Japo Wakristo na Waislamu ni Watoto wa Baba Mmoja, Nabii Ibrahim na Mungu ni Mmoja, Kati ya Ismail na Isaka ni nani aliyetolewa Sadaka ya Kuchinja?

Japo Wakristo na Waislamu ni Watoto wa Baba Mmoja, Nabii Ibrahim na Mungu ni Mmoja, Kati ya Ismail na Isaka ni nani aliyetolewa Sadaka ya Kuchinja?

Naomba utuelimishe kidogo kuhusu Quran Tukufu, una maanisha nini kusema "Hizo za binadam kuchinjwa binafsi natofautiana haa na Waislam, hakuna habari hiyo kwenye Qur'an, kilipachikwa tu hicho kisa kutokea nje ya Qur'an"?.

Kwako wewe Sikukuu ya Eid el Hajj yaani Iddi ya kuchinja, ina maana sio maelekezo ya Mola?. Kisa cha Nabii Ismail hakipo kwenye Qur'an Tukufu?.
P
Kama nilivyoeleza, hakuna habari hiyo ya Ibrahim kutaka kumchinja mwanawe kwenye Qur'an.

Unataka nieleze nini zaidi kwa kitu ambacho hakipo kwenye Qur'an?

Weka wewe ushahidi kuwa kipo kwenye Qur'an. Tupeane ilm.
 
Wanabodi,
Leo ni sikukuu ya Eid El Haji, Iddi ya Kuchinja.

Leo ni siku ya Sikukuu ya Idd El Haj, ni iddi ya kuchinja, asubuhi nilikuwa naangalia matangazo ya mubashara ya Baraza la Iddi kupitia TBC, kutoka Msikiti wa Mfalme Mohammed VI wa Morroco, Bwakwata, Kinondoni jijini Dar es Salaam, kumbe Msikiti Mkuu wa Bakwata, sasa umebadilishwa jina!, na kupewa jina la Mfalme wa Morroco!.

Mgeni rasmi kwenye Baraza la Iddi ni Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa, ambaye ameandamana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, ambaye amesilimishwa na kupewa jina la Aboubakar Chalamila!, na mawaziri akiwemo Waziri Mhe. Mohamed Mchengerwa. Baadhi ya watu maarufu niliowaona ni pamoja na Alhaj Sheikh Ali Nguruko, Alhaj Chande, Idda Azan, Shaweji Abdalah, Salum Mwalimu, Juma Simba Gadafi, Salum Abladaha "TRY Again", Katibu Mkuu wa Bakwata, Sheikh Mruma, Kadhi wa Dar es Salaam, Shamin Khan, mwenyekiti wa JUAKITA, pia kulikuwa na mabalozi wa Balozi wa Moroko, na wa Comoro.

Katika salam zake, Sheikh Aboubakar Chalamila alisema utulivu wa jiji la Dar es Salaam, unawategemea sana viongozi wa Dini.

Salaam za Waislamu, zimetolewa na Alhaj Sheikh Nuru Mruma, Katibu Mkuu wa Bakwata ambaye amewasisitiza Waislamu kudumisha amani na kuilinda amani. Wazazi watakiwa kulea watoto wao kwa tabia njema, kujenga taifa la kizazi cha watu wema ambao hawatapokea rushwa wala kufanya ufisadi.

Amesema kupanda miti na utunzaji wa mazingira ni ibada muhimu kwa Waismamu wote.

Pia amewataka Waislamu kujitokeza kwa wingi, kujiandikisha kwenye uboreshaji daftari la kudumu la wapiga kura.
na wametakiwa kujitokeza kwa wingi kutumia haki yao ya kidemokrasia kugombea nafasi mbalimbali za uongozi.

Salaam za Mufti, zimetolewa na Kaimu Mufti Sheikh Ali Muhidin Mporogore, Mjumbe wa Baraza la Maulamaa wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania, Bwakwata. Aamezungumzia Watanzania tutafakari, sadaka ya kuchinja siku ya Iddi El Haj, ni iddi ya kuchinja. Zamani ilikuwa sio kuchinja tuu wanyama, bali walichinja hata binadamu ana akatolea mfano Sadaka ya Nabii Ibrahim kutaka kumtoa mwanae Ismail, kwa sadaka ya kuchinja.

Hakuna ubishi kuhusu Wakristo na Waislamu, kuwa ni watoto wa Baba mmoja, Nabii Ibrahim hivyo huu ni uthibitisho wa Mungu wa Wakristo na Waislamu ni Mungu Mmoja, ila kuna watu wanafundishwa ukweli na kuna watu wanadanganywa!.

Hakuna ubishi kuwa mtoto wa kwanza wa Ibrahim ni Ismail aliyezaa na mjakazi wa Kimisri, Hagir, na Isaka ni mtoto wa pili wa Ibrahim, aliyemzaa na mkewe Sarah.

Hakuna ubishi Ibrahim alitaka kumtoa mtoto wake Sadaka ya kuchinja.

Waislamu na Kitabu chao Kitukufu cha Quran Tukufu, kinamtaja mtoto huyo aliyetaka kutolewa sadaka ya kuchinja ni Ismail.
Wakristo na Kitabu chao Kitakatifu cha Biblia Takatifu, kinamtaja mtoto huyo aliyetaka kutolewa sadaka ya kuchinja ni Isaka.

Jee ukweli halisi ni upi?.
Hii maana yake
Kama tukio la Ibrahim kutaka kumchinja mwanae kumtoa sadaka ni tukio moja, then
1. Hii maana yake ni kuna watu wanadanganywa, haiwezekani kwa Waislamu mtoto huyo awe ni Ismail na kwa Wakristu mtoto huyo awe ni Isaka, hii maana yake kuna kitabu hapo kinasema kweli na kuna kitabu kinasema uongo!, jee ukweli ni upi?.

Umuhimu wa kuujua ukweli huu, unakupa fursa ya kujua ukweli ni upi, hivyo ufuate mafundisho yapi ambayo ndio mafundisho ya kweli!.

Bandiko hili linakutaka kwanza uwe open minded, kama wewe ni mfia dini, unaamini dini yako ni ya ukweli mtupu, bandiko hili halikufai.

Pili unatakiwa uwe na ngozi ngumu ya kuukubali ukweli halisi hata uwe mchungu vipi!, ikitokea ni dini yako unayoiamini kuwa ni dini ya kweli, kumbe ni dini ya uongo, uwe na uwezo wa kustahimili maana...

Nawatakia Waislamu wote,
Iddi Mubarak njema ya kuchinja.

Paskal
Duuu sadaka ya Waislam si inahuaiana na Hijja? inamaana kama Ibrahim alimtoa sadaka Ismail basi alifanya kama Waislam wanavyofanya kwa huyu maskini Ngamia wa watu!!??

View: https://x.com/Salwan_Momika1/status/1803438507127366084
 
Kama nilivyoeleza, hakuna habari hiyo ya Ibrahim kutaka kumchinja mwanawe kwenye Qur'an.

Unataka nieleze nini zaidi kwa kitu ambacho hakipo kwenye Qur'an?

Weka wewe ushahidi kuwa kipo kwenye Qur'an. Tupeane ilm.
We dada, ni wewe Faiza mwenyewe au kuna mtu kaiba simu yako?
Quran ina kisa hicho katika Surah ya 37:100-107
Surat Saffat. Ina maana hujui?
Pascal Mayalla nimemuwekea hapo reference.
 
No siwachokonoi ila kuna wanaofundishwa mafundisho ya ukweli na kuna wanao danganywa!. Lengo hapa ni kuutafuta ukweli ili tusiendelee Kudanganywa!.
P
Mimi huwa nawa challenge wakristo katika kitu kimoja.Iko hivi....hivi kwa akili tu ya kawaida,Mungu anaweza kukujaribu Imani yako kwa kumuuwa mtoto wako wa pili na sio mtoto wa kwanza wa pekee?Mana Mke wa Ibrahim yule wa kwanza aliona Bora Ibrahim azae na Hajra mana kwa upande wake imeshindikana na umri wao umeenda sana...hii ikimaanisha kwa upande wa Ibrahim mtoto Ismael ndio alikuwa mtoto wa kipekee kwa wakati huo na alikuwa hana mbadala.Sasa Mungu aache kumuuwa Ismael angoje mpaka Ishaq azaliwe ndio ampe jaribu la kumuuwa???Hata Mimi kwa Imani yangu ndogo hilo jaribu ningelishinda,mana najua anakufa huyu Ishaq lakini pembeni nna mtoto mwingine Ismael.Kwa akili ya kawaida bila tu Ismael ndio alikuwa atolewe sadaka na babake Ibrahim.
 
Hebu ngoja tuone MUNGU anasemaje kupitia maneno yake matukufu ndani ya kitabu cha Quran.


Quran 3:1-4


Alif Laam Miim.


Mwenyezi Mungu, hakuna mungu ila Yeye Aliye Hai, Msimamizi wa yote milele.

Amekuteremshia Kitabu kwa haki, kinacho sadikisha yaliyo kuwa kabla yake. Na aliteremsha Taurati na Injili

Kabla yake, ziwe uwongofu kwa watu. Na akateremsha Furqani (Upambanuo). Hakika walio zikanusha Ishara za Mwenyezi Mungu watakuwa na adhabu kali. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na Mwenye kulipa.
 
Laiti viongozi wetu wa serikali wangekuwa wanaapishwa kwa kutumia viapo vya kitamaduni, kama kulamba asali ,viapo vya damu na udongo , kuwa waadilifu, kuliko kutumia hivi viapo vya dini hizi za kuletewa , ambavyo havina matokea yoyote hata mtu akivivunja .

Hakuna hata dini moja yenye ukweli wowote kwetu sisi ngozi nyeusi.
 
Wakristo wengi wanatumia hoja kuwa Quran haiwezi kuwa ni Kitabu cha Mungu kwa sababu kina miaka 1400 hapa duniani wakati injili ina miaka 2000.

Ni hoja dhaifu kwasababu walitakiwa wajiulize tu mbona taurati iliitangulia injili kwa miaka mingi sana? Je hii inaondoa ukweli kwa Injili nayo ni kitabu cha Mungu?

Vp leo hii waikatae Quran kwa sababu ilikuja miaka 600 baada ya injili?
 
Kuhusu ni nani alipaswa kuchinjwa kati ya Ismael na Ishaq( isaac) ni wazi kuwa ni Ismael .

Yeyote atakaetuliza kichwa na kuisoma biblia atagundua kuwa mtoto aliyetolewa sadaka alikuwa ni ismael. Ntaweka na ushahidi wa maandiko
 
BIBLIA INASEMA Ibrahim aliambiwa amtoe sadaka mwanawe wa PEKEE (only son)...Je ni nani kati ya Ismael na isaka alikuwa mwana wa pekee wa ibrahim? Kumbuka Ibrahim alimpata Ismael akiwa na miaka 86 na kwa miaka 14 ,Ismael aliendelea kuwa ndio mtoto wa pekee wa Ibrahim mpaka pale alipokuja mpata Isaka akiwa na miaka 14. Baada ya hapo Isaka hawezi kuwa mtoto wa pekee maana tayari alishamkuta kaka yake ambaye ni Ismael akiwa na miaka 14.

Pia mtihani wa kumtoa mtoto wa pili (ambaye sie wa pekee) hauwezi kuwa sawa na mtihani wa kumchinja mtoto wa kwanza ilihali alishatafuta mtoto kwa zaidi ya miaka 60 bila ya mafanikio...mpaka alipompata ismael akiwa na miaka 86


Mwanzo 22:1-2

Sasa baada ya mambo hayo Mungu wa kweli akamjaribu+ Abrahamu, akamwambia: “Abrahamu!” akajibu: “Mimi hapa!” 2 Kisha Mungu akamwambia: “Tafadhali, mchukue mwana wako, mwana wako wa pekee unayempenda sana,+ Isaka,+ usafiri kwenda katika nchi ya Moria+ nawe umtoe kuwa dhabihu ya kuteketezwa juu ya mlima mmoja nitakaokuonyesha.”
 
Wanabodi,
Leo ni sikukuu ya Eid El Haji, Iddi ya Kuchinja.

Leo ni siku ya Sikukuu ya Idd El Haj, ni iddi ya kuchinja, asubuhi nilikuwa naangalia matangazo ya mubashara ya Baraza la Iddi kupitia TBC, kutoka Msikiti wa Mfalme Mohammed VI wa Morroco, Bwakwata, Kinondoni jijini Dar es Salaam, kumbe Msikiti Mkuu wa Bakwata, sasa umebadilishwa jina!, na kupewa jina la Mfalme wa Morroco!.

Mgeni rasmi kwenye Baraza la Iddi ni Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa, ambaye ameandamana na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, ambaye amesilimishwa na kupewa jina la Aboubakar Chalamila!, na mawaziri akiwemo Waziri Mhe. Mohamed Mchengerwa. Baadhi ya watu maarufu niliowaona ni pamoja na Alhaj Sheikh Ali Nguruko, Alhaj Chande, Idda Azan, Shaweji Abdalah, Salum Mwalimu, Juma Simba Gadafi, Salum Abladaha "TRY Again", Katibu Mkuu wa Bakwata, Sheikh Mruma, Kadhi wa Dar es Salaam, Shamin Khan, mwenyekiti wa JUAKITA, pia kulikuwa na mabalozi wa Balozi wa Moroko, na wa Comoro.

Katika salam zake, Sheikh Aboubakar Chalamila alisema utulivu wa jiji la Dar es Salaam, unawategemea sana viongozi wa Dini.

Salaam za Waislamu, zimetolewa na Alhaj Sheikh Nuru Mruma, Katibu Mkuu wa Bakwata ambaye amewasisitiza Waislamu kudumisha amani na kuilinda amani. Wazazi watakiwa kulea watoto wao kwa tabia njema, kujenga taifa la kizazi cha watu wema ambao hawatapokea rushwa wala kufanya ufisadi.

Amesema kupanda miti na utunzaji wa mazingira ni ibada muhimu kwa Waismamu wote.

Pia amewataka Waislamu kujitokeza kwa wingi, kujiandikisha kwenye uboreshaji daftari la kudumu la wapiga kura.
na wametakiwa kujitokeza kwa wingi kutumia haki yao ya kidemokrasia kugombea nafasi mbalimbali za uongozi.

Salaam za Mufti, zimetolewa na Kaimu Mufti Sheikh Ali Muhidin Mporogore, Mjumbe wa Baraza la Maulamaa wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania, Bwakwata. Aamezungumzia Watanzania tutafakari, sadaka ya kuchinja siku ya Iddi El Haj, ni iddi ya kuchinja. Zamani ilikuwa sio kuchinja tuu wanyama, bali walichinja hata binadamu ana akatolea mfano Sadaka ya Nabii Ibrahim kutaka kumtoa mwanae Ismail, kwa sadaka ya kuchinja.

Hakuna ubishi kuhusu Wakristo na Waislamu, kuwa ni watoto wa Baba mmoja, Nabii Ibrahim hivyo huu ni uthibitisho wa Mungu wa Wakristo na Waislamu ni Mungu Mmoja, ila kuna watu wanafundishwa ukweli na kuna watu wanadanganywa!.

Hakuna ubishi kuwa mtoto wa kwanza wa Ibrahim ni Ismail aliyezaa na mjakazi wa Kimisri, Hagir, na Isaka ni mtoto wa pili wa Ibrahim, aliyemzaa na mkewe Sarah.

Hakuna ubishi Ibrahim alitaka kumtoa mtoto wake Sadaka ya kuchinja.

Waislamu na Kitabu chao Kitukufu cha Quran Tukufu, kinamtaja mtoto huyo aliyetaka kutolewa sadaka ya kuchinja ni Ismail.
Wakristo na Kitabu chao Kitakatifu cha Biblia Takatifu, kinamtaja mtoto huyo aliyetaka kutolewa sadaka ya kuchinja ni Isaka.

Jee ukweli halisi ni upi?.
Hii maana yake
Kama tukio la Ibrahim kutaka kumchinja mwanae kumtoa sadaka ni tukio moja, then
1. Hii maana yake ni kuna watu wanadanganywa, haiwezekani kwa Waislamu mtoto huyo awe ni Ismail na kwa Wakristu mtoto huyo awe ni Isaka, hii maana yake kuna kitabu hapo kinasema kweli na kuna kitabu kinasema uongo!, jee ukweli ni upi?.

Umuhimu wa kuujua ukweli huu, unakupa fursa ya kujua ukweli ni upi, hivyo ufuate mafundisho yapi ambayo ndio mafundisho ya kweli!.

Bandiko hili linakutaka kwanza uwe open minded, kama wewe ni mfia dini, unaamini dini yako ni ya ukweli mtupu, bandiko hili halikufai.

Pili unatakiwa uwe na ngozi ngumu ya kuukubali ukweli halisi hata uwe mchungu vipi!, ikitokea ni dini yako unayoiamini kuwa ni dini ya kweli, kumbe ni dini ya uongo, uwe na uwezo wa kustahimili maana...

Nawatakia Waislamu wote,
Iddi Mubarak njema ya kuchinja.

Paskal
mkuu
Usijichoshe. mtume muhamad kazaliwa mwaka 570 baada ya Kristo na ndiye muislam wa kwanza na ndiye mwandishi wa korani. kisa cha Ibrahim ni cha miaka mingi nyuma kabla ya mtume
usahihi ni kuwa Isaka kwa kuwa biblia ni ya kale kuliko koran
 
Nimeisikiliza khutba yote sijasikia hata sehemu moja ikiinukuu Qur'an kuhusu mtu kutaka kuchinjwa, kama umeisikia tueleze ni dakika ya ngapi?
Rejea kwenye video,

View: https://youtu.be/79NTc1Qfgrw

  1. anzia dakika ya 43
  2. MC anamuita mtu wa ku recite Quran
    .Ustaadh anakuja na ku recite kwa Kiarabu kwa muda wa dakika 6 mpaka dakika ya 49

    Kisha msikilize Kaimu Mufti Sheikh Ali Muhidin Mporogore, Mjumbe wa Baraza la Maulamaa wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania, Bwakwata anatafsiri kwa Kiswahili kile kilichosemwa kwenye Quran kwa muda wa dakika 23 na ndipo alipozungumzia kuhusu sadaka ya kuchinja mtu, na kisa cha Nabii Ibrahim na mwanae Ismael aliyetaka kuchinjwa sadaka.
    P
 
Naomba utuelimishe kidogo kuhusu Quran Tukufu, una maanisha nini kusema "Hizo za binadam kuchinjwa binafsi natofautiana haa na Waislam, hakuna habari hiyo kwenye Qur'an, kilipachikwa tu hicho kisa kutokea nje ya Qur'an"?.

Kwako wewe Sikukuu ya Eid el Hajj yaani Iddi ya kuchinja, ina maana sio maelekezo ya Mola?. Kisa cha Nabii Ismail hakipo kwenye Qur'an Tukufu?.
P
Ibrahim alifikaje Mecca na wakati Gani wa Umri wake
 
Mimi huwa nawa challenge wakristo katika kitu kimoja.Iko hivi....hivi kwa akili tu ya kawaida,Mungu anaweza kukujaribu Imani yako kwa kumuuwa mtoto wako wa pili na sio mtoto wa kwanza wa pekee?Mana Mke wa Ibrahim yule wa kwanza aliona Bora Ibrahim azae na Hajra mana kwa upande wake imeshindikana na umri wao umeenda sana...hii ikimaanisha kwa upande wa Ibrahim mtoto Ismael ndio alikuwa mtoto wa kipekee kwa wakati huo na alikuwa hana mbadala.Sasa Mungu aache kumuuwa Ismael angoje mpaka Ishaq azaliwe ndio ampe jaribu la kumuuwa???Hata Mimi kwa Imani yangu ndogo hilo jaribu ningelishinda,mana najua anakufa huyu Ishaq lakini pembeni nna mtoto mwingine Ismael.Kwa akili ya kawaida bila tu Ismael ndio alikuwa atolewe sadaka na babake Ibrahim.
Waislam wanasema Ismael alitaka kuchinjwa Mecca, but swali langu ni wakati Gani Ibrahim aliishi Mecca?
 
BIBLIA INASEMA Ibrahim aliambiwa amtoe sadaka mwanawe wa PEKEE (only son)...Je ni nani kati ya Ismael na isaka alikuwa mwana wa pekee wa ibrahim? Kumbuka Ibrahim alimpata Ismael akiwa na miaka 86 na kwa miaka 14 ,Ismael aliendelea kuwa ndio mtoto wa pekee wa Ibrahim mpaka pale alipokuja mpata Isaka akiwa na miaka 14. Baada ya hapo Isaka hawezi kuwa mtoto wa pekee maana tayari alishamkuta kaka yake ambaye ni Ismael akiwa na miaka 14.

Pia mtihani wa kumtoa mtoto wa pili (ambaye sie wa pekee) hauwezi kuwa sawa na mtihani wa kumchinja mtoto wa kwanza ilihali alishatafuta mtoto kwa zaidi ya miaka 60 bila ya mafanikio...mpaka alipompata ismael akiwa na miaka 86


Mwanzo 22:1-2

Sasa baada ya mambo hayo Mungu wa kweli akamjaribu+ Abrahamu, akamwambia: “Abrahamu!” akajibu: “Mimi hapa!” 2 Kisha Mungu akamwambia: “Tafadhali, mchukue mwana wako, mwana wako wa pekee unayempenda sana,+ Isaka,+ usafiri kwenda katika nchi ya Moria+ nawe umtoe kuwa dhabihu ya kuteketezwa juu ya mlima mmoja nitakaokuonyesha.”
Kumbuka mama yake Ismail alifukuzwa na Sara pamoja na mtoto wake
 
Back
Top Bottom