Japo Wakristo na Waislamu ni Watoto wa Baba Mmoja, Nabii Ibrahim na Mungu ni Mmoja, Kati ya Ismail na Isaka ni nani aliyetolewa Sadaka ya Kuchinja?

Kitu usichoelewa ni kuwa, Qur'an imekuja maandiko ya zamani baaday akutiwa mikono ya watu.

Unaweza kukuta majina yanafanana lakini visa na "roles" zao ni tofauti kabisa na utazozisoma kwenye biblia.

Qur'an ni "Furqan" (criterion) iliyokuja kubainisha (Mubyin) ukweli.
 
Sawa, tupo pamoja tuendelee..
Naam, na aya hii tafadhali nijulishe umeelewa nini hapa, Qur'an 11:71:

وَٱمْرَأَتُهُۥ قَآئِمَةٌۭ فَضَحِكَتْ فَبَشَّرْنَـٰهَا بِإِسْحَـٰقَ وَمِن وَرَآءِ إِسْحَـٰقَ يَعْقُوبَ ٧١
 
Hapo ni Mke wa Ibrahim alicheka baada ya kuambiwa habari za kupata mtoto hasa akizingatia umri wake na wa Mme wake tayari ulikua ni mkubwa sana,...so alipewa bishara ya kumpata Is'haka ambapo kutokana na Isihaka akapatikana na Yakub.
 
Hapo ni Mke wa Ibrahim alicheka baada ya kuambiwa habari za kupata mtoto hasa akizingatia umri wake na wa Mme wake tayari ulikua ni mkubwa sana,...so alipewa bishara ya kumpata Is'haka ambapo kutokana na Isihaka akapatikana na Yakub.
Umeoina eeh? kabashiriwa kupatikana watoto nani na nani?

Tutaelewana tu kidogo kidogo bila kutia yetu, Qur'an ni muujiza.
 
Umeoina eeh? kabashiriwa kupatikana watoto nani na nani?

Tutaelewana tu kidogo kidogo bila kutia yetu, Qur'an ni muujiza.
Kabashiriwa Mtoto mmoja ambae ni Isihaka....ambapo kutokana na Isihaka baadae atapatikana mjukuu yaani Yakub.

Yap,.. twende taratibu majibu yatapatikana.
 
Kabashiriwa Mtoto mmoja ambae ni Isihaka....ambapo kutokana na Isihaka baadae atapatikana mjukuu yaani Yakub.

Yap,.. twende taratibu majibu yatapatikana.
Sasa unaanza kuongeza yako, haifai. Hilo la mjukuu kuwa ni Yaakoub umelitoa wapi? tafadhali Sheikh, usifate matamanio yako, fata Qur'an. Kama Allah hajakuwekea kwenye hiyo aya, usiongeze lako.

Au una aya nyingine inasema Yaakoub ni mjukuu wa Ibrahim?
 
Hapana sijaongeza yangu....bali inapaswa tutumie akili zetu vizuri kwenye kuelewa Aya husika hapo kwenye aya hilo neno (وَمِن وَرَاءِ) lipo kukuonyesha kwamba Yakub atatoka kwa Is'haka....ingekua bishara ni ya watoto wawili basi ingetumika tu herufi 'وَ' kutenganisha... ambapo ingemaanisha Mke wa Ibrahim anapewa bishara ya watoto Isihaka "na" Yakub..lakini kwenye hiyo aya haipo hivyo.

Kisha,..nikija kukuelewesha zaidi kwamba Qur'an imeweka wazi kwamba Yakub anamtambua Isihaka kama Baba yake... ilhali wewe unasema hiyo aya inaonyesha Isihaka na Yakub ni mtu na Kaka yake....

Tazama hapa chini uone Yakub anamtambua Isihaka kama nani...?👇🏼

Qur'an 2:133: "When death approached Jacob, he said to his sons, 'What will you worship after me?' They said, 'We will worship your God and the God of your fathers, Abraham and Ishmael and Isaac—one God. And we are Muslims [in submission] to Him
 
Huna sababu ya kutumia akili yako ukaiona ya maana sana kuliko maandiko ya Allah. Hilo neno halimaanishi Yaakoub kuzaliwa na Is'hak. Wacha uongo, simply linamaanisha "na nyuma yake".

Huwa sikisii, kijana, usitake kuongeza yako yasiyokuwepo, ni shirki hiyo.

Narudi chini hapo...
 
Hapo umeanza kuzuga tena, usiseme uongo, hiyo aya mbona hukuiweka? halafu umejifdai kuja na ytafsiri ya Kingereza? Ilhali ulisema unaielewa Qur'an na nikaanza kukuwekea ayat bila tadiri, tulianza vizuri sana, sasa umeona hapatoshi unaanza kuja na porojo zako.

Au huelewi Kiswahili unataka tuanze mjadala kwa Kingereza?

Hii aya uliyoweka namba zake tu, jisomee useme i[po sawa na hiyo tafsiri yako ya Kingereza: Qur'an 2:233

أَمْ كُنتُمْ شُهَدَآءَ إِذْ حَضَرَ يَعْقُوبَ ٱلْمَوْتُ إِذْ قَالَ لِبَنِيهِ مَا تَعْبُدُونَ مِنۢ بَعْدِى قَالُوا۟ نَعْبُدُ إِلَـٰهَكَ وَإِلَـٰهَ ءَابَآئِكَ إِبْرَٰهِـۧمَ وَإِسْمَـٰعِيلَ وَإِسْحَـٰقَ إِلَـٰهًۭا وَٰحِدًۭا وَنَحْنُ لَهُۥ مُسْلِمُونَ ١٣٣

Twena hapo ndiyo wazi kabisa Yaakoub anaambiwa na wanawe kuhusu baba'ke ambae ni Ibrahim, au huelewi unachokisoma?


Huwa sikisii.
 

Umeandika mtungo wa story mkuuubwa usio na ushahidi wala references , huku ukiongopa kuwa versions za biblia hazina tofauti


Matoleo ya Biblia ya Kingereza

Katika utangulizi wa toleo la Biblia linalotumika sana, la Revised Standard Version, mtunzi ameandika yafuatayo:

"Biblia ya Revised Standard Version, ni marekebisho yaliyoidhinishwa ya toleo la American Standard Version, lilochapwa 1901, na ambalo nalo pia lilikuwa ni marekebisho ya toleo la King James Version, lilochapwa 1611…

Toleo la King James Version lililazimika kushindana na Biblia ya Geneva Bible (1560) juu ya kutumiwa na watu wengi; lakini hatimaye lilienea, na kwa zaidi ya karne mbili na nusu hakuna tafsiri ya Biblia kwa Kingereza iliyoandikwa na kuidhinishwa.

Toleo la King James Version likawa ndilo "toleo lililoidhinishwa" kwa wanaoongea Kingereza… Ndio, Toleo la King James Version lina dosari kubwa mno.

Kufikia katikati ya karne ya kumi na tisa, maendeleo ya tafiti za Kibiblia vilevile kugunduliwa kwa miswada mingi ambayo ni ya kale zaidi kuliko ile iliyotegemewa na Toleo la King James Version, yamefanya toleo hilo kuwa ni wazi kuwa lina dosari nyingi na mbaya mno na kusababisha kuitishwa kufanyika marekebisho ya tafsiri ya kingereza.

Kazi ikafanywa, kwa idhini ya Kanisa la Uingereza, mwaka 1870. Toleo la Biblia la English Revised Version lilichapwa mwaka 1881 – 1885; na Toleo la American Standard Version, lahaja zake zimejiingiza katika upendeleo wa wanazuoni wa Kimarekani walioshiriki katika kazi hiyo, nalo lilichapishwa mwaka 1901.

Toleo la King James Version la Agano Jipya liliegemea matini za kigiriki zilizovurugwa kimakosa, ikiwemo kujilimbikizia makosa ya karne ya kumi na nne ya kunukuu miswada. Nalo kimsingi, lilikuwa ni matini ya Kigiriki ya Agano Jipya kama lilivyoandikwa na Beza, 1589, ambaye kwa ukaribu zaidi alifuata chapa hiyo ya Erasmus, 1516 – 1535, iliyoegemea juu ya miswada ya zama za kati.

Mswada wa kwanza na ulio bora zaidi miongoni mwa miswada minane aliyoishirikisha ulikuwa ni wa karne ya kumi, naye akautumia kidogo mno mswada huo kwa sababu unatofautiana sana na matini za kawaida zilizopokelewa; Beza alipata miswada miwili ya thamani kubwa mno, ikiwa ni ya karne ya tano na ya sita, lakini aliitumia kidogo mno kwa sababu inatofautiana na matini iliyochapwa ya Erasmus.

Toleo la American Standard Version lilipewa haki miliki ya kuzuia matini yake isibadilishwe bila idhini. Mnamo 1928 haki hiyo ilipatikana kutoka katika Baraza la Kimataifa la Elimu na Dini, na kwa hiyo likawekwa katika umiliki wa makanisa ya Marekani na Canada yaliyoshiriki katika baraza hilo kwa kupitia bodi zao za elimu na uchapaji.

Baraza hilo liliainisha kamati ya wasomi kusimamia matini ya ya Toleo la American Standard Version na kufanya uchunguzi na kujua kama marekebisho zaidi yanahitajika… [Baada ya miaka miwili] uamuzi
ulifikiwa; nao ni kuwa; kunahitaji marekebisho kikamilifu katika toleo la 1901, ambalo litabakia kuwa lipo karibu na mapokeo ya Tyndale-King James kama itakavyokuwa… Mnamo 1937 na marekebisho yalipewa idhini kwa kura ya Baraza hilo."

"Wasomi thelathini na wawili walitumika kama wanakamati wa kamati iliyotakiwa kufanya marekebisho hayo, nao waliyalinda mabadiliko na kuishauri Bodi ya Ushauri ya wawakilishi hamsini wa madhehebu ili kushirikiana kufanya kazi hiyo…

Toleo la Agano Jipya la Revised Standard Version lilichapwa mwaka 1946."

Toleo la Biblia la Revised Standard Version, linajumuisha Agano la Kale na Jipya, nalo lilichapwa mnamo Septemba 30, 1952, na likakubalika sana.


REFERENCE

The Holy Bible: Rivised Standard Version, p. iii-iv.

Ibid, p. iv.

Ibid, p. vi.

The Holy Bible: Rivised Standard Version, p. 96.

The Holy Bible: (King Jems Version)
 
Umefunga kazi kisomi kabisa na kwa ushahidi kamili. Heko.
 

Sasa unakuja na sababu ya kukopi kutoka kwa wayahudi. Hao Mitume unaodai ni wa kiyahudi akina Nabii Mussa walikuwa na dini gani ?? tuanzie hapo
 

Mimi niko mtupu kichwani kwani sitoi ya kichwani mwangu , DOMO NI NYUMBA YA MANENO

Unapoandika kitu tuwekee Reference au ushahidi, wewe hujashushiwa aya na Mungu kuambiwa maana ya hizo aya za biblia

Hayo uliyoandika hapo juu uliyatoa biblia ipi au kitabu kipi ??
 
Hiyo ni burial site sidhani kma mtu n Akili yake akiambiwa amtolee sadaka mungu atamtolea eneo alilopanga kwa makaburi.Nahisi kwenye bible imeandikwa Hajra alifukuzwa n salha ndio maana Sehemu aliyotolea kafara mtoto wake wa pekee sipo alipokuwa anaishi n salha.Hajra alikuwa make halali hivyo alikuwa na wajibu wa kumuhudumia n kumtembelea(hakuna mtume aliwah kuzini)
 
Ndivyo anavyowaambia Nabii wenu Tito??
Yeremia 8:8
Mwasemaje, sisi tuna akili, na torati ya Bwana tunayo pamoja nasi?
Lakini, tazama, kalamu yenye uongo ya waandishi imeifanya kuwa uongo.
..............
Biblia ni tamu sana kwa wanaoielewa.
Mwasemaje kuwa ninyi mna akili, na torati ya Bwana ipo pamoja nanyi,
wakati hiyo torati haina Amri Kumi alizopewa Musa ?
Hiyo torati imeharibiwa na kalamu za waandishi wa kitabu chenu.
Na mkiwaamini hao waandishi (Yeremia aliamua kutumia tafsida tu)
Alitaka kuwaambia ukweli kuwa kama mnaiamini hiyo Torati isiyo na Amri Kumi za Musa basi ninyi hamna akili.
.............
Yeremia 8:8
Mwasemaje, sisi tuna akili, na torati ya Bwana tunayo pamoja nasi?
Lakini, tazama, kalamu yenye uongo ya waandishi imeifanya kuwa uongo.
...........
Mwasemaje kuwa ninyi mna akili? 🤣🤣🤣
Biblia sio kitabu cha mchezo mchezo dogo.
Ndio maana wahusika wote wa kwenye kitabu chenu wamechukuliwa kwenye Biblia, isipokuwa mhusika mmoja tu Mwarabu, hali ya kuwa kimeandikwa Uarabuni na Waarabu.
 
Sijakuelewa hapo unapoandika "wamechukuliwa", wamechukuliwa kupelekwa wapi?
 
Kulingana na family three Yako hapa mtiririko wote unaishia Kwa Yusuf, swali linakuja je Yusuf alitia mimba Hadi akazaliwa huyo Yesu?
Na kama hajatia mimba why kumnasibisha Yesu na hivyo vizazi vya Ibrahim?
Kama Yesu kazaliwa toka kiunoni Kwa Yusuf yaani amemwagilia basi huyo ni mwana wa Yusuf na anastahiki hiyo family three Yako ila kama hakumwagilia basi huyo ni Mtoto wa Mariam pekee so why katika uislamu wanamuita mwana wa Mariam.
Ila nyie mmevuka mipaka eti mwana wa mungu na si wa Yusuf daah...........
Mimi nimejikita kwenye hiyo family three Yako nayo naweza sema ni feki
 

Huna kazi ya kufanya? Kakojowe ukalale
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…