RIWAYA : MPANGO WA CONGO
SEHEMU YA 29
SIMU : 0758573660
***
Usiku ndio muda ambao Mtega nyoka alipanga kufika tena kule makanisa matatu na kwa ushushu wake aliokuwa ameufanya mchana mzima alikuwa amefanikiwa kujua eneo lile huwa lina ulinzi wa kawaida tu nyakati za usiku.
Hivyo usiku ulipofika aliondoka kuelekea huko makanisa matatu.
Alishuka kwenye pikipiki iliomfikisha pale. Akajichanya kwenye vichochoro viwili vitatu lengo likiwa ni kuendelea kusoma ulinzi ulivyowekwa eneo lile.
Lakini pia alijiuliza endapo kulikuwa kuna umuhimu wa kuwa na ulinzi kwenye kanisa lile na nyumba zake.
Hakuona umuhimu huo.
Ilikuwa yapata saa tano usiku,mitaa ile ilikuwa imeishiwa pilikapilika na hivyo kukabaki kimya kabisa.
Mara akiwa ametulia pahali aliweza kuona tena mwanamke mwenye hijabu akikatiza maeneo yale akiwa na haraka zake.
Bado aliutazama mwendo wa mwanamke yule jinsi ulivyokuwa unautata.
Kwa kawaida mwanamke huwa hanyanyui nyayo za miguu yake.
Huburuza.
Ila mwanamke yule alikuwa ananyanyua nyayo zake juu kabisa kama dume.
Akapotelea kwenye kigiza.
Mtega nyoka akaachana nae.
Akarudisha macho yake pale kwenye malango matatu ya kanisa.
Lango la katikati lilikuwa linafunguliwa na wakatoka watu watatu waliokuwa wamevalia suti safi nyeusi.
Watu wale waliangaza huku na huko kisha mmoja akarudi ndani na wawili wakabaki wanaangalia tu.
Kama ungewatazama haraka basi ungejua ni walinzi wa Rais ama Makamu wake.
Baada ya dakika tatu tu likatoka gari la wagonjwa upande wa pili wa lango la kushoto ambako kulikuwa kuna nyumba za watumishi.
Gari ile ilifika hadi karibu na lango lile la katikati ikapaki.
Na ilikinga lango hivyo Mtega nyoka kutoka alipo alishindwa kujua inapakia nini eneo lile.
Baadae kidogo gari ile ikatoka na kuanza safari ya kuelekea mjini.
Na nyuma yake kulifuatia magari mengine kama sita hivi yote yalifanana isipokuwa yalitofautishwa na namba tu za usajili.
Mtega nyoka akataka kutoka pale alipokuwa na kuanza kuyafuatilia ila hakuona usafiri eneo lile na mara nyingi hakupendelea usafiri wa gari zaidi ya pikipiki.
Akaendelea kuvuta subira.
Haikupita nusu saa likaja gari lingine nalo likapaki pale pale na kushusha watu wengine kama sita walikuwa ni wa kiume wote na wakaingia ndani ya Lango lile la katikati.
Mtega nyoka ni kama wazo fulani likamjia.
Akataka kwenda na yeye pale pale langoni ashuhudie kinachoendelea.
Ila akapanga kudandia ukuta na kutokea nyumba za watumishi ambazo kwa haraka alitambua zina milango ya kuingilia ndani ya makanisa yale.
Hivyo akahepa kutoka alipokuwa na kuzunguka mtaa wa nyuma ambao ulikuwa umetulia isipokuwa mbwa waoga walikuwa wanabweka huku na huko.
Akadunda mara ya kwanza na mara ya pili akafanikiwa kuwa juu ya kichochoro fulani cha ukuta na kwa kukitumia akafanikiwa kudaka kingo ya ukuta wa nyumba aliotaka kuingia.
Akafanikiwa kutua kwenye kichaka cha maua na kutulia.
Alimaliza dakika mbili akiwa kimya ili kujua kama kuna aina yoyote ya kiumbe eneo lile.
Hakusikia!!
Akataka kutoka, akasita.
Alisikia sauti ya watu wakiteta
Lakini walionekana wamelewa.
Ajabu hii!!.
.
Watumishi wanalewa!!
Sauti za watu wale zilizidi kukaribia alipokuwa na dhahiri shahiri watu wale walikuwa wamelewa si mchezo.
Waliongea lugha walioelewana wao kwa wao tu.
Waliongea kilevi!!
Hakuna alichojua watu wale walikuja kufanya nje ila akasikia wakiondoka na kuelekea ndani.
Nae haraka akachoropoka na kuingia ndani ya kibalaza walichpoitia watu wale.
Hakuona mtu.
Kwa tahadhari kubwa akaingia ndani ya nyumba ile.
Akapokelewa na sebule tupu.
Nini hiki!!
Akafanya utalii kwenye vyumba alivyoona ni rahisi kukagulika.
Hakuona kitu.
Akaelekea upande kulikokuwa na jiko.
Hakukua na chombo hata kimoja kilichokuwa ndani ya jiko ile.
Ila kuna kitu kilimvutia kwenye ukuta wa jiko lile.
Kulikuwa na kitu kama ufa hivi.
Akaugusa.
Ajabu ukafunguka mithili ya vyumba vinavyotembea ndani ya majengo marefu.
Akapokelewa na hewa safi ya kiyoyozi na taa za rangi.
Akaingia na nyuma ule mlango ukajifunga.
Alijikuta yupo kwenye njia ambayo hakujua ingemfikisha wapi.
Akaifuata!
Akajikuta anaishia kwenye lango lingine ambalo lilikuwa na watu wawili wamesimama na kuliweka kati.
Watu wale walikuwa wamevaa suti kama za wale watu aliowaona wakipokea gari la wagonjwa.
Watu wale wakaziba njia baada ya kumuona na mmoja akanyoosha mkono.
Mtega nyoka hakuelewa ile ilimaanisha nini.
Akapotezea kama anajipapasa mifukoni.
Aligusa kadi!!
Haraka akili yake ikakumbuka kadi aliochukua kwa mvamizi wa Kasuku Contractors.
Akaitoa!!
Alieipokea akaikagua huku na huku aliporidhika akamrudishia kadi ile na kumpisha njiani.
Kanisa gani hili!
Alijiwazia.
Alipoukaribia mlango ule nao ukajifungua kama wa mwanzo na hapo ndipo alipojikuta roho yake ikikosa amani kwa alichokiona.
Langoni alikutana na maandishi makubwa yaliokuwa yamepambwa kwa nakshi nyingi za kuvutia.
WELCOME TO HEAVEN CLUB D
Ndio maneno aliyoyasoma Mtega nyoka.
Miaka buku hii hakuna ambae angeijua!!
Alijiwazia.
Akashuka ngazi zilizokuwa zinaelekea chini na hiyo ilimaanisha anaelekea chini ya majengo yale.
Club D kweli ilikuwa ni kama peponi.
Kulipendezeshwa kuanzia kuta zake hadi sehemu ya kukanyaga na kila hatua aliopiga alipishana na wanaume waliobambiana na wadada walioko uchi huku mziki laini ukitoka kwenye sipika zilizokuwa zimefungwa kitalamu bila kuonekana.
Alizidi kuingia ndani ya Club na hapo alikutana na watu wengine ambao walikuwa wamekaa wanakunywa tu.
Wote walionekana ni watu wa shari nyusoni mwao.
Alifika hadi sehemu kulikokuwa na kaunta ambapo wahudumu wa kike waliokuwa uchi kabisa.
Na kitu alichogundua ni kuwa kila mwanamke aliekuwa mle hakuwa na nguo na hakukutaa kila alieenda kumbambia.
Ufusika ulifanyika hadharani.
Alipewa kinywaji na kukaa viti virefu huku akijizuia kushangaashangaa.
Akiwa bado ametulia akafuatwa na dada mmoja aliekuwa uchi na kumbusu nae akakubali kisha akavutwa mkono na yule dada na taratibu akashuka na kumfuata binti yule ambae alimwonesha ishara ya kidole cha kati ya kuwa huko wanaenda kuburudika kwa ngono.
Waliingia mlango mwingine ambao sasa uliwafikisha kwenye ufuska kamili.
Huko kulikuwa na watu wengi kuliko alikotoka na ngono ilifanyika wazi wazi kwenye jukwaa lililokuwa na warembo waliokuwa wanacheza uchi huku wanaume wakipanda na kufanya nao ngono kidogo na watu wanashangilia kweli kwa kitendo kile.
Macho ya mtega nyoka yalinasa mlango mwingine mbele kidogo ya jukwaa. Mlango ule kulikuwa kuna watu wawili na kila baada ya dakika tatu kuna mtu anaingia na kutoka na mkoba mweusi.
Mtega nyoka alibambiwa na mwanadada aliempeleka kule nae akabambia likawa kosa.
Alisikia tu kucha ikimkwaruza na haikupita hata dakika moja akaanza kuona nyota za rangi nyinginyingi.
Mtega nyoka akawa matatani
******
NB: HAPA NDO MWISHO WA SIMULIZI HII KURUKA HAPA JUKWAANI.
SIMULIZI NYINGI NIMEKUWA NIKIWEKA BURE HAPA MWANZO MWISHO SASA NI WAKATI WAKO NAWE KUUNGA JUHUDI ZA MWANDISHI.
RIWAYA HII SASA UNAWEZA KUIPATA KWA TSH 1000/= NA UTALIPA HAPA 0758573660.
HIYO NI BEI YA KILA MMOJA KUWEZA KUIMUDU HIVYO TUNAOMBA USHIRIKIANO WAKO.
AHSANTENI.
Sasa unaweza kusoma riwaya nyingine hapa
Hekaheka za Komando Zedi Wimba na Jasusi Honda huko Somalia - JamiiForums