Japo Wakristo na Waislamu ni Watoto wa Baba Mmoja, Nabii Ibrahim na Mungu ni Mmoja, Kati ya Ismail na Isaka ni nani aliyetolewa Sadaka ya Kuchinja?

Japo Wakristo na Waislamu ni Watoto wa Baba Mmoja, Nabii Ibrahim na Mungu ni Mmoja, Kati ya Ismail na Isaka ni nani aliyetolewa Sadaka ya Kuchinja?

Nilikuambia mapema QUR'AN siyo biography,ndiyo maana bible ni tabu kubwa la story za watu wakati QUR'AN imeja tawhiid,sheria na maelekezo,ni muongozo siyo kitabu Cha story

Sio kitabu cha stori wakati zipo stori humo ndani ya Quran.
Unataka kusema Jambo gani?

Kwenye Quran Kuna stori nyingi sana na unazijua.
Kusema sio kitabu cha stori za watu wakati zipo baadhi ya stori hoja yako inapoteza nguvu
 
Biblia inasema Isaka alipozaliwa
Ismael na mama yake walifukuzwa hapo nyumbani kwa Ibrahimu kwenda Jangwani
Hapakua na amani baada ya Isaka kuzaliwa hivyo familia hiyo ilitengana
Akabaki Isaka na Sara na Ibrahim
Isaka akakua ndo badae likaja jaribu la mtoto kuchinjwa
Hapo Ismail na mamaye kitambo washapewa chemchem ya Zamzam jangwani huko
Tafadhali fanya hesabu,..kisha rudia tena je Biblia haijaweka wazi umri wa Ibrahim baina ya watoto wake wawili.?

According to the Bible:

1. When Ismail was born Ibrahim (Abraham) was 86 years old when Ismail (Ishmael) was born. This is mentioned in Genesis 16:16: "Abram was eighty-six years old when Hagar bore Ishmael to Abram."

2. When Isaac was born: Ibrahim (Abraham) was 100 years old when Isaac was born. This is mentioned in Genesis 21:5: "Abraham was a hundred years old when his son Isaac was born to him."
 
Nimeona hayo ni mawazo yake,..cha msingi ni kuweka hoja zenye mantiki ili athibitishe madai yake..

Kwa mfano,.. muulize Je, Isihaka ashawahi kuwa mtoto wa pekee wa Ibrahim?

Na, Je, Kati ya Ismail na Isihaka yupi alipitia kipindi ambacho alikua ndiyo mtoto pekee wa Ibrahim?

Hizo ndiyo hoja za msingi.
Kama unataka kurefer Biblia huku inawataja wote kwa marefu na mapana hakuna mkanganyiko
 
Sio kitabu cha stori wakati zipo stori humo ndani ya Quran.
Unataka kusema Jambo gani?

Kwenye Quran Kuna stori nyingi sana na unazijua.
Kusema sio kitabu cha stori za watu wakati zipo baadhi ya stori hoja yako inapoteza nguvu
يَغْفِرْ لَكُمْ مِنْ ذُنُوبِكُمْ وَيُؤَخِّرْكُمْ إِلَىٰ أَجَلٍ مُسَمًّى ۚ إِنَّ أَجَلَ اللَّهِ إِذَا جَاءَ لَا يُؤَخَّرُ ۖ لَوْ كُنْتُمْ تَعْلَمُونَ
Atakughufirieni madhambi yenu, na atakuakhirisheni mpaka muda ulio wekwa. Hakika muda wa Mwenyezi Mungu utapo fika haucheleweshwi. Laiti mngejua!

Msome nuhu kwenye QUR'AN upate kumjua,surah nzima ya 71 amepewa yeye,we umemgeuza kuwa fundi mitumbwi,heshimu manabii na ujuvi wako
 
Hilo jina Isaka hapo limepachikwa Kwa kulazimishwa
Isaka hajawahi kuwa mtoto wa pekee Kwa Ibrahim Kwa sababu yeye ni mtoto wa pili

Ila Ishmael ndio aliwahi kuwa mtoto wa pekee Kwa Ibrahim

Wakati Isaka hajazaliwa Ishmael ndio alikuwa mtoto wa pekee Kwa Ibrahim

Nyinyi wagalatia mmedanganywa sana na Wazungu
Wazungu walipelekewa injili kama sisi Afrika tulivoletewa, ni ignorance kusema wazungu wametudanganya.

Hii ndio ideology nambie kama nimekosea, uko radhi usiamini early literatures zilizoandika matukio ya Ibrahim, literature zilizoandikwa na uzao wake(Mussa) lakini ni sawa kwako kuamini late literatures ambazo zimekuja takribani miaka 2000 baada ya matukio ya Ibrahim, does that make sense??

Uko radhi kuamini maneno ya Muhammad aliyekuja miaka 600 baada ya yesu kuliko eye witnesses kama Mathayo, Yohana na Petro waliomwona yesu, wakatembea nae, wakaishi nae na wakaandika waliyoshuhudia lakini hapana bora umwamwini Muhammad ambaye hakumwona wala hakuzaliwa in the same era as Jesus Christ, unaamini maneno yake zaidi ya eye witnesses??
Help me understand your ideology....kwasababu mfano nikitaka kujua mambo kuhusu Nyerere, je, nitatafuta kitabu alichoandika mtu aliyezaliwa mwaka 2005 au nitatafuta vitabu walivoandika watu waliokuwa karibu nae, waliomwona na kumsikia, waliomshuhudia akipambania uhuru, nadhani jibu utakuwa nalo.

Haihitaji IQ kubwa sana kuchanganua mambo ya dini, inahitaji uelewa tuu wa kawaida kama niliokupa.

Pascal Mayalla
 
Kwanza mimi sijasoma theology. Nasoma biblia kujifunza tu.

Documentary Hypothesis
nimeiosoma ila ni mawazo ya wanadamu tu hasa wanatheology wanaotumia hekima za kibidamu yenye kikomo, ndio maana kuna mambo mengi watu wameyatambua mpaka kwenye ujio wa Yesu alipokuja. D hypothesis kama ni kwel basi biblia yote haina maana ni story za kusadikika.

Ukiangalia matukio ya Mwanzo 12;12-20, 20:1-8, 26:6-10 ni tofauti kabisa japo yanafanani. Ila ni Mungu ndio aliyefanya kwasabab hawezi kuchanganya uzao wake na wanadamu ndio maana kila wakati alikua anazui hichi kitu. Soma Mwanzo 6.

Twende kwenye maswali yako.

Beersheba inaanza kuonekana kwenye Mwanzo 21:14 kuwa palikua na jangwa la Beersheba Ibrahimu na Ismael walipita tu kwenye jangwa hili. Mwanzo 21: 21 inaonesha Ibrahimu na Ismael alilipita jangwa la Beersheba akenda mpaka jangwa la parani ambapo Ismael aliishi parani.

Kwaio hapa tuna miji mitatu Hebron, Beersheba na parani utasoma hizi sehem tatu vizur.

Mwanzo 21;22 Abimeleki baada ya kuona Ibrahimu amemsogelea kwa kuogopa yaliomtokea miaka ya nyuma kwenye Mwanzo 20. Ndio maan alikuja kutafta mapatano na Ibrahimu. Ibrahimu alikua anashuka kusini kwasabb ya njaa kali na kusini palikua kuna hauweni ya malisho kwa ajiri ya mifugo yake. Mwanzo 26:1.

Mwanzo 22:19 baada ya jaribu la kumtoa isaka kafara. Ibrahimu alirudi mpaka Beersheba, inaonesha makazi ya Ibrahimu na Isaka ilikua ni Beersheba kama Mwanzo 21:34. Inayosema Ibrahim alikaa na wafilisti miaka mingi kabla ya jaribu la kumtoa kafara Isaka.

Hata ukisoma Mwanzo 28:10 na Mwanzo 46:5 yote yanaonesha Beersheba waliishi Ibrahimu na Isaka. Maana ibrahim, isaka na yakobo wote waliishi hapo kama Mungu anavyojitambulisha.

Hapa nakujibu swali la umri wa isaka wakati wa kutolewa kafara hakuwa mchanga. Kama unabisa lete ushaidi wa maandiko. Kama utatumia Qur'an pia itakua vizur

Kulingana archiological research Parani ni Eneo kati ya Sinai na Mashariki ya mto Jordan

Bersheba ni Eneo karibu na Negev desert Hadi Leo Israel wana Mji unaitwa Ber sheva

Ibrahim alikuwa na Kuzikwa Hebron (Waislam na Wayahudi wanakubaliana na hili).

Kulingana na Tamaduni za Kiyahudi Jiwe linalosemekana Isaka alilala ili atolewe Sadaka liko Yerusalem kwenye Al-Aska Mosque ni kweli bila Shaka lile Jengo lililoko Yerusalem lenye paa la Dhahabu nimefunika Jiwe(Yes ni Jiwe, Jengo zima lote linatunza Jiwe)

Kwa Logic na vielelezo hivi ya kihistoria bila Shaka Hadithi za Wayahudi zina mantiki na zinaaminika kuliko za Waislam.
 
Umri huo hauhusiani na Kafara isipokuwa tohara.
Ishmael alifanyiwa tohara akiwa na miaka 13 kwenda kumi na nne. Ibrahim akiwa na miaka 100, Isaka akiwa na siku nane.

Sio tukio la Kafara
Lakini pia kumbuka baada ya Isihaka kuzaliwa....ile condition ya " Mtoto wa pekee wa Ibrahim" inakua haipo tena kwa kuwa tayari Ismail alikuepo kabla....hii unaiteteaje?
 
Sio kitabu cha stori wakati zipo stori humo ndani ya Quran.
Unataka kusema Jambo gani?

Kwenye Quran Kuna stori nyingi sana na unazijua.
Kusema sio kitabu cha stori za watu wakati zipo baadhi ya stori hoja yako inapoteza nguvu
Kwa ufupi ili kuweka mambo sawa,maana wayahudi na wakiristo pale Makkah na Madina walikua wakimzulia Mungu na manabii wake uwongo,Ila siyo priority ya Quran kuelezea historia,na walikua wakimjaribu ikiwa kweli ni mtume wa Mungu je atayajua ya kale!?
 
Tafadhali fanya hesabu,..kisha rudia tena je Biblia haijaweka wazi umri wa Ibrahim baina ya watoto wake wawili.?

According to the Bible:

1. When Ismail was born Ibrahim (Abraham) was 86 years old when Ismail (Ishmael) was born. This is mentioned in Genesis 16:16: "Abram was eighty-six years old when Hagar bore Ishmael to Abram."

2. When Isaac was born: Ibrahim (Abraham) was 100 years old when Isaac was born. This is mentioned in Genesis 21:5: "Abraham was a hundred years old when his son Isaac was born to him."
IMG_7303.jpeg

Hii ni Biblia
Mwanzo 22
Huku mambo yako bayana kama movie
Mtoto wa jaribio la kuchinjwa ni Isaka sio Ismael
 
Lakini pia kumbuka baada ya Isihaka kuzaliwa....ile condition ya " Mtoto wa pekee wa Ibrahim" inakua haipo tena kwa kuwa tayari Ismail alikuepo kabla....hii unaiteteaje?
Ismail alifukuzwa na mamaye Hajir kwenda Jangwani
Biblia iko bayana
Hivyo mtoto pekee anabaki kuwa Isaka

Kwani chemchem ya Zamzam Ismail na Mamaye waliivumbua wakati gani? Hadi leo hii mnaenda Hijja ipo
 
Wala hakuna JIna la Ismael katika biblia
Kwenye Qur'an lipo lakini sifahamu kwanini watafsiri wamelihusisha kuwa ni mtoto wa Nabii Ibrahim.

Jina Sarah hakuna kwenye Qur'an pia sifahamu kwanini watafsiri wa Qur'an wamepiga porojo na kulihusisha na kisa cha Nabii Ibrahim cha kwenye Qur'an, wakati halipo kabisa jina Sarah kwenye Qur'an.
 
يَغْفِرْ لَكُمْ مِنْ ذُنُوبِكُمْ وَيُؤَخِّرْكُمْ إِلَىٰ أَجَلٍ مُسَمًّى ۚ إِنَّ أَجَلَ اللَّهِ إِذَا جَاءَ لَا يُؤَخَّرُ ۖ لَوْ كُنْتُمْ تَعْلَمُونَ
Atakughufirieni madhambi yenu, na atakuakhirisheni mpaka muda ulio wekwa. Hakika muda wa Mwenyezi Mungu utapo fika haucheleweshwi. Laiti mngejua!

Msome nuhu kwenye QUR'AN upate kumjua,surah nzima ya 71 amepewa yeye,we umemgeuza kuwa fundi mitumbwi,heshimu manabii na ujuvi wako

Biblia imempa sura kama tano hivi.
Ila lengo kuu ni kujenga Safina na kuokoa kizazi chake full stop.

Nuhu hana dini na hajawahi kuwa na Dini.

Mpango wa dini ulianza baada ya watu kuanza kuabudu Sanamu kama miungu. Ndio Mungu akamteua Ibrahim kuanzisha Dini.

Sijui kama unaelewa mambo haya.
 
View attachment 3021844
Hii ni Biblia
Mwanzo 22
Huku mambo yako bayana kama movie
Mtoto wa jaribio la kuchinjwa ni Isaka sio Ismael
Lete facts,....hapo inaonyesha kama unafanya ushabiki kitu ambacho hakiwezi kutupa ukweli....

Kumbuka hiyo Biblia kuna sehemu inasema Mungu alipigana mieleka na Yakobo,..Mungu akapigwa.
 
Biblia imempa sura kama tano hivi.
Ila lengo kuu ni kujenga Safina na kuokoa kizazi chake full stop.

Nuhu hana dini na hajawahi kuwa na Dini.

Mpango wa dini ulianza baada ya watu kuanza kuabudu Sanamu kama miungu. Ndio Mungu akamteua Ibrahim kuanzisha Dini.

Sijui kama unaelewa mambo haya.
Biblia Haina sura,we mbona hupenda kubishabisha tu!!?..biblia vifungu na mistari
 
Kwa ufupi ili kuweka mambo sawa,maana wayahudi na wakiristo pale Makkah na Madina walikua wakimzulia Mungu na manabii wake uwongo,Ila siyo priority ya Quran kuelezea historia,na walikua wakimjaribu ikiwa kweli ni mtume wa Mungu je atayajua ya kale!?

Mbona hizo stori za Quran nyingi zinauongo mwingi na hazina detail za muhimu.
Ndio maana hata nikikuuliza hapa Ishmael alitaka kutolewa Kafara wapo hautanijibu.

Au Issa Alizaliwa mji gani hutonijibu.
 
Back
Top Bottom