Je, bodaboda wa Dar es Salaam kulipwa fidia? Rejea maneno ya Lema: “Bodaboda sio ajira”.

Je, bodaboda wa Dar es Salaam kulipwa fidia? Rejea maneno ya Lema: “Bodaboda sio ajira”.

Pantosha

JF-Expert Member
Joined
Sep 22, 2022
Posts
640
Reaction score
958
IMG_0679.png


Watanzania wengi hawapendi kujua ukweli. Nadhani hulka hii inatokana na wananchi kufungiwa nchini mwao na hivyo kukosa nafasi ya kuona jinsi nchi zingine zilivyoendelea.

Kuna siku Lema alisema bodaboda sio ajira, watu walikuja juu na kusema kuwa kawakosea watu na ni kama anadharau ajira za watu. Wadiriki kusema kuwa bodaboda ni Kama ajira zingine. Cha kushangaza leo hii viongozi hao hao waliomsema Lema, wamewafungia bodaboda wasifanye kazi ili wapishe mkutano, je watatoa fidia kwa bodaboda?
 
Yule Mwenyekiti wa Boda boda aliyeunga mkono juhudi za CCM Yuko Wapi?
 
Kwanini umesema bodaboda tu? Hata magari ya kawaida kwa hizo siku hayataingis mjini. Polisi wamesisitiza bodaboda kwasababu huwa hawatii maagizo. Na ni rahisi wao kupenya vizuizi.
BTW huko mjini Posta bodaboda na bajaj zipigwe marufuku kabisa. Kuna sehemu nyingine nyingi tu wanaweza kufanya kazi sio Posta tu.
 
View attachment 3214254

Watanzania wengi hawapendi kujua ukweli. Nadhani hulka hii inatokana na wananchi kufungiwa nchini mwao na hivyo kukosa nafasi ya kuona jinsi nchi zingine zilivyoendelea.

Kuna siku Lema alisema bodaboda sio ajira, watu walikuja juu na kusema kuwa kawakosea watu na ni kama anadharau ajira za watu. Wadiriki kusema kuwa bodaboda ni Kama ajira zingine. Cha kushangaza leo hii viongozi hao hao waliomsema Lema, wamewafungia bodaboda wasifanye kazi ili wapishe mkutano, je watatoa fidia kwa bodaboda?
Watanzania wengi hawapendi kujua ukweli. Nadhani hulka hii inatokana na wananchi kufungiwa nchini mwao na hivyo kukosa nafasi ya kuona jinsi nchi zingine zilivyoendelea.
 
BTW huko mjini Posta bodaboda na bajaj zipigwe marufuku kabisa. Kuna sehemu nyingine nyingi tu wanaweza kufanya kazi sio Posta tu.
Posta ni kwa nani?
Kwanini wapigwe marufuku?
Je wanamkosea nani?
Je kama wewe una sababu za kuwakataa, huko kwingine wana sababu gani za kuwataka?
 
Dar ina barabara tisa tu?

Tatizo hoja zinazojengwa hazina mashiko!
 
View attachment 3214254

Watanzania wengi hawapendi kujua ukweli. Nadhani hulka hii inatokana na wananchi kufungiwa nchini mwao na hivyo kukosa nafasi ya kuona jinsi nchi zingine zilivyoendelea.

Kuna siku Lema alisema bodaboda sio ajira, watu walikuja juu na kusema kuwa kawakosea watu na ni kama anadharau ajira za watu. Wadiriki kusema kuwa bodaboda ni Kama ajira zingine. Cha kushangaza leo hii viongozi hao hao waliomsema Lema, wamewafungia bodaboda wasifanye kazi ili wapishe mkutano, je watatoa fidia kwa bodaboda?
Elimu yako imeishia wapi mpk usijue maana ya fidia
 
Back
Top Bottom