Je, baba alitutesa au alitufundisha maisha?

Naon kabisa mzee alifeli kukukomaza bado ni mtoto wa mama unalia lia Jf na mambo madogo. .

Kuna mshikahu mzee wake alimpa kazi ya kunya kwenye shamba lote heka tatu kwa sababu yeye ni mfugo unatakiwa atoe mbolea (hakuwa na mifugo mingine). .
 
Naon kabisa mzee alifeli kukukomaza bado ni mtoto wa mama unalia lia Jf na mambo madogo. .

Kuna mshikahu mzee wake alimpa kazi ya kunya kwenye shamba lote heka tatu kwa sababu yeye ni mfugo unatakiwa atoe mbolea (hakuwa na mifugo mingine). .
Mkuu hahaha matukio madogo tu nimayaeleza hapo juu Kuna mengi mengine sio ya kusimulia

Kunya shambani mbona simple tu au labda kwa siku moja amalize shamba lote ni tatizo
 

Mshua alichofanya alitimiza wajibu wake Kama baba ili msije kumlaumu au kulaumiwa na wanajamii hapo baadae. Madingi wa hivi wako wachache sana zama hizi
 
Mkuu hahaha matukio madogo tu nimayaeleza hapo juu Kuna mengi mengine sio ya kusimulia

Kunya shambani mbona simple tu au labda kwa siku moja amalize shamba lote ni tatizo
Karibu ya shamba lao kuna shule ya msingi ukinya lazima wakuone😀

Sasa wewe bab yako si alikuadhibu lipompoteza jogoo mkamtafute. Ingekuwaje kama angekuadhibu uwike kama jogoo kila saa kumi usiku😀
 
Mshua alichofanya alitimiza wajibu wake Kama baba ili msije kumlaumu au kulaumiwa na wanajamii hapo baadae. Madishi wa hivi wako wachache sana zama hizi
Kwer mkuu wazazi wa saiz wanaogopa kesi za child abuse zimekuwa nyingi afu watoto wa siku hizi wako vizuri kwenye kujieleza
Tofauti na wazaman ni kutii maagizo hakuna kuhoji
 
Karibu ya shamba lao kuna shule ya msingi ukinya lazima wakuone😀

Sasa wewe bab yako si alikuadhibu lipompoteza jogoo mkamtafute. Ingekuwaje kama angekuadhibu uwike kama jogoo kila saa kumi usiku😀
😁😁😁😁🙌
Aisee ningetoloka nyumbani tatizo sio kutafuta jogoo ni mda alitutoa nje haukuwa rafiki afu ukichek tulikuwa watoto
 
Naona kwenye tofali alikua anakomoa ila mengine mfano kumwagilia kuzingatia kuku wameingia wote alikua anawafundisha namna gani ya kuwa na usimamizi wa mambo yako na kama mwanaume lazima uwe na mazingira yako. Mimi hapa nacomment ila namwagilia migomba yangu kadhaa na miembe hii inasaidia siku za kumwagilia lazima niwahi na kufanya kazi sio dhambi
 
Sahihi mkuu alitufundisha tuishi Kama wanaume respect nyingi kwa mshua
 
Alitakiwa kuwa-treat zaidi ya hapo.
Nina matukio mengi Sana nitakuwa nayaandika hapa kidogo lengo sio kumchafua mzee, ili tuweze kujifunza na sisi tunaitwa baba now vip tupambane na watoto wetu kwenye malezi
 
Bahati nzuri umeuliza swali na jibu lake ni HAPANA.

Wakati nasoma nilikuwa naishi na kaka yangu ambae pia ni askari wa JW mpaka hivi sasa.Nakumbuka mwaka 2011 nikiwa form two baada ya kujikuta nimechelewa kwenda shule na inatakiwa nisafishe banda la kuku ikabidi nisogeze kile kinyesi cha kuku pembeni kwenye kona humohumo bandani nikasepa zangu shule. Wakati narudi kutoka shule namkuta yeye anafyeka nje ya fance nikampita chap kwa haraka asinione ili nikatoe kile kinyesi nilichoacha asubuhi kwa kudhani atakuwa hajakiona.

Naingia bandani nakuta pamefagiliwa safi,ikabidi niende fasta ndani kwangu nikabadilishe nguo ili nikapike chakula cha mbwa. Ile nafungua mlango wa chumbani kwangu nakutana na kinyesi cha kuku hapo chin,niliishiwa nguvu kwakwel. Lakini hapohapo nikaanza kujiuliza,yaani hiki kitu kidogo tu ndyo apaniki kiasi cha kuniwekea uchafu tena kinyesi cha kuku ndani ninakolala binadamu?

Wakati naendelea kujiuliza swali hilo kugeuka nyuma jamaa huyu hapa,"unashaangaa nini? Unadhani wale kuku walikuwa hawaoni kinyaa?. Sasa hicho kinyesi hakuna kutoa na hakuna kuwasha feni ili ujue kuwa na wao walikuwa wanaumia" maelekezo yake hayo.

Usiku ilibidi niamke kwenda kujisomea japo sikuwa na utaratibu huo bila kutaka kutokana na harufu kali iliyokuwa imeenea chumba kizima. Na tangu siku hiyo sijawahi kuchukulia kitu chochote masihara.
 
We tofali 100 tu unalia wenzio tulikua tunabeba tofari 5000 tunapanga tanuru. Kiufupi babayenu alikua anawaanda muwe watu ambao sio tegemezi hapo kesho. So apigiwe salute zake za kutosha KUDOS DINGI
 
Mkuu tuliishi kijeshi Sana respect Sana kwao makamanda wetu
 
We tofali 100 tu unalia wenzio tulikua tunabeba tofari 5000 tunapanga tanuru. Kiufupi babayenu alikua anawaanda muwe watu ambao sio tegemezi hapo kesho. So apigiwe salute zake za kutosha KUDOS DINGI
Malezi ni tofauti mkuu sis wengine tumezaliwa town Kaz ngum hatukuzoea
 
Huyu sasa ndio aliwafundisha Kwa vitendo bila kukutesa,aliwaonyesha umuhimu wa kuyachukulia mambo serious.

Nakumbuka na Sisi tulifundishwa Kwa vitendo Jambo Fulani,ilikuwa mwaka Mpya,baada ya shamra shamra za kuingia mwaka Mpya,hatukuingia ndani kulala badala yake tulikesha Kwa disco,kufika asubuhi mshua akatumbia hakuna kulala tuchukue majembe na kulima bustani,daah sio poa,hivi umeshawi ona mtu analala huku amesimama na jembe mkononi?

Basi hakika alitufundisha kitu ambacho hatukukisahau
 
Chief

Kwa upande wangu naona Mzee wenu ingawa alikuwa na Nia ya kuwafundisha lakini hakuwa na namna nzuri ya kufanya hivyo,Bali aliwapelekesha kijeshi jeshi Tu.

Mfano muamshwe usiku WA manane kumtafuta jogoo,je mngepata madhara ya kuumwa na viumbe kama nyoka ingekuwaje Kwa usiku huo?

Ila kuhusu kumwagilia mimea hakika nakubaliana nae,ingawa Napo kuna changamoto moja,je kama mimea ingenyauka Kwa ugonjwa,nyie kosa lenu ni lipo?

Anyways ndio changamoto za kuwa na wazazi wajeda,mambo ya kazini wanayaleta home.
 
He was molding you to be PERSISTENT in whatever you are doing. Nothing bad !!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…