Mkwawe
JF-Expert Member
- Jun 10, 2016
- 3,132
- 5,508
Ndani ya hii miaka miwili Kuna muingiliano mkubwa sana wa jamii wa watu wa hadza na watu wa ulimwengu wa kwanza kitu ambacho binafsi naona kama kitachangia sana kuharibu mfumo wa mzuri wa kiasili waliouzoea kuishi na kuondoa kabisa ule utambulishi wao kama wahadzabe
Wageni wengi wanaokuja kuwaona na hata wenyeji wanaowaongoza hao wageni kutokea mijini hutambulisha vitu visivyo vya msingi kabisa kama vinywaji vya kusindika vyenye kemikali na mivyakula yenye sumu za viwandani kadhalika na mavazi ambayo hayana tija kwa jamii hiyo. Ninachoona si kwamba jamii hii haijui chochote kuhusu ulimwengu wa kisasa maana wao pia huku manyara huonekana kwenye minada mingi sana wakiuza zana za kuwindia na wao kupata bidhaa zingine, ila ninachoamini ni kuwa waliamua kwa dhati kujitenga na ulimwengu huu wa kisasa ili waishi kwa namna watakavyopendezwa wao
Muingiliano huu wa jamii ya hadza na watu kisasa unahatarisha hata kingamwili zao na harakati zao za kawaida kwa kuwa ni kama wanabugudhiwa na hawa watu wanaowatembelea na kuwapa vitu vigeni bila utaratibu maana hawa jamaa kwa kiasi kikubwa wako huru nje ya magonjwa tunayopambana nayo huku mjini kwa hiyo Wana kingamwili zao binafsi hivyo kuruhusu watu wawatembelee kiholela kunaweza kuhatarisha ustawi wai na mtindo mzima wa maisha yao
Serikali ya Tanzania kupitia wizara ya maliasili na hata wizara ya mambo ya ndani ninaomba waweke marufuku au taratibu Kali au ikiwezekana kutoruhusu kabisa kuwasumbua wahadzabe kwa kuwa hawa jamaa ni moja ya jamii adhimu sana duniani ambazo zineamua kuishi utaratibu wao binafsi
Leo hii Afrika kusini amebakia mtu mmoja tu ambaye anatenda tamaduni za Khoisan naye ni mzee sana kwa kuwa jamii yao hao watu imeshamezwa na usasa. Hakuna faida yoyote wanayopata wahadzabe kwa kuingiliana na watu mjini au wa nje ya nchi zaidi ya hao watu kuwatumia kwa maudhui yao ya mtandaoni na kujitengenezea umaarufu na kipato huku wakiwaharibia mazingira na tamaduni zao
SERIKALI IWAPIGE MARUFUKU WATU WOTE WANAWAKARIBIA WAHADZABE
Wageni wengi wanaokuja kuwaona na hata wenyeji wanaowaongoza hao wageni kutokea mijini hutambulisha vitu visivyo vya msingi kabisa kama vinywaji vya kusindika vyenye kemikali na mivyakula yenye sumu za viwandani kadhalika na mavazi ambayo hayana tija kwa jamii hiyo. Ninachoona si kwamba jamii hii haijui chochote kuhusu ulimwengu wa kisasa maana wao pia huku manyara huonekana kwenye minada mingi sana wakiuza zana za kuwindia na wao kupata bidhaa zingine, ila ninachoamini ni kuwa waliamua kwa dhati kujitenga na ulimwengu huu wa kisasa ili waishi kwa namna watakavyopendezwa wao
Muingiliano huu wa jamii ya hadza na watu kisasa unahatarisha hata kingamwili zao na harakati zao za kawaida kwa kuwa ni kama wanabugudhiwa na hawa watu wanaowatembelea na kuwapa vitu vigeni bila utaratibu maana hawa jamaa kwa kiasi kikubwa wako huru nje ya magonjwa tunayopambana nayo huku mjini kwa hiyo Wana kingamwili zao binafsi hivyo kuruhusu watu wawatembelee kiholela kunaweza kuhatarisha ustawi wai na mtindo mzima wa maisha yao
Serikali ya Tanzania kupitia wizara ya maliasili na hata wizara ya mambo ya ndani ninaomba waweke marufuku au taratibu Kali au ikiwezekana kutoruhusu kabisa kuwasumbua wahadzabe kwa kuwa hawa jamaa ni moja ya jamii adhimu sana duniani ambazo zineamua kuishi utaratibu wao binafsi
Leo hii Afrika kusini amebakia mtu mmoja tu ambaye anatenda tamaduni za Khoisan naye ni mzee sana kwa kuwa jamii yao hao watu imeshamezwa na usasa. Hakuna faida yoyote wanayopata wahadzabe kwa kuingiliana na watu mjini au wa nje ya nchi zaidi ya hao watu kuwatumia kwa maudhui yao ya mtandaoni na kujitengenezea umaarufu na kipato huku wakiwaharibia mazingira na tamaduni zao
SERIKALI IWAPIGE MARUFUKU WATU WOTE WANAWAKARIBIA WAHADZABE