Uchaguzi 2020 Je, Halima Mdee amefanya nini Kawe kwa miaka 10 ya ubunge wake kustahili kuendelea? Sikia ya Askofu Gwajima, 28 Oktoba fanya uamuzi sahihi

Kwanza jibu hili

WEWE KWANINI ULIKATWA UCHAGUZI WA NDANI?
Mimi sikukatwa uchaguzi wa ndani, anayekatwa ni yule aliyeshinda kura za maoni, halafu vikao vya uteuzi vikalikata jina lake na kumchukua mshindi wa pili au watatu.

Mimi ni wajumbe walifanya yao, kura hazikutosha.
P
 
Mimi sikukatwa uchaguzi wa ndani, anayekatwa ni yule aliyeshinda kura za maoni, halafu vikao vya uteuzi vikalikata jina lake na kumchukua mshindi wa pili au watatu.

Mimi kura hazikutosha.
P
Wewe si kwamba tu hazikutosha walikuona haufai kabisa, mimi nakufahamu wewe tokea mwanza paschal si mtu sahihi kabisa. Kama unashabikia mtu kama gwajima aisee paschal nazidi kukuondolea nyota kabisa.
 
Paskali, ukiona hadi wanyama hayawani (mbuzi, sijui kama mbuzi kweli [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]) wanabandua picha ya mgombea wako, ujue huo ni ujumbe tosha. Gwajima bado sana kuwa mbunge. Gwajima amechanganya sana madesa, muacheni kwanza ayaweke sawa then mara nyingine ateuliwe agombee kama atakuwa ameshatubu kumkufuru Mungu.
 
Wewe si kwamba tu hazikutosha walikuona haufai kabisa, mimi nakufahamu wewe tokea mwanza paschal si mtu sahihi kabisa. Kama unashabikia mtu kama gwajima aisee paschal nazidi kukuondolea nyota kabisa.
Anamuunga mkono Gwajima ili aonekane alivunja kambi ya kampeni na kurejesha umoja utakaisaidia ushindi ili baadaye ahurumiwe apewe teuzi.
 
Wewe si kwamba tu hazikutosha walikuona haufai kabisa, mimi nakufahamu wewe tokea mwanza paschal si mtu sahihi kabisa. Kama unashabikia mtu kama gwajima aisee paschal nazidi kukuondolea nyota kabisa.
It's true wajumbe wana uhuru kamili wa mawazo yao, hivyo they are right kumuona mtu yoyote hafai, ila kuna uwezekano baadhi ya waliopitishwa, mimi nina afadhali!.

Unaweza kuiangalia self assessment yangu kama Mbunge, nilitaka kwenda Bungeni kufanya nini?
Je, wajua kuna watu wazuri, waadilifu wenye uwezo, wanaotaka kuingia Bungeni kulisaidia Taifa, Bunge na kumsaidia JPM kwa dhati, lakini kwa vile...
P
 
Ukiacha ile kauli yake ya udini, naona Gwaji upepo kdg unaanza kumuendea vzr hii style ya kuzunguka mtaa kwa mtaa ,nyumba kwa nyumba inamuweka karibu na watu
 
Ukiacha ile kauli yake ya udini, naona Gwaji upepo kdg unaanza kumuendea vzr hii style ya kuzunguka mtaa kwa mtaa ,nyumba kwa nyumba inamuweka karibu na watu
Wala hakuna kitu usidanganywe na mtu anapokukenulia meno ukadhani anakupenda kura ni siri ya mtu, upepo ukivuma unakusanya kila taka taka ndicho kinachotokea kwa gwajima. Kawe si ya mchezo mchezo tu
 
Mwanasheria na mwanahabari msomi, kazi ya mbunge ni kuwakilisha wanajimbo wake Bungeni, Kazi ambayo Mh Mdee ameifanya vizuri. Kazi ya kujenga miundombinu jimboni ni ya serikali inayokusanya kodi. Hata Mdee akitumia mshahara wake kujenga barabara ya lami, hautoshi hata kumaliza km 1. It is sad that hata wasomi wetu hamwelewi such a basic fact. Expectations za watu kwa mbunge kujenga miundombinu ni za kipumbavu na zinafanya maisha ya wabunge kujaa stress.
 
Wala hakuna kitu usidanganywe na mtu anapokukenulia meno ukadhani anakupenda kura ni siri ya mtu, upepo ukivuma unakusanya kila taka taka ndicho kinachotokea kwa gwajima. Kawe si ya mchezo mchezo tu
Ni kweli Mkuu ,ila naona kaamua kuja na style ya kuzunguka mitaani sasa
 
So unasema gwajima hakufaa kabisa kuteuliwa kuwa mgombea wa kawe???
 
Ni kweli Mkuu ,ila naona kaamua kuja na style ya kuzunguka mitaani sasa
Anajichosha tu kitu cha msingi ataifanyia nini kawe na watu wake?? Swala la nyumba kwa nyumba halisaidii watu watakupokea jinsi unavyokuja kisha wanaachana na wewe na habari inaishia hapo. Afanye vikao atangaze sera zake lakin siyo kudanganya watu kuwapeleka Birmingham.
 
straight talk
 
Naona wewe unajibu swali ambalo halijaulizwa; ingekuwa mtihani ungepata sifuri
Mtoa mada ameuliza atajiwe mambo aliyo yafanya Halima Mdee kwa miaka 10; wewe unaleta swali tofauti kabisa na kulitoa jibu? Jifunzeni basi kujibu maswali
 
Akagombee Uaskofu Mkuu wa makanisa ya TAG lakini sio Ubunge.
Hatutaki udini na ukabila hapa Tanzania .

Kuna baadhi ya watu wa dini nyingine wanakwazwa na huyu ASKOFU lakini wanamvumilia wakijua kuwa anahubiri dini yake kumbe anawaza kuingia serikalini ili atimize azma yake ya kugeuza misikiti kua kumbi zake za Kuwashambulia watu kama alivyomshambulia Kadinali Pengo.

Kama anafaa sana kuwa Mbunge kutokana sifa alizonazo kwa awamu hii basi Kuna nafasi kumi za Uteuzi wampe moja.

Na tumeharibiwa sana nchi yetu. Tunadanganywa maendeleo hayana Chama lakini mtu akijaribu kuhamasisha maendeleo basi ni lazima ajiingize kwenye siasa za CCM au ajipendekeze kwa watawala.
Sadaka anazokusanya kutoka kwa maskini na misaada toka kwa mabeberu anazitumia kwenye siasa badala ya kutangaza injili na kuwasaidia wasiojiweza.

Wanakawe wa dini zote tumtie adabu huyu mdini mwenye imani Kali na muasi kwa kumnyima kura .

Siasa ni fani awaachie wenyewe . Vinginevyo asimame kwenye kweli ya neno la Mungu na aonyeshe kukerwa na siasa za kibaguzi za CCM na dhulma ambazo anazitegemea zimpe kura za wizi.
Awe tu tayari kukataa kura za wizi ili asianguke kwenye mtego wa shetani.

Halima Mdee aliwawakilisha watu wake Jimboni ipasavyo ndio maana alikua anafukuzwa Bungeni huku bunge likiwa gizani ili tusione dhulma walizokuwa wanafanyiwa wapinzani hasa Halima na Sugu.

CCM isiangalie Kawe tu yapo Majimbo mengi sana itapoteza kutokana na Dhoruba ya ghafla iliyowafikia baada ya kurejea TL.
Mwaka huu ni Mwendo wa sala na Albadir mtu atakayeharibu uchaguzi lazima awe kichaa au ajiandae tu kivingine mana Albadiri haitamuacha mtu.
Wamemdhihaki Mungu vya kutosha.
Watu wanasema tumweke Mungu mbele halafu wanafuta formu za watu ili zionekane zimekosewa.
Watu walioapa kutenda haki wanafanya uhuni na dhulma bila hofu.
Watu wanajipendekeza kwa wanadamu kuliko kumtii Mungu.

Hivi Gwajima anaweza kumlaumu JK wakati Makanisa yote ya watu Binafsi yalistawi kipindi cha JK.
Ukata ndio umewapelekea kwenda kuwasujudia watawala na kumdhihaki Mungu.
Kama walimdhihaki JK wakati aliwapa fursa wengine wakafungua mpaka Mabenki ya Hayo makanisa yao leo hii wanakimbilia siasa ili wajiweke kwenye nafasi ya kuonekena mbele za watu.

Ni Lini Sadaka zinazotolewa kwa ajili ya Misikiti ikatangazwa?

Hivi mtu kama Bakhressa akitangaza kuwa ametoa misaada kwenye misikiti si itabidi agombee Urais kabisa ??
Yani tuvisima tuchache alivyochimba ndio anajiona amekua ni mdogo wake mtume Muhammad ,mtume wa Mwenyezi Mungu.

Waislam Msimchague Gwajima kwa Kusumangwa na Visima mbele ya watu.
Sadaka huwa ni siri kama alivyoelekeza mwenyezi Mungu.

Alitoa misaada kama sehemu ya sadaka anazopokea . Sasa asitumie sadaka hizo kama wakoloni kuwa fimbo ya kuwatawala watu na kuwafanya watumwa wake. Hakuna mtu aliyemuomba Bali aliamua mwenyewe.
Na sisi atuache tuamue wenyewe kumpa kura au kutompa .Asitupangie.

Majimbo ya CCM hakuna mtu anayeruhusiwa kutoa rushwa kama misaada wakati wa kujipanga ili achaguliwe lakini kwa wapinzani ni Ruksa kama alivyofanya Gwajima na Tulia Aksoni kwa miaka mitano.
Na wote wataangukia Pua. Huyu akienda Bungeni atarejesha sheria ya Rushwa kama ilivyokua awamu ya tatu iliyotuletea Rushwa ya Takrima bila aibu.

Haki huinua Taifa .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…