Jaribio la Utekaji wa Deogratius Tarimo: LHRC yahimiza uchunguzi wa haraka, jamii kutimiza wajibu wa kulinda uhai kila mtu

Jaribio la Utekaji wa Deogratius Tarimo: LHRC yahimiza uchunguzi wa haraka, jamii kutimiza wajibu wa kulinda uhai kila mtu

The Sheriff

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2019
Posts
747
Reaction score
2,112
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimeshtushwa na video zinazozunguka mtandaoni zikionyesha jaribio la utekaji dhidi ya Ndugu Deogratius Tarimo, mfanyabiashara na mkazi wa Kibaha, mkoani Pwani, tukio lililotokea nje ya hoteli ya Rovvenpec Resort, Kiluvya Madukani, Wilaya ya Ubungo, Dar es Salaam, Jumatatu, Novemba 11, 2024.

Soma, Pia: Inasemekana tukio hili la utekaji limetokea Kiluvya, kutokana na uzito wa jamaa walishindwa kumchukua. Hakuna aliyetoka kumsaidia

LHRC imeeleza kusikitishwa kwake na kuongezeka kwa matukio ya utekaji nchini, huku ikisisitiza kuwa matukio haya yanakiuka haki za binadamu na Katiba ya Tanzania nakutoa wito kwa Jeshi la Polisi kuchukua hatua za haraka kuchunguza tukio hili na serikali kuhakikisha matukio haya yanakomeshwa.

LHRC 1.jpg

LHRC 2.jpg
Soma: Polisi watoa tamko tukio la jaribio la utekaji Kiluvya, wasema uchunguzi umeanza toka aliporipoti Novemba 11, 2024
 
Hawa ndio walitakiwa wawe wanatoa matamko ya mwendelezo kudai majibu ya uchunguzi ila na wao kama polisi wametoa tamko hivi ndo wamemaliza
 
Novemba 13 - Taarifa kwa Umma_page-0001.jpg

Novemba 13 - Taarifa kwa Umma_page-0002.jpg
Kama Watanzania mbalimbali walivyoshtushwa na kugadhabishwa na tukio hili, Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimesema kimestushwa na video zinazosambaa mtandaoni zikionesha jaribio la utekaji dhidi ya Deogratius Tarimo, Mfanyabiashara na Mkazi wa Kibaha, Mkoani Pwani ambapo kimetoa wito kwa Polisi kuharakisha uchunguzi wa tukio hili na kuhakikisha Wahalifu wanatiwa mbaroni na matokeo ya uchunguzi huo yatangazwe kwa umma ili kurejesha imani ya
usalama.

Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Dr. Anna Henga amesema “Tukio hilo liliripotiwa kutokea nje ya hoteli ya Rowenpec Resort, Kiluvya Madukani, Wilaya ya Ubungo, Dar es Salaam, siku ya Jumatatu, Novemba 11, 2024, LHRC inasikitishwa na kuongezeka kwa matukio ya utekaji nchini yanayokiuka haki za binadamu, utu wa Mtu, na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977, mara nyingi matukio haya yamekuwa yakijitokeza na kukosa ufatiliaji wa kina kutoka kwa Mamlaka hususani Jeshi la Polisi”

“Hali hii ni hatari na inakinzana na misingi ya usalama, haki na utawala wa sheria, kwa mujibu wa Ibara ya 15 ya Katiba, ni marufuku kwa Mtu kukamatwa au kunyang’anywa uhuru wake kinyume na sheria, Polisi ichukue hatua madhubuti kwa mujibu wa sheria ili kukomesha matukio kama haya, LHRC inatoa wito kwa Polisi kuharakisha uchunguzi wa tukio hili na kuhakikisha Wahalifu wanatiwa mbaroni, matokeo ya uchunguzi huo yatangazwe kwa umma ili kurejesha imani ya usalama”

“Serikali isione tukio hili kama tukio, la pekee bali kama ishara ya muendelezo wa matukio ya utekaji, hatua za haraka zichukuliwe, ikiwemo kuhakikisha wahalifu wote
wanaohusika na matukio kama haya wanakamatwa na kufikishwa mbele ya sheria”

“Jamii iwe macho na itimize wajibu wa kulinda uhai wa kila mtu, kwa mujibu wa Ibara ya 14 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ianzishe taasisi ya upelelezi ya kitaifa (National Bureau of Investigation) kama ilivyopendekezwa na Tume ya Haki Jinai. Taasisi hii itakuwa na jukumu la kuchunguza matukio ya utekaji na kupotea kwa watu kwa kina ili kulinda uhuru, usalama, na maisha ya watu wote Nchini”

Pia, Soma: Jaribio la Utekaji wa Deogratius Tarimo: LHRC yahimiza uchunguzi wa haraka, jamii kutimiza wajibu wa kulinda uhai kila mtu
 
Hiyo video nimeona kuna mwamba mmoja anapita pembeni anajifanya hajui chochote. Yule ndio inatakiwa tupige viboko. Amevaa shati lina namba
 
Hiyo video nimeona kuna mwamba mmoja anapita pembeni anajifanya hajui chochote. Yule ndio inatakiwa tupige viboko. Amevaa shati lina namba
Maigizo ya mitaani ukiingilia kwenye maigizo hujui hata watu walipotokea wanakuja kukwambia wapo kwenye scene wanaigiza ndio maana watu wanajifunza hayo mambo hawaingilii sababu watu wanaonekana wanaigiza

Nitakupa kisa kimoja maeneo ya Mabibo NIT geti la kuingilia hapa karibu na mahakama ya Ndizi soko la Ndizi la Mabibo pale wanakaaga wapiga debe kupigia debe wanafunzi wanaotoka Chuoni kuelekea kwengineko km Magomeni, Posta, K/Koo nk sasa kuna siku wale jamaa walikua wawili mmoja Ras mwingine ana Dongo walianza kugombea 500 tu ambayo mmoja alichukua wakati hajapiga Debe wakaanza kuzipanga palingi mtu 2

Watu wapo pale wanaangalia wakapelekana mpaka barabarani pigana sana ngumi watu wanaangalia tu ikafika hatua mmoja alipoona anazidiwa akaanza kutafuta silaha ili ammalize mwenzie ndio bahati nzuri kuna dereva alikua anatokea Mabibo anawajua na wao wanamjua akaja pale akawatenganisha wakamuheshimu wakaacha kupigana lakini watu wengine walikua wanawaangalia tu alichokifanya yule dereva akamchukua yule aliekua anagombea 500 akampa 1000 akamwambia panda kwenye gari tuondoke hapa na usije tena hapa ndio yule mmoja kwa nidhamu akatii akaingia kwenye gari

Ushanielewa lakini watu wengi walikua wanajua jamaa wanaigiza tu japokua walikua wanatoana damu kweli kweli wamepasuana vichwa na pua kwa makonde watu wanaona km maigizo tu
 
Back
Top Bottom