Japo Wakristo na Waislamu ni Watoto wa Baba Mmoja, Nabii Ibrahim na Mungu ni Mmoja, Kati ya Ismail na Isaka ni nani aliyetolewa Sadaka ya Kuchinja?

Sawa vizuri,...Biblia imetaja kuhusu Bakka...Je unaweza kutusaidia ni wapi Bakka?
 
Define spirituality without religion,I can picture you were christian,unakua na moyo mzito kuvuka upande wa pili
 
Surah Al-Baqarah (Chapter 2), Verse 62:

"Indeed, those who believed and those who were Jews or Christians or Sabeans - those [among them] who believed in Allah and the Last Day and did righteousness - will have their reward with their Lord, and no fear will there be concerning them, nor will they grieve." (Qur'an 2:62)
 
Kingine Yuda Alifanya madudu na Tamari mkwewe umesahau??
Huo ndio mpango wa Mungu ili Yuda apate uzao!. Sometimes Mungu hutumia njia za ajabu sana kufanikisha mipango yake. Yuda alilaaniwaga kwa kulala na concubine wa baba yake!. Mtoto wake Eri alipomuoa Tamari, Mungu akamuua, mtoto wake wa pili Onani akatakiwa kumrithi Tamara ili amzalie Eri watoto, Onani akawa anamwaga nje, Mungu akamuua, Yuda akamrejesha Tamari kwao, kumsubiria Sheri, mtoto wa mwisho wa Yuda, akue, amuoe. Sheri alipokuwa mkubwa Tamari akarejea, Yuda hakumuoza kwa Sheri kwa kuogopa asije na yeye akafa, hivyo wakawa wana mzuga zuga tuu Tamara, Mungu pia akamuua, na mke wa Yuda pia akafa. Sasa Yuda hana mke, hana mtoto, wanaishi na Tamara tuu. Ndipo Tamara akafanya maarifa ya kike, Mzee Mzima Yuda akaingia line, Tamari akashika ujauzito na kuwazaa mapacha Peresi na Zera, hivyo ukoo ndio ukaendelea!.

Kitu kama hiki pia kilifanywa kwa mabinti wawili wa Lutu, ambao wote walikuwa sealed, baada ya Mama yao kugeuka jiwe la chumvi wakati wa kuikimbia Sodoma na Gomora, mabinti wakasemezana baba yetu amekuwa mzee na hana mtoto wa kiume kuendeleza ukoo, wamamlewesha baba yao mzazi na kulala nae kwa zamu, wote wawili wakashika ujauzito, ukoo ukaendelea!.

Hata Mfalme Daudi, alimzaa Mfalme Suleiman kupitia kwa mke wa Uria!. Hiyo ndio mipango ya Mungu!.
P
 
Define spirituality without religion,I can picture you were christian,unakua na moyo mzito kuvuka upande wa pili
Nimewahi kuwa Christian tena nilikuwa Mchungaji Nimewahi kuwa Muslim na nimewahi kuwa jewz..
Hakika katika Vyote Hivyo hakuna Upendo ni chuki iliyokithiri ndiyo hufundishwa Ndani..

Chuki Ambayo watu hudanganywa Ni Upendo..Bado nawasoma hinduism na Budha ni watu wenye Upendo wa Hali ya Juu sana Pengine kuliko Wakristo na Waislamu..

Spirituality without religion ni kama personal quest for understanding and connection with something larger than oneself ambayo Ndo Emmanuel au Mungu yaani kuamini kwamba Una Mungu ndani yako, kuamini kwamba We are All connected all creature, Kuamini kwamba Hakuna Kitu chenye thamani dhidi ya kingine..

Muhubiri 3

Yaani focuses on inner peace, harmony, na kuamini Duniani Hjaja Kwa bahati mpaka Kuwa kila kitu kinakuja On purpose na Kuamini Kila Hatua unayopiga ni funzo na Ndyo hasa Njia uliyoitwa Kuifanya Duniani...
Kuamini Kwamba Bila Upendo Sisi Ni kitu Bure..


Kuamini kwamba Vitabu vyote Vitakatifu vyafaa kwa ajili ya Kuonya katika njia ya Haki ila Tumeharibu Ujumbe wake na tunautumia Kinyume na maana zake

Kuishi maisha ya Adabu katika kila kitu hata kula
Mwisho kutafuta maana ya Kuishi...
 
Your Implication??

The day of Judgements? Ehh
Hivi unajua kuwa Wayahdi hawana Siku ya Qiyama wala siku Ambayo Kila mtu atahukumiwa??
 
Uthibitisho?
Sababu Mji wa Mecca ya Leo ni mji mpya sana.. Waarabu walikuwa wanakaa Petra/Jordan ya Leo (Bonde/Jiwe) Watu wameaanza kuishi Mecca Miaka karibu 1400 tu iliyopita.

Bekka uliyoitaja pia means Bonde/Jiwe

Waarabu walikuwa wanatamaduni kukusanyika na kufanya ibada zao kwenye mawe, kadri Miaka ilivokuwa inapitia Ndio wakaiweka Mecca ya Leo kuwa sehemu ya hijja



Hili Moja ya majengo ya aina yake yaliyojengwa Petra na Nabateans (WaNabayati) mmoja kati ya watoto wa Ishmael na Asili ya mwanzo kabisa ya Waarabu na Kiarabu unachokijua.

Hawa Ndio waanzilishi wa kuzunguka mawe na Ndio first Arabs civilization.

So ni swala la debate ya Wanazuoni kuwa Kaaba ya Wana wa Ismael ilijengwa Petra au Mecca
 
Naelewa Then kama Ni mpango wa Mungu kwanini Yuda ahukumiwe na Kulaaniwa kwa sababu hiyo?
Unahisi kuna Fair Treatment?

Na kwanini Mungu kama alitaka Yuda apate uzao asitafute Uzao kwa Wanawake wengine mpaka kwa Mke wa Mtoto wake?

Unafahamu Jinsi Yesse Alivyopatikana??
Ile story ya Naomi na Mama yake Mkwe mpaka kufikia kwa Daudi?

vItu vingi Ukivisoma Utasikitika Sana..
 
Duh,. hizo habari kwamba baraka alizopewa Ismail amepewa na Mungu tu hazikupitia kwa Baba yake ni uongo.......maana Ibrahim mwenyewe ndiyo alimuombea Ismail apewe baraka na Mungu......sasa hayo madai yako umeyatoa wapi?
Alimuombea lakini hakumuambia nakubariki wewe Ibrahim alimwambia nitambariki na yeye Kwa kua umeomba. Hakuna popote anapomwombea baraka Isaka. Anachofanya kabla ya kufa ni kumbariki. Hakumuomba Mungu ambariki Isaka ila alimuombea Ishmael Baraka kutoka kwa Mungu. Why?
 
Uko Vizuri sana Kwenye Dini na Elimu ya Dini sema unakosa kitu kidogo Tu Connection na Logical ya Kiushawishi..
Hapana bro namuomba Mungu anitakase kwa ajili yake. Dini imekua mlango wa kufunga watu wasimuendee Mungu. Wengi wanakosana na Mungu sio kwa sababu hawana uwezo wa kumpenda Mungu Bali Kwa sababu dini imekua mbele kama tanzi. Paulo aliweza kuepuka hiyo ila Petro ilibidi akomewe ili akivuke hicho kitanzi. Sitamani kinishike kabisa.
 
Yeremia anazungumzia Taifa la Yuda. Sio Yuda mtoto wa Yakobo Bali watoto wake waliounda Taifa la Yuda. Unachanganya mambo hapo.
 
Your Implication??

The day of Judgements? Ehh
Hivi unajua kuwa Wayahdi hawana Siku ya Qiyama wala siku Ambayo Kila mtu atahukumiwa??
Implication ya kuweka hiyo aya hapo ni kuonyesha kwamba as long as Mtu ameamua kuamini uwepo wa Mungu Muumba na kuishi a righteous life basi Mtu huyo atawekwa miongoni mwa wema na atalipwa kadri ya wema wake ...regardless of his religious affiliation as long as moyo wake ulijitahidi kuwa na good intentions kwenye maisha yake na akaishi hivyo.......

Kuhusu Wayahudi kutokua na day of Judgement kwenye mafundisho yao,..hiyo sio concern yangu maana wao hawana mamlaka yoyote ya kuamua whether day of Judgement iwepo ama isiwepo....Wayahudi ni watu kama walivyo watu wengine. Yaani hatuwezi kusema Qiyama hakipo kwasababu Wayahudi wanasema hakipo...La!
Sio wao peke yao zipo jamii nyingine ambazo kwenye mafundisho yao hutokuta habari kuhusa Qiyama.
 
Na Mimi kama wewe spiritual but not religious shida tu sijui upande wa pili maana wanaotumia lugha ngumu.
 
Your Implication??

The day of Judgements? Ehh
Hivi unajua kuwa Wayahdi hawana Siku ya Qiyama wala siku Ambayo Kila mtu atahukumiwa??
Kama wayahudi wanaamini kitabu cha Daniel basi wanatakiwa waamini ipo siku ya mwisho yenye hukumu. Daniel anaelezea vision ya kuona siku kiti Cha Enzi kimewekwa mbinguni na Mzee wa Siku ameketi juu yake. Alipoletwa Mwana wa Mtu akaletwa na kuwekwa mbele ya Mzee wa Siku. Naye akapewa mamlaka ya kuhukumu. Hiyo tayari ni tafsiri kwamba kuna siku ya mwisho Kwa viumbe vyote vilivyoumbwa.
 
Dini ya usilamu haimpi sana nafasi mtoto wa kike kuchimba masula ya dini na hata kuwa kiongozi wa dini. Hivyo, siyo kosa lake nyanya Feiza kutojua Qur an.
 
Hizo zako zote ni porojo.

Dhabah au Dhibihi i;liyotumika hapo inamaanisha "incision" hiyo ni tafsida ya jando.

Nenda ukaijuwe maana ya neno Dhabah na dhabih katika Lisan Al Arab cha Ibn manzour.

Unasema kichinjwacho wakati hujakioandika hicho kichinjwacho? Hakuna.

Hapo panada ushuke inabaki kuwa ni jando ytu. Watafsiri wa Kiislam walifata matamanio yao au walikuwa na agenda zao.

Jiulize, hivi Allah kweli anahitaji kafara ya damu hata aagize mtu amchinje mwanawe? Bado hujaiona "plot" iliyotumiwa na watafsiri waliopotosha.

Hakuna mtoto wala mtu mzima aliyetaka kuchinjwa na hakuna hata jina Sarah katika Qur'an mmelitowa wapi?
 
Kumbe
 
Nimekwambia kasome kuhusu "Locution" au "lexicon" ndiyo utanielewa. Nimekwambia hiyo hapo kwa Ibtrahim na Ishaka imetumika kama tafsida, lakini siyo mtu kuchinjwa kukatwa shingo.

Mfanoi ukiambiwa "serikali ina mikono mirefu" unaelewa nini? Au ukisikia mashabiuki wa mpira wakisema "alotaka kufunga akakatwa mtama" inamaanisha nini?

Ukiyaelewa hayo utaelewa maana ya "Lisan" (locution) ambayo imetajwa sana kwenye Qur'an.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…