Wanabodi,
Kwa maslahi ya taifa, leo naomba kuendesha somo kuhusu kitu kinachoitwa ubatili na haramu.
Ubatili ni kitu ama kilichofanyika kinyume cha sheria, taratibu na kanuni hivyo jambo likifanyika kwa ubatili jambo hilo linakuwa ni batili.
Haramu ni jambo ambalo limefanyika kinyume cha imani na sio lazima iwe ni kinyume cha sheria.
Huu ubatili na uharamu unafanyika katika nyanja nyingi za maisha yetu, kisiasa, kiuchumi na kijamii.
Sasa ili batili iwe ni batili kweli, lazima batili hiyo ibatilishwe, batili isipobatilishwa inakuwa ni halali!. Vivyo hivyo kwa haramu, ili jambo fulani kuwa ni haramu, lazima haramu hiyo iharimishwe, haramu isipoharimishwa inakuwa ni halali.
Mada kuu ya bandiko hili ni maswali kuhusu uchaguzi mkuu uliopita wa 2020, kuna watu mpaka leo zaidi ya miaka miwili imepita, bado hawataki kukunali matokeo, bado wanaamini uchaguzi ule haukua huru na wa haki hivyo kwao matokeo ya uchaguzi huo sio halali na wengine hata kuuita ulikuwa sio uchaguzi bali ni uchafuzi na matokeo yake ni haramu, hivyo kuendelea kususa hadi leo, hawayatambui matokeo, hawamtambui rais, hawalitambui Bunge hadi kususia nafasi za viti maalum!, hivyo nina viswali kidogo kwako, kuwa japo uchaguzi wa 2020 ni Uchaguzi halali, kwa kanuni ya "the end justifys the means", aliyetangazwa mshindi ndie mshindi halali, jee ushindi wa kishindo wa CCM wa kukomba kila kitu ni ushindi halali au batili na haramu?. Wapinzani ni wameshindwa kihalali kwa kukataliwa na wananchi au ni wameshindwa kwa kudhulumiwa na kufanyiwa Figisu hivyo kushindwa kwao sio halali ni wameshindishwa kwa ubatili na haramu?.
Naomba kukiri nimekuwa inspired kupandisha bandiko hili baada ya kusoma hoja hii ya mwana jf huyu
Mkuu
WALOLA VUNZYA kwanza naomba kukiri post yako hii imenimotivate kupandisha bandiko linalojitemea, thanks for motivation.
Ili jambo lolote haramu liwe ni haramu kweli ni lazima liharimishwe, ukifanya jambo la haramu, lisipo harimishwa linakuwa ni halali, yaani kitendo cha kutoiharimisha haramu yoyote, kunakuwa ni kuihalalisha hiyo haramu inakuwa halali mpaka pale yule YEYE anapoingilia kati kwa karma ama kuibatilisha haramu hiyo ama kuiacha na hivyo kuibariki.
Kwa vile issues zs uhalali na uharamu ni issues ngumu kueleweka kirahisi, naomba nifungie darasa kabisa niwapige shule kwa kutoa mifano ila pia kwa vile humu tuna simple readers na deep readers, simple readers hawataki vitu virefu, wanataka vitu short, simple and clear, hawa wanaweza kuishia hapa na ku jump kwenye conclusion, wale ma deep readers, tuendelee.
Conclusion
Vivyo hivyo kwa haramu ya demokrasia na ubakwaji wa demokrasia, ili haramu iwe ni haramu kweli lazima haramu hiyo iharimishwe, haramu isipoharimishwa, na batili isipo batilishwa inageuka halal!.
Swali la kujiuliza kuhusu uchaguzi wa 2020 jee kuna mgombea yoyote aliyelalamika rasmi popote kuhusu uchaguzi huo?. Jibu ni hakuna!. Hivyo kwasababu hakuna mtu yoyote aliyelalamika popote, then kumehalalisha kila kilichofanyika kwa kuitumia ile kanuni ya "the end justifies the means" kwa hoja hizo, na kwa muktadha huo, Uchaguzi wa 2020 ni uchaguzi halali, na sio uchafuzi kama unavyodaiwa na baadhi ya walioshindwa!, CCM imeshinda ushindi wa kishindo kihalali, na wapinzani wamekataliwa na wananchi na kushindwa kihalali!, the winner takes it all!, the looser standing small.
Paskali