warumi
R I P
- May 6, 2013
- 16,218
- 18,440
- Thread starter
-
- #181
@MosDef,
Umeongea vitu vingi sana lakini inaonekana unachanganya mambo! Kwanza, unaposema cjui XYZ alikopi idea unapaswa kufahamu kwamba hakuna hatimiliki ya idea, yaani wazo... Kwa maana nyingine, haikatazwi kutumia idea ya movie nyingine! Ninachoona ni kwamba unachanganya kati ya Idea (Wazo) na Maudhui (Contents)... hivi ni vitu viwili tofauti! Mwandishi wa JB ameeleza vizuri... alichokopi yeye sio idea/wazo bali ni maudhui/content! Kwa bahati mbaya sijaziona filamu zote mbili lakini inavyoelekea ni kwamba hizo filamu zimefanana sana... kama hivyo ndivyo, basi kilichokuwa copied sio idea kama unavyoeleza!
Unapochukua maudhui ya filamu ya mtu mwingine lazima mfanye makubaliano... haitoshi tu ku-acknowledge. Ngoja nikuulize... umeshapata kusikia kampuni ya utengenezaji filamu imenunua filamu ambayo imeshachezwa? Kama hujasikia, basi mazingira yenyewe ndo kama haya ya JB na filamu ya Kihindi, kwamba baada ya JB kuiona hiyo hiyo fulani na kuipenda basi alitakiwa kuongea na wenyewe na kufikia makubaliano... ama kwa kuuziana au kupeana bure! Lakini hata kama angepewa bure, bado mmiliki wa Ladies VS Ricky Bahl angependa kufahamu what will happen akitokea mtu mwingine akaiona filamu ya JB ambayo maudhui ni ya Ladies VS Ricky Bahl! Assume kuna Peoducer wa Hollywood ameiona filamu ya JB na akaipenda na hivyo kuamua kuinunua ili akaitengeze upya (hii inafanyika sana Hollywood)! Sasa katika mazingira kama hayo haiwezekani, kwa mfano huyo Producer wa Hollywood amlipe JB $ 500 million halafu pesa hiyo iwe ya JB wakati original work ni ya Mdosi! Ndio maana nikasema kwamba, hata ikitokea Mdosi amempa JB filamu bure na yeye kusubiria tu acknowledgement lakini lazima atahitaji kufahamu anapotokea mtu mwingine nani atapata nini! Hii haitofautiani sana na suala la uuzaji wa wachezaji! Leo hii TP Mazembe wakimuuza Mbwana Samatta, lazima kutakuwa na mgao utakaokuja Simba!
Pili umezungumzia suala la Hollywood kutengeneza filamu zao kwa kutokea kwenye novel na religious books! Tuache hilo la religious books na tujikite kwenye novels! Kwanza kabisa, sina hakika kama umewahi kuiona mikataba ya uuzianaji wa script kwa Hollywood! Kwenye mkataba, Mwandishi lazima useme ikiwa script ni original material or adapted material (from novel)! Kama material ume-adapt kutoka kwenye novel, hiyo script huwezi kuuza wala ku-option unless umethibitisha kwamba umekuwa granted right ya ku-adapt novel husika lakini sio unasema tu based on novel so and so, ndo basi tena!
Hilo la sequel labda nikuambie jambo moja! Producer/Production Company inaponunua script yako, kwenye mkataba lazima utakuta kipengele kinachosema wazi kwamba script unayouza unauza pamoja na haki ya utengenezaji wa sequel kupitia script yako! Therefore hata sequel nazo zinakuwa zimelipiwa!!! Leo hii ukitengeneza T-shirt ukazi-lable Taken kwa kumaanisha hiyo movie, basi lazima nayo uwalipe wamiliki wa filamu husika! Na hapa ndio maana linapokuja suala la mikataba, Hollywood wanataka ONLY Entertainment Lawyer coz' kuna mambo mengi kwa lawyer asiye kwenye industry hawezi kuyafahamu! Hii maana yake ni nini? Ingawaje Mkataba unamtaka Mwandishi anapouza script yake anauza na haki yakutengeneza sequel plus any other materials kama vile T-Shirt lakini Mwanasheria wa Mwandishi wa Script nae atataka kufahamu kwamba, pamoja na kwamba mteja wake anauza hadi haki ya utengenezaji wa sequel, t-shirts na mambo mengine... je, atakuwa compensated vipi? Hapa ndo unakuta mkataba unasema pamoja na kwamba anauza hizo haki, lakini akitokea mtu mwingine akataka kutengeneza series kupitia the same script basi mwandishi atapata kiasi fulani kwa idadi fulani ya episodes! Au, atapewa one payment ya kiasi fulani!
Mwisho umemalizia kwamba hata Hollywood ideas zimeisha na wamebakia kwenye re-make... you're right lakini naomba nikukumbushe tena tusichanganya idea na contents... hivi ni vitu viwili tofauti! Aidha kwamba movie fulani ya Hollywood ni copy and paste ya movie nyingine ya UK nayo sio hoja kwavile hakuna anayekataa kwamba hakuna copy and paste provided wahusika walikubaliana!
Kwa waliipitia chuo watakuwa wanaelewa kuhusu INTELLECTUAL PROPERTY RIGHTS ambapo uko utakuta mambo ya patents, copyrights na mambo ya trade mark. Ninaposema IPR namaanisha creations of minds kama music, literature and other artistic works, alichokifanya JB ni COPYRIGHT INFRINGEMENT, yaani ka produce kitu ambapo kimeshakuwa produced, sio haki kisheria, ndio maana kila siku wasanii mnapigiwa makerere mrudi shuleni ndo matokeo yake haya