Je, dini inaweza kukupeleka kwa Mungu?

Je, dini inaweza kukupeleka kwa Mungu?

MrfursaTZA

Member
Joined
Jul 26, 2024
Posts
29
Reaction score
94
IMG_8888.jpeg

Ningependa kujua, je, inawezekana kuwa Rais wa nchi wakati wewe si Raia wa nchi hiyo?

Pia ningependa kufahamu, Mungu ni wa dini gani? Je, ni Muislamu au Mkristo?

Kwa nini Masheikh na Wachungaji husema kwamba dini haiwezi kukufikisha Mbinguni?

Kama Dini haziwezi kutupeleka Mbinguni, basi kwa nini zipo? Kama Mungu yuko upande wa Wakristo, kwa nini hawapendelei?

Na kama Mungu ni wa Waislamu, kwa nini nao hawapendelei? Je, inamaanisha nini kusema kwamba Mungu ni wa kila mtu?

Kwa nini alitufanya tofauti kwa rangi? Na kwa nini alitufanya tofauti hata kwa jinsi tunavyoishi duniani au kwa kipato?

Kwanini aliumba shida na matatizo?

Na kusema kwamba alituumba kwa mfano wake, ningependa kujua, kama sisi ni mfano wa Mungu, je, hii inamaanisha kwamba Mungu anakula chakula, anaenda chooni, na pia anakabiliana na matatizo kama sisi?

Kama jibu ni hapana, kwa nini sisi, ambao ni mfano wa Mungu, tunateseka hivi wakati yeye ana uwezo mkubwa wa kutusaidia?
 
Dini tofauti zina maoni tofauti kuhusu njia ya kufika mbinguni au kupata wokovu.

1. Ukristo: Wanaamini kuwa imani kwa Yesu Kristo kama Mwokozi ndiyo njia ya pekee ya kufika mbinguni. Wanaamini kuwa kwa kumwamini Yesu na kufuata mafundisho yake, mtu anaweza kupata wokovu na kuingia mbinguni.

2. Uislamu: Unafundisha kuwa kufuata mafundisho ya Mwenyezi Mungu kama yalivyofunuliwa kwa Mtume Muhammad (SAW) na kuishi maisha ya wema kunaweza kumpeleka mtu Peponi. Muislamu anatakiwa kufuata nguzo za Uislamu na kuishi maisha yanayompendeza Mwenyezi Mungu.

3. Uhindu: Unahusisha dhana ya karma na samsara (mzunguko wa kuzaliwa upya). Mtu anayefanya matendo mema anaweza kufikia hali ya moksha (ukombozi) ambayo ni hali ya kutokuwa na kuzaliwa tena na kuungana na Mungu.

4. Ubuddha: Unasisitiza kupata ukombozi kupitia mwanga wa kiroho na kuacha mzunguko wa kuzaliwa upya. Hii inafanyika kwa kufuata Njia ya Miduara Minane (Noble Eightfold Path) na kufikia hali ya Nirvana.

Kwa hivyo, kama dini inaweza kukupeleka mbinguni au la, inategemea zaidi na imani yako na dini unayofuata. Kila dini ina njia yake ya kuuelewa wokovu na maisha baada ya kifo.
 
Mungu hajawahi kuwepo, hayupo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.

Dini ni utumwa wa fikra.

Mbingu Haipo.

Heaven is the promise for the poor so that they don't demand happiness on earth.
Hii unaitoa wapi Mkuu? Au maneno ya mitandaoni na fikra za watu wenye pesa nyingi hasa Wazungu?
Kwa mfano simu yako ikiwa mbovu si lazima utaipeleka kwa fundi ikatengenezwe? Au kama ina warrant ikisumbua ukairudisha ulipoinunua unaweza ukabadilishiwa na ukapewa simu nyingine? Kama unaweza ukafanya hivyo Kwanini hauamini kuna uumbaji? Mungu yupo lakini kwenye hizi dini ndio kuna changamoto lakini la msingi amini kile unachokiamini na Mungu yupo. Hayo mengine yanayotokea Shida, magonjwa,vifo ni matokeo ya matendo yetu sisi wanadamu.
 
Hii unaitoa wapi Mkuu?
Kwani lazima itoke mahali?

Imetoka kwangu.
Au maneno ya mitandaoni na fikra za watu wenye pesa nyingi hasa Wazungu?
Kuwa na pesa, kutokuwa na pesa hakuhusiani na uwepo wa huyo Mungu.

Huyo Mungu hayupo.

Kwa mfano simu yako ikiwa mbovu si lazima utaipeleka kwa fundi ikatengenezwe? Au kama ina warrant ikisumbua ukairudisha ulipoinunua unaweza ukabadilishiwa na ukapewa simu nyingine? Kama unaweza ukafanya hivyo Kwanini hauamini kuna uumbaji?
Kama kila kitu lazima kina uumbaji, Hata huo uumbaji utahitaji kuwa na uumbaji mwingine, Na huo uumbaji mwingine uwe na uumbaji mwingine. Hivyo hivyo pasipo kukoma.

Na kama si lazima kila kitu kina uumbaji, Hata Dunia haihitaji uumbaji.
Mungu yupo lakini kwenye hizi dini ndio kuna changamoto lakini la msingi amini kile unachokiamini na Mungu yupo. Hayo mengine yanayotokea Shida, magonjwa,vifo ni matokeo ya matendo yetu sisi wanadamu.
Huyo Mungu angekuwepo kweli, Kusingekuwa hata na haja ya kuamini au kuhoji uwepo wake.

Kila mtu angejua kwa uhakika kabisa bila kuhitaji imani au dini kwamba Mungu huyo yupo.

Mnahangaika sana kumwelezea na kumuongelea huyo Mungu, Kwa vile hajawahi kuwepo kujiongelea, kujitetea na kujidhihirisha mwenyewe yeye kama yeye kwamba yupo.

Mungu huyo ni fictional character, Hajawahi kuwepo, Hayupo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.
 
Wazazi tunapombana kusomesha watoto wetu, na tunapo risk hata mali zetu na maisha yetu kwa ajili yenu basi muwe na huruma, kwasababu hatutegemei kuona mnauliza maswali kama haya na kuona kuwa mna mitazamo kama hii. Tunataka watoto wenu na wajukuu zenu wasipitie aina ya maisha tuliyoyapitia sisi, inauma sana ...
 
Dini ni mfumo wa imani kuhusu mambo ya kiroho unaoendeshwa kupitia matendo ya kibinadamu. Matendo haya ni yale yenye uelekeo, utaratibu, na masharti yenye kuthibitisha utiifu wa mtu kwa mfumo huo husika..

Masharti hayo humfanya muumini ama mfuasi wa dini aamini uwepo wa mamlaka kuu ya kiroho ama kitu chochote kile kisichoonekana chenye kustahili kuabudiwa na wanadamu.

Dini ni mfumo wa maisha ya kibinadamu ukijumuisha miiko, utaratibu, au ustaarabu wa kufuata. Muundo huu wa kidini huambatana na msururu wa vyeo vya kimamlaka pamoja na safu mbalimbali za viongozi wenye madaraka tofauti ili kuweza kuulinda mfumo husika, ulio na wafuasi chini yake wanaowaongaza,.

Ili kuweza kuilinda mfumo huu, ni lazima imani ya dini husika ijengeke ili kuweza kulinda maslahi, mustakabali, pia na mwenendo mzima wa dini husika. Kila dini huamini yenyewe ndiyo pekee iliyoasisiwa na mungu wake mwenyewe.

Nukuu ifuatayo kutoka katika maandiko matakatifu inatupa picha kamili kuhusu dini na imani tofauti za kidini,

YAKOBO 1:
26 “Mtu akidhani ya kuwa anayo dini, wala hauzuii ulimi wake kwa hatamu, hali akijidanganya moyo wake, dini yake mtu huyo haifai.

27 Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa.”

Kwa hiyo basi, si jambo baya mtu kuwa chini ya mfumo wa kidini. Cha msingi ni kuishi chini ya imani ya kweli na halisi ya Mungu Muumba.
 
Ni kitu gani kinashindwa kuwafanya muelewe na mjue kuwa hizi dini na mambo ya imani kwa ujumla ni moja ya ubunifu na mtindo wa maisha ya mtu wa kale? Ndio ilikuwa aina ya uongozi katka jamiii nisawa na leo hii mgombea wa uraisi wa marekani anajinadi kwa kuilinda demokrasia na kupambana na rushwa ila sisi tunajinadi na nitajenga daraja, na barabara na hospital na hata shule? .
 
Hii unaitoa wapi Mkuu? Au maneno ya mitandaoni na fikra za watu wenye pesa nyingi hasa Wazungu?
Kwa mfano simu yako ikiwa mbovu si lazima utaipeleka kwa fundi ikatengenezwe? Au kama ina warrant ikisumbua ukairudisha ulipoinunua unaweza ukabadilishiwa na ukapewa simu nyingine? Kama unaweza ukafanya hivyo Kwanini hauamini kuna uumbaji? Mungu yupo lakini kwenye hizi dini ndio kuna changamoto lakini la msingi amini kile unachokiamini na Mungu yupo. Hayo mengine yanayotokea Shida, magonjwa,vifo ni matokeo ya matendo yetu sisi wanadamu.
Mungu muweza wa yote na mwenye upendo wote na anaejua kila kitu hawezi kushindwa kuzuia wewe usiumwe na au kuumba kizazi ambacho anajua kabisa kitamsaliti na atakiangamiza kwa garika au kukichoma moto siku ya mwisho, kufananisha uwezo wa mungu na uwezo wa mtengeneza simu ni dhahiri pia mungu huwa ana beti kwamba hajui kama yanga ingeweza kumfunga azamu 4_1
 
Mungu muweza wa yote na mwenye upendo wote na anaejua kila kitu hawezi kushindwa kuzuia wewe usiumwe na au kuumba kizazi ambacho anajua kabisa kitamsaliti na atakiangamiza kwa garika au kukichoma moto siku ya mwisho, kufananisha uwezo wa mungu na uwezo wa mtengeneza simu ni dhahiri pia mungu huwa ana beti kwamba hajui kama yanga ingeweza kumfunga azamu 4_1
😂😂😂
Mbona umeingiza swaga za mashahidi wa Jehovah ukaja ukaingiza na mambo ya mpira???
Pole Dada haya mambo ukiyafuatilia sana unakuwa kichaa. Ishi kwenye kusudi lako tu.
 
Dini ni imani juu ya mambo ya dhahania, yasiyokuwepo wala hayathibitishiki.

Vitabu vya dini ni masimulizi ya aina mbalimbali ya dhahania. Genre zake ni kutoka fables, fantasy, legends n.k.
Masimulizi yake yanaakisi maisha ya kawaida kwa kiwango fulani lakini haimaanishi kwamba hao characters (including mungu) ni halisia.
Ni watu wamejiundia kwa faida zao binafsi.

Unapofikia umri wa utu uzima, una wajibu wa kutambua uongo na ukweli. Ukiamua kuamini kuna nyoka aliongea na mwanamke ndiyo maana watu wanakufa, shauri zako.

NB: Tuwe wema, wenye upendo na utu.
Tusiache chuki na hofu za mafundisho ya dini yakatawala akili zetu.
 
Mungu hajawahi kuwepo, hayupo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.

Dini ni utumwa wa fikra.

Mbingu Haipo.

Heaven is the promise for the poor so that they don't demand happiness on earth.

kwa mujibu wa kitabu kipi ulichosoma ??
 
Dini ni mfumo wa imani za kuhusu mambo ya kiroho unaoendeshwa kupitia matendo ya kibinadamu. Matenso haya ni yale yenye uelekeo, utaratibu, na masharti yenye kuthibitisha utiifu wa mfumo husika..

Masharti hayo humfanya muumini ama mfuasi aamini uwepo wa mamlaka kuu ya kiroho ama kitu chochote kile kisichoonekana chenye kustahili kuabudiwa na wanadamu.

Dini ni mfumo wa maisha ya kibinadamu ukijumuisha miiko, utaratibu, au ustaarabu wa kufuata. Muundo wa kidini huambatana na msururu vyeo na safu za viongozi, mamlaka na madaraka juu ya uongozi wa mfumo husika, ulio na wafuasi chini yake wanaowaongaza, ili kuweza kuilinda imani na mwenendo mzima wa dini husika.

Nukuu ifuatayo kutoka katika maandiko matakatifu inatupa picha kamili kuhusu dini na imani tofauti za kidini,

YAKOBO 1:
26 “Mtu akidhani ya kuwa anayo dini, wala hauzuii ulimi wake kwa hatamu, hali akijidanganya moyo wake, dini yake mtu huyo haifai.

27 Dini iliyo safi, isiyo na taka mbele za Mungu Baba ni hii, Kwenda kuwatazama yatima na wajane katika dhiki yao, na kujilinda na dunia pasipo mawaa.”

Kwa hiyo basi, si jambo baya mtu kuwa chini ya mfumo wa kibinadamu. Cha msingi ni kuishi chini ya imani ya kweli na halisi ya Mungu Muumba.


View: https://youtu.be/WkBDXlkARlc
 
Kwani lazima itoke mahali?

Imetoka kwangu.

Kuwa na pesa, kutokuwa na pesa hakuhusiani na uwepo wa huyo Mungu.

Huyo Mungu hayupo.


Kama kila kitu lazima kina uumbaji, Hata huo uumbaji utahitaji kuwa na uumbaji mwingine, Na huo uumbaji mwingine uwe na uumbaji mwingine. Hivyo hivyo pasipo kukoma.

Na kama si lazima kila kitu kina uumbaji, Hata Dunia haihitaji uumbaji.

Huyo Mungu angekuwepo kweli, Kusingekuwa hata na haja ya kuamini au kuhoji uwepo wake.

Kila mtu angejua kwa uhakika kabisa bila kuhitaji imani au dini kwamba Mungu huyo yupo.

Mnahangaika sana kumwelezea na kumuongelea huyo Mungu, Kwa vile hajawahi kuwepo kujiongelea, kujitetea na kujidhihirisha mwenyewe yeye kama yeye kwamba yupo.

Mungu huyo ni fictional character, Hajawahi kuwepo, Hayupo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.
Bro mimi naona Huna haja ya kuongeza sana kuhusu uwepo wa mungu au kutokuwepo kwake, nimejaribu kwa nguvu zote kuwaelewa hawa watu wanaopinga uwepo wa mungu lakini nilichogundua ni kwamba hawa watu wana upeo mdogo sana wa kufikiri, ndio maana wanaopinga kwa nguvu zote uwepo wa mungu, na haitokaa itokee kuwa na imani thabiti kwa chochote wanachokiamini, kwa sababu kitendo chat kupinga tu uwepo wa mungu ni uwendawazimu, Mungu sio mtu wa mchezo mchezo eti umuwazie vile unavyo fikiri Wewe, wanachltakiwa waelewe kwanza ili uweze kumuwazia au kumfikiria mungu na uwezo wake lazima uwe na akili kubwa, na kuwa na akili kubwa sio tu lazima uwe na uwezo wa kuvumbua mambo kama kina Newton na wavumbuzi wengine, ile kukubali tu kama yuko mungu na mwenyewe uwezo wa kufanya yale ambayo kiumbe mwengine hawezi basi pia ni akili kubwa, kinyume na hapo ni uwendawazimu. Kitendo chat kufikirua tu kuwa hakuna mungu. Basi elewa kuna hitilafu kwenye mfumo wako wa kufikiri, na kama ni hivyo ni lazima uone ni kawaida kuwaza hakuna mungu na hapo hapo uendelee kuishi kwa amani, au tunaweza kusema Wewe maisha yako ni hopless kabisa. Cha muhimu ni kuwaonea tu huruma hawa watu, kuendelea kuwalaumu na fikira zao finyu pia kunatufanya na sisj wenye akili timamu tupoteze utimamu wetu.
 
Bro mimi naona Huna haja ya kuongeza sana kuhusu uwepo wa mungu au kutokuwepo kwake, nimejaribu kwa nguvu zote kuwaelewa hawa watu wanaopinga uwepo wa mungu lakini nilichogundua ni kwamba hawa watu wana upeo mdogo sana wa kufikiri, ndio maana wanaopinga kwa nguvu zote uwepo wa mungu, na haitokaa itokee kuwa na imani thabiti kwa chochote wanachokiamini, kwa sababu kitendo chat kupinga tu uwepo wa mungu ni uwendawazimu, Mungu sio mtu wa mchezo mchezo eti umuwazie vile unavyo fikiri Wewe, wanachltakiwa waelewe kwanza ili uweze kumuwazia au kumfikiria mungu na uwezo wake lazima uwe na akili kubwa, na kuwa na akili kubwa sio tu lazima uwe na uwezo wa kuvumbua mambo kama kina Newton na wavumbuzi wengine, ile kukubali tu kama yuko mungu na mwenyewe uwezo wa kufanya yale ambayo kiumbe mwengine hawezi basi pia ni akili kubwa, kinyume na hapo ni uwendawazimu. Kitendo chat kufikirua tu kuwa hakuna mungu. Basi elewa kuna hitilafu kwenye mfumo wako wa kufikiri, na kama ni hivyo ni lazima uone ni kawaida kuwaza hakuna mungu na hapo hapo uendelee kuishi kwa amani, au tunaweza kusema Wewe maisha yako ni hopless kabisa. Cha muhimu ni kuwaonea tu huruma hawa watu, kuendelea kuwalaumu na fikira zao finyu pia kunatufanya na sisj wenye akili timamu tupoteze utimamu wetu.
Wewe mwenye huo upeo mkubwa wa kufikiri thibitisha uwepo wa huyo Mungu, Sio kufosi imani zako uchwara zisizo na uthibitisho wowote ule.

Kama huyo Mungu yupo, Kwa nini uhitaji imani ya kuamini yupo badala ya kujua kwa uhakika kabisa huyo Mungu yupo?

Huyo Mungu angekuwepo kweli Kusingekuwa hata na haja ya kuhoji na kuuliza uwepo wake, Kila mtu angejua Mungu huyo yupo.

Mungu huyo hayupo ndio maana mnahangaika sana kumwelezea na kumuongelea kwa vile Hayupo na hajawahi kuwepo kujidhihirisha na kujitetea mwenyewe.

You are trying to defend a fictional character.
 
Hii unaitoa wapi Mkuu? Au maneno ya mitandaoni na fikra za watu wenye pesa nyingi hasa Wazungu?
Kwa mfano simu yako ikiwa mbovu si lazima utaipeleka kwa fundi ikatengenezwe? Au kama ina warrant ikisumbua ukairudisha ulipoinunua unaweza ukabadilishiwa na ukapewa simu nyingine? Kama unaweza ukafanya hivyo Kwanini hauamini kuna uumbaji? Mungu yupo lakini kwenye hizi dini ndio kuna changamoto lakini la msingi amini kile unachokiamini na Mungu yupo. Hayo mengine yanayotokea Shida, magonjwa,vifo ni matokeo ya matendo yetu sisi wanadamu.
Toa hoja acha blabla watu wanaamini mungu kwa kuwa wametishwa tuu
 
View attachment 3066660

Ningependa kujua, je, inawezekana kuwa rais wa nchi wakati wewe si raia wa nchi hiyo?

Pia ningependa kufahamu, Mungu ni wa dini gani? Je, ni Muislamu au Mkristo?

Kwa nini Masheikh na Wachungaji husema kwamba dini haiwezi kukufikisha mbinguni?

Kama dini haziwezi kutupeleka mbinguni, basi kwa nini zipo? Kama Mungu yuko upande wa Wakristo, kwa nini hawapendelei?

Na kama Mungu ni wa Waislamu, kwa nini nao hawapendelei? Je, inamaanisha nini kusema kwamba Mungu ni wa kila mtu?

Kwa nini alitufanya tofauti kwa rangi? Na kwa nini alitufanya tofauti hata kwa jinsi tunavyoishi duniani au kwa kipato?

Kwanini aliumba shida na matatizo?

Na kusema kwamba alituumba kwa mfano wake, ningependa kujua, kama sisi ni mfano wa Mungu, je, hii inamaanisha kwamba Mungu anakula chakula, anaenda chooni, na pia anakabiliana na matatizo kama sisi?

Kama jibu ni hapana, kwa nini sisi, ambao ni mfano wa Mungu, tunateseka hivi wakati yeye ana uwezo mkubwa wa kutusaidia?
ukimkiri Yesu kuwa Bwana na mkombozi wako utaokoka kupitia Yesu kristo mnazareth mkombozi ukimkiri kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yako utaenda mbinguni hila usipomkubali mbingu hutaiona pia ukishamkubali kuwa mwokozi wako acha dhambi kaa katika utakatifu acha dhambi kabisa omba toba kaa kwenye utakatifu utaenda mbinguni kwa Baba yetu aliyeziumba mbingu na nchi kwa hiyo kuanzia sasa kubali kumpokea Yesu kuwa Bwana na mkombozi wa maisha yako kwa kuomba toba 🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏
 
Back
Top Bottom