Jamii ya wahadzabe ilindwe, baada ya miaka 8 hawatokuwepo tena

Jamii ya wahadzabe ilindwe, baada ya miaka 8 hawatokuwepo tena

Ndani ya hii miaka miwili Kuna muingiliano mkubwa sana wa jamii wa watu wa hadza na watu wa ulimwengu wa kwanza kitu ambacho binafsi naona kama kitachangia sana kuharibu mfumo wa mzuri wa kiasili waliouzoea kuishi na kuondoa kabisa ule utambulishi wao kama wahadzabe

Wageni wengi wanaokuja kuwaona na hata wenyeji wanaowaongoza hao wageni kutokea mijini hutambulisha vitu visivyo vya msingi kabisa kama vinywaji vya kusindika vyenye kemikali na mivyakula yenye sumu za viwandani kadhalika na mavazi ambayo hayana tija kwa jamii hiyo. Ninachoona si kwamba jamii hii haijui chochote kuhusu ulimwengu wa kisasa maana wao pia huku manyara huonekana kwenye minada mingi sana wakiuza zana za kuwindia na wao kupata bidhaa zingine, ila ninachoamini ni kuwa waliamua kwa dhati kujitenga na ulimwengu huu wa kisasa ili waishi kwa namna watakavyopendezwa wao

Muingiliano huu wa jamii ya hadza na watu kisasa unahatarisha hata kingamwili zao na harakati zao za kawaida kwa kuwa ni kama wanabugudhiwa na hawa watu wanaowatembelea na kuwapa vitu vigeni bila utaratibu maana hawa jamaa kwa kiasi kikubwa wako huru nje ya magonjwa tunayopambana nayo huku mjini kwa hiyo Wana kingamwili zao binafsi hivyo kuruhusu watu wawatembelee kiholela kunaweza kuhatarisha ustawi wai na mtindo mzima wa maisha yao

Serikali ya Tanzania kupitia wizara ya maliasili na hata wizara ya mambo ya ndani ninaomba waweke marufuku au taratibu Kali au ikiwezekana kutoruhusu kabisa kuwasumbua wahadzabe kwa kuwa hawa jamaa ni moja ya jamii adhimu sana duniani ambazo zineamua kuishi utaratibu wao binafsi

Leo hii Afrika kusini amebakia mtu mmoja tu ambaye anatenda tamaduni za Khoisan naye ni mzee sana kwa kuwa jamii yao hao watu imeshamezwa na usasa. Hakuna faida yoyote wanayopata wahadzabe kwa kuingiliana na watu mjini au wa nje ya nchi zaidi ya hao watu kuwatumia kwa maudhui yao ya mtandaoni na kujitengenezea umaarufu na kipato huku wakiwaharibia mazingira na tamaduni zao

SERIKALI IWAPIGE MARUFUKU WATU WOTE WANAWAKARIBIA WAHADZABE
Unawalinda ili iweje ikiwa wenyewe hawataki kulindwa? Wanataka kuishi maporini na kula vya bure na hawataki kulipia LUKU.
 
Ndani ya hii miaka miwili Kuna muingiliano mkubwa sana wa jamii wa watu wa hadza na watu wa ulimwengu wa kwanza kitu ambacho binafsi naona kama kitachangia sana kuharibu mfumo wa mzuri wa kiasili waliouzoea kuishi na kuondoa kabisa ule utambulishi wao kama wahadzabe

Wageni wengi wanaokuja kuwaona na hata wenyeji wanaowaongoza hao wageni kutokea mijini hutambulisha vitu visivyo vya msingi kabisa kama vinywaji vya kusindika vyenye kemikali na mivyakula yenye sumu za viwandani kadhalika na mavazi ambayo hayana tija kwa jamii hiyo. Ninachoona si kwamba jamii hii haijui chochote kuhusu ulimwengu wa kisasa maana wao pia huku manyara huonekana kwenye minada mingi sana wakiuza zana za kuwindia na wao kupata bidhaa zingine, ila ninachoamini ni kuwa waliamua kwa dhati kujitenga na ulimwengu huu wa kisasa ili waishi kwa namna watakavyopendezwa wao

Muingiliano huu wa jamii ya hadza na watu kisasa unahatarisha hata kingamwili zao na harakati zao za kawaida kwa kuwa ni kama wanabugudhiwa na hawa watu wanaowatembelea na kuwapa vitu vigeni bila utaratibu maana hawa jamaa kwa kiasi kikubwa wako huru nje ya magonjwa tunayopambana nayo huku mjini kwa hiyo Wana kingamwili zao binafsi hivyo kuruhusu watu wawatembelee kiholela kunaweza kuhatarisha ustawi wai na mtindo mzima wa maisha yao

Serikali ya Tanzania kupitia wizara ya maliasili na hata wizara ya mambo ya ndani ninaomba waweke marufuku au taratibu Kali au ikiwezekana kutoruhusu kabisa kuwasumbua wahadzabe kwa kuwa hawa jamaa ni moja ya jamii adhimu sana duniani ambazo zineamua kuishi utaratibu wao binafsi

Leo hii Afrika kusini amebakia mtu mmoja tu ambaye anatenda tamaduni za Khoisan naye ni mzee sana kwa kuwa jamii yao hao watu imeshamezwa na usasa. Hakuna faida yoyote wanayopata wahadzabe kwa kuingiliana na watu mjini au wa nje ya nchi zaidi ya hao watu kuwatumia kwa maudhui yao ya mtandaoni na kujitengenezea umaarufu na kipato huku wakiwaharibia mazingira na tamaduni zao

SERIKALI IWAPIGE MARUFUKU WATU WOTE WANAWAKARIBIA WAHADZABE
Wanyama wanapokuwa wapo hatarini kutoweka, serikali na wanasayansi huwa wanafanya utaratibu wa kuwachukua waliopo na kuwatengenezea (simulate) artificial environment ili wazaliane (rejea vyura vya Kihansi).
Labda wafanye hivyo pia kuokoa jamii ya wahadzabe sambamba na kupunguza mwingiliano na jamii hiyo.
 
Mbona ni mawazo kandamizi sana haya.
Ni sawa na Mwenyekiti yule kukalia chama miaka na mikaka.
Hayafai
Ni sawa na M7 kubakia miaka na mikaka madarakani,Haifai.
 
Hivi hawa jamaa, jamii yao Kuna familia/koo mbalimbali zikijitegemea au ni kundi Moja tu Lina move pamoja?
 
Huu uzi ni wa ajabu na watu waliocomment before this ni watu anbao sijui ni wa kundi gani

Sisi sote tulikuwa uncivilised sasa tuko civilized. Hakuna sifa kuwa au kuishi kama hazabe, watoto hawasomi na wala hawapati mahitaji muhimu za kibinadamu.

Hatuwezi kufagilia au kufurahia wahazabe waishi kama wanyama

Si kweli wana haki ya utandawazi, usasa. Ni haki yao

Dunia ni kijiji sasa, tunajenga madaraja kuunganisha watu, alafu kuna watu wanataka kujenga ukuta kufunga watu


Siafiki
Soma post #4, mimi na wewe tuna fikiri sawasawa
 
Wasipewe Cocacola, kompyuta. Ni sawa na kuwanyima haki ya kuishi
Upuuzi mtupu kwani waliwahi kuja kuwaomba hizo coca-cola na kompyuta zenu?

Au bila hizo wao hawatapata furaha maishani mwao?

Wewe unayekunyw coca-cola na kompyuta mbona unalalamika maisha magumu kila siku?
 
Hoja ya KIPUMBAVU sana. Nenda kasome theory ya evolution by Charles Darwin. Binadamu siyo static kama jiwe bali ana cope ma mazingira na kubadilika.

Hata wewe pimbi tuki trace uzao wako miaka 1000 nyuma utakuta babu zako walikuwa wanaishi kama Wahadzabe. Ila nyakati zikapita kutoka early stone age hadi iron age.

Wahadzabe wako hivyo kwa sababu hawajachanganyikana. Lakini yale siyo maisha mazuri. Kutaka wabakie hivyo hivyo ni sawa na kuwafanya ni wanyama na siyo binadamu
Kudadadeki natamani nikutukane bongesa la mtusiiiii

Wewe huyo Charles Darwin umewahi kumuona?
Amekusaidia kwenye kupunguza ugumu wa maisha?

Pumbavu zako
 
Huwezi kushindana na usasa, hata wafichwe vipi watakutana tu na usasa......wao sio wanyama!
Wasilazimishwe waache waufuate wenyewe huo usasa
Wako huru na maisha yao msiwaingilie
 
Yan watu hamna akili,
Kwa hio wew upo happy binadamu kuishi vile karne ya 21?
Wale inabid wafanyiwe forced civilization kabisa, wapelekewe shule, hospital, wafanyiwe forced education, mpaka waelewe, tunapoteza madaktar wengi kwa kujifanya tunatunza asili za wamasai na wahadzabe
 
Kutaka Wahandzabe waendelee kuishi maisha ya kijima ili kulinda historia yao ni roho mbaya sana
 
acheni ujinga hatuwezi kuwaacha vile yani mtu anang'ata kopo la fanta tusimuelekeze namna ya kuifungua!!!
nao wanastahili kula,kulala pazuri na maisha standard binadamu tumeshatoka huko aisee!.
nao wanastahili elimu, na mambo mengine
 
Huu uzi ni wa ajabu na watu waliocomment before this ni watu anbao sijui ni wa kundi gani

Sisi sote tulikuwa uncivilised sasa tuko civilized. Hakuna sifa kuwa au kuishi kama hazabe, watoto hawasomi na wala hawapati mahitaji muhimu za kibinadamu.

Hatuwezi kufagilia au kufurahia wahazabe waishi kama wanyama

Si kweli wana haki ya utandawazi, usasa. Ni haki yao

Dunia ni kijiji sasa, tunajenga madaraja kuunganisha watu, alafu kuna watu wanataka kujenga ukuta kufunga watu


Siafiki
Wewe una mawazo ya kishamba sana, kuwa civilized ndo nini?
Ndo kuishi katika ubepari? Mfumuko wa gharama za maisha na kupambana na magonjwa ya maabara?
Au kuhangaikia ajira ndo kuwa civilized?

Kuna ulazima gani kuishi katika "kuwa civilized" ikiwa wao wenyewe Wana furaha na maisha yao?
 
Yule mpishi anavyolamba mwiko hapana kwakweli, halafu wanapika utumbo wa Nyani ptyuuu .!!
 
Hayo maisha yao ni mazuri kwa upande wao
Hakuna stress kabisa
Hiki ndicho tunachokupigania
Waachwe, maana hata sisi tunaojiona tumestaatabika maisha yetu hayana nafuu yoyote zaidi ya Sonona na kuwafanyia kazi mabepari
 
kuna jamaa nilisoma nae ni muhazabe aisee jamaa nywele za kichwani zilikua hazioti kabisaa anakwambia anaweza kunyoa mara mbili tuh kwa mwaka
 
Back
Top Bottom