Uchaguzi 2020 Japokuwa kukaa kimya ni jibu, Serikali inatakiwa ijibu hizi tuhuma

Uchaguzi 2020 Japokuwa kukaa kimya ni jibu, Serikali inatakiwa ijibu hizi tuhuma

Kadiri kampeni zinavyodhidi kunoga ndio kila siku tunazidi kusikia kila aina ya tuhuma, tuhuma ambazo wagombea urais wanaona zinaweza kuwapa kete ya kupata kura.

Akiwa Kamachumu mkoani Kagera mgombea wa urais kwa kupitia Chadema ametoa tuhuma ambazo kwangu mimi naona kama zinahitaji kupatiwa majibu. Maana kwa taifa kama Tanzania ambalo linafuata misingi ya katiba na sheria tuhuma kama hizi ni kama nchi yetu inachafuliwa, japokuwa ni kipindi cha kampeni. Sheria ya uchaguzi na maadili ya uchaguzi yanataka wagombea wawe wanakosoana kwa sera au hoja ambazo zina ukweli, sio uzushi.

Akiwa Kamachumu Lissu amesikika akidai kuwa serikali ya CCM ilitaka kumuua mwandishi wa habari Ansbert Ngurumo ndio maana akakimbilia ughaibuni, pia amesisitiza walewale waliompiga risasi na kumfanya awe kilema ndio waliotaka kumuua Ansbert Ngurumo.

Hizi tuhuma kwa Taifa letu ambalo limesaini mikataba mingi tu ya kimataifa kulinda haki za raia wake na hata kwenye katiba ya JMT haki ya kuishi imetambuliwa wazi, sio tuhuma nzuri na zinalichafua Taifa letu.

Kwa hiyo Serikali kukaa kimya bila kukanusha au kuzitolea ufafanuzi, tuhuma hizi zinalipaka matope Taifa letu na huenda zikaaminiwa na watu kuwa ni kweli.

Hivyo kama ambavyo imekuwa ikitoa ufafanuzi juu ya masuala mbali mbali yanayopotoshwa, hata juu ya hizi tuhuma tuambiwe kama ni kweli au si kweli.
Saaa ni uongo?
 
Muongeaji Lisu alionyesha hati ya ardhi kama ushahidi? Au alikuwa akitoa mimacho tu anapoongea ? Yeye ndie aonyeshe hati na ushahidi
 
Kadiri kampeni zinavyodhidi kunoga ndio kila siku tunazidi kusikia kila aina ya tuhuma, tuhuma ambazo wagombea urais wanaona zinaweza kuwapa kete ya kupata kura.

Akiwa Kamachumu mkoani Kagera mgombea wa urais kwa kupitia Chadema ametoa tuhuma ambazo kwangu mimi naona kama zinahitaji kupatiwa majibu. Maana kwa taifa kama Tanzania ambalo linafuata misingi ya katiba na sheria tuhuma kama hizi ni kama nchi yetu inachafuliwa, japokuwa ni kipindi cha kampeni. Sheria ya uchaguzi na maadili ya uchaguzi yanataka wagombea wawe wanakosoana kwa sera au hoja ambazo zina ukweli, sio uzushi.

Akiwa Kamachumu Lissu amesikika akidai kuwa serikali ya CCM ilitaka kumuua mwandishi wa habari Ansbert Ngurumo ndio maana akakimbilia ughaibuni, pia amesisitiza walewale waliompiga risasi na kumfanya awe kilema ndio waliotaka kumuua Ansbert Ngurumo.

Hizi tuhuma kwa Taifa letu ambalo limesaini mikataba mingi tu ya kimataifa kulinda haki za raia wake na hata kwenye katiba ya JMT haki ya kuishi imetambuliwa wazi, sio tuhuma nzuri na zinalichafua Taifa letu.

Kwa hiyo Serikali kukaa kimya bila kukanusha au kuzitolea ufafanuzi, tuhuma hizi zinalipaka matope Taifa letu na huenda zikaaminiwa na watu kuwa ni kweli.

Hivyo kama ambavyo imekuwa ikitoa ufafanuzi juu ya masuala mbali mbali yanayopotoshwa, hata juu ya hizi tuhuma tuambiwe kama ni kweli au si kweli.
Ww ni mgeni Tz?

Huyo Ngurumo alikimbia nini?

Na wale wa kwenye viroba ufukweni mwa bahari na mto Ruvu awamu hii hii ya 5, walijiingiza humo virobani wenyewe?!
 
Kadiri kampeni zinavyodhidi kunoga ndio kila siku tunazidi kusikia kila aina ya tuhuma, tuhuma ambazo wagombea urais wanaona zinaweza kuwapa kete ya kupata kura.

Akiwa Kamachumu mkoani Kagera mgombea wa urais kwa kupitia Chadema ametoa tuhuma ambazo kwangu mimi naona kama zinahitaji kupatiwa majibu. Maana kwa taifa kama Tanzania ambalo linafuata misingi ya katiba na sheria tuhuma kama hizi ni kama nchi yetu inachafuliwa, japokuwa ni kipindi cha kampeni. Sheria ya uchaguzi na maadili ya uchaguzi yanataka wagombea wawe wanakosoana kwa sera au hoja ambazo zina ukweli, sio uzushi.

Akiwa Kamachumu Lissu amesikika akidai kuwa serikali ya CCM ilitaka kumuua mwandishi wa habari Ansbert Ngurumo ndio maana akakimbilia ughaibuni, pia amesisitiza walewale waliompiga risasi na kumfanya awe kilema ndio waliotaka kumuua Ansbert Ngurumo.

Hizi tuhuma kwa Taifa letu ambalo limesaini mikataba mingi tu ya kimataifa kulinda haki za raia wake na hata kwenye katiba ya JMT haki ya kuishi imetambuliwa wazi, sio tuhuma nzuri na zinalichafua Taifa letu.

Kwa hiyo Serikali kukaa kimya bila kukanusha au kuzitolea ufafanuzi, tuhuma hizi zinalipaka matope Taifa letu na huenda zikaaminiwa na watu kuwa ni kweli.

Hivyo kama ambavyo imekuwa ikitoa ufafanuzi juu ya masuala mbali mbali yanayopotoshwa, hata juu ya hizi tuhuma tuambiwe kama ni kweli au si kweli.
Twambie nani alimuua ALPHONSO MAWAZO?
Nani alimteka ben Sanane?
Nani alikuwa anauwa watu kule MKIRU?
Nani alimshambulia TL?
Nani alimuua AKWILINE AKWILINA?
Wambie wakikanusha watolee maelezo hayo yote
 
Ww ni mgeni Tz?

Na wale wa kwenye viroba ufukweni mwa bahari na mto Ruvu awamu hii hii ya 5, walijiingiza humo virobani wenyewe?!
Nikuulize wewe mwenyeji. Ni akina nani hao waliowatupa? Kama unao ushahidi umechukua hatua gani? Kulalamika kwenye majukwaa?
 
Twambie nani alimuua ALPHONSO MAWAZO?
Nani alimteka ben Sanane?
Nani alikuwa anauwa watu kule MKIRU?
Nani alimshambulia TL?
Nani alimuua AKWILINE AKWILINA?
Wambie wakikanusha watolee maelezo hayo yote
Umeamka toka usingizini?
 
Hongera kwa post iliyoshiba masini kwa mara ya kwanza nimekukubali.
 
Mimi nijibu kama nani?
Unataka serikali ijibu ukiwa kama nani? Na kwann unataka wajibu la ngurumo tu hayo mengine yakiwemo kujenga viwanja vya ndege bila kutangaza tenda? Kuwapa wapwa kuwa walipaji wakuu wa serikali na kuita watengeneza ndege kujifungia nao ndani bila kufuata sheria ya manunuzi
Ukimalizia na mporaji wa KOROSHO za watu huko kusini
Yajibiwe kwa pamoja na hiyo serikali yako ya kidhalimu
 
Kwani Lisu kaenda kulalamika polisi au mahakamani?
Mgonjwa mahututi anao uwezo wa kwenda polisi au mahakamani ambae kapelekwa Kenya hafahamu lolote? Mo alipo potea alipiga simu polisi na kusema kama ametekwa au polisi walifanya kazi yao ya uchunguzi? Na kwa Lissu wangefanya uchunguzi


Ndukiiiii 🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
 
Asante mkuu umeleta mada nzuri sana mezani ambayo inatakiwa kufafanuliwa vizuri.

Kwa kuongezea hoja yako hata mimi sijaelewa kitu gani kinafanyika hapa nchini. Yaani serikali inapewa lawama na tuhuma za muaji, ukandamizwaji na kunyimwa kwa haki za binadam, kama wapinzani wanavyo dai, alafu wahusika wa vyombo vya serikali wanao takiwa kujibu tuhuma hizo wako tu Domant na Rais Magufuli na makada wa CCM hawana lolote wanalo lisema kuhusiana na tuhuma hizo.

Rais Magufuli kama unadanganywa na watu wako kuwa huu uchaguzi umesha shinda kwa mambo ambayo umeyafanya hii miaka mitano, mimi ningekushauri kuwa imani hiyo kwa sasa iondoe. Maana ninachojua mimi ni kwamba hivi sasa nguvu nyingi kutoka nje inatumika na hata viongozi wa dini nao wanatumiwa ili kukuondoa wewe na chama chako madarakani.

Njia mojawapo inayo tumiwa ni ya kuku attack wewe personally kwa mambo ya uongo na uzushi kuhusu matukio yaliyo tokea na bdo hayajapata ufumbuzi na sio wao kuzungumzia sera zao. Wanajua fika kuwa kwenye misingi hiyo hawawezi ambulia kitu na ndiyo maana wanatumia hizo Personal attack kwako na kwa baadhi ya viongozi na vyombo vya usalama. Hiyo ni strategy yao kwa sababu wanajua kuwa watanzania wengi ni watu wa kupeana udaku udaku kwa hiyo njia hiyo itawasaidia kuweza kuwavuta watanzania wengi kwao.

Na ukiangalia unaona kwa namna fulani wanaanza ku-gain Momentum ya kuwavuta vijana wengi kwenye mikutano yao. Hivi sasa inaonekana vijana wengi wamesha sahahu matatizo mengi waliyo kuwa wanayapata kila siku huko nyuma kuhusiana na rushwa maofisini na pia elimu ya malipo na matatizo ya matibabu mahospitalini na hata shida za umeme, maji ni mitandao.

Naomba ni ulize swali, ina maana serikali imesalm amri kwa mabeberu kwa kuogopa kushtakiwa in The Hauge?

Rais Magufuli kukaa kimya kwako na makada wa chama chako kuto jibu tuhuma au lawama ambazo serikali yako inasingiziwa hiyo hakumaanishi kuwa eti ukijibu tuhuma hizo ndiyo hujaendesha uchaguzi bora na wenye haki. Definition ya uchaguzi bora na wenye haki hauwi definiere kwa kuto jibu mapigo ya tuhuma mbaya ambazo zina haribu taswira ya nchi na credibility yako, Definition ya uchaguzibbora na wa haki ni pale matokea ya uchaguzi yanapo tangazwa na kupewa ushindi yule mtu kweli aliye shinda kwa majority ya kura zilizo pigwa na sio kwa kuto jibu mapigo ya tuhuma za kusingizwa.

Hawa watu wanatakiwa wajibiwe kihuni kama wao wanavyo fanya na hata ikibidi tumieni kusambaza Audio na clips za maneno na matendo yao machafu waliyo yafanya ili watanzania wayaone na kuyasikia.

Nilitamani kwa mfano wakati Kamanda wa Polis wa kanda Maalum ya DSM Mambosasa alipo kanusha madai ya mgombea Urais kwa Ticket ya ACT, Mr Bernad Membe kuonyesha clips za kukamatwa kwake ili watanzania waone na wasiwaamini. Lakini kukanusha kwa maneno tu hilo halisadii sana, maana inatakiwa itambulike kuwa serikali na vyombo vya usalama na hasa polisi inahisiwa kufanya maovu wakati wote. Na ili kujenga credibility ionyeshe hizo clips na kurusha audios kama vile ilivyo watokea akina Membe na wengineo. Vitu kama hivi vina saidia sana kujenga imani kwa wananchi.

Mnakumbuka miaka minne iliyopita kwenye kampeni za uchaguzi wa Amerika kati ya Trump na Hillary Clinton. Trump alilenga attacks zake kwa Mrs Clinton directly na kumletea ushindi. Na ndiyo tactic ambazo Lissu na wengineo wanazitumia. Hawa watu hawana hata ethic, wana waingiza mpaka wamachinga, Bodaboa na mama ntilie! Oh my goodness!


Wapelelezi wa kifo cha Beni Saanane na wenye viti wa CHADEMA walio okotwa Coco Beach umefikia wapi, wakati indications zote zinaonyesha kuwa Mwenyekiti wao Mbowe na baadhi ya makada wa CHADEMA wanahusika?

Ningetegemea mhusika mkuu wa upepelezi kuweza kuweka hili jambo hewani wakaelezea hisia zao na conditions ambazo zingeweza sababisha kupotea kwake.

Rais Magufuli unajua jinsi watanzania walivyo kuwa mabogus wa kuamini kila kitu wanacho ambiwa? Na hiyo ndiyo strategy ya Lissu na CHADEMA kupublish uongo huku wakiwa na uhakika kuwa watanzaia wata wa amini na kuchukua hatua zinazo faa kwenye Sanduhr la kura. Cha kushangaza ni kwamba wewe Rais na makada wote wa chama chako na wahusika wa serikali mko tu kimya na kuwaacha hawa wahuni na majambazi yakitapika uongo kila siku ya mungu.

Hii hali inasikitisha sana na kwa upande mwingine inawafanya hata wazalendo wanao ipenda nchi yao kuvunjika moyo maana watu na viongozi tunao wategemea na kuwaamni wamekaa tu kimya na hawatoe tamko lolote la kuondoa shutuma hizo.

Rais Magufuli na makada wote wa CCM, wasomi wetu wa sheria na mambo ya kiutawala na kudiplomasia na hata vyombo vya usalama tumieni vipaji vyenu na utaalam wenu kuyashushua haya majambazi. Mnataka nchi yetu ishikwe na Pimbi kama Lissu na Juncky kama Mbowe ambayo hata kuongoza chama chao kinawashinda?
Nitarudia mara kwa mara, tuhuma za Lissu ni za kuichokoza Serikali akiamini ina wajinga wa kuingia kwenye mitego yake ya kitoto ajibiwe. Atapewa majibu wakati mwafaka kwa kuwa tayari yupo nchini na hana ujanja wa kusepa kimya kimya. Hawezi kufanya hivyo kwa sababu anabeba dhamana ya CHADEMA, chama kikuu cha upinzani. Kama Mgombea wa Urais wa chama, amekwisha kipa matumaini ya kuwa Chama Tawala.

Lissu anayotuhuma Serikali na hasa Magufuli ni mapya kwake mwenyewe na wala si kwa Watanzania. Ushahidi ni kushindwa vibaya kwa CHADEMA kwenye chaguzi ndogo, viongozi wake wakitumia tuhuma hizo hizo kuomba kura. Au tumesahau?

Nani anajua vizuri adha ya kilimo (kahawa au korosho) kama siyo mkulima mwenyewe? Mtanzania gani hajui mabadiliko ya mara kwa mara ya bei za bidhaa km sukari hutokana na wafanya biashara makajanja na juhudi za Serikali kuthibiti mfumko wa bei?

Kiongozi gani haba tuhuma nzito, zingine za uhaini. Viongozi wa juu wa CHADEMA wana tuhuma nzito ambazo zitawekwa wazi muda mwafaka kabla kipenga cha kupiga kura hakijapulizwa.

Lissu na CHADEMA yake wanajua hilo na Watanzania wanajua kwamba katika dunia ya TEHEMA hapafichwi kitu.
 
CCM hawawezi jibu tuhuma zipo nyingi wananchi wanataka majibu Kuna ile ishu ya vyeti vya kuzaliwa vya mgombea wao nao wamepoteana wananchi wanataka aonyeshe cheti Chake cha kuzaliwa, pili ishu ya karagwe kuporwa ardhi kibabe, uporaji wa ardhi za wananchi na kuzigeuza hifadhi, mikataba ya miradi nk.
 
Back
Top Bottom