Japo Wakristo na Waislamu ni Watoto wa Baba Mmoja, Nabii Ibrahim na Mungu ni Mmoja, Kati ya Ismail na Isaka ni nani aliyetolewa Sadaka ya Kuchinja?

Hakuna yeyote aliyetakiwa kuchinjwa, watafsiri wa Qur'an wamekosea sana tafsiri, sijuwi hilo la kuchinjwa mtoto wamelitowa wapi.


Nijuavyo limetumika neno "dhabih" ambalo kitafsida linamaanisha kukatwa jando.

MAJIBU YA FAIZFOX HAYO
Kateleza tu
 
Hakuna yeyote aliyetakiwa kuchinjwa, watafsiri wa Qur'an wamekosea sana tafsiri, sijuwi hilo la kuchinjwa mtoto wamelitowa wapi.


Nijuavyo limetumika neno "dhabih" ambalo kitafsida linamaanisha kukatwa jando.

MAJIBU YA FAIZFOX HAYO
Mwambie asome comment/post yangu #310
 
Kwani urithi ulikuwa Ni nini ningependa Kujua..
Maana nikiangalia Biblia Nakuta kuwa Ishmael au Waishmael ndo wafanya Biashara wakubwa sana wa Agano la kale..

Umeuliza swali zuri Sana na ambalo ndilo kiini cha hiyo Sadaka na dhabihu.

Urithi unaozungumziwa hapa ni ile ahadi ya Mungu kwa Ibrahim iliyomfanya amtoe Uhuru wa ukaldayo mpaka Hapo Kanaani.

Mungu alimpa Ibrahim ahadi kuu tatu;
1. Kumpa nchi ya Kanaani. Ndio maana akamhamisha kutoka Íraq mpaka Canaan.
Ahadi hii imetimizwa kutoka kwa mtoto wa ahadi ambaye ni Isaka
2. Kumfanya kuwa Maarufu.
Ahadi hii pia imetimizwa kwa mtoto wake Isaka.
3. Kumfanya kuwa taifa kubwa
Ahadi hii imetimizwa kwa mtoto Ishmael.
Ingawaje bado upo utata na hakuna ushahidi wa moja kwa moja kuwa Ishmael kuwa Baba wa waarabu.

Urithi wa kuhakikisha ardhi(nchi ya Kanaani) inakuwa mikononi mwa damu ya Ibrahim.

Ahadi za kiroho hizo tuachane nazo ila za kimwili ushahidi huo tunaompaka hivi sasa kuwa aliyepewa urithi alikuwa Babu wa waisrael.

Tukio la kutolewa kafara kwenye Biblia linakuja baada ya Ishmael kuondolewa kwa sababu alikuwa nje ya mipango.

Zingatia, Ishmael kuzaliwa ni matokeo ya Mwanamke kutokuwa na imani na Ahadi ya Mungu. Yaani ulikuwa mpango wa Sarah baada ya kuona ahadi ya Mungu inachelewa
 
Kasema nani Quran haijitoshelezi!?.. haijitoshelezi kwenye nini,kufuga nyuki

Kama inajitosheleza.
Quran haionyeshi wala kutaja ni mtoto gani aliyetolewa kafara.
Quran haionyeshi ni wapi tuko hilo la kutaka kutolewa kafara kwa mtoto huyo lilifanyika.

Kama Quran unayotumia wewe inaonyesha hayo unaweza kutuwekea hapa.

Na kama haina. Basi kubali kuwa Quran hazijitoshelezi hasa kwenye mambo ya msingi inapoelezea jambo.
Na hii inamaanisha nini ujue?
 
Sijaona kwenye Qur'an kuwa Ibrahim alikuwa na mtoto anitwa Ismail, au hayo ni mafundisho nje ya Qur'an?
Kwa kweli sijawahi kukutana na hoja kama hii, ila naomba niulize ikiwa ushahidi upo kwenye hadithi unaukubali ama wewe ushahidi ni lazima utoke kwenye Quran?

Natambua kuwa kuna mjadala kuhusu mtoto yupi alipaswa kutolewa sadaka kati ya Ismail na Isaak ila sijawahi kukutana na shaka ya wote kuwa ni watoto wake.

Anyway nategemea kujifunza zaidi hapa
 

FaizaFixy anahoja.
Ndio maana nikakuambia Mahakamani Quran itashindwa kuthibitisha aliyechinjwa ni Ishmael kwa sababu hata watoto wanaotambuliwa na Quran kuwa ni watoto w Ibrahim huyo Ishmael hayupo ila Isaka yupo.

Mambo ya hadithi hapa hayana nafasi
 

Mgao wa urithi wa nani?
 
Kusema kwamba watoto wanaotambuliwa na Qur'an kuwa ni watoto wa Ibrahim Ishmael hayupo.., ni UONGO maana kuna aya imewataja watoto wote wawili tena kwenye ascending order......hii hapa QURAN 14:39 "Praise to Allah, who has granted to me in old age Ishmael and Isaac. Indeed, my Lord is the Hearer of supplication."
 
Unafikiri kwa nini Quran haijazungumzia Wana wa Ishmael?
QUR'AN siyo biography kijana,ni kitabu Cha muongozo wa mahusiano ya binaadam na mola wake,vipi Aishi na vipi aabudu,inapozungumzia Wana wa Israel au Maryam ni kwa kuwa Kuna controversy na yenyewe huweka sawa,sala ya maria inamtaja maria Kama mama wa Mungu,yesu Kama Mungu/mwana wa Mungu,so QUR'AN inaweka sawa hayo mambo,haizungumzii kila kitu,sura ya wanawake inazungumzia mambo ya wanawake ikiwemo ndoa na hedhi zao,Sasa wewe unataka imzungumzie Ishmael na kila mtu unayemjua!!
 
Kwanini na Isaka asiwe mwana wa Sara?


Vizuri kwa kuliweka hili Sawa.
FaizaFixy FaizaFoxy Quran unayotumia haina aya hii?

Turudi kwenye hoja.
Nani aliyetaka kutolewa dhabihu?

Quran kwa Ishmael ingawaje haijamtaja ila moja kwa moja mtu anayesoma Quran atajua ni Ishmael lakini Biblia na vitabu vya kiyahudi vinamtambua Isaka.

Kwa nini Ibrahim alimfukuza Hajiri na Ishmael huku akijua mtoto wa kwanza ndiye mrithi?
 
"The Sacrifice Of Abraham" The Sacrifice Of Abraham

Quran haisemi pia mtume alizaliwa lini na wapi,sababu siyo muhimu
 
Umeuliza swali zuri Sana na ambalo ndilo kiini cha hiyo Sadaka na dhabihu.

Urithi unaozungumziwa hapa ni ile ahadi ya Mungu kwa Ibrahim iliyomfanya amtoe Uhuru wa ukaldayo mpaka Hapo Kanaani.
Haiitwi Uhuru wa wakaldayo inaitwa Uru wa wakaldayo au Ur of Chaldeans..
Hilo la kwanza..

unahisi Ishamael hakuwa na Nchi aliyopewa?
Ishmael aliishi Parani akiwinda Huko..
Hizo ahadi zote ulizotaja Ni ahadi sawa na alizoahidiwa Ishmael

Haya tusome mwanzo 17:20


kwa lugha ya Anko charles Pale Uk

Mwanzo 17:20

"And as for Ishmael, I have heard thee: Behold, I have blessed him, and will make him fruitful, and will multiply him exceedingly; twelve princes shall he beget, and I will make him a great nation."


Kwanza Mungu amesema
  • Amembariki (Blessed Him)
  • Amemzidisha (Make Him fruitful)
  • Atamzidisha Uzao wake (Multiply Him Exceddingly)
  • Atazaa watawala 12 (12 Prince)
  • Naye atamfanya Awe Taifa kuu..

Hoja zako Nchi ya Kanaani
Isaka Alipewa kanaani ila Ishamael alipewa Beersheba, na Parani

We unahisi kwanini Watoto wengine wa Ibrahimu Hawatajwi sana au hawatajwi kabisa Kwa sababu waliobarikiwa Na kupewa Urithi ni wawili tu..

Ketura MKEWE MWINGINE WA IBRAHIMU ALIKUWA NA WATOTO 6 Ila sijaona mkiwajadili wengine wala hawajawahi kujadiliwa kabisa..


Kingine kuhusu Kwamba Isaka ni maarufu kuliko Ishmael...

kwa mfano nikikupa nafasi uandike Historia Ya ukoo wenu Je Utaweza kuniandikia Historia ya Kaka Yake na Babu yako?

waandishi wa Biblia wote ni Waebrani ana Wayahudi wote wametoka kwenye Uzao wa Watoto 12 wa Yakobo mtoto wa Isaka na ndo maana Hata Historia ya Esau (Edomu) pia huwezi kuipata..
 

Kwa hiyo mtu akisema Ishmael aliishi Dar es salaam na akataka kutolewa kafara na Babake Ibrahim Quran haina Mamlaka wala ushahidi wa kupinga hilo?

Unajua muongozo ni pamoja m biography?
Kujua ni kwa nini Mungu alimtumia fulani, wapi, wakati gani.

Quran sio biography Kwa sababu imeandikwa wa wakati mmoja yaani zama moja. Hivyo haina full details za nyakati zilizopita.
 
Mimi nimeshangaa sana kusikia Hivyo maana Kuna aya Zaidi ya 10 zikimtaja Ismili na kuna moja illnataka kuhusu dua yake nimesahau ilipo nilikunbuka nitaileta..
Faiza kiukweli Anateleza
 
Quran sio kitabu cha Historia ni kitabu kama chenye mashairi kama Unapozungumzia Zaburi au Mithali au Muhubiri..
Hivyo ni vigumu kuwa na Hadithi au Story ya mambo..
 
Maandiko yenu yenyewe ndo yanasema Sara alikasirika kwa kuwa alimuona Ismail anamfanyia dhihaka Isaac ndo akaamuru wafukuzwe, sasa historia ipi hiyo inayoenda kinyume na maandiko yenu?
Maandiko yetu tena? Si Musa huyo ndiyo aliripoti
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…