Tambukareli
Member
- May 8, 2020
- 35
- 64
Namna ambavyo Rais magufuri amejipambanua kukabiliana na janga la corona ni dhahiri amekonga nyoyo za walio wengi na hii imepelekea kupata uungwaji mkono na maelfu ya watanzania wakiwemo wa vyama vya upinzani.
Kitendo cha Rais Magufuli kutokubaliana na agenda ya kujifungia (LOCK DOWN) ambayo ndio ilikuwa agenda kuu ya upinzani, wananchi wamekipokea kama maamuzi sahihi ya kuwavusha katika kipindi hiki cha janga la corona dhidi ya baa la njaa na matatizo mengine ya kiuchumi.
Leo Rais Magufuli ametoa tamko la kufungua vyuo na shule kwa wanafunzi wa form six hili pia wananchi wamelipokea kama uamuzi wa busara kwa sababu linasaidia kulinda ajira za walimu wa shule na vyuo binafsi ambao walikuwa wanaishi katika kipindi kigumu kutokana na kusitishiwa mishahara yao. Hali kadhalika uamuzi huu unasaidia kulinda usalama wa wanafunzi dhidi ya vishawishi mitaani na hatari ya mimba za utotoni.
Kwa namna Rais Magufuli amejitoa na hatua alizochukua kukabiliana na corona hakika amepata wafuasi wengi hasa katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi mkuu. kwahivyo vyama vya upinzani vijipange kisawa sawa kwa sababu uchaguzi ujao utakuwa ni mgumu kwa upande wao baada ya kupoteza wafuasi wake kutokana na agenda zilizokosa credibility katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa corona.
Sambamba na hatua nzuri anazochukua Rais Magufuli kupambana na corona ni vema sasa akaangalia areas of weakness ambazo bado zinahitaji utatuzi mathalani suala la ajira kwa vijana, azitatue ili kufikia October wananchi wawe na kazi moja pekee ya kuchukua na kuweka waaa.
Kitendo cha Rais Magufuli kutokubaliana na agenda ya kujifungia (LOCK DOWN) ambayo ndio ilikuwa agenda kuu ya upinzani, wananchi wamekipokea kama maamuzi sahihi ya kuwavusha katika kipindi hiki cha janga la corona dhidi ya baa la njaa na matatizo mengine ya kiuchumi.
Leo Rais Magufuli ametoa tamko la kufungua vyuo na shule kwa wanafunzi wa form six hili pia wananchi wamelipokea kama uamuzi wa busara kwa sababu linasaidia kulinda ajira za walimu wa shule na vyuo binafsi ambao walikuwa wanaishi katika kipindi kigumu kutokana na kusitishiwa mishahara yao. Hali kadhalika uamuzi huu unasaidia kulinda usalama wa wanafunzi dhidi ya vishawishi mitaani na hatari ya mimba za utotoni.
Kwa namna Rais Magufuli amejitoa na hatua alizochukua kukabiliana na corona hakika amepata wafuasi wengi hasa katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi mkuu. kwahivyo vyama vya upinzani vijipange kisawa sawa kwa sababu uchaguzi ujao utakuwa ni mgumu kwa upande wao baada ya kupoteza wafuasi wake kutokana na agenda zilizokosa credibility katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa corona.
Sambamba na hatua nzuri anazochukua Rais Magufuli kupambana na corona ni vema sasa akaangalia areas of weakness ambazo bado zinahitaji utatuzi mathalani suala la ajira kwa vijana, azitatue ili kufikia October wananchi wawe na kazi moja pekee ya kuchukua na kuweka waaa.