍﻟﻠَّﻪِ ﻭَ ﻟَﮑِﻨَّﻬُﻢُ ﺍﻟَّﺬِﯾﻦَ ﯾُﻤْﺴِﮑُﻮﻥَ ﺃَﺯِﻣَّﺔَ ﻗُﻠُﻮﺏِ ﺿُﻌَﻔَﺎﺀِ ﺍﻟﺸِّﯿﻌَﺔِ ﮐَﻤَﺎ ﯾُﻤْﺴِﮏُ ﺻَﺎﺣِﺐُ ﺍﻟﺴَّﻔِﯿﻨَﺔِ ﺳُﮑَّﺎﻧَﻬَﺎ ﺃُﻭﻟَﺌِﮏَ ﻫُﻢُ ﺍﻟْﺄَﻓْﻀَﻠُﻮﻥَ ﻋِﻨْﺪَ ﺍﻟﻠَّﻪِ ﻋَﺰَّ ﻭَ ﺟَﻞَّ .
"Lau kama si kubakia kwa Maulamaa baada ya kughibu kiuongozi wetu, wenye kulingania kwake yeye, na kuwaongoza watu kwake yeye, na kujitolea katika njia yake kwa Hoja (na Dalili) za Allah..
Wenye kuwaokoa waja wa Allah walio dhaifu (kihoja na Maarifa) kutoka katika nyavu sha Ibilisi na watu wake, na (kuwaokoa kutoka katika) Mitego ya Nawaaswib[1], basi asingebaki yeyote ispokuwa angeritadi kutoka katika Dini ya Allah..
Lakini wao ndio ambao hushikilia nyoyo za Wafuasi wetu waliodhaifu, kama vile nahodha anavyoshikilia usalama wa abiria wake katika Safina, wao (Maulamaa) ndio (watu) bora mbele ya Allah".
 
Mtume hakuwa nadhehebu sababu zama zake kulikuwa hakuna haja jambo hilo kwani ilikuwa jambo likiwatatiza maswahaba wanapata majibu moja kwa moja kutoka kwake.

Ulitakiwa kabla ya kuniuliza swali hilo ujiulize ni ipi historia ya kutokea kwa haya madhehebu. Halafu ukisema madhehebu haya ni ike namna ya ufahamu wa wanazuoni katika kuzielewa nususi za Qur'an na Sunna ili kupata hukumu ya jambo fulani.

Madhehebu hayahusiani na itikadi,maimamu wa madhehebu zote nne za kifiqihi katika uislamu walikuwa wana itikadi moja bali walitofautiana katika mambo hukumu za kiislamu,zikiwemo miamalati,ibada na mfano wa hayo.

Kwa maana nyingine madhehebu sio mapote na madhehebu hayajishughulishi na itikadi.

Shia ni pote ambalo linaingia katika sifa ya dini. Ukiambiwa kundi fulani au pote fulani ujue lina itikadi zake na mienendo yake tofauti na wengine au asili.
Sasa kama unajua Mtume hakuwa na dhehebu lolote/ na hakuacha dhehebu la aina yeyote. Umetumia kifungu gani kwa kutaka kuaminisha umma wa JF kuwa Jamhuri ya kiislamu ya Iran sio waislamu...?
 
Write your reply...nachosema nadhani sijaeleweka,mtume kaacha dini inaitwa islam na kitabu kinaitwa quran ambacho waislamu ndo wanakitumia kama kitabu kinachowaongoza,then miaka mingi baadae yakazuka makundi kufuatana na kila kundi limetafsiri na kuelewa vipi maandiko,ndo kisa cha haya madhehebu suni,shia,sufii,etc lakini kila kundi lengo lake ni kumuabudu mungu,kisha wanatokea watu hao mnaita ulamaa,wanasema na kuleta mafundisho ambayo hayapo katika quran ama labda wao wametafsiri walivyoelewa wao,so hapo tabu iko wapi kama quran ipo maana ubaya wote wa shia mlioutaja ni tofauti baina yenu mlivyoelewa maandiko
 
Write your reply...hivi kwani tunafuata maulamaa au tunafuata quran?,kwamfano mimi sijui hata ulamaa mmoja sasa ukileta habari kuwa shia ni makafiri kwakuwa ulamaa fulani kasema hivi ntakushangaa tu,maana mimi hakuna ulamaa naemjua na hawana maana yeyote kati yao na mahusiano baina yangu mimi na Mungu
Jibu jingne hili apa kwa dalili

984. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w., amesema Waqayi-ul-Ayyam, Uk. 439:
“Kutakuja zama miongoni mwa watu kuwa:
1. Wao hawatawaheshimu Wanazuoni wao (yaani Maulamaa) ila kwa mavazi yao mazuri;
2. wao hawatasikiliza Qur'an Tukufu ila kwa sauti ya kuvutia;
3. Na wao hawatamwabudu Allah swt isipokuwa katika mwezi wa Ramadhani tu;
4. wanawake wao hawatakuwa na aibu,
5. maskini miongoni mwao hawatakuwa na subira,
6. na matajiri wao hawatakuwa wakarimu, kwani wao hawataridhirika kwa kidogo na wala hawatakinai kwa wingi.
7. Wao hawatashiba kwa kingi, wao watafanya kila jitihada kwa ajili ya matumbo yao;
8. dini yao itakuwa ni mapesa (mali na utajiri);
9. na wake zao ndio watakuwa Qiblah zao (tunapoelekea kusali huko Al-Ka’abah tukufu);
10. na majumba yao ndio itakuwa Misikiti yao;
11. wao watakimbia kutoka Maulamaa wao kama vile kondoo anavyo kimbia kutoka kwa mbwa mwitu.
Hapo watapokuwa kama hivyo (basi Allah swt atawatumbukiza katika mambo matatu).
1. Atawaondolea baraka katika mali zao.
2. Watakufa (kutoka humu duniani) wakiwa hawana imani iliyo halisi.”
3. Watatawaliwa na mtawala dhalimu.
985. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. amesema , Bihar al-Anwaar, J. 23, Uk. 22:
“Utafika wakati katika umma wangu kwamba :
1. watawala wao watakuwa wakatili na wadhalimu,
2. Maulamaa na Wanazuoni wao watakuwa waroho wa mali na utajiri na watakuwa na imani kidogo,
3. waumini wao watakuwa ni wanafiki,
4. wafanya biashara wao watakuwa wakijishughulisha kwa kutoa na kupokea riba na kuficha maovu na kasoro ya vitu wanavyonunua na kuuza na
5. wanawake wao watakuwa wamejihusisha mno na mambo ya kujirembesha ya dunia.
6. Hivyo, wakati huo, mwovu kuliko wote miongoni mwao ndio watakaokuwa wakiwaongoza wao, na
7. wema miongoni mwao watakuwa wakiwaita watu lakini hakuna mtu atakaye wajibu.”
986. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w., amesema Al-Ithna-'Asheriyyah, Uk. 202:
“Utafika wakati katika Umma wangu ambapo wao watakuwa wakipenda vitu vitano na kuvisahau vitu vitano:
1. Wao watakuwa wakiipenda dunia na kuipuuzia Akhera.
2. Wao watapenda mali na kusahau hesabu ya siku ya Qiyamah
3. Waume zao watawapenda wanawake waovu na kuwasahau Hur al-‘Ayn
4. Wao watapenda majumba na watayasahau makaburi yao.
5. Wao watajipenda wenyewe kupita kiasi na kumsahau muumba wao.
Kwa hakika watu kama hawa hawanipendi mimi na mimi pia siwapendi wao.”
 
Write your reply...hivi kwani tunafuata maulamaa au tunafuata quran?,kwamfano mimi sijui hata ulamaa mmoja sasa ukileta habari kuwa shia ni makafiri kwakuwa ulamaa fulani kasema hivi ntakushangaa tu,maana mimi hakuna ulamaa naemjua na hawana maana yeyote kati yao na mahusiano baina yangu mimi na Mungu
Na ninaomba kama unawatetea mashia bc watetee kwa dalili bc wote tujue

Kama vile ambvyo cc tunawapinga kwa dalili ikhwa
 
Back
Top Bottom