Japo Wakristo na Waislamu ni Watoto wa Baba Mmoja, Nabii Ibrahim na Mungu ni Mmoja, Kati ya Ismail na Isaka ni nani aliyetolewa Sadaka ya Kuchinja?

Japo Wakristo na Waislamu ni Watoto wa Baba Mmoja, Nabii Ibrahim na Mungu ni Mmoja, Kati ya Ismail na Isaka ni nani aliyetolewa Sadaka ya Kuchinja?

Kwani Nyie huwa hamsomi Biblia au Mnaongozwa na Chuki..
Hebu someni Mwanzo 16:3 halafu Ichambue bila chuki Au mnataka mpaka tulete Hebrew Version of it tuichambue

Hakuna anayeongozwa na chuki Mkuu.

Hiyo aya ya tatu endelea ya nne.
Mwanzo 16:4
[4]Basi akamwingilia Hajiri, naye akapata mimba. Naye alipoona ya kwamba amepata mimba, bibi yake alikuwa duni machoni pake.
And he went in unto Hagar, and she conceived: and when she saw that she had conceived, her mistress was despised in her eyes.

Alafu nenda sura ya 21.
Biblia haimtambui Hajiri kama mke wa Ibrahim.
Kuruhusiwa kulala naye ndicho kinachorejelea neno ili awe mkewe. Yaani ili alale naye, amuingilie.

Lakini haina maana kuwa Sarah na Hajiri watageuka kuwa katika level moja ya Uke wenza.

Ndio maana aya ya 21 Ibrahim maelezo yake hayamtambui Hajiri kama mkewe Bali kama kijakazi wa Sarah.

Ukishaoa mke wa pili au watatu wake wote wanakuwa sawa.
 
Wanabodi,
Leo ni sikukuu ya Eid El Haji, Iddi ya Kuchinja.

Leo ni siku ya Sikukuu ya Idd El Haj, ni iddi ya kuchinja, asubuhi nilikuwa naangalia matangazo ya mubashara ya Baraza la Iddi kupitia TBC, kutoka Msikiti wa Mfalme Mohammed VI wa Morroco, Bwakwata, Kinondoni jijini Dar es Salaam, kumbe Msikiti Mkuu wa Bakwata, sasa umebadilishwa jina!, na kupewa jina la Mfalme wa Morroco!.

Mgeni rasmi kwenye Baraza la Iddi ni Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa, ambaye ameandamana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, ambaye amesilimishwa na kupewa jina la Aboubakar Chalamila!, na mawaziri akiwemo Waziri Mhe. Mohamed Mchengerwa. Baadhi ya watu maarufu niliowaona ni pamoja na Alhaj Sheikh Ali Nguruko, Alhaj Chande, Idda Azan, Shaweji Abdalah, Salum Mwalimu, Juma Simba Gadafi, Salum Abladaha "TRY Again", Katibu Mkuu wa Bakwata, Sheikh Mruma, Kadhi wa Dar es Salaam, Shamin Khan, mwenyekiti wa JUAKITA, pia kulikuwa na mabalozi wa Balozi wa Moroko, na wa Comoro.

Katika salam zake, Sheikh Aboubakar Chalamila alisema utulivu wa jiji la Dar es Salaam, unawategemea sana viongozi wa Dini.

Salaam za Waislamu, zimetolewa na Alhaj Sheikh Nuru Mruma, Katibu Mkuu wa Bakwata ambaye amewasisitiza Waislamu kudumisha amani na kuilinda amani. Wazazi watakiwa kulea watoto wao kwa tabia njema, kujenga taifa la kizazi cha watu wema ambao hawatapokea rushwa wala kufanya ufisadi.

Amesema kupanda miti na utunzaji wa mazingira ni ibada muhimu kwa Waismamu wote.

Pia amewataka Waislamu kujitokeza kwa wingi, kujiandikisha kwenye uboreshaji daftari la kudumu la wapiga kura.
na wametakiwa kujitokeza kwa wingi kutumia haki yao ya kidemokrasia kugombea nafasi mbalimbali za uongozi.

Salaam za Mufti, zimetolewa na Kaimu Mufti Sheikh Ali Muhidin Mporogore, Mjumbe wa Baraza la Maulamaa wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania, Bwakwata. Aamezungumzia Watanzania tutafakari, sadaka ya kuchinja siku ya Iddi El Haj, ni iddi ya kuchinja. Zamani ilikuwa sio kuchinja tuu wanyama, bali walichinja hata binadamu ana akatolea mfano Sadaka ya Nabii Ibrahim kutaka kumtoa mwanae Ismail, kwa sadaka ya kuchinja.

Hakuna ubishi kuhusu Wakristo na Waislamu, kuwa ni watoto wa Baba mmoja, Nabii Ibrahim hivyo huu ni uthibitisho wa Mungu wa Wakristo na Waislamu ni Mungu Mmoja, na sheria za dini hizi zote mbili Wakristu na Waislamu, ni sheria moja ile ile ya Musa, ila kuna watu wanafundishwa ukweli na kuna watu wanadanganywa!.

Hakuna ubishi kuwa mtoto wa kwanza wa Ibrahim ni Ismail aliyezaa na mjakazi wa Kimisri, Hagir, na Isaka ni mtoto wa pili wa Ibrahim, aliyemzaa na mkewe Sarah.

Hakuna ubishi Ibrahim alitaka kumtoa mtoto wake Sadaka ya kuchinja.

Waislamu na Kitabu chao Kitukufu cha Quran Tukufu, kinamtaja mtoto huyo aliyetaka kutolewa sadaka ya kuchinja ni Ismail.
Wakristo na Kitabu chao Kitakatifu cha Biblia Takatifu, kinamtaja mtoto huyo aliyetaka kutolewa sadaka ya kuchinja ni Isaka.

Jee ukweli halisi ni upi?.
Hii maana yake
Kama tukio la Ibrahim kutaka kumchinja mwanae kumtoa sadaka ni tukio moja, then
1. Hii maana yake ni kuna watu wanadanganywa, haiwezekani kwa Waislamu mtoto huyo awe ni Ismail na kwa Wakristu mtoto huyo awe ni Isaka, hii maana yake kuna kitabu hapo kinasema kweli na kuna kitabu kinasema uongo!, jee ukweli ni upi?.

Umuhimu wa kuujua ukweli huu, unakupa fursa ya kujua ukweli ni upi, hivyo ufuate mafundisho yapi ambayo ndio mafundisho ya kweli!.

Bandiko hili linakutaka kwanza uwe open minded, kama wewe ni mfia dini, unaamini dini yako ni ya ukweli mtupu, bandiko hili halikufai.

Pili unatakiwa uwe na ngozi ngumu ya kuukubali ukweli halisi hata uwe mchungu vipi!, ikitokea ni dini yako unayoiamini kuwa ni dini ya kweli, kumbe ni dini ya uongo, uwe na uwezo wa kustahimili maana...

Nawatakia Waislamu wote,
Iddi Mubarak njema ya kuchinja.

Paskal
Je, kanuni ya Mungu ya kutoa sadaka(mrithi) kwa kipindi hicho ilikuwa ni mtoto mwenye haki zipi?

Tukilijadili hili litatupa mwanga kidogo.
 
Habari Ammoshi!
Ibrahimu alimuoa Hajiri na alikuwa Mke wake wa Ndoa (Mwanzo 16:3)..

Ibrahimu Alimbariki na Kuomba Baraka kwa Mungu Naye Mungu akamsikia na kumbariki Ishamael soma Mwanzo 21..

Maagano kipindi Yanatoka Ibrahimu alikuwa na Miaka 99 na Ishmael alikuwa na miaka 13 Hivyo alitahiriwa na familia yake yote na hilo ndilo agano la.kwanza..

Kuhusu kutafutiwa Mke Unajisahau kabisa kwamba Isaka alikuwa Uzao wa Nadhiri Na Ishmael alikuwa uzao wa Mwili???

Wagalatia 4:28-29

"Basi, ndugu zangu, kama Isaka sisi tu watoto wa ahadi.
Lakini kama vile siku zile yule aliyezaliwa kwa mwili alivyomwudhi yule aliyezaliwa kwa Roho, ndivyo ilivyo na sasa."

Wazao wa Nadhiri wote Hutafutiwa Mke ndani ya Ukoo Na ulinzi wa Baba zao..(Fuatilia Kisa Cha Esau (Edomu) na Yakobo)

Kuhusu Urithi na kuwa Pamoja Je Hukusoma Kuwa Isaka na Ishmaeli walimzika Baba Yao alipofariki akiwa na Miaka 175??
‭Wagalatia 4:30 SRUV‬
[30] Lakini lasemaje andiko? Mfukuze mjakazi na mwanawe, kwa maana mwana wa mjakazi hatarithi kabisa pamoja na mwana wa muungwana.
 
Hapa Nakuunga Mkono kwa 95% Uko sawa kabisa..
ILa Ibrahimu Hakuwa Myahudi 🤣..

alikuwa Anamfata Mungu wa Babu zake Yaani Unajua kwa Ibrahimu Ndo Ucha Mungu wa Imani ndo ulipoanzia hasa kwa hyo yeye Ndo alijitenga Na Watu wa nyumbani na kumtegemea Mungu..

Kipindi Hicho Yehuda (Yuda hajazaliwa)

Yeah ni kweli
Hata Biblia yenyewe neno wayahudi limeanza kutumika baadaye sana.
 

Attachments

  • Screenshot_20240621_113317_Samsung Internet.jpg
    Screenshot_20240621_113317_Samsung Internet.jpg
    359.8 KB · Views: 7
Naomba usichanganye vitu viwili
1. Being - yaani uwepo wa Mungu mmoja ambaye ndie alimuumba binadamu hadi Nabii Ibrahim

2. Nabii Ibrahim akapata watoto wawili, wa kwanza ni Ishmael/Ismail aliyemzaa na mjakazi wa Kimisri. Hagir na wa pili ni Izaka/Ishaq aliyezaa na mkwe Sarah uzeeni.

3. Ukoo wa Ishaq ndio alizaliwa Mtume na Uislam. Ukoo wa Izaka ndio alizaliwa Yesu Kristo wa Wakristo.

Hivyo Wakristo na Waislamu ni watoto wa Baba mmoja, na Mungu mmoja. Hili halina ubishi!.

Sasa tukija kwa Wakristo kuamini the holy trinity, hayo ni yao and they have nothing to do with God!. Wao kuamini Mungu ana nafsi tatu, Mungu Baba, Mungu Mwana na Roho Mtakatifu, hizi ni derivation za Ukiristo hazimfanyi Mungu asiwe Mungu,

Wala Wakristo kutomuamini Mtume Mohamed (SAW) hakumfanyi asiwe Mtume!.

Mungu ni mmoja, anaitwa kwa jina lolote, Allah, Mungu, Mulungu, Almighty, Supreme Being, Aire, Yahwe, etc, it doesn't matter, ni Mungu yule yule.

Hata waumimi walioaminishwa yuko juu mbinguni, mawinguni, peponi, ahera, ni imani tuu, lakini Mungu wa kweli ni Omnipresence yuko kote akiwemo ndani yetu!.
P
Correction Ibrahimu Alikuwa na Watoto Nane..
6 kwa mkewe Ketura ,1 kwa mkewe Hajiri na 1 kutoks kwa mkewe Sara (Mtoto wa ahadi)
 
Naomba usichanganye vitu viwili
1. Being - yaani uwepo wa Mungu mmoja ambaye ndie alimuumba binadamu hadi Nabii Ibrahim

2. Nabii Ibrahim akapata watoto wawili, wa kwanza ni Ishmael/Ismail aliyemzaa na mjakazi wa Kimisri. Hagir na wa pili ni Izaka/Ishaq aliyezaa na mkwe Sarah uzeeni.

3. Ukoo wa Ishaq ndio alizaliwa Mtume na Uislam. Ukoo wa Izaka ndio alizaliwa Yesu Kristo wa Wakristo.

Hivyo Wakristo na Waislamu ni watoto wa Baba mmoja, na Mungu mmoja. Hili halina ubishi!.

Sasa tukija kwa Wakristo kuamini the holy trinity, hayo ni yao and they have nothing to do with God!. Wao kuamini Mungu ana nafsi tatu, Mungu Baba, Mungu Mwana na Roho Mtakatifu, hizi ni derivation za Ukiristo hazimfanyi Mungu asiwe Mungu,

Wala Wakristo kutomuamini Mtume Mohamed (SAW) hakumfanyi asiwe Mtume!.

Mungu ni mmoja, anaitwa kwa jina lolote, Allah, Mungu, Mulungu, Almighty, Supreme Being, Aire, Yahwe, etc, it doesn't matter, ni Mungu yule yule.

Hata waumimi walioaminishwa yuko juu mbinguni, mawinguni, peponi, ahera, ni imani tuu, lakini Mungu wa kweli ni Omnipresence yuko kote akiwemo ndani yetu!.
P
Naona wewe unachanganya mada mbili au zaidi pamoja.

Kuhusu Ismail na Sarah na Ibrahim, hilo sijawahi kuliona popote kwenye Qur'an.

Hilo la "mungu", Uislam upo wazi kabisa "Hakuna Mungu isipokuwa Allah.
 
Mkuu toriyama , asante sana kutuletea hii family tree ya Mtume
View attachment 3021896
Kuna vitu they look a bit strange to me!, alioa wake 12, kati ya hao wake 12, ni wake wawili tuu ndio waliojaaliwa kumzalia watoto, Mke Mkubwa au mke wa kwanza Bi Khadija aliyemzalia binti UmKuluthum na vidume wawili Abdullah na Kasim, kisha mke wa mwisho wa 12, Bi. Marriah aliyemzalia kidume Ibrahim, lakini wake wengine hao wote 10, hakuna aliyebahatika kupata mtoto?!, hii naiona kama a bit strange!, kwasababu kwa mujibu wa hadhithi, alikuwa ni mtu wa kazi kweli kweli!. Nadhani hii family tree haiko sawa.

Kwenye hiyo family tree, kumeonyesha mabinti wengine watatu, Zainab, Rhukaya na Fatma, bila kuonyesha mama zao ni nani!, ina maana...
Hawa wote walikuwa watoto wa hadija zainab l, Rhka..na Fatma
Ila kitu strange zaidi ni ukoo huendelezwa kwa watoto wa kiume ambao ndio damu yako, hii family tree inaonyesha hao watoto wote watatu wa kiume, hakuna aliyewahi kuoa wala kupata mtoto ili kuendeza damu ya ukoo, hao wajukuu wote ni wajukuu wa watoto wa kike, sio damu ya ukoo!. Kwangu mimi hii haijakaa sawa, nadhani hii family tree is not right, I serious doubt if this is true unless nithibitishiwe humu na wanazuoni wetu wa humu jf kuwa hiyo family tree is true.

P
Kwa bahati mbaya Watoto wa kiume wa Mtume walifariki wakiwa wadogo
 
Edom ni Jumuisha eneo zima lilivokuja kuitwa miaka michache baadae
Edom imevumbuliwa na Edom mwenyewe Yaani Esau..

Alipokimbia Kwenda Nchi hiyo yeye ndio aliianzisha na Yeye ndo baba wa WaEdom wote hakuna Edom bila Esau..

Mwanzo 25:30

"Esau akamwambia Yakobo, Tafadhali, unipe hicho chakula chekundu nile, kwa kuwa ninazimia mimi. Kwa hiyo wakamwita jina lake Edomu."

unaweza ukasoma pia

Mwanzo 36:8-9

Esau akakaa katika mlima Seiri, Esau ndiye Edomu. Hivi ni vizazi vya Esau, baba ya Edomu yote katika mlima Seiri.

"And these are the generations of Esau the father of the Edomites in mount Seir:"



Nakuongeza Fungu moja..

Mwanzo 36:19

"Hao ni wana wa Esau, na hao ndio majumbe wao; naye Esau ndiye Edomu."
 
Hakuna anayeongozwa na chuki Mkuu.

Hiyo aya ya tatu endelea ya nne.
Mwanzo 16:4
[4]Basi akamwingilia Hajiri, naye akapata mimba. Naye alipoona ya kwamba amepata mimba, bibi yake alikuwa duni machoni pake.
And he went in unto Hagar, and she conceived: and when she saw that she had conceived, her mistress was despised in her eyes.

Alafu nenda sura ya 21.
Biblia haimtambui Hajiri kama mke wa Ibrahim.
Kuruhusiwa kulala naye ndicho kinachorejelea neno ili awe mkewe. Yaani ili alale naye, amuingilie.

Lakini haina maana kuwa Sarah na Hajiri watageuka kuwa katika level moja ya Uke wenza.

Ndio maana aya ya 21 Ibrahim maelezo yake hayamtambui Hajiri kama mkewe Bali kama kijakazi wa Sarah.

Ukishaoa mke wa pili au watatu wake wote wanakuwa sawa.
Swali linakuja kwanini unaichukua Aya ya 3 mpaka uiruke na kwanini unabagua aya..

Unataka Niamini maneno ya Yesu alipowaambia Walimu na Mafarisayo..

Kuwa wanachuja Mbu na Kumeza Ngamia????
Yaani wanachukua baadhi ya Mafundisho na mengine kuyaacha (Yale yasiyoyapenda?)

Namimi Nakuuliza EWE Mtibeli KWANINI UNACHUJA MBU N KUMEZA NGAMIA???

Mathayo 23:23-25

Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnalipa zaka za mnanaa na bizari na jira, lakini mmeacha mambo makuu ya sheria, yaani, adili, na rehema, na imani; hayo imewapasa kuyafanya, wala yale mengine msiyaache.

Viongozi vipofu, wenye kuchuja mbu na kumeza ngamia.

Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnasafisha nje ya kikombe na chano, na ndani yake vimejaa unyang’anyi na kutokuwa na kiasi.
 
‭Wagalatia 4:30 SRUV‬
[30] Lakini lasemaje andiko? Mfukuze mjakazi na mwanawe, kwa maana mwana wa mjakazi hatarithi kabisa pamoja na mwana wa muungwana.
Unatoaje Authentification ya Tukio lililokwisha Kuwa Completed Kwenye Agano LA Kale ukatafute maelezo yake kwenye Agano jipya..

Unahisi Paulo ana majibu Ya yaliyotokea Kipindi cha Ibrahimu??
Unahisi Maelzo ya Musa hayatoshi kukupa Majibu
 
Kwa misingi ipi arabuni ni saudia pekee!?..saudia ya mwaka/mipaka gani?
Iraq ilikuwa Mesopatamia, Misri iliitwa misri hivyo hivyo wakati huo Irani imeanza kuwa Arabuni miaka ya karne ya 18..

Sasa sjui Kama unaijua Historia vzuri kuwa..
Wana historia wanaporefer Arabuni Humaanisha Macca na medina au Saudia peke yake
 
Unatoaje Authentification ya Tukio lililokwisha Kuwa Completed Kwenye Agano LA Kale ukatafute maelezo yake kwenye Agano jipya..

Unahisi Paulo ana majibu Ya yaliyotokea Kipindi cha Ibrahimu??
Unahisi Maelzo ya Musa hayatoshi kukupa Majibu
Biblia inajikamilisha kuanzia agano la kale na jipya , ndo maana kitabu cha Isaya kimeongelea maisha ya Yesu Kristo before Yesu ajazaliwa kwa uweza wa Roho mtakatifu.
 
Ndio maana FaizaFoxy amesema someni maandiko yenu line by line you are now contradicting your own Quran.

Katika Quran Hajiri alifukuzwa Ishmael alipokuwa mkubwa si alipokuwa mdogo
Nakupa ya mwisho.baada ya tukio lile la kutaka kuchinjwa ismael.mungu ndo akambashiria Ibrahim kuwa atampa mtoto isihaka.
Soma kwa makini hizo AYA.
 

Attachments

  • Screenshot_20240621_120931_Chrome.jpg
    Screenshot_20240621_120931_Chrome.jpg
    433.9 KB · Views: 7
Nimesema Sina Uthibitisho wa Quran
Jikumbushe ulivyoandika "Katika Quran Hajiri alifukuzwa Ishmael alipokuwa mkubwa si alipokuwa mdogo.

Hilo "katika Qur'an" ulimaanisha nini? Kama sai uzushi? Kama hauna uthibitisho wa Qur'an usitie maneno yako au maoni ya watu binafsi kusema ni ya Qur'an au ya Kiislam.
 
Back
Top Bottom