JamiiForums wakitoa ofa ya kumpa ban mtu mmoja, utamban nani?

Duuuh mbona chuki nzito hivyo mkuu?
Amekuudhi nini!
 
Huwezi amini tangu jana naumiza kichwa nimtaje nan wa kupewa BAN nimekosa[emoji1] [emoji23]
Kama itakuwa na umuhimu zaidi wa mtu mmoja Lazima apigwe ban nitajitaja mimi mwenyewe, sababu nauona umuhimu wa kila mtu katika nafasi yake 'peace n lov'
Wew mtu wa pekee, umevaa viatu vya Musa aliyemkosoa Mungu kuwa hsifai kuangamiza watu wake kwani mataifa watamshangaa...nimependa hivyo.

ANGALIZO
unapoona wew unawavumilia wengine kwa mapungufu yao
UJUE
wao nao wanakuvumilia kwa udhaifu wako
HEKIMA yako ni upumbavu kwa wengine.
FURAHA yako ni chuki kwa wengine.


HAKUNA HAJA KUCHUKIANA KWA TOFAUTI ZETU
 
SIWAPENDI WATU WANAOTAKA UBISHANI WAKATI FACT ZIPO TENA NI WAJINGA WAJINGA SANA HUMU JAMIIFORUMS WENGINE WANABISHIA UWEPO WA MUNGU HAWA NDIO WAKUTIA BAN KABISAA WANAVICHWA VIGUMU ZAIDI YA TOFALI
 
Mende msafi....huyu ningeomba apigwe ya maisha...na hata kama mods wanasoma naomba waufanyie kazi ushauri wangu
 
Mimi ningewapiga ban watu wawili wanaotumia verified user names:
1. Mpendazoe
2. Juliana Shonza hahahahaha
 
Hongera sana kwa kupoteza muda wako kunidiss
...najua huwezi kuwa km mimi

Siku nyingine nitakupa zawadi ya "Uafisa habari wa Makapuku" ili uwe msemaji wangu hapa Jf
[emoji2] [emoji2] [emoji2]
Hapana mkuu atatuvuruga, atuache tu na ukapuku wetu
 
Hahahahaha yaani wewe ni sawa na mtu asiyekula nyama halafu anatembea kwenye mbuga za wanyama wakali kama Simba na nyati halafu ategemee nyati asimdhuru kwa kuwa hali nyama hahahahaha
 
Hahahahaha yaani wewe ni sawa na mtu asiyekula nyama halafu anatembea kwenye mbuga za wanyama wakali kama Simba na nyati halafu ategemee nyati asimdhuru kwa kuwa hali nyama hahahahaha
Fafanua nikuelewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…