Jamii ya wahadzabe ilindwe, baada ya miaka 8 hawatokuwepo tena

Jamii ya wahadzabe ilindwe, baada ya miaka 8 hawatokuwepo tena

Mkwawe

JF-Expert Member
Joined
Jun 10, 2016
Posts
3,132
Reaction score
5,508
Ndani ya hii miaka miwili Kuna muingiliano mkubwa sana wa jamii wa watu wa hadza na watu wa ulimwengu wa kwanza kitu ambacho binafsi naona kama kitachangia sana kuharibu mfumo wa mzuri wa kiasili waliouzoea kuishi na kuondoa kabisa ule utambulishi wao kama wahadzabe

Wageni wengi wanaokuja kuwaona na hata wenyeji wanaowaongoza hao wageni kutokea mijini hutambulisha vitu visivyo vya msingi kabisa kama vinywaji vya kusindika vyenye kemikali na mivyakula yenye sumu za viwandani kadhalika na mavazi ambayo hayana tija kwa jamii hiyo. Ninachoona si kwamba jamii hii haijui chochote kuhusu ulimwengu wa kisasa maana wao pia huku manyara huonekana kwenye minada mingi sana wakiuza zana za kuwindia na wao kupata bidhaa zingine, ila ninachoamini ni kuwa waliamua kwa dhati kujitenga na ulimwengu huu wa kisasa ili waishi kwa namna watakavyopendezwa wao

Muingiliano huu wa jamii ya hadza na watu kisasa unahatarisha hata kingamwili zao na harakati zao za kawaida kwa kuwa ni kama wanabugudhiwa na hawa watu wanaowatembelea na kuwapa vitu vigeni bila utaratibu maana hawa jamaa kwa kiasi kikubwa wako huru nje ya magonjwa tunayopambana nayo huku mjini kwa hiyo Wana kingamwili zao binafsi hivyo kuruhusu watu wawatembelee kiholela kunaweza kuhatarisha ustawi wai na mtindo mzima wa maisha yao

Serikali ya Tanzania kupitia wizara ya maliasili na hata wizara ya mambo ya ndani ninaomba waweke marufuku au taratibu Kali au ikiwezekana kutoruhusu kabisa kuwasumbua wahadzabe kwa kuwa hawa jamaa ni moja ya jamii adhimu sana duniani ambazo zineamua kuishi utaratibu wao binafsi

Leo hii Afrika kusini amebakia mtu mmoja tu ambaye anatenda tamaduni za Khoisan naye ni mzee sana kwa kuwa jamii yao hao watu imeshamezwa na usasa. Hakuna faida yoyote wanayopata wahadzabe kwa kuingiliana na watu mjini au wa nje ya nchi zaidi ya hao watu kuwatumia kwa maudhui yao ya mtandaoni na kujitengenezea umaarufu na kipato huku wakiwaharibia mazingira na tamaduni zao

SERIKALI IWAPIGE MARUFUKU WATU WOTE WANAWAKARIBIA WAHADZABE
 
Ndani ya hii miaka miwili Kuna muingiliano mkubwa sana wa jamii wa watu wa hadza na watu wa ulimwengu wa kwanza kitu ambacho binafsi naona kama kitachangia sana kuharibu mfumo wa mzuri wa kiasili waliouzoea kuishi na kuondoa kabisa ule utambulishi wao kama wahadzabe

Wageni wengi wanaokuja kuwaona na hata wenyeji wanaowaongoza hao wageni kutokea mijini hutambulisha vitu visivyo vya msingi kabisa kama vinywaji vya kusindika vyenye kemikali na mivyakula yenye sumu za viwandani kadhalika na mavazi ambayo hayana tija kwa jamii hiyo. Ninachoona si kwamba jamii hii haijui chochote kuhusu ulimwengu wa kisasa maana wao pia huku manyara huonekana kwenye minada mingi sana wakiuza zana za kuwindia na wao kupata bidhaa zingine, ila ninachoamini ni kuwa waliamua kwa dhati kujitenga na ulimwengu huu wa kisasa ili waishi kwa namna watakavyopendezwa wao

Muingiliano huu wa jamii ya hadza na watu kisasa unahatarisha hata kingamwili zao na harakati zao za kawaida kwa kuwa ni kama wanabugudhiwa na hawa watu wanaowatembelea na kuwapa vitu vigeni bila utaratibu maana hawa jamaa kwa kiasi kikubwa wako huru nje ya magonjwa tunayopambana nayo huku mjini kwa hiyo Wana kingamwili zao binafsi hivyo kuruhusu watu wawatembelee kiholela kunaweza kuhatarisha ustawi wai na mtindo mzima wa maisha yao

Serikali ya Tanzania kupitia wizara ya maliasili na hata wizara ya mambo ya ndani ninaomba waweke marufuku au taratibu Kali au ikiwezekana kutoruhusu kabisa kuwasumbua wahadzabe kwa kuwa hawa jamaa ni moja ya jamii adhimu sana duniani ambazo zineamua kuishi utaratibu wao binafsi

Leo hii Afrika kusini amebakia mtu mmoja tu ambaye anatenda tamaduni za Khoisan naye ni mzee sana kwa kuwa jamii yao hao watu imeshamezwa na usasa. Hakuna faida yoyote wanayopata wahadzabe kwa kuingiliana na watu mjini au wa nje ya nchi zaidi ya hao watu kuwatumia kwa maudhui yao ya mtandaoni na kujitengenezea umaarufu na kipato huku wakiwaharibia mazingira na tamaduni zao

SERIKALI IWAPIGE MARUFUKU WATU WOTE WANAWAKARIBIA WAHADZABE
true
 
Ndani ya hii miaka miwili Kuna muingiliano mkubwa sana wa jamii wa watu wa hadza na watu wa ulimwengu wa kwanza kitu ambacho binafsi naona kama kitachangia sana kuharibu mfumo wa mzuri wa kiasili waliouzoea kuishi na kuondoa kabisa ule utambulishi wao kama wahadzabe

Wageni wengi wanaokuja kuwaona na hata wenyeji wanaowaongoza hao wageni kutokea mijini hutambulisha vitu visivyo vya msingi kabisa kama vinywaji vya kusindika vyenye kemikali na mivyakula yenye sumu za viwandani kadhalika na mavazi ambayo hayana tija kwa jamii hiyo. Ninachoona si kwamba jamii hii haijui chochote kuhusu ulimwengu wa kisasa maana wao pia huku manyara huonekana kwenye minada mingi sana wakiuza zana za kuwindia na wao kupata bidhaa zingine, ila ninachoamini ni kuwa waliamua kwa dhati kujitenga na ulimwengu huu wa kisasa ili waishi kwa namna watakavyopendezwa wao

Muingiliano huu wa jamii ya hadza na watu kisasa unahatarisha hata kingamwili zao na harakati zao za kawaida kwa kuwa ni kama wanabugudhiwa na hawa watu wanaowatembelea na kuwapa vitu vigeni bila utaratibu maana hawa jamaa kwa kiasi kikubwa wako huru nje ya magonjwa tunayopambana nayo huku mjini kwa hiyo Wana kingamwili zao binafsi hivyo kuruhusu watu wawatembelee kiholela kunaweza kuhatarisha ustawi wai na mtindo mzima wa maisha yao

Serikali ya Tanzania kupitia wizara ya maliasili na hata wizara ya mambo ya ndani ninaomba waweke marufuku au taratibu Kali au ikiwezekana kutoruhusu kabisa kuwasumbua wahadzabe kwa kuwa hawa jamaa ni moja ya jamii adhimu sana duniani ambazo zineamua kuishi utaratibu wao binafsi

Leo hii Afrika kusini amebakia mtu mmoja tu ambaye anatenda tamaduni za Khoisan naye ni mzee sana kwa kuwa jamii yao hao watu imeshamezwa na usasa. Hakuna faida yoyote wanayopata wahadzabe kwa kuingiliana na watu mjini au wa nje ya nchi zaidi ya hao watu kuwatumia kwa maudhui yao ya mtandaoni na kujitengenezea umaarufu na kipato huku wakiwaharibia mazingira na tamaduni zao

SERIKALI IWAPIGE MARUFUKU WATU WOTE WANAWAKARIBIA WAHADZABE
Mfumo upi mzuri wa asili??
 
Huwezi kushindana na usasa, hata wafichwe vipi watakutana tu na usasa......wao sio wanyama!
 
Huu uzi ni wa ajabu na watu waliocomment before this ni watu anbao sijui ni wa kundi gani

Sisi sote tulikuwa uncivilised sasa tuko civilized. Hakuna sifa kuwa au kuishi kama hazabe, watoto hawasomi na wala hawapati mahitaji muhimu za kibinadamu.

Hatuwezi kufagilia au kufurahia wahazabe waishi kama wanyama

Si kweli wana haki ya utandawazi, usasa. Ni haki yao

Dunia ni kijiji sasa, tunajenga madaraja kuunganisha watu, alafu kuna watu wanataka kujenga ukuta kufunga watu


Siafiki
 
Na si kweli kwamba wana kinga ya asili ya magonjwa kifupi magonjwa yanasababishwa na njia nyingi imiwemo wanyama ambao wamewazunguka na hata hali ya hewa..

Hawa wahazabe mbali na kuwa maporoni jamii yao haikui kwa kasi kivile. Ingetakiwa wawe wengi ila bado wamebaki sehemu ndogo ya kijamii

Hazabe wapate huduma za kibinadamu ikiwemo elimu na afya. Kuhusu asili yao wana haki ya kuitunza leo hii makabila mengi yanatambila licha ya civilisation..

I stay to be corrected
 
Dudukwe ana mbwembwe pale anapoonja supu🤣🤣🤣🤣😂😂😂kile kichwa anavyokipeleka upande daah hadi unaona supu zao tamu kuliko zetu
Una mpenda sana dudukwe 😁mimi mwenyewe muhadzabe wa kisukuma
 
Hayo maisha yao ni mazuri kwa upande wao
Hakuna stress kabisa
 
Kwa kuwaangalia tu ni burudani ila mmh maisha halisi hapana kwa kweli wachafuuu. Halafu saiv wasukuma mnakuja juu sana tiktok shida ni video za kuchapana viboko vya makali kwa makosa madogo madogo daah
Una mpenda sana dudukwe 😁mimi mwenyewe muhadzabe wa kisukuma
 
Usihofu mimi ni educated kabsa
Kwa kuwaangalia tu ni burudani ila mmh maisha halisi hapana kwa kweli wachafuuu. Halafu saiv wasukuma mnakuja juu sana tiktok shida ni video za kuchapana viboko vya makali kwa makosa madogo madogo daah
 
Mimi nimekulia usukumani centre tu mjini mjini mwanza, simiyu(bariadi) , geita, dodoma(chamwino) , Kagera(huko) arusha(kaloleni, Sakina) , daslamkwahyo nimemix sehemu nyingi nyingi kidogo
Kwa kuwaangalia tu ni burudani ila mmh maisha halisi hapana kwa kweli wachafuuu. Halafu saiv wasukuma mnakuja juu sana tiktok shida ni video za kuchapana viboko vya makali kwa makosa madogo madogo daah
 
Back
Top Bottom