Januari Makamba kukataliwa na Wajumbe 1,463 kati ya 1,915 inatoa taswira gani kisiasa?

Januari Makamba kukataliwa na Wajumbe 1,463 kati ya 1,915 inatoa taswira gani kisiasa?

Januari Yusuph Makamba, Mwanasiasa kijana mwenye ushawishi mkumbwa ndani ya Chama cha Mapinduzi ambaye Mwaka 2015 aliingia 5 bora ya wagombea wa Urais.

Hivi majuzi tumeona kwenye uchaguzi wa kuwania nafasi ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) akishika nafasi ya 11 kwa kupata kura kiduchu 452 kati ya kura 1915 kwa tasfiri nyepesi wajumbe 1,463 walimkataa kwenye sanduku la kura.

Ni nini hasa kimemdondosha kisiasa kijana huyu machachari kutoka 5 bora za Urais 2015 hadi nafasi 11 na kushindwa hata kuingia 10 bora licha ya taarifa kudaiwa ndiye mgombea aliyetumia pesa nyingi kuliko wagombea wote wa NEC.

we jamaa huyu January huyu dah.
 
Ajitafakari. Asidhanie hatujui jinsi anavyoiba na kutaabisha watu kwenye umeme. Ili apate fedha za kuja kuhonga kwenye uchaguzi
 
Januari Yusuph Makamba, Mwanasiasa kijana mwenye ushawishi mkumbwa ndani ya Chama cha Mapinduzi ambaye Mwaka 2015 aliingia 5 bora ya wagombea wa Urais.

Hivi majuzi tumeona kwenye uchaguzi wa kuwania nafasi ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) akishika nafasi ya 11 kwa kupata kura kiduchu 452 kati ya kura 1915 kwa tasfiri nyepesi wajumbe 1,463 walimkataa kwenye sanduku la kura.

Ni nini hasa kimemdondosha kisiasa kijana huyu machachari kutoka 5 bora za Urais 2015 hadi nafasi 11 na kushindwa hata kuingia 10 bora licha ya taarifa kudaiwa ndiye mgombea aliyetumia pesa nyingi kuliko wagombea wote wa NEC.

Domo chafu la babake
 
Kwamba anaudhawishi mkubwa hahahah kura zake zinakaribiana na shilole
 
Tatizo ukipenda, chongo utaita kengeza

Kila nililotaja hapo juu naweza kukupa mfano

Na kama unafahamiana nae muulize labda kwa jambo moja. Muulize ule mlolongo wote uliomfanya sio tu waziri, pia waziri wa Nishati. Muulize ilikuwaje hadi kupewa kwanza uwaziri, pili wa nishati. Je Samia ndio alimchagulia wizara? Nani walihusika katika kuwa kwake waziri?

Pili muulize ilikuwaje alipopewa uwaziri kina Tito Mwinuka ikabidi waondoke waje kina Maharage Chande. Nani alileta hiyo ajenda? Kama ni yeye alitumia ushawishi gani hadi Raisi akakubali? Nani walimuunga mkono kumshawishi Samia? Nini alichofanya au anachofanya Maharage Chande ambacho Mwinuka hakuwa anafanya? Tanesco imekuwa bora zaidi?

Kwa hiyo kama ni chuki unaziongelea hapa, labda ushauri wako kampe huyo January kwanza, ndio uje kutuambia sisi. Unachukia hadi watu waliokufa na kusema hutaki kufanya kazi na walioteuliwa nao, uko sawa wewe!

Tanesco inaongozwa na aliekuwa mkurugenzi wa Vodacom sijui, Wizara ya nishati inaongozwa na mtu ambae background yake hasa ni kuandika hotuba za Kikwete, kasomea fasihi sijui. Halafu tunapata matokeo madudu kabisa mnasema acheni chuki binafsi. Kuna watu mnafanya utani na nchi hii.

Watu kama January uwepo wao katika baraza la mawaziri na connection zao kwa baba yake na kina Kikwete unamfanya Samia awe kiongozi weak, na hilo Samia anapaswa kulitambua, na nitasema hata mbele yake.
Huna lolote la maana.

Hizi ni blabla tu za wasaka madaraka.

Kundi lenu lina chuki kubwa sana kwa Rais Samia. Hamuwezi kumshambulia yeye moja kwa moja hivyo mnashusha chuki zenu kuputia kwa Januari.

Nakuhakikishia,Januari ataendelea kuwa kwenye siasa za juu za nchi kwa kuwa anauwezo mkubwa. Halikadhalika,anazo nguvu kubwa za kisiasa.
 
Huna lolote la maana.

Hizi ni blabla tu za wasaka madaraka.

Kundi lenu lina chuki kubwa sana kwa Rais Samia. Hamuwezi kumshambulia yeye moja kwa moja hivyo mnashusha chuki zenu kuputia kwa Januari.

Nakuhakikishia,Januari ataendelea kuwa kwenye siasa za juu za nchi kwa kuwa anauwezo mkubwa. Halikadhalika,anazo nguvu kubwa za kisiasa.
Una analysis ya ajabu sana. Mie nimchukie Samia kwa ajili ya January? Basi ungejua namuonea huruma Samia kwa ajili ya January, na sikumpenda kabisa Magufuli. Lakini wewe naona unanichukia mie kwa kuwa unampenda January, na unampenda Samia kwa kuwa amem-favor January. Ningependa niwe mshauri wa Samia nimwambie katika watu wa kuondoa mara moja kwenye baraza lake ni January, la sivyo ampe wizara nyingine kama utamaduni na michezo au habari. Si mwandishi bwana

Mie sina mapenzi na watu bwana, nina mapenzi na nchi yangu. Samia akifanya ovyo nitasema, Magu alipofanywa ovyo nilisema. Sio wewe unaehusudu watu. Kama unampenda January kiasi hicho mwambie alete posa kwenu basi. Mwisalamu yule anaweza kukuongeza.

Kabla hujafanya conclusion zako za kitoto take trouble kuangalia thread zangu nyingine sio unakuwa na kiherehere cha ku-conclude mambo kama kinanii cha kwanza.
 
Januari Yusuph Makamba, Mwanasiasa kijana mwenye ushawishi mkumbwa ndani ya Chama cha Mapinduzi ambaye Mwaka 2015 aliingia 5 bora ya wagombea wa Urais.

Hivi majuzi tumeona kwenye uchaguzi wa kuwania nafasi ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC) akishika nafasi ya 11 kwa kupata kura kiduchu 452 kati ya kura 1915 kwa tasfiri nyepesi wajumbe 1,463 walimkataa kwenye sanduku la kura.

Ni nini hasa kimemdondosha kisiasa kijana huyu machachari kutoka 5 bora za Urais 2015 hadi nafasi 11 na kushindwa hata kuingia 10 bora licha ya taarifa kudaiwa ndiye mgombea aliyetumia pesa nyingi kuliko wagombea wote wa NEC.

Ukiona umechukua yeye kati ya wote 14 ujue tayari umeelewa nguvu yake. Swala la muda tu. JK 2002 alikuwa wa 12 kwenye NEC. Kama hujui historia itakuja kukuadhibu.
 
Back
Top Bottom