Uchaguzi 2020 Japo ni mchungu 'Kumesa' lakini ndio ukweli wenyewe; watakaorudi Bungeni ni 'wa kijani', kubali kataa. Mwenye masikio na asikie!

Uchaguzi 2020 Japo ni mchungu 'Kumesa' lakini ndio ukweli wenyewe; watakaorudi Bungeni ni 'wa kijani', kubali kataa. Mwenye masikio na asikie!

Mwenyezi mungu atatuondolea huyu shetani. Kwani yeye ndiye muumba wa kila kitu. Naamini tutarudia tena uchaguzi siku si nyingi.
 
Wakijani watarudi mjengoni,siyo kwa sababu wanapendwa Sana na Watz Baki, ni kwa sababu chama kile kimeshika Hatamu kwenye kila nyanja.
 
Wanabodi,

"Watakao Rudi Bungeni ni 'Wakijani' "

Haya sii maneno yangu, na sio maneno ya kuambiwa ni maneno yaliyotamkwa na ambayo nimeyasikia mwenyewe kwa masikio yangu mwenyewe!.

Japo maneno haya ni maneno machungu kumeza, kwasababu Tanzania ni ya Watanzania wote na siyo ya 'wakijani' tuu, na katika uchaguzi uliopita, wasio wa kijani waliungwa mkono na Watanzania zaidi ya milioni 6, na kuna wabunge 145 wasio wa kijani, na kwa upande wa Zanzibar na Pembe kwa mujibu wa matokeo halali ya NEC, wasio wa kijani ndio wengi kuliko kura zote za kijani!, hivyo wote hawa ni Watanzania wenye haki sawa licha ya kutofautiana rangi!. Kauli hii ndio ukweli wenyewe wa uchaguzi wa 2020!, Watanzania woote katika Umoja wao, wamewakubali sana 'wakijani' na hili watalithibitisha tarehe 28 October, 2020. Mwenye masikio na asikie!.

Sisemi yamesemwa na nani na yamesemwa wapi, bali nawaomba tuu mniamini!.

Hongereni sana 'Wakijani'

Tulipokuwa tukiwaeleza humu kuhusu Watanzania tujifunze kuukubali ukweli hata uwe ni mchungu vipi kama ukweli huu
Kupata maendeleo ya kweli, Watanzania ni lazima tujifunze kuukubali ukweli!. Hili la CCM kutawala milele ni kweli!.
Mlinibeza!

Niliposema kuhusu hoja ya wabunge wasio wa kijani, wakitaka kurejea Bungeni 2020 ni lazima wajitambue
Trend Reading: Wanaohamia CCM wasibezwe! Wanaona mbali, 2020 Majimbo yote kurejeshwa. Je tunarejea nchi ya Chama kimoja?
Pia mlinibeza humu.

Sasa leo Bunge limevunjwa rasmi, tegemeeni "the mass exodus" kwa wabunge wasio 'wakijani' watakao jitambua, they will do the needful, by jumping ships, kwa ving'ang'anizi na wenye misimamo, ambao watashikilia msimamo kwa kusimama na wanachokiamini, hawa ni mashujaa!, watakufa kizungu na tai shingoni na kama ni meli au jahazi, hata likumbwe na tufani kubwa kiasi gani, wao hawata jump ship na ku abandon, hawa watang'ang'ania meli yao, kwa kujishika kwenye milingoti, huku wakijiangalia na watazama na meli yao au jahazi lao na kufa kishujaa na watatamkwa ni mashujaa waliokufa kishujaa kuifia meli yao!. Hoja ya kati ya "waliojitambua" hai, waka abandon meli yao na ku jump ships hivyo kubaki hai na kusurvive na 'mashujaa' wafu, waliokubali kufa huku wanajiona kwa kuifia meli yao, nani ni muhimu zaidi?. This is debatable!

Kwaheri ya kuonana hadi Novemba

2020... "ndani ya nyumba" panapo majaaliwa!.

Paskali
YAMETIMIA! SASA WAWEZA KUWARUHUSU WATUMISHI WAKO WAENDELEE KUTUMIA MAGARI NA MAFUTA KWA KWENDA MBELE!! JE WOTE WATARUDI UTEUZINI? AU NASI SAFARI HII TUTAKUWEMO?
 
Back
Top Bottom