Jamiiforums GYM (mazoezi ) thread

Jamiiforums GYM (mazoezi ) thread

Mazoezi ni mazuri na ni kitu cha muhimu sana kwenye mwili wa binadamu kama ukiweza kuyazingatia.

Napenda kukimbia lakini napata shida kwenye magoti nikikimbia wiki mbili tu nahisi kama kuna vidonda,nimeanza dozi ya kila siku asubuhi na jioni nakula bamia mbichi tano nahisi zimenisaidia though nilisimama nataka nxt monday nirudi barabarani nione,mleta mada shukrani kwa kutu-inspire ktk hili.
 
Wakuu mambo vipi....Binafsi sio mkufunzi(gym trainer) ila napenda sana mazoezi na ninayajua mazoezi kuliko hata hawa wanaojiita ma-trainer,nimeanza kupenda mzoezi ya gym nikiwa form 3 (2013) so unaweza kuona nina experience ya miaka 11.

Mazoezi pia yanaambatana na aina ya vyakula tunavyokula ukiwa mwanamazoezi automatically kuna vyakula utaanza kuviepuka kama soda na vyakula vya mafuta.Binafsi nina mwaka wa 7 sijui soda na mwaka 4 sijui chips zikoje.Mimi nafanya mazoezi sili chipsi(mafuta food) wewe je nyama uzembe.Week inasiku 7 unahitaji siku tatu mfululizo za mazoezi na siku 4 unapumzika .anza leo after 6 monthes utaona matokeo.

Nitakuwepo hapa kuwapa-assistance kwa bigginer wote.hapa ni uwanja wa mazoezi ya aina zote both weight lift and cardio(mazoezi ya kukimbia na kucheza mziki,kupunguza mafuta na kutafuta pumzi)

Uzi huu ukawe wa kuhamasishana mazoezi na kupeana tips mbali mbali najua humu kuna wataalamu zaidi na wajuzi wa lishe wa kutosha.

Zifuatazo ni Faida za Mazoezi mwilini

1. Kuboresha Afya ya Moyo.
Mazoezi ya mara kwa mara husaidia kuimarisha moyo na kuboresha mzunguko wa damu, kupunguza hatari ya magonjwa ya moyo.

2.Kuongeza Nguvu na Uimara.
Mazoezi ya nguvu huongeza misuli na kuimarisha mifupa, huku mazoezi ya uvumilivu yakisaidia kuboresha uwezo wa mwili kustahimili uchovu.

3. Kupunguza Uzito.
Mazoezi husaidia kuchoma kalori na kupunguza mafuta mwilini, hivyo kusaidia katika kupunguza uzito.

4.Kuboresha Mvuto wa Mwili
Mazoezi ya mara kwa mara husaidia kuimarisha misuli na kufanya mwili kuwa na muonekano mzuri na wenye nguvu.

5.Kupunguza Stress na Kuboresha Hisia.
Mazoezi yanaweza kusaidia katika kupunguza viwango vya stress na kuboresha hisia kwa kuongeza uzalishaji wa endorphins, kemikali zinazofanya mtu ajihisi vizuri.

6.Kuboresha Usingizi.
Mazoezi yanaweza kusaidia kuboresha ubora wa usingizi, hivyo kukufanya uamke ukiwa na nguvu na mchangamfu.

Jinsi ya Kuanza Mazoezi
Najua wabongo wengi hatupendi mazoezi kutoka na mfumo wetu na ukuaji wetu wa maisha maana mazoezi ni sehemu ya maisha ni hii husaidia sana watu kuiishi umri ya miaka 70 mpaka 90.

1. Anza Kidogo Kidogo.
Usijaribu kufanya mazoezi mengi mara moja. Anza na mazoezi madogo na polepole ongeza muda na kiwango cha mazoezi.

2. Chagua Mazoezi Unayoyafurahia.
Tafuta aina ya mazoezi unayopenda, iwe ni kutembea, kukimbia, kuogelea, kucheza dansi, au hata mazoezi ya nyumbani. Kama unajifurahisha, utapata rahisi kuendelea.

3.Panga Ratiba.
Weka ratiba ya mazoezi na ujitahidi kuifuata. Hakikisha una muda maalum wa kufanya mazoezi kila siku au kila wiki.

4.Tumia Rafiki.
Kufanya mazoezi na rafiki kunaweza kufanya mazoezi yawe na furaha zaidi na kukuongezea motisha.

5.Lenga Malengo Madogo na Yanayowezekana.
Weka malengo madogo na yanayoweza kufikiwa. Kwa mfano, lengo la kutembea kwa dakika 20 kila siku kwa wiki moja.

6. Sikiliza Mwili Wako
Usijilazimishe kufanya mazoezi zaidi ya uwezo wako. Sikiliza mwili wako na pumzika unapohisi uchovu.
Oya kwa dar gym ga I nzuri ambayo wapo warembo classic
 
Mazoezi ni mazuri na ni kitu cha muhimu sana kwenye mwili wa binadamu kama ukiweza kuyazingatia.

Napenda kukimbia lakini napata shida kwenye magoti nikikimbia wiki mbili tu nahisi kama kuna vidonda,nimeanza dozi ya kila siku asubuhi na jioni nakula bamia mbichi tano nahisi zimenisaidia though nilisimama nataka nxt monday nirudi barabarani nione,mleta mada shukrani kwa kutu-inspire ktk hili.
Magoti shida....mzee utakuwa unakamia sana wakati wa kugegeda 🤣🤣🤣🤣🤣
 
Magoti shida....mzee utakuwa unakamia sana wakati wa kugegeda 🤣🤣🤣🤣🤣
😂😂😂😂 Mkuu lakini simfikii muwakilishi wetu mzee wa kuwauwa wima wima kimya kimya
 
Aisee wahi mapema hiyo shida kuna mshkaji wangu alipuuzia amefanyiwa operation ya ligament juzi hapa
Tatizo ni hilo hilo mkuu, sijui shida ni nini haswa, vipi yeye operation yake wamemfanyia kwa sh ngapi goti moja na ni hospitali gani?
 
Tatizo ni hilo hilo mkuu, sijui shida ni nini haswa, vipi yeye operation yake wamemfanyia kwa sh ngapi goti moja na ni hospitali gani?
MOI nenda kamuulizie dr sabas mshkaji na mwamba sana jamaa alifanya kwa bima.. by the way unaweza fanyiwa tiba bila operation inategemea na tatizo.
 
Saint Anno II

Nadhani muhimu ufanye vipimo kwanza kuhusu hayo magoti kabla hujaendelea sababisha uharibifu zaidi. Kama kuna shida utaambiwa na namna ya kupata matibabu.

Muda mwingine kulingana na hali ya magoti itakavyo onekana kwenye vipimo, waweza katazwa kabisa kukimbia, mbadala wake unatembea tu.

Magoti ni kiungo muhimu sana na ndo "the largest and very complex joint in human body".

Kila la heri.
 
Pia unaweza pata tiba bila operation.. jamaa yangu alifuga tatizo.
Niko interested mkuu, hali inakiwa tete kadri siku zinasonga mbele.

Mama yangu mzazi yeye ligament zimeisha kabisa, ni mifupa inasagika tu, nilitaka kuchukua maamuzi magumu ya kuuza kakibanda akapate tiba, akagoma.. Kipindi hiko tuliambiwa mguu mmoja eti milioni 12, yote miwili ni 24, na hapo kuna uwezekano wa kutembelea kiti maisha yako yote, akagoma kabisaa, tokea hapo sikufuatilia tena.
 
Kacheki mapema afya ya hilo goti pale moi kama upo dar kuna wataalam wazuri.. ukipenda nitakudirect magoti ni sensitive sana ukipuuzia utakuja fanyia OP
Hii changamoto ninayo, maana nakimbia sana kwenye lami, ngoja nijipange nikawachek wataalam hao.
 
Today Morning Run
1000005923.png
1000005924.png
 
Back
Top Bottom