January Makamba Apewe Nafasi... Mtoto Akianguka Humkati Miguu

January Makamba Apewe Nafasi... Mtoto Akianguka Humkati Miguu

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
pic-makamba.jpg
Na. M. M. Mwanakijiji

Mzazi yeyote anajua mojawapo ya kanuni kubwa za kumfunza mtoto; ni kumuacha wakati mwingine aanguke. Sasa humuachi aanguke mahali pa hatari au ambapo anaweza kuumia vibaya; bali unamuacha aangukie mahali ambapo ataweza kujipukuta na kusimama tena hata kama baadaya kulia. Hata ukimwambia pole; unajua hajaaumia sana lakini pia unajua atakuwa mwangalifu mara nyingine tena. Kuteleza na kuanguka, na hata kuchubuka ni alama za mafunzo ya maisha. Wengine bado tunatembea na makovu ya utotoni; ama ulianguka kwenye jiwe, ulijikwaa mahali, au ulichezea wembe. Mdogo wangu anajereha la toka akiwa na miaka kama mitano hivi baada ya kujikata kwa wembe akikakata mrija wa jani la mpapai ili kutengeneza filimbi! Hakuugusa wembe tena!

Katika makala yangu HII HAPA nilionesha haja ya vijana "watatu au wanne" kuangaliwa upya na kupewa nafasi nikiamini kuwa watakuwa wamejifunza. Hata mtoto afanye kosa kubwa kiasi gani mara nyingi kama wazazi tunawapa nafasi ya kutengeneza tena. Ni pale mtoto anapofanya kosa lisilosameheka kwa wazazi kiasi cha wazazi kumpa laana; yaani kumkana kabisa. NI wazazi wachache sana wanafikia sehemu ya kumpa mtoto laana; na wakati mwingine hata huyu akirejea na kujuta hujikuta anasamehewa.

January kama ilivyokuwa kwa Nape na Mwigulu walijaribu kuinua mapembe yao kwenye zizi la fahali mmoja. Wakajikuta wameondolewa nafasi zao na kwa aibu kidogo. Kwa baadhi yetu tuliona kuwa ilikuwa ni nafasi ya vijana hawa kujiangalia na kujitafakari uongozi wanaoutaka. Na kweli karibu wote hawa vijana waliweza kutulia. Waliweza kuwa nje ya madaraka makubwa na kurudi nyuma. Japo wengine bado walikuwa wanahisiwa kuwa wanachokonoa chokonoa katika kuonesha kutokusalimu amri kwao.

Sasa, kurudishwa kwa Mwigulu Nchemba na kwa sasa January Makamba kunatufundisha kuwa Rais Samia ameonelea kutokuwatupa vijana hawa nyota wa CCM. Na labda kuwaita "vijana" tena siyo sahihi sana. Hawa wote wanakaribia miaka hamsini sasa kwa hiyo ni "watu wazima" na neno sahihi labda ni "watu wa makamo". Ujana hauwezi tena kuwa kisingizio wala sababu ya hawa kutokuwa na hekima katika uongozi au kufanya mambo yanayotakiwa kufanywa na vijana wa chini ya miaka 40! Naamini sasa wamejifunza kitu. Rais Samia inawezekana amewapa nafasi yao ya mwisho kuweza kujitengeneza na kuwa sauti na nguvu ya kisiasa Tanzania kuelekea uchaguzi wa 2030.

Kwa January hili lina maana moja kubwa; ni lazima amuunge mkono Rais wake kwa asilimia 100. Wizara ya Nishati ni Wizara ambayo January alikuwa anapenda sana kuiongoza. Ana mawazo mengi kuhusu sekta hii hasa kwa vile aliona mambo yote yaliyokuwemo toka enzi za Dowan na madudu yake. Lakini pia nina uhakika anakumbuka kilichomuondoa Ibrahim Msabaha linapokuja suala la mikataba ya Nishati. Uzuri ni kuwa January amepewa nafasi ya kuongoza Wizara ya Nishati ambayo hatimaye ilitenganishwa kutoka Wizara ya Madini (hili lilikuwa ni jaribu kubwa sana kwa Waziri yeyote yule). Kupewa Nishati kunamfanya awe na nafasi ya kuweza kushughulikia sekta ambayo marafiki zake na watu mbalimbali wanaweza kumsaidia sana katika masual aya sera. Mwisho wa siku ni jukumu lake kuhakikisha kuwa sekta hii inasimamia taifa kwani bila nishati ya uhakika, nafuu, na inayowafikia wananchi kwa uharaka Tanzania itakuwa bado ina ndoto. Kazi kubwa ni kuona Bwawa la Umeme la Nyerere linakamilika kwa wakati; kuhakikisha hatua za awali na za kudumu za kusambaza umeme zinafanyika nchi nzima lakini pia kuhakikisha kuwa gharama ya umeme na upatikanaji wa vyanzo mbadala (alternative/renewable energy source) zinapatikana, ni rahisi na vyenye kuchochea uwekezaji wa ndani vinapatikana.

Ninanua kuna watu ambao kwa vile wanawafahamu vijana hawa kwa karibu na hususan January Makamba (rejea mada zilizorejeshwa JamiiForums baada ya uteuzi wake tena). Kuna watu ambao hawakufurahia wala kuona umuhimu wa Makamba kurudi tena kwenye nafasi kubwa kama hii. Binafsi, licha ya kuyajua yote yanayotajwa, madhaifu na Archille's heel yake naamini sasa hivi siyo tu anaweza kutulia lakini akawa na hekima ya kutenganisha siasa na harakati za kisiasa na kuzama katika kutumikia taifa, kuinua sekta aliyodhaminiwa kwayo na zaidi ya yote kutokusababisha serikali kuingia matatani ama kwa mikataba mingine mibovu ya nishati, au katika kudhoofisha juhudi za kujitegemea katika nishati na kufanya upatikanaji wa nishati ya uhakika uwe utakaosababisha Dowans na Richmon 2.0.

Binafsi, nampa nafasi na nitamhukumu kwa utendaji wake katika wizara hii nyeti licha ya kutambua matatizo yake ya huko nyuma. Ninaamini yeye na vijana wengine kwenye serikali hii (kama bado namuweka kundi la vijana) wana nafasi ya kuonesha kwanini Rais Samia amewapa nafasi hiyo tena; siyo kwa sababu ya kuwabeba (tukumbuke January alikuwa Ofisi ya Makamu wa Rais kabla ya kuondolewa na Magufuli). Tunataka tuamini kuwa Rais Samia anaamini katika uwezo wake wa kiuongozi na siyo kumbeba kama mama (political matronage).

Tumpe Nafasi January Makamba, na tumuunge mkono bila kusita kumkosoa inapostahili kwani nyota yake bado inang'aa haijafifia na ni jukumu lake kuhakikisha kuwa inaendelea kung'ara.

MM Mwanakijiji.
New Nguvumali, Tanga.
 
Abebwe mara ngapi. January has never stood up for himself, and be a man of his own making, yeye mara zote amekwea madaraka kwa kutumia mbeleko za wengine.

Ni mbunge wa zaidi ya miaka 10+, lakini hajaonesha uwezo wowote wa ajabu ndani ya bunge. Ukiambiwa uonyeshe mchango wowote significant aliofanya akiwa bungeni, hakuna.

Tukisema azidi kupewa nafasi, ni kuzidi kupromote nepotism. Madaraka sio ya kujaribu jaribu, kwasababu unakuwa unadeal na maisha ya watu. Kama alishindwa kuonyesha uwezo mara kadhaa huko nyuma, awekwe pembeni, kuna watu wenye uwezo ila wanakosa nafasi kwa sababu zinazibwa na watu kama kina January wanaobebwa kila saa.
 
Uteuzi wa January unaendana na tangazo la mama Samia kuweka nia ya kugombea muhula wa pili wa uraisi.

Hii inanipa mawazo ya ajabu kwamba amepewa nafasi hiyo si kwa sababu ya uwezo wake bali ni kumuingiza kundini kwenye kundi la shughuli ile iliyofanyika Masaki wakati wa uchaguzi mkuu wa 2015. Anahitajika sana kwenye timu ya ushindi ya Mh.Samia 2025.

Haya ni mawazo yangu tu na siyo taarifa kamili au iliyo sahihi.
 
Nchi hii haina Sheria kila mtu afanya akakalo ,apewe muda gani January ndiye mwenye laana ya kuiba kura 2015 huyu ni dictator kama mwendazake,kama Hangaya
 
Siasa za PR...
Pole sana mkuu Mzee Mwanakijiji kama umefikia huku katikati ya vita ya
1.Kudai katiba mpya
2.Utawala wa sheria
3. Nafasi kwenye demokrasia
4.Uhuru wa watu kufanya siasa

Poleni sana sana..
 
Makamba amekuwa waziri kwa wizara tofauti karibia awamu tatu, alichokifanya sijakiona, zaidi ya kuendeleza ndoto zake za Urais, kubebwa na mamlaka za nchi kumemdumaza akili anaamini ataupata urais kwa mtindo huo.

Though it's possible akawa Rais wa kubebwa kama "familly friend" akilipitisha jina lake kwenye KK, the rest inaachiwa tume ya uchaguzi, baada ya hapo nae anaanza kuitwa Rais wa JMT.
 
siku zote fadhila ,huwa ni fadhila ,ndani ya fadhila hakuna kuangalia creativity au value!!
 
Nadhani mzee unataka kupata lawama za "mtoto mtukutu aliyelelewa na babu/bibi", labda tu nikukumbushe misemo yenu wazee;

1. Sumu haijaribiwi kwa kuonjwa
2. Mjasiri haachi asili
3. La kuvunda halina ubani
4. Wa mbili havai moja
5. Heri kenda, shika nenda kuliko kumi
6. Mwenda tezi na omo, marejeo ngamani
7. Majuto ni mjukuu
8. Samaki mkunje angali mbichi
9. Usimchezee chatu, utaukosa ushindi
10. Za mwizi ni arobaini

Asante.
 
Hili taifa bado tuna shida kubwa Sana katika kufanya maamuzi sahihi ya kulifanya taifa liwe na maendeleo ya kweli kila siku tutakuwa pale pale kupiga debe teuzi ziende kwa mtu fulani wakati huo huo wapo watu wengi Sana na wenye sifa.
 
Tumekusoma, tumekuelewa.
Kijana Makamba anafaa sana kuwepo katika hii Wizara.

Ni kusahau tu kwa watu, ila makamba ametupambania sana wkt wa mgao wa umeme nchi hii. Sasa aoneshe kweli anastahili.
 
Huwa nakuheshimu sana mwanakijiji kwa makala zako na comments zenye afya kwa nchi lakini leo umechemsha sana sana.January Makamba kurudi kupewa uwaziri ina maana yeye tu ndiye mwenye weledi na kazi ya uwaziri kati ya watanzania million 60?

Huko mitaani kuna watanzania wengi tu wenye weledi na usomi wa hali ya juu.Lakin wanaachwa na wala hawafikiriwi kwa kuwa tu January Makamba alikuwa mwandishi wa Kikwete.

Ndugu huyu ,sijui kama ana weledi wa aina yeyote .Ni waziri mzigo tu .Kwa kuwa hata elimu yake ya kidato cha NNE ilipatikana kwa kuiba mitihani.Mama Samia, ulisema kuwa watanzania wote wana nafasi ya kulitumikia Taifa lao.

Leo waliofeli ndio wanarudishwa.Au mama umesahau maneno yako uliyosema.Tunapoelekea si pazuri.Katiba mpya ni muhimu.Watanzania tuchangamke.Tuanzishe vyama vipya vya kuingoa CCM.Wapinzani hawawezi.
 
Kwani wameisha watu wanaostahili kushika wadhifa kama aliopewa January?
Jamaa ni tatizo kubwa sana.

Bahati mbaya kwetu amekabidhiwa wizara ambayo ina muingiliano wa kimaslahi na matajiri ambao wakati fulani hujaribu kumuweka madarakani raisi atakaye watumikia wao na maslahi yao.

Kwa vile huyu mtu anautamani sana uraisi basi anaweza kuingia mikononi mwao kiurahisi na kuliumiza taifa kwa mategemeo ya kutimiza ndoto yake ya uraisi.

Huyu ni mtu hatari sana kwa maslahi ya taifa letu. Hiyo wizara inatingishwa sana na kingmakers.
 
Abebwe mara mangapi. January has never stood up for himself, and be a man of his own making, yeye mara zote amekwea madaraka kwa kutumia mbeleko za wengine...
Binafsi ninaamini hii ni nafasi yake ya mwisho. Kati ya vitu ambavyo nilikuwa napenda vingetokea ni yeye kushinda uchaguzi wa bunge bila "kupita bila kupingwa".

Kwa sababu fulani amekuwa akipata matatizo sana kule Lushoto. Yaani, hata kama sasa atashindwa kujionesha anastahili basi kuna watu watasema "habebeki".
 
Kwani wameisha watu wanaostahili kushika wadhifa kama aliopewa January?
Jamaa ni tatizo kubwa sana...
Hapa nafikiri naweza ni kama kosa fulani; hakutakiwa really kurudishwa kwenye nafasi nyeti kama hii... angerudishwa na kupewa wizara nyingine ili ajipapambanue; lakini ni wazi hii ni wizara ambayo ilikuwa ni "chaguo" lake kuliko nyingine yeyote.
 
Huwa nakuheshimu sana mwanakijiji kwa makala zako na comments zenye afya kwa nchi.Lakini leo umechemsha sana sana.January Makamba kurudi kupewa uwaziri ina maana yeye tu ndiye mwenye weledi na kazi ya uwaziri kati ya watanzania million 60?Huko mitaani kuna watanzania wengi tu wenye weledi na usomi wa hali ya juu.Lakin wanaachwa na wala hawafikiriwi kwa kuwa tu January Makamba alikuwa mwandishi wa Kikwete.Ndugu huyu ,sijui kama ana weledi wa aina yeyote .Ni waziri mzigo tu .Kwa kuwa hata elimu yake ya kidato cha NNE ilipatikana kwa kuiba mitihani.Mama Samia, ulisema kuwa watanzania wote wana nafasi ya kulitumikia Taifa lao.Leo waliofeli ndio wanarudishwa.Au mama umesahau maneno yako uliyosema.Tunapoelekea si pazuri.Katiba mpya ni muhimu.Watanzania tuchangamke.Tuanzishe vyama vipya vya kuingoa CCM.Wapinzani hawawezi.
Soma vizuri; wakati mwingine mchawi anatakiwa kupewa nini... mfumo wetu kwa bahati mbaya sana unafunga sana wigo wa watu kuteuliwa kutoka kwa wabunge...
 
Back
Top Bottom