#COVID19 January Makamba: Kauli ya Askofu Gwajima kuhusu chanjo na dhamira ya Serikali haikubaliki

Hata corona nayo inafanyiwa utafiti, lakini inakula vichwa sana! Dawa zote ni sumu, kutokana na matumizi! Mliambiwa mjifukize, sijui mle malimao na tangawizi, utafiti, hata wa hiyo Vodafasta, ulifanyika?!
Yeah! Malimao na tangawizi yana virutubisho vinavyosaidia sana metabolism ya mwili na kuimarisha mfumo wa kinga wa mwili. Ilishathibitishwa zamani sana.
 
Yeah! Malimao na tangawizi yana virutubisho vinavyosaidia sana metabolism ya mwili na kuimarisha mfumo wa kinga wa mwili. Ilishathibitishwa zamani sana.
Watu wanakula vyote hivyo, mpaka wana toa jasho linalonukia malimao na kucheua malimao, lakini bado corona inaondoka nao!
Chanjo ya corona unayo pinga, inaweza kuwa na side effect, ni kawaida ya madawa, hata ukichanjwa yellow fever, Unaweza kuharisha usiku kucha! Lakini uharaka wa kutumia hii chanjo unatokana na fact kwamba, hakuna muda, lazima ukimbie na kasi ya gonjwa lenyewe!
Jambo lingine la msingi, hatujaanza leo kuchanjwa, labda hata Wewe Una kialama kwenye bega, ulichanjwa! Watoto wanachanjwa michanjo kibao, tangu wanapo zaliwa! Kama mzungu angekuwa na nia ya kuifuta Africa kwenye uso wa nchi, iwe kwa chanjo au njia zingine, angaweza kwa urahisi tu!
Chanjo za kiafrika, zipo! Unachanjwa chale mpaka kudako, lakini bado unalogeka kitahisi tu, na magonjwa pia yanafanya himaya kwenye mwili huo huo uliochanjwa!
 
Watu wanakula vyote hivyo, mpaka wana toa jasho linalonukia malimao na kucheua malimao, lakini bado corona inaondoka nao!
Kwa kutumia hiyohiyo mantiki yako: wengi wa waliokufa duniani ni hao waliokuwa na lockdown, social distancing, matumizi ya sanitizer,n.k. na hawa ambao wameshapewa chanjo dose kamili. Na bado wamepukutika kama njugu. Sasa kuna haja gani?

Chanjo ya corona unayo pinga, inaweza kuwa na side effect, ni kawaida ya madawa, hata ukichanjwa yellow fever, Unaweza kuharisha usiku kucha!
Kuharisha usiku kucha hakuwezi kuwa na madhara sawa na damu kuganda, vital organs kama ini kupata hitilafu, hormones ku-misbehave na madhara mengine kama hayo.

Jambo lingine la msingi, hatujaanza leo kuchanjwa, labda hata Wewe Una kialama kwenye bega, ulichanjwa!
Chanjo tulizochanjwa zimepitia hatua zote za Kisayansi, hata manufactures na serikali wana confidence nazo na ndiyo maana huwezi kuwasikia wanajitenga na madhara yanayoweza kujitokeza.

Ukiamua kuchanjwa ni hiari yako, lakini usiwapotoshe wengine waangamie. Achana na propaganda za mabeberu, wao wanafanya biashara.
 
Kama usalama wa chanjo ni sahihi, kuna ubaya gani kupinga?
 
Eti wazungu wanaionea wivu Tanzania!

Dah kuna baadhi ya wabongo wapumbavu sana. Hao wazungu hata kuchamba tu wamekufundisha wao wangetaka kukuua si wangetumia hata hizo pedi na madawa mengine ya misaada wanayotupa?
Kwanini wanalazimisha watu kupiga chanjo, kuna ng'ombe mwenye kiu analazimishwa kunywa maji?
 
Ubeberu na mabeberu ni propaganda pia, lakini ya kijinga sana, hasa kama huwa unavaa suruali, shati au tishirt na kama unatumia vifaa vya kielekitroniki, na kama ulisoma shule, japo kidogo!
Suala la hao kufa sana, na Sisi kutokufa sana halina mantiki yoyote, kwa sababu Sisi hatukuwa na takwimu zozote, sasa unalinganishaje?! Labda Wewe Upo Dar, unajuaje taarifa za wanao kufa Naibili huko Siha, wakati utoaji wa takwimu, ni kosa la mtandao, na vyombo halali havitowi pia?!
 
Kwanini chanjo iwe lazima, wacha iwe jambo la hiyari, mwenye kutaka na akachome
 
Waziri wa Afya wa uingereza alipata chanzo zote 3 na amepata corona kwa mara ya pili je hilo nalo mnasemaje
 
Umeshabadili mada.
 
Waziri wa Afya wa uingereza alipata chanzo zote 3 na amepata corona kwa mara ya pili je hilo nalo mnasemaje
Kwani wangapi wanapata Covid-19 na hawana chanjo ila wamepona mara nyingi tu?
 
Askofu Rashid Gwajima ameishika CCM na Serikali yake pabaya wamebakia kubweka bweka tu lakini hawana cha kumfanya. Gwajima ana 'watu'.
 
Ok, Subiri mpaka iingie kwenye inner circle yako ndiyo utajua what are we talking about .....!!
nisubiri mpaka lini ?

toka March 2020 m leo ni miezi 15

huyo Covid hafiki tu ?

yani mnashangaa, hamuelewi kwa nini Mwafrika hajahitaji dawa ambayo Mzumgu anaihitaji...

acheni hizo plantation mentality

to hell na machanjo yenu hayo
 
Huyu alianza kwa kuutangazia Umma kuwa ana uwezo wa kufufua watu waliokuwa. Siku hizi hayo huwezi kuyasikia tena.

Sasa wanatafuta mkakati wa kuaminiwa tena. Hata hivyo Mimi najiuliza kauli zake hizo si miongoni mwa Chokochoko?
Si chokochoko. Chokochoko hutoka upande ulee?
 
Kumnbukeni huyu ni Mbunge naona ubunge alipewa na Magufuli. Niambie mbunge gani Ana akili? Yote Yana akili ya kuku. Bunge liliwekwa Dodoma ili waheshimiwa wabunge wawe karibu na hospitali ya Milembe. Ni watu wanaolipwa mabilioni na hawajui kazi zao. Only Musikuma knows his job!
 
Gwajima akili nyingi yule
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…