Jasusi Honda ndani ya mpango wa Congo

Jasusi Honda ndani ya mpango wa Congo

RIWAYA : MPANGO WA CONGO

SEHEMU YA 28


*****

Sundi alirejea nyumbani kwake jua likiwa linaelekea kuwa la utosi.

Alifanya haraka haraka na kuelekea jikoni kupika chakula.

Alipokwisha kupika alihitaji kwenda kufungua na kusafisha majeraha ya Salomoni.

Alivaa mavazi maalumu na kuvaa kitambaa maalumu chenye kamba zilizoenda kushika masikio huku kikiwa kimeziba mdomo na pua.

Sundi alifunua mapazia yaliokuwa yamekizunguka kitanda alicholalia Solomoni Bukaba.


Alikuta Solomoni akiwa ameshazinduka kutoka usingizini.

"Wajisikiaje mpenzi!" aliuliza Sundi huku akimtizama Solomoni usoni.

Macho yao yalipogongana yaliongea Lugha ya upendo wa hali ya juu.

Walipendana kiukweli.

"Naendelea vyema hivi sasa mpenzi wangu" alijibu Solomoni kwa uchovu.


"mmh pole,ngoja nikusafishe ili uendelee kupumzika" alisema Sundi huku akimwanamia Solomoni.

Macho yao yaligongana tena.

Solomoni aliona kitu.
Kitu hicho ndicho alichokiona siku anavamiwa ndani kwake.

Macho!!

Uangaliaji ule ulifanana sawasawa na ule alioangaliwa na mwanamke aliekuwa amevaa kininja.

Macho yalikuwa ni yale yale.

Alikumbuka sawia.
.

Akajikaza bila kuuliza hilo jambo.

Sundi aliendelea kumshugulikia Solomoni.

Alimaliza kumsafisha majeraha kisha akavua mavazi aliokuwa amevaa na kuyatundika mle chumbani kisha akamuomba Solomoni aende sebuleni kwa ajili ya chakula.

Solomoni aliamka kivivu na kwenda sebuleni.

Dakika kadhaa badae walikuwa wanakula chakula kitamu alichopika Sundi huku kila mara Sundi akimsaidia Solomoni kumlisha.

Walikuwa wakitaniana hapa na pale ili mradi kila mtu anaonesha kumjali mwenzie.

Walipomaliza kula walielekea bafuni ambako Sundi alimwogesha Solomoni huku wakitaniana hapa na pale huko bafuni.

Walimaliza kuogeshana wakaelekea chumbani na kujilaza kitandani.

"Mpenzi sijakuuliza kilichokupata jana mana niliona ulikuwa hujiwezi kabisa" alisema Sundi.

"Kwani hujasoma magazeti leo!? Nyumba yangu iliungua moto ila kabla nilivamiwa na watu walionishambulia namna hii kama unavyoona" alijibu Solomoni huku akimtizama Sundi usoni.

Sundi alitazama pembeni.

"hao watu walisema wanataka nini kwako?" aliuliza Sundi.

"Hawakusema wanachotaka" alijibu Solomoni alijibu huku akiwa bado anamtazama usoni.


Sundi alikaa kimya kidogo kisha akamchumu midomoni na kumpa ulimi Solomoni ambae nae aliupokea na wakagandana huku mikono yao ikitalii kwenye miili yao.

"Mmh unaumwa Solo wangu, tuishie hapa" alisema Sundi huku akijinasua Mikononi mwa Solomoni.

Kabla Solomoni hajasema lolote kengele ikalia.

Wakaangaliana.

Kengele ikaendelea kulia kwa fujo.

Sundi akatupa kanga aliokuwa amevaa,harakaharaka akavaa suruali aliokota chini na shati pana jeupe hakujali kuvaa hata chupi akaenda kufungua mlango.

Alipigwa na butwaa!!

"Mbona nyinyi leo mnamabalaa hivi" alisema na mtu aliekuwa getini.

"Mambo yanazidi kuwa mabaya tu" alijibu mtu aliekuwa getini.

"Duh afu niliwambiaje kuingia hapa kabla hatujawasiliana?" alihoji Sundi huku akifungua geti.

Alimfungulia Mwasu.

Mwasu alikuwa anamajeraha mwili mzima ya kuchanika chanika hasa usoni.

Haraka akapelekwa kwenye chumba kilichokuwa na vifaa tiba na kuanza kuhudumiwa.

Huduma ilichukua si zaidi ya saa mbili tayari majeraha yalikuwa yamesafishwa na kushonwa vizuri.


Hakuwa na majeraha makubwa sana hivyo akawa yupo timamu kimwili.

Walitoka kukaa sebuleni.

Walimkuta Solomoni akiwa ametulia akitazama runinga.

Mwasu akamtazama Sundi.

Sundi akatoa ishara ya kuwa asijali.

Wakaenda kukaa wote sebuleni huku Mwasu akipeana salamu na Solomoni.


Kitu ambacho Sundi alikijua na Mwasu hakujua kama Sundi anajua ni kuwa katika mipango yao endapo akitokea mtu hatarishi wa kushugulikiwa basi picha yake husambazwa kwa wote na akishakufa pia taarifa hufika kwa wote.

Hivyo Mwasu alishangaa sana kumkuta Solomoni nyumbani kwa Sundi.

Alimchukulia Sundi kama ni msaliti kati yao.

Akapanda kufanya jambo.


Waliendelea kuangalia runinga huku wakisemezana hili na lile.

Mwasu akaomba kutoka nje kidogo akapunge upepo kwa madai amechoka kukaa na majeraha yalimuuma.

Alikubaliwa huku Sundi akijua ni nini Mwasu anaenda kufanya huko nje.

Hakutaka alilowaza litokee.

Mwasu alipofika nje tu akatoa simu yake harakaharaka akatafuta namba za Elchapo ili apige.

Ni wakati simu yake inaita ndipo akajikuta yupo chini bila kupenda.

Sundi alikuwa amempiga teke la mgongoni.

Ngumi zikapangwa na watu walianza kupigana vita ya hatari.

Solomoni Bukaba akisikia vishindo huko nje,mwanzo alipotezea lakini vishindo viliongezeka.

Nae akatoka.


Alijikuta akishuhudia mpambano safi wa wanawake wanaojua vizuri mchezo wa ngumi.

Sundi alikuwa anacheka ili kumgadhabisha Mwasu.

Kicheko chake kilielea vyema kwenye ngome za masikio ya Solomoni.

Alikumbuka kicheko kile.

Ni cha yule yule mwanamke aliemvamia usiku wa balaa kwake.

Ebana eeh!

"Sundi ni nani na anashirikiana na nani!?" alijiuliza Solomoni.

Ni hadi pale alipoona Mwasu akichomoa kisu kutoka maungoni mwake na kwa ustadi wa hali ya juu akakirusha kumwendea Sundi. Na Sundi nae kwa wepesi wa ajabu akajikunja na kisu kikampita sentimita chache tu.

Solomoni hakujua kama Sundi wake laini laini anaweza kuzichapa kiasi kile.

Ilikuwa ni ajabu ila ndivyo ilikuwa.

Sundi alienda juu kama nyani na aliporudi akaachia teke safi lililoishia shingoni kwa Mwasu na kumsambaratisha chini kama mzigo.

Sundi aliona kumwachia Mwasu ni kujizika zaidi yeye hivyo akachomoa bastola ambayo Solomoni hakujua ilitokea wapi mana Sundi alivaa wakati yeye akiwepo na hakuiona.

Hatari hii.

Kisha akashuhudia Sundi akiachia risasi sita bila huruma ambazo zote zilijaa kifuani kwa Mwasu na kumwacha akiwa hana uhai.

"Why!!" aliuliza Solomoni baada ya kuona Sundi amegeuka na kumnyooshea bastola yeye.

Sundi alitamani apasue kichwa cha Solomoni ila nguvu ya mapendo ilizidi utimamu wa akili.

Akajikuta akishusha silaha chini.

"Tuondoke hapa hakutufai" alisema Sandi huku akiishindilia risasi simu ya Mwasu iliokuwa chini.

Iliwabidi kuondoka eneo lile.

Hekaheka za Komando Zedi Wimba na Jasusi Honda huko Somalia - JamiiForums
 
RIWAYA : MPANGO WA CONGO

SEHEMU YA 28


*****

Sundi alirejea nyumbani kwake jua likiwa linaelekea kuwa la utosi.

Alifanya haraka haraka na kuelekea jikoni kupika chakula.

Alipokwisha kupika alihitaji kwenda kufungua na kusafisha majeraha ya Salomoni.

Alivaa mavazi maalumu na kuvaa kitambaa maalumu chenye kamba zilizoenda kushika masikio huku kikiwa kimeziba mdomo na pua.

Sundi alifunua mapazia yaliokuwa yamekizunguka kitanda alicholalia Solomoni Bukaba.


Alikuta Solomoni akiwa ameshazinduka kutoka usingizini.

"Wajisikiaje mpenzi!" aliuliza Sundi huku akimtizama Solomoni usoni.

Macho yao yalipogongana yaliongea Lugha ya upendo wa hali ya juu.

Walipendana kiukweli.

"Naendelea vyema hivi sasa mpenzi wangu" alijibu Solomoni kwa uchovu.


"mmh pole,ngoja nikusafishe ili uendelee kupumzika" alisema Sundi huku akimwanamia Solomoni.

Macho yao yaligongana tena.

Solomoni aliona kitu.
Kitu hicho ndicho alichokiona siku anavamiwa ndani kwake.

Macho!!

Uangaliaji ule ulifanana sawasawa na ule alioangaliwa na mwanamke aliekuwa amevaa kininja.

Macho yalikuwa ni yale yale.

Alikumbuka sawia.
.

Akajikaza bila kuuliza hilo jambo.

Sundi aliendelea kumshugulikia Solomoni.

Alimaliza kumsafisha majeraha kisha akavua mavazi aliokuwa amevaa na kuyatundika mle chumbani kisha akamuomba Solomoni aende sebuleni kwa ajili ya chakula.

Solomoni aliamka kivivu na kwenda sebuleni.

Dakika kadhaa badae walikuwa wanakula chakula kitamu alichopika Sundi huku kila mara Sundi akimsaidia Solomoni kumlisha.

Walikuwa wakitaniana hapa na pale ili mradi kila mtu anaonesha kumjali mwenzie.

Walipomaliza kula walielekea bafuni ambako Sundi alimwogesha Solomoni huku wakitaniana hapa na pale huko bafuni.

Walimaliza kuogeshana wakaelekea chumbani na kujilaza kitandani.

"Mpenzi sijakuuliza kilichokupata jana mana niliona ulikuwa hujiwezi kabisa" alisema Sundi.

"Kwani hujasoma magazeti leo!? Nyumba yangu iliungua moto ila kabla nilivamiwa na watu walionishambulia namna hii kama unavyoona" alijibu Solomoni huku akimtizama Sundi usoni.

Sundi alitazama pembeni.

"hao watu walisema wanataka nini kwako?" aliuliza Sundi.

"Hawakusema wanachotaka" alijibu Solomoni alijibu huku akiwa bado anamtazama usoni.


Sundi alikaa kimya kidogo kisha akamchumu midomoni na kumpa ulimi Solomoni ambae nae aliupokea na wakagandana huku mikono yao ikitalii kwenye miili yao.

"Mmh unaumwa Solo wangu, tuishie hapa" alisema Sundi huku akijinasua Mikononi mwa Solomoni.

Kabla Solomoni hajasema lolote kengele ikalia.

Wakaangaliana.

Kengele ikaendelea kulia kwa fujo.

Sundi akatupa kanga aliokuwa amevaa,harakaharaka akavaa suruali aliokota chini na shati pana jeupe hakujali kuvaa hata chupi akaenda kufungua mlango.

Alipigwa na butwaa!!

"Mbona nyinyi leo mnamabalaa hivi" alisema na mtu aliekuwa getini.

"Mambo yanazidi kuwa mabaya tu" alijibu mtu aliekuwa getini.

"Duh afu niliwambiaje kuingia hapa kabla hatujawasiliana?" alihoji Sundi huku akifungua geti.

Alimfungulia Mwasu.

Mwasu alikuwa anamajeraha mwili mzima ya kuchanika chanika hasa usoni.

Haraka akapelekwa kwenye chumba kilichokuwa na vifaa tiba na kuanza kuhudumiwa.

Huduma ilichukua si zaidi ya saa mbili tayari majeraha yalikuwa yamesafishwa na kushonwa vizuri.


Hakuwa na majeraha makubwa sana hivyo akawa yupo timamu kimwili.

Walitoka kukaa sebuleni.

Walimkuta Solomoni akiwa ametulia akitazama runinga.

Mwasu akamtazama Sundi.

Sundi akatoa ishara ya kuwa asijali.

Wakaenda kukaa wote sebuleni huku Mwasu akipeana salamu na Solomoni.


Kitu ambacho Sundi alikijua na Mwasu hakujua kama Sundi anajua ni kuwa katika mipango yao endapo akitokea mtu hatarishi wa kushugulikiwa basi picha yake husambazwa kwa wote na akishakufa pia taarifa hufika kwa wote.

Hivyo Mwasu alishangaa sana kumkuta Solomoni nyumbani kwa Sundi.

Alimchukulia Sundi kama ni msaliti kati yao.

Akapanda kufanya jambo.


Waliendelea kuangalia runinga huku wakisemezana hili na lile.

Mwasu akaomba kutoka nje kidogo akapunge upepo kwa madai amechoka kukaa na majeraha yalimuuma.

Alikubaliwa huku Sundi akijua ni nini Mwasu anaenda kufanya huko nje.

Hakutaka alilowaza litokee.

Mwasu alipofika nje tu akatoa simu yake harakaharaka akatafuta namba za Elchapo ili apige.

Ni wakati simu yake inaita ndipo akajikuta yupo chini bila kupenda.

Sundi alikuwa amempiga teke la mgongoni.

Ngumi zikapangwa na watu walianza kupigana vita ya hatari.

Solomoni Bukaba akisikia vishindo huko nje,mwanzo alipotezea lakini vishindo viliongezeka.

Nae akatoka.


Alijikuta akishuhudia mpambano safi wa wanawake wanaojua vizuri mchezo wa ngumi.

Sundi alikuwa anacheka ili kumgadhabisha Mwasu.

Kicheko chake kilielea vyema kwenye ngome za masikio ya Solomoni.

Alikumbuka kicheko kile.

Ni cha yule yule mwanamke aliemvamia usiku wa balaa kwake.

Ebana eeh!

"Sundi ni nani na anashirikiana na nani!?" alijiuliza Solomoni.

Ni hadi pale alipoona Mwasu akichomoa kisu kutoka maungoni mwake na kwa ustadi wa hali ya juu akakirusha kumwendea Sundi. Na Sundi nae kwa wepesi wa ajabu akajikunja na kisu kikampita sentimita chache tu.

Solomoni hakujua kama Sundi wake laini laini anaweza kuzichapa kiasi kile.

Ilikuwa ni ajabu ila ndivyo ilikuwa.

Sundi alienda juu kama nyani na aliporudi akaachia teke safi lililoishia shingoni kwa Mwasu na kumsambaratisha chini kama mzigo.

Sundi aliona kumwachia Mwasu ni kujizika zaidi yeye hivyo akachomoa bastola ambayo Solomoni hakujua ilitokea wapi mana Sundi alivaa wakati yeye akiwepo na hakuiona.

Hatari hii.

Kisha akashuhudia Sundi akiachia risasi sita bila huruma ambazo zote zilijaa kifuani kwa Mwasu na kumwacha akiwa hana uhai.

"Why!!" aliuliza Solomoni baada ya kuona Sundi amegeuka na kumnyooshea bastola yeye.

Sundi alitamani apasue kichwa cha Solomoni ila nguvu ya mapendo ilizidi utimamu wa akili.

Akajikuta akishusha silaha chini.

"Tuondoke hapa hakutufai" alisema Sandi huku akiishindilia risasi simu ya Mwasu iliokuwa chini.

Iliwabidi kuondoka eneo lile.
Aiseee hatari sana mapenzi yana nguvu
 
Duuh
RIWAYA : MPANGO WA CONGO

SEHEMU YA 28


*****

Sundi alirejea nyumbani kwake jua likiwa linaelekea kuwa la utosi.

Alifanya haraka haraka na kuelekea jikoni kupika chakula.

Alipokwisha kupika alihitaji kwenda kufungua na kusafisha majeraha ya Salomoni.

Alivaa mavazi maalumu na kuvaa kitambaa maalumu chenye kamba zilizoenda kushika masikio huku kikiwa kimeziba mdomo na pua.

Sundi alifunua mapazia yaliokuwa yamekizunguka kitanda alicholalia Solomoni Bukaba.


Alikuta Solomoni akiwa ameshazinduka kutoka usingizini.

"Wajisikiaje mpenzi!" aliuliza Sundi huku akimtizama Solomoni usoni.

Macho yao yalipogongana yaliongea Lugha ya upendo wa hali ya juu.

Walipendana kiukweli.

"Naendelea vyema hivi sasa mpenzi wangu" alijibu Solomoni kwa uchovu.


"mmh pole,ngoja nikusafishe ili uendelee kupumzika" alisema Sundi huku akimwanamia Solomoni.

Macho yao yaligongana tena.

Solomoni aliona kitu.
Kitu hicho ndicho alichokiona siku anavamiwa ndani kwake.

Macho!!

Uangaliaji ule ulifanana sawasawa na ule alioangaliwa na mwanamke aliekuwa amevaa kininja.

Macho yalikuwa ni yale yale.

Alikumbuka sawia.
.

Akajikaza bila kuuliza hilo jambo.

Sundi aliendelea kumshugulikia Solomoni.

Alimaliza kumsafisha majeraha kisha akavua mavazi aliokuwa amevaa na kuyatundika mle chumbani kisha akamuomba Solomoni aende sebuleni kwa ajili ya chakula.

Solomoni aliamka kivivu na kwenda sebuleni.

Dakika kadhaa badae walikuwa wanakula chakula kitamu alichopika Sundi huku kila mara Sundi akimsaidia Solomoni kumlisha.

Walikuwa wakitaniana hapa na pale ili mradi kila mtu anaonesha kumjali mwenzie.

Walipomaliza kula walielekea bafuni ambako Sundi alimwogesha Solomoni huku wakitaniana hapa na pale huko bafuni.

Walimaliza kuogeshana wakaelekea chumbani na kujilaza kitandani.

"Mpenzi sijakuuliza kilichokupata jana mana niliona ulikuwa hujiwezi kabisa" alisema Sundi.

"Kwani hujasoma magazeti leo!? Nyumba yangu iliungua moto ila kabla nilivamiwa na watu walionishambulia namna hii kama unavyoona" alijibu Solomoni huku akimtizama Sundi usoni.

Sundi alitazama pembeni.

"hao watu walisema wanataka nini kwako?" aliuliza Sundi.

"Hawakusema wanachotaka" alijibu Solomoni alijibu huku akiwa bado anamtazama usoni.


Sundi alikaa kimya kidogo kisha akamchumu midomoni na kumpa ulimi Solomoni ambae nae aliupokea na wakagandana huku mikono yao ikitalii kwenye miili yao.

"Mmh unaumwa Solo wangu, tuishie hapa" alisema Sundi huku akijinasua Mikononi mwa Solomoni.

Kabla Solomoni hajasema lolote kengele ikalia.

Wakaangaliana.

Kengele ikaendelea kulia kwa fujo.

Sundi akatupa kanga aliokuwa amevaa,harakaharaka akavaa suruali aliokota chini na shati pana jeupe hakujali kuvaa hata chupi akaenda kufungua mlango.

Alipigwa na butwaa!!

"Mbona nyinyi leo mnamabalaa hivi" alisema na mtu aliekuwa getini.

"Mambo yanazidi kuwa mabaya tu" alijibu mtu aliekuwa getini.

"Duh afu niliwambiaje kuingia hapa kabla hatujawasiliana?" alihoji Sundi huku akifungua geti.

Alimfungulia Mwasu.

Mwasu alikuwa anamajeraha mwili mzima ya kuchanika chanika hasa usoni.

Haraka akapelekwa kwenye chumba kilichokuwa na vifaa tiba na kuanza kuhudumiwa.

Huduma ilichukua si zaidi ya saa mbili tayari majeraha yalikuwa yamesafishwa na kushonwa vizuri.


Hakuwa na majeraha makubwa sana hivyo akawa yupo timamu kimwili.

Walitoka kukaa sebuleni.

Walimkuta Solomoni akiwa ametulia akitazama runinga.

Mwasu akamtazama Sundi.

Sundi akatoa ishara ya kuwa asijali.

Wakaenda kukaa wote sebuleni huku Mwasu akipeana salamu na Solomoni.


Kitu ambacho Sundi alikijua na Mwasu hakujua kama Sundi anajua ni kuwa katika mipango yao endapo akitokea mtu hatarishi wa kushugulikiwa basi picha yake husambazwa kwa wote na akishakufa pia taarifa hufika kwa wote.

Hivyo Mwasu alishangaa sana kumkuta Solomoni nyumbani kwa Sundi.

Alimchukulia Sundi kama ni msaliti kati yao.

Akapanda kufanya jambo.


Waliendelea kuangalia runinga huku wakisemezana hili na lile.

Mwasu akaomba kutoka nje kidogo akapunge upepo kwa madai amechoka kukaa na majeraha yalimuuma.

Alikubaliwa huku Sundi akijua ni nini Mwasu anaenda kufanya huko nje.

Hakutaka alilowaza litokee.

Mwasu alipofika nje tu akatoa simu yake harakaharaka akatafuta namba za Elchapo ili apige.

Ni wakati simu yake inaita ndipo akajikuta yupo chini bila kupenda.

Sundi alikuwa amempiga teke la mgongoni.

Ngumi zikapangwa na watu walianza kupigana vita ya hatari.

Solomoni Bukaba akisikia vishindo huko nje,mwanzo alipotezea lakini vishindo viliongezeka.

Nae akatoka.


Alijikuta akishuhudia mpambano safi wa wanawake wanaojua vizuri mchezo wa ngumi.

Sundi alikuwa anacheka ili kumgadhabisha Mwasu.

Kicheko chake kilielea vyema kwenye ngome za masikio ya Solomoni.

Alikumbuka kicheko kile.

Ni cha yule yule mwanamke aliemvamia usiku wa balaa kwake.

Ebana eeh!

"Sundi ni nani na anashirikiana na nani!?" alijiuliza Solomoni.

Ni hadi pale alipoona Mwasu akichomoa kisu kutoka maungoni mwake na kwa ustadi wa hali ya juu akakirusha kumwendea Sundi. Na Sundi nae kwa wepesi wa ajabu akajikunja na kisu kikampita sentimita chache tu.

Solomoni hakujua kama Sundi wake laini laini anaweza kuzichapa kiasi kile.

Ilikuwa ni ajabu ila ndivyo ilikuwa.

Sundi alienda juu kama nyani na aliporudi akaachia teke safi lililoishia shingoni kwa Mwasu na kumsambaratisha chini kama mzigo.

Sundi aliona kumwachia Mwasu ni kujizika zaidi yeye hivyo akachomoa bastola ambayo Solomoni hakujua ilitokea wapi mana Sundi alivaa wakati yeye akiwepo na hakuiona.

Hatari hii.

Kisha akashuhudia Sundi akiachia risasi sita bila huruma ambazo zote zilijaa kifuani kwa Mwasu na kumwacha akiwa hana uhai.

"Why!!" aliuliza Solomoni baada ya kuona Sundi amegeuka na kumnyooshea bastola yeye.

Sundi alitamani apasue kichwa cha Solomoni ila nguvu ya mapendo ilizidi utimamu wa akili.

Akajikuta akishusha silaha chini.

"Tuondoke hapa hakutufai" alisema Sandi huku akiishindilia risasi simu ya Mwasu iliokuwa chini.

Iliwabidi kuondoka eneo lile.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tuko kwa Hela hela Maxmillian yamemkuta huko
 
RIWAYA : MPANGO WA CONGO

SEHEMU YA 29

SIMU : 0758573660


***

Usiku ndio muda ambao Mtega nyoka alipanga kufika tena kule makanisa matatu na kwa ushushu wake aliokuwa ameufanya mchana mzima alikuwa amefanikiwa kujua eneo lile huwa lina ulinzi wa kawaida tu nyakati za usiku.

Hivyo usiku ulipofika aliondoka kuelekea huko makanisa matatu.

Alishuka kwenye pikipiki iliomfikisha pale. Akajichanya kwenye vichochoro viwili vitatu lengo likiwa ni kuendelea kusoma ulinzi ulivyowekwa eneo lile.

Lakini pia alijiuliza endapo kulikuwa kuna umuhimu wa kuwa na ulinzi kwenye kanisa lile na nyumba zake.

Hakuona umuhimu huo.

Ilikuwa yapata saa tano usiku,mitaa ile ilikuwa imeishiwa pilikapilika na hivyo kukabaki kimya kabisa.

Mara akiwa ametulia pahali aliweza kuona tena mwanamke mwenye hijabu akikatiza maeneo yale akiwa na haraka zake.

Bado aliutazama mwendo wa mwanamke yule jinsi ulivyokuwa unautata.

Kwa kawaida mwanamke huwa hanyanyui nyayo za miguu yake.
Huburuza.

Ila mwanamke yule alikuwa ananyanyua nyayo zake juu kabisa kama dume.

Akapotelea kwenye kigiza.

Mtega nyoka akaachana nae.

Akarudisha macho yake pale kwenye malango matatu ya kanisa.

Lango la katikati lilikuwa linafunguliwa na wakatoka watu watatu waliokuwa wamevalia suti safi nyeusi.

Watu wale waliangaza huku na huko kisha mmoja akarudi ndani na wawili wakabaki wanaangalia tu.

Kama ungewatazama haraka basi ungejua ni walinzi wa Rais ama Makamu wake.

Baada ya dakika tatu tu likatoka gari la wagonjwa upande wa pili wa lango la kushoto ambako kulikuwa kuna nyumba za watumishi.

Gari ile ilifika hadi karibu na lango lile la katikati ikapaki.

Na ilikinga lango hivyo Mtega nyoka kutoka alipo alishindwa kujua inapakia nini eneo lile.

Baadae kidogo gari ile ikatoka na kuanza safari ya kuelekea mjini.

Na nyuma yake kulifuatia magari mengine kama sita hivi yote yalifanana isipokuwa yalitofautishwa na namba tu za usajili.

Mtega nyoka akataka kutoka pale alipokuwa na kuanza kuyafuatilia ila hakuona usafiri eneo lile na mara nyingi hakupendelea usafiri wa gari zaidi ya pikipiki.


Akaendelea kuvuta subira.

Haikupita nusu saa likaja gari lingine nalo likapaki pale pale na kushusha watu wengine kama sita walikuwa ni wa kiume wote na wakaingia ndani ya Lango lile la katikati.

Mtega nyoka ni kama wazo fulani likamjia.

Akataka kwenda na yeye pale pale langoni ashuhudie kinachoendelea.

Ila akapanga kudandia ukuta na kutokea nyumba za watumishi ambazo kwa haraka alitambua zina milango ya kuingilia ndani ya makanisa yale.

Hivyo akahepa kutoka alipokuwa na kuzunguka mtaa wa nyuma ambao ulikuwa umetulia isipokuwa mbwa waoga walikuwa wanabweka huku na huko.

Akadunda mara ya kwanza na mara ya pili akafanikiwa kuwa juu ya kichochoro fulani cha ukuta na kwa kukitumia akafanikiwa kudaka kingo ya ukuta wa nyumba aliotaka kuingia.

Akafanikiwa kutua kwenye kichaka cha maua na kutulia.

Alimaliza dakika mbili akiwa kimya ili kujua kama kuna aina yoyote ya kiumbe eneo lile.

Hakusikia!!

Akataka kutoka, akasita.

Alisikia sauti ya watu wakiteta

Lakini walionekana wamelewa.

Ajabu hii!!.
.
Watumishi wanalewa!!

Sauti za watu wale zilizidi kukaribia alipokuwa na dhahiri shahiri watu wale walikuwa wamelewa si mchezo.

Waliongea lugha walioelewana wao kwa wao tu.

Waliongea kilevi!!

Hakuna alichojua watu wale walikuja kufanya nje ila akasikia wakiondoka na kuelekea ndani.

Nae haraka akachoropoka na kuingia ndani ya kibalaza walichpoitia watu wale.


Hakuona mtu.

Kwa tahadhari kubwa akaingia ndani ya nyumba ile.

Akapokelewa na sebule tupu.

Nini hiki!!

Akafanya utalii kwenye vyumba alivyoona ni rahisi kukagulika.

Hakuona kitu.

Akaelekea upande kulikokuwa na jiko.

Hakukua na chombo hata kimoja kilichokuwa ndani ya jiko ile.

Ila kuna kitu kilimvutia kwenye ukuta wa jiko lile.

Kulikuwa na kitu kama ufa hivi.

Akaugusa.

Ajabu ukafunguka mithili ya vyumba vinavyotembea ndani ya majengo marefu.

Akapokelewa na hewa safi ya kiyoyozi na taa za rangi.

Akaingia na nyuma ule mlango ukajifunga.

Alijikuta yupo kwenye njia ambayo hakujua ingemfikisha wapi.

Akaifuata!

Akajikuta anaishia kwenye lango lingine ambalo lilikuwa na watu wawili wamesimama na kuliweka kati.

Watu wale walikuwa wamevaa suti kama za wale watu aliowaona wakipokea gari la wagonjwa.

Watu wale wakaziba njia baada ya kumuona na mmoja akanyoosha mkono.

Mtega nyoka hakuelewa ile ilimaanisha nini.

Akapotezea kama anajipapasa mifukoni.


Aligusa kadi!!

Haraka akili yake ikakumbuka kadi aliochukua kwa mvamizi wa Kasuku Contractors.

Akaitoa!!

Alieipokea akaikagua huku na huku aliporidhika akamrudishia kadi ile na kumpisha njiani.

Kanisa gani hili!

Alijiwazia.

Alipoukaribia mlango ule nao ukajifungua kama wa mwanzo na hapo ndipo alipojikuta roho yake ikikosa amani kwa alichokiona.

Langoni alikutana na maandishi makubwa yaliokuwa yamepambwa kwa nakshi nyingi za kuvutia.

WELCOME TO HEAVEN CLUB D

Ndio maneno aliyoyasoma Mtega nyoka.

Miaka buku hii hakuna ambae angeijua!!

Alijiwazia.

Akashuka ngazi zilizokuwa zinaelekea chini na hiyo ilimaanisha anaelekea chini ya majengo yale.


Club D kweli ilikuwa ni kama peponi.

Kulipendezeshwa kuanzia kuta zake hadi sehemu ya kukanyaga na kila hatua aliopiga alipishana na wanaume waliobambiana na wadada walioko uchi huku mziki laini ukitoka kwenye sipika zilizokuwa zimefungwa kitalamu bila kuonekana.

Alizidi kuingia ndani ya Club na hapo alikutana na watu wengine ambao walikuwa wamekaa wanakunywa tu.

Wote walionekana ni watu wa shari nyusoni mwao.


Alifika hadi sehemu kulikokuwa na kaunta ambapo wahudumu wa kike waliokuwa uchi kabisa.

Na kitu alichogundua ni kuwa kila mwanamke aliekuwa mle hakuwa na nguo na hakukutaa kila alieenda kumbambia.

Ufusika ulifanyika hadharani.

Alipewa kinywaji na kukaa viti virefu huku akijizuia kushangaashangaa.

Akiwa bado ametulia akafuatwa na dada mmoja aliekuwa uchi na kumbusu nae akakubali kisha akavutwa mkono na yule dada na taratibu akashuka na kumfuata binti yule ambae alimwonesha ishara ya kidole cha kati ya kuwa huko wanaenda kuburudika kwa ngono.

Waliingia mlango mwingine ambao sasa uliwafikisha kwenye ufuska kamili.

Huko kulikuwa na watu wengi kuliko alikotoka na ngono ilifanyika wazi wazi kwenye jukwaa lililokuwa na warembo waliokuwa wanacheza uchi huku wanaume wakipanda na kufanya nao ngono kidogo na watu wanashangilia kweli kwa kitendo kile.

Macho ya mtega nyoka yalinasa mlango mwingine mbele kidogo ya jukwaa. Mlango ule kulikuwa kuna watu wawili na kila baada ya dakika tatu kuna mtu anaingia na kutoka na mkoba mweusi.

Mtega nyoka alibambiwa na mwanadada aliempeleka kule nae akabambia likawa kosa.

Alisikia tu kucha ikimkwaruza na haikupita hata dakika moja akaanza kuona nyota za rangi nyinginyingi.

Mtega nyoka akawa matatani

******


NB: HAPA NDO MWISHO WA SIMULIZI HII KURUKA HAPA JUKWAANI.
SIMULIZI NYINGI NIMEKUWA NIKIWEKA BURE HAPA MWANZO MWISHO SASA NI WAKATI WAKO NAWE KUUNGA JUHUDI ZA MWANDISHI.

RIWAYA HII SASA UNAWEZA KUIPATA KWA TSH 1000/= NA UTALIPA HAPA 0758573660.
HIYO NI BEI YA KILA MMOJA KUWEZA KUIMUDU HIVYO TUNAOMBA USHIRIKIANO WAKO.

AHSANTENI.

Sasa unaweza kusoma riwaya nyingine hapa
Hekaheka za Komando Zedi Wimba na Jasusi Honda huko Somalia - JamiiForums
 
Back
Top Bottom