Je, funga ya Waislamu ni kula na kunywa tu?

Je, funga ya Waislamu ni kula na kunywa tu?

Bidhaa hupanda bei kama uhitaji ni mkubwa kuliko upatikanaji.

Kipindi cha Ramdhani demand inaongezeka kwa maana ulaji wa vyakula unaongezeka kuliko kipindi cha kawaida.

Waulize wapishi majumbami watakujuza ni kipindi gani wanapika Sana utagundua kipindi cha mfungo wa mwezi mtukufu ndio wanapika Sana na wengi hasa Wafanyakazi wa majumbami hawakipendi kipindi hiki kwa kuwa kazi za kupika zinaongezeka maradufu siku nzima inakua maandalizi ya kupika kupika na kufanya usafi hasa wa vyombo vingi.

Tupunguze kula kipindi cha mfungo ili demand na supply ziendelea kuwa kama kipindi kisicho cha mfungo na bei iwe kawaida.
Ili iweje!?..unawanunulia wewe chakula!?
 
Kama una watoto jiulize huwa unawalazimisha wakugeshimu au wanahiyari!?...yaani wanakuheshimu kwa kuwa unawapa mahitaji muhimu au wanakuheshimu kwa kuwa wanatakiwa kukuheshimu,wasipokuheshimu utachukua hatua gani?
Swali nililo uliza kutokana na maelezo ya mleta mada na maswali yako kuna uwiano wowote ?
 
Baada ya kuandika post ambayo ilikuwa inahusiana na Dhana ya Futari na Daku kumeibuka maswali mengi na kashfa nyingi kuhusiana na funga ya Waislamu kwamba, wamebadili ratiba ya kula,mara sijui wanakula usiku mzima na bla bla bla nyingine kibao.

Sasa Jamiiforums ni jukwaa la elimu na maarifa hivyo nikaona si vibaya nikaja na post nyingine ili tutoane ukungu kwenye bongo zetu.

Kwahiyo tutaona nini maana ya Swaumu/ funga na lengo lake.

Maana ya Swaumu (Funga)

Kilugha; neno “Swaum” lina maana ya kujizuilia kufanya jambo lolote la kawaida. Katika Qur-an tunafahamishwa kuwa Bibi Maryam baada ya kumzaa nabii Isa (A.S) alijizuilia (alikuwa katika Swaum ya) kutosema na mtu yoyote juu ya mtoto wake.

“... Na kama ukimuona mtu yeyote (akauliza habari za mtoto huyu) sema: `Hakika mimi nimeweka nadhiri kwa Mwingi wa Rehema ya Swaum (kufunga), kwa hiyo leo sitasema na mtu’” (19:2 6).

Katika Sharia ya Kiislamu kufunga (Swaum) ni kujizuilia kula, kunywa, kujamii, kuingiza kitu chochote katika matundu ya mwili na kujizuilia kumuasi Allah (S.W) kuanzia alfajiri ya kweli mpaka kuingia ma gharibi.

Lengo la Swaumu

Lengo la Swaum katika Uislamu ni kumuwezesha mja awe mcha Mungu kwa kufuata maamrisho yote ya Allah (s.w) na kuacha makatazo yake yote. Hivyo, ili lengo hili litimie mfungaji pamoja na kujizuilia kula, kunywa, kujamii, hanabudi pia kujizuilia na kitendo chochote kitakachompelekea kuvunja amri ya Allah (s.w) na Mtume wake (s.a.w).

Kwa maana nyingine, ili Swaum ya mfungaji iwe na maana na yenye kufikia lengo, mfungaji hana budi kukizuilia (kukifungisha) kila kiungo chake cha mwili - macho, ulimi, masikio, mikono na miguu pamoja na fikra na hisia zake -na matendo aliyoyakataza Allah (s.w.).

Funga ya macho ni kujizuilia kutazama yale yote aliyoyakataza Allah (s.w), funga ya ulimi ni kujizuilia na mazungumzo yote aliyoyakataza Allah (s.w), kama vile kusengenya, kusema uwongo, kugombana n.k, funga ya masikio ni kujizuilia kusikiliza yale yote aliyoyaharamisha Allah (s.w); funga ya miguu ni kujizuilia kuendea yale yote aliyotukataza Allah (s.w); funga ya fikra na hisia, ni kujizuilia na fikra na dhana mbaya ambazo zinampelekea mja kuvunja amri na makatazo ya Allah (s.w). Ni katika maana hii Mtume (s.a.w) anasema katika Hadith zifuatazo:

“Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: Yule ambaye haachi kusema uwongo na haachi kufanya vitendo viovu, Allah hana haja na kuona kuw a anaacha chakula chake na kinyw aji chake - ( Allah (s.w) hana haja na funga yake). (Bukhari).

Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema; Ni wangapi wamefunga lakini hawana funga ila kukaa na kiu tu, ni wangapi wanaoswali usiku ambao hawana swala ila huambulia kupoteza usingizi tu. (Darimi).

Hadith hizi zinatuthibitishia kuwa ufungaji usioambatana na kujizuilia na maovu na machafu, haumpatii mfungaji faida yoyote.

Naona mpaka hapo tutakuwa tumepata faida ya kujua funga na makusudio yake

Ni hayo tu!
safi sana mwalimu wengi tume kufahamu ila wachache tu wakina miujiza kawada yao kujitoa akili
 
Bidhaa hupanda bei kama uhitaji ni mkubwa kuliko upatikanaji.

Kipindi cha Ramdhani demand inaongezeka kwa maana ulaji wa vyakula unaongezeka kuliko kipindi cha kawaida.

Waulize wapishi majumbami watakujuza ni kipindi gani wanapika Sana utagundua kipindi cha mfungo wa mwezi mtukufu ndio wanapika Sana na wengi hasa Wafanyakazi wa majumbami hawakipendi kipindi hiki kwa kuwa kazi za kupika zinaongezeka maradufu siku nzima inakua maandalizi ya kupika kupika na kufanya usafi hasa wa vyombo vingi.

Tupunguze kula kipindi cha mfungo ili demand na supply ziendelea kuwa kama kipindi kisicho cha mfungo na bei iwe kawaida.
huo ni msimu wakulima wa mihogo magimbi viazi wamesubilia mfungo kupiga hela hacha watu wanufaike uapo sema watu wanakula sana wafungaji hata wakala si wanakula .hela yao
 
Kipindi cha kuwapa likizo kidogo,wazinzi mashoga,wafiraji,wasengenyaji,mafisadi,waongo na washenzi kama hao,huku kikichangizwa na unafiki mwingi,ila baada ya hapo ni fungulia dog miezi 11 mbele,hizi dini zimejaa wanafiki wengi sana ndio mana kila siku zinapoteza mwitikio na umaana mbele ya wanao jitambua.

Dini ya kweli ni kutenda haki na kusaidia wahitaji,hizi zingine mbwembwe na unafiki tu.
 
Chief

Kama ilivyo wakati WA sikukuu mbali mbali ziwe x-mas ,Eid au pasaka Kwa kawaida wafanyabiashara huona kama hii ni fursa ya kupata faida zaidi.

The same Kwa ramadhamani wafungaji ni wengi Sana kwasababu waislamu Wana mwitikio mkubwa WA kutekeleza ibada hii,kwahiyo wafanyabiashara wanatumia huu mwanya kupata faida zaidi.

Nadhani Jambo liko wazi kabisa hauhitaji hata mchumi kuliona hili
[emoji120]
 
Mokiti swali lako limejibiwa huku
Ukweli ni kwamba mfungo wa Ramadan ni sherehe ya kula
Ndio maana uitaji wa chakula unakuwa mkubwa mno na price inapanda , ni kama waislamu wanashindana na sikuu za Christmas wanavyo waona wakristo mwezi mzima wanasherehekea ,

waislamu mwezi wa Ramadan wanachukua likizo makazini wanaingia kwenye madeni makubwa kisa kula sana

Shida kubwa inakuja kuvimbiwa chakula Cha kula usiku saa 10 tena umeshindilia Sana ili usisikie njaa mchana , ukikutana akicheua mavimbizi ni hatari
 
Punguzeni makasiriko kwenye comment imani yetu tunatelekeza jambo letu nyie mnaumia nini na eti wazinzi wanapumzika embu ona jinsi gani tunavyo uheshimu mwezi wetu inaezekana iyo kupumzika ikambadilisha moja kwa moja.
 
Kwahiyo hiyo ndio ishu!

Jibu liko wazi funga ya Ramadhani ni maarufu kuliko kwaresma na INA mwitiko mkubwa Sana kuliko kwaresma.

Kwahiyo bilashaka hiyo ni fursa Kwa wafanyabiashara kutaka kupata faida zaidi ingawa inawaumiza walengwa ambao ni wafungaji

Sasa mwalimu inakuwaje kama funga ni kupunguza kula kwa ajili ya kutoa sadaka halafu kinyume chake uhitaji wa chakula unaongezeka mpaka bei inapanda!!!

Nilitegemea sababu waislam wanaacha kula asubuhi,mchana ila tu jion,bas vyakula vishuke bei maana watumiaji wamepungua???hii inakaaje.

Wachana na kwarezma maana hutakaa umsikie mkristo anakwambia nimefunga usile mbele yangu.
 
Ukweli ni kwamba mfungo wa Ramadan ni sherehe ya kula
Ndio maana uitaji wa chakula unakuwa mkubwa mno na price inapanda , ni kama waislamu wanashindana na sikuu za Christmas wanavyo waona wakristo mwezi mzima wanasherehekea ,

waislamu mwezi wa Ramadan wanachukua likizo makazini wanaingia kwenye madeni makubwa kisa kula sana

Shida kubwa inakuja kuvimbiwa chakula Cha kula usiku saa 10 tena umeshindilia Sana ili usisikie njaa mchana , ukikutana akicheua mavimbizi ni hatari

Maandazi,uji wa mhogo na ukwaju,chapati za maji,ubwabwa au tambi.futali ya mihogo na ndizi za nazi[emoji3063][emoji3063],hii ni 3 in 1 bado usiku.
 
M
Baada ya kuandika post ambayo ilikuwa inahusiana na Dhana ya Futari na Daku kumeibuka maswali mengi na kashfa nyingi kuhusiana na funga ya Waislamu kwamba, wamebadili ratiba ya kula,mara sijui wanakula usiku mzima na bla bla bla nyingine kibao.

Sasa Jamiiforums ni jukwaa la elimu na maarifa hivyo nikaona si vibaya nikaja na post nyingine ili tutoane ukungu kwenye bongo zetu.

Kwahiyo tutaona nini maana ya Swaumu/ funga na lengo lake.

Maana ya Swaumu (Funga)

Kilugha; neno “Swaum” lina maana ya kujizuilia kufanya jambo lolote la kawaida. Katika Qur-an tunafahamishwa kuwa Bibi Maryam baada ya kumzaa nabii Isa (A.S) alijizuilia (alikuwa katika Swaum ya) kutosema na mtu yoyote juu ya mtoto wake.

“... Na kama ukimuona mtu yeyote (akauliza habari za mtoto huyu) sema: `Hakika mimi nimeweka nadhiri kwa Mwingi wa Rehema ya Swaum (kufunga), kwa hiyo leo sitasema na mtu’” (19:2 6).

Katika Sharia ya Kiislamu kufunga (Swaum) ni kujizuilia kula, kunywa, kujamii, kuingiza kitu chochote katika matundu ya mwili na kujizuilia kumuasi Allah (S.W) kuanzia alfajiri ya kweli mpaka kuingia ma gharibi.

Lengo la Swaumu

Lengo la Swaum katika Uislamu ni kumuwezesha mja awe mcha Mungu kwa kufuata maamrisho yote ya Allah (s.w) na kuacha makatazo yake yote. Hivyo, ili lengo hili litimie mfungaji pamoja na kujizuilia kula, kunywa, kujamii, hanabudi pia kujizuilia na kitendo chochote kitakachompelekea kuvunja amri ya Allah (s.w) na Mtume wake (s.a.w).

Kwa maana nyingine, ili Swaum ya mfungaji iwe na maana na yenye kufikia lengo, mfungaji hana budi kukizuilia (kukifungisha) kila kiungo chake cha mwili - macho, ulimi, masikio, mikono na miguu pamoja na fikra na hisia zake -na matendo aliyoyakataza Allah (s.w.).

Funga ya macho ni kujizuilia kutazama yale yote aliyoyakataza Allah (s.w), funga ya ulimi ni kujizuilia na mazungumzo yote aliyoyakataza Allah (s.w), kama vile kusengenya, kusema uwongo, kugombana n.k, funga ya masikio ni kujizuilia kusikiliza yale yote aliyoyaharamisha Allah (s.w); funga ya miguu ni kujizuilia kuendea yale yote aliyotukataza Allah (s.w); funga ya fikra na hisia, ni kujizuilia na fikra na dhana mbaya ambazo zinampelekea mja kuvunja amri na makatazo ya Allah (s.w). Ni katika maana hii Mtume (s.a.w) anasema katika Hadith zifuatazo:

“Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: Yule ambaye haachi kusema uwongo na haachi kufanya vitendo viovu, Allah hana haja na kuona kuw a anaacha chakula chake na kinyw aji chake - ( Allah (s.w) hana haja na funga yake). (Bukhari).

Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema; Ni wangapi wamefunga lakini hawana funga ila kukaa na kiu tu, ni wangapi wanaoswali usiku ambao hawana swala ila huambulia kupoteza usingizi tu. (Darimi).

Hadith hizi zinatuthibitishia kuwa ufungaji usioambatana na kujizuilia na maovu na machafu, haumpatii mfungaji faida yoyote.

Naona mpaka hapo tutakuwa tumepata faida ya kujua funga na makusudio yake

Ni hayo tu!
MashaaAllah
Baraka Llahu Fiikum
 
Back
Top Bottom