Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 53,857
- 121,995
Wanabodi,
Hii ni Makala yangu gazeti la Mwananchi Jumatano ya leo, 2 October, 2024
Watanzania walio wengi, hata wenye uwezo, hawazijui haki zao, kunapotokea vifo vya kizembe vya wapendwa wao, lakini hata wakizijua haki zao, Watanzania walio wengi ni masikini wa kutupwa, hivyo hata wakizijua haki zao, hawana uwezo wa kuajiri wakili kuwatetea, hivyo hili ni bandiko la kuwaomba mawakili, tujitolee kuwatetea bure masikini hawa Watanzania ambao damu zao zinamwagwa kizembe zikiwemo hizi damu zinazomwagwa na wasiojulikana na 'wasiojulikana' just like that huku maisha yakiendelea as if nothing happened!.
Vitabu vya dini zote vinafundisha ukiua kwa upanga, utauawawa kwa upanga!, ukimwaga damu ya mtu, damu yako pia itamwagwa!, hivyo japo vifo vyote vya umwagaji damu isiyo na hatia, hufidiwa na karma kwa kuwashughulikia kikamilifu wamwaga damu wote, hata wasiojulikana wanashughulikiwa, lakini sisi wanasheria na mawakili, tunawajibika kujitolee kutetea bure, hizi damu za Watanzania masikini zinazomwagika kizembe kwa kisingizio chochote!.
Alipouwawa kwa makosa aliyekuwa DGIS, Imran Kombe, familia yake kwa vile ina uwezo na ufahamu, ilidai fidia na ilifidiwa!, vifo vingapi vya kizembe vinatokea mikononi mwa polisi, au kusababishwa na polisi kama Daudi Mwangosi na Aquiline Akwilina na hakuna fidia yoyote iliyodaiwa?.
Watanzania wangapi wanapoteza maisha mahospitalini, makazini na kwenye vyombo vya usafiri kwa ajali za kizembe lakini hakuna hatua zozote za kisheria zinachukuliwa kudai fidia?.
Naamini kama kila tone la damu za Watanzania, machozi, jasho na damu, vingekuwa vinafidiwa kisheria, amini usiami, hata hawa wasiojulikana wangepungua au kuisha kabisa kwasababu wanajua wangedakuliwa na kutundikwa msalabani.
Kwa vile na mimi licha ya kuwa ni mwandishi wa habari wa kujitegemea kwa kujitolea, mimi pia ni mwanasheria na wakili wa kujitegemea kwa kujitolea, nimeamua kujikita kwenye eneo la utoaji wa elimu ya katiba, sheria na haki, kupitia vyombo vya habari vya TV, redio, magazeti na mitandao ya kijamii,
View: https://youtu.be/ZJIKhnZCf04?si=rX-8-1r28_5Q2N6A
Wanasheria na mawakili wenzangu, tujitolee kuwasaidia bure Watanzania wenzetu masikini wa kutupwa wasio na uwezo wa kuajiri wakili kutetea damu za wapendwa wao zinazomwagwa kila uchao!.
Jumatano njema
Paskali
Hii ni Makala yangu gazeti la Mwananchi Jumatano ya leo, 2 October, 2024
Watanzania walio wengi, hata wenye uwezo, hawazijui haki zao, kunapotokea vifo vya kizembe vya wapendwa wao, lakini hata wakizijua haki zao, Watanzania walio wengi ni masikini wa kutupwa, hivyo hata wakizijua haki zao, hawana uwezo wa kuajiri wakili kuwatetea, hivyo hili ni bandiko la kuwaomba mawakili, tujitolee kuwatetea bure masikini hawa Watanzania ambao damu zao zinamwagwa kizembe zikiwemo hizi damu zinazomwagwa na wasiojulikana na 'wasiojulikana' just like that huku maisha yakiendelea as if nothing happened!.
Vitabu vya dini zote vinafundisha ukiua kwa upanga, utauawawa kwa upanga!, ukimwaga damu ya mtu, damu yako pia itamwagwa!, hivyo japo vifo vyote vya umwagaji damu isiyo na hatia, hufidiwa na karma kwa kuwashughulikia kikamilifu wamwaga damu wote, hata wasiojulikana wanashughulikiwa, lakini sisi wanasheria na mawakili, tunawajibika kujitolee kutetea bure, hizi damu za Watanzania masikini zinazomwagika kizembe kwa kisingizio chochote!.
Alipouwawa kwa makosa aliyekuwa DGIS, Imran Kombe, familia yake kwa vile ina uwezo na ufahamu, ilidai fidia na ilifidiwa!, vifo vingapi vya kizembe vinatokea mikononi mwa polisi, au kusababishwa na polisi kama Daudi Mwangosi na Aquiline Akwilina na hakuna fidia yoyote iliyodaiwa?.
Watanzania wangapi wanapoteza maisha mahospitalini, makazini na kwenye vyombo vya usafiri kwa ajali za kizembe lakini hakuna hatua zozote za kisheria zinachukuliwa kudai fidia?.
Naamini kama kila tone la damu za Watanzania, machozi, jasho na damu, vingekuwa vinafidiwa kisheria, amini usiami, hata hawa wasiojulikana wangepungua au kuisha kabisa kwasababu wanajua wangedakuliwa na kutundikwa msalabani.
Kwa vile na mimi licha ya kuwa ni mwandishi wa habari wa kujitegemea kwa kujitolea, mimi pia ni mwanasheria na wakili wa kujitegemea kwa kujitolea, nimeamua kujikita kwenye eneo la utoaji wa elimu ya katiba, sheria na haki, kupitia vyombo vya habari vya TV, redio, magazeti na mitandao ya kijamii,
View: https://youtu.be/ZJIKhnZCf04?si=rX-8-1r28_5Q2N6A
Wanasheria na mawakili wenzangu, tujitolee kuwasaidia bure Watanzania wenzetu masikini wa kutupwa wasio na uwezo wa kuajiri wakili kutetea damu za wapendwa wao zinazomwagwa kila uchao!.
Jumatano njema
Paskali