Jamiiforums GYM (mazoezi ) thread

Jamiiforums GYM (mazoezi ) thread

Mkuu usinmbie unatamani upungue mpaka 60kg huko mbali sana watu watajua una ngwengwe.....mimi nina 78kg namaintain hapahapa.

Anza kumbia au kuruka kamba hilo ndio zoezi kuu la kupunguza uzito.
Mzee zamani nilikuwa frexble sa hivi hata kupanda juu ya paa unaona uoga so why nataka kupunguza potelea mbali maneno ya watu.
Njia ya msosi nimefeli
 
Mimi sijaongezeka uzito toka mwaka 2015 nilipopima, kweli mazoezi nafanya hasa kukimbia na kuruka kamba ila hata nikiacha kufanya mazoezi kwa muda mrefu bado uzito huwa unabaki pale pale haupandi au ikitokea na ni nadra sana itaongezeka kg 1 tu au grams halafu unarudi pale pale hii iko sawa wadau ? Sina ugonjwa wowote !
nina kg 60 urefu 5.8
Unatak kuongezeka au kupungua.
 
Safi sana kaka kwa kupenda mazoezi hii maana yake unajua umuhimu wa mazoezi.tips zitaendelea siku na siku maana hapa tutakuwa tunajadili mazoez na aina gani ya vyakula inatupasa kula.

Kutembea kwa ukakamavu inabidi uende mpaka km 10 au ukubali kukimbia km5-6

Mwili umegawanyika kuna upper body na lower body...upper ni kuanzia kiunoni kwenda juu yani kifua(chest),mgongo(back),mabega(shoulder) na mikono(biceps and triceps)

Lowe body ni kiunoni kushuka chini yahn miguu na kalio....huku chini wengi wanapasahau(wavivu) na kupelekea mwili kuwa mkubwa juu na chini kuwa mdogo(funguo)

Pia zoezi la mguu ni gumu sana hivyo lazima ukaze kweli kweli kama uchumi unaruhu nunua bike..itakupa matokeo kwa haraka

Umeona mguu wa mabeste.
Mkuu nimeelewa sana.
10Km!!!! Duu
Huwa natembea tatu tu.
Ngoja nifanye reformation na kuongeza usiriasi zaidi. Barikiwa sana.
 
Kaka kwa nyie watu warefu mnachelewa sana kujaa kwa mazoezi ya gym ila mkijaa huwa mnakuwa vipande vya watu.....hapo ili upunguze kalio anza kubeba weight.
Mkuu hapa sijakuelewa nielekeze Pia mbinu Gani AU mazoezi Gani kufanya mwili Uwe strong nilipanga kila jmos na jpili nitembee km 40 then siku za kawaida 10 day naomba unielewe kuhusu weight Pia ntatumia Muda Gani?
 
Mzee zamani nilikuwa frexble sa hivi hata kupanda juu ya paa unaona uoga so why nataka kupunguza potelea mbali maneno ya watu.
Njia ya msosi nimefeli
Anza kukimbia kwa week mara 2 km5 ...then punguza kula kwa siku kula mara mbili na ule kwa kiasi...ukiweza usiku unapiga vyakula vyepesi kama matunda na juice

Punguza kula punguza kula...ukishindwa kujizuia kula basi nenda mloganzila ukaweke puto.
 
Mkuu hapa sijakuelewa nielekeze Pia mbinu Gani AU mazoezi Gani kufanya mwili Uwe strong nilipanga kila jmos na jpili nitembee km 40 then siku za kawaida 10 day naomba unielewe kuhusu weight Pia ntatumia Muda Gani?
Utembee km40 hizo utachoka sana lengo la mazoeiz sio kuchosha mwili.
 
Umenikumbusha mbali sana
Hivi kipindi kile cha jiwe MO alitekwa gym gani?
 
Anza kukimbia kwa week mara 2 km5 ...then punguza kula kwa siku kula mara mbili na ule kwa kiasi...ukiweza usiku unapiga vyakula vyepesi kama matunda na juice

Punguza kula punguza kula...ukishindwa kujizuia kula basi nenda mloganzila ukaweke puto.
Sio mlaji kivile mzee..... Kuna kipindi nilikuwa nchi jirani Fanya kazi ngumu na kupiga tizi kurudi bongo home walinikataa asee.
Sema miaka 2 mwili umefutuka
 
Leo nina muda, ngoja nichukue viatu vyangu nikacheze mpira, mazoezi pekee napenda ni kucheza mpira, changamoto magoti yangu yamekuwa mabovu, haswa la kushoto ni tabu mnoo.
Aisee wahi mapema hiyo shida kuna mshkaji wangu alipuuzia amefanyiwa operation ya ligament juzi hapa
 
Soda ni hatari sana kwa afya zetu ni vile madhara yake huchelewa sana kuonekana.

Ukitaka kuacha soda tumia mbinu hii ukiona kiu kimekubana tumia maji.
Madhara ya soda yanakuja baada ya muda gani?
 
Chagua Mazoezi Unayoyafurahia.
Tafuta aina ya mazoezi unayopenda, iwe ni kutembea, kukimbia, kuogelea, kucheza dansi, au hata mazoezi ya nyumbani. Kama unajifurahisha, utapata rahisi kuendelea.
Wale wazee wa kukimbiza upepo wenzangu, tumia application ya adidas running ili ui enjoy your running.
1000005910.png
1000005911.png
 
Back
Top Bottom