Uchaguzi 2020 Je, Halima Mdee amefanya nini Kawe kwa miaka 10 ya ubunge wake kustahili kuendelea? Sikia ya Askofu Gwajima, 28 Oktoba fanya uamuzi sahihi

Uchaguzi 2020 Je, Halima Mdee amefanya nini Kawe kwa miaka 10 ya ubunge wake kustahili kuendelea? Sikia ya Askofu Gwajima, 28 Oktoba fanya uamuzi sahihi

Ask what u will do for Tanzania and not what Tanzania will do for u!! HILI NDIO NDIO MSINGI WA SWALI LA PASCAl Je mdeee Kalifanyia nini jumbo LA Kawe kama sio Kuomba Seikali kila siku pamoja na kwamba serikali inajukumu kuhusu wana kawe Je mbunge Wa wanakawe pasipo Serikali kafanya nini
Mimi nitamchagua Mdee kwa sababu amekuwa mstari wa mbele katika kulitetea Jimbo letu. Suala la ujenzi wa barabara, shule, maji n.k. Ni kazi ya Serikali. Huwezi kukuta barabara imejengwa kwa kiwango Cha lami eti useme amejenga Mbunge wakati kilomita moja tu ya lami inagarimu zaidi ya billion moja.
 
Pascal huu ni muda wa kuchutama! Naona unapima urefu wa kina cha maji kwa kutumia miguu miwili. Pamoja na maelezo yako memgi huku JF kweli unajitoa ufahamukuwa hujui kazi za mbunge?? Hadi uje na hoja ya kusambaza maji? My brother unajimaliza kitaaluma.

Kweli kabisa ndo umefikia ukomo wa kufikiri kuhusu kazi za mbunge? Hivi uliomba nafasi ya uwakilishi ili ufanye nini? Nimeanza kuhoji credibility ya taaluma yako!!

Ushauri wangu anza kujisomea vitabu ujue kazi za wawakilishi kuanzia mwenyekiti wa mtaa/vitongoji hadi walau ubunge. Kisha ujipamge ugombee kipi. Kwa bandiko hili waliokupiga chini walikuwa na haki yaani hukustahili.
 
Askofu Gwajima alisema atageuza misikiti kuwa Sunday nadhani hakukosea kwa muktadha wa injili ya Kristo.

Ukristo haulazimishwi bali unahubiriwa kwa upendo na ni uamuzi wa anaesikia kuamini au kutokuamini.

Kwa Mkristo au muislamu alie Kawe, hatakiwi kuishi na hofu kw msingi Gwajima akichaguliwa kuwa mbunge, atawabadilisha imani wawe walokole.

Kwa misingi ya siasa za Tanzania, mbunge ni mtunga sheria; ila kwa utamaduni; mbunge anatakiwa kuwa lobbyist kwa serikali ili kwenye mkate mdogo uliopo, basi awashawishi wakusanya kodi ili nae apate sehemu ya mgao kutatua kero za wana jimbo.

Mdee kwa miaka 10, je aliweze kufanya kazi kama sio ku-lobby serikalini basi kwa development partners kwa kuandika projects ambazo kwa nafasi yake angeweza kuzipatia fedha ili utekelezaji ufanyike.

Nataka kuamini, kama hayo ya kuchimba visima Gwajima kafanya, huenda zilikuwa fedha toka kwa development partners; kama kaweza ku-lobby kama askofu; bila shaka akipata kofia ya ubunge ataweza ku-lobby serikalini na kwadevelopment partners.

Tuwape muda wana Kawe kuamua tarehe 28.10;
 
Tatizo la Watanzania wengi ni waoga wa kuhoji. Lazima aseme amefanya nini kwa wakazi wake ambao walimpa kura. Hakuchaguliwa aende kuuza sura.
 
Ask what u will do for Tanzania and not what Tanzania will do for u!! HILI NDIO NDIO MSINGI WA SWALI LA PASCAl Je mdeee Kalifanyia nini jumbo LA Kawe kama sio Kuomba Seikali kila siku pamoja na kwamba serikali inajukumu kuhusu wana kawe Je mbunge Wa wanakawe pasipo Serikali kafanya nini
Magufuli bila pesa za kodi zetu,kaifanyia nini nchi hii?
 
Wameifanyia nini Kawe ni Swali zuri sana kwa serikali iliyoko/iliyokuwa madarakani na bashite akiwa kama mwakilishi wa raisi katika mkoa wote wa dar, nilitegemea uwe na uwezo wa kujua kwamba mkusanyaji wa kodi ndo mwenye jukumu la kupeleka maendeleo katika sehemu wanazochukua kodi.
 
Sasa mbona Pasikali mwanzo ulidai sio kampeni? wakati kila neno uliloandika ni kampeni tena umetudhalilisha sana watu wa jimbo hili mzee kwa kutuletea hoja zilizopitwa na wakati. Hoja kama hizi zinafaa sehemu zingine sio Kawe ambako wengi wetu tunajitambua. Hivi kweli unajua hata wajibu wa mbunge ni upi au unatuona sisi ndo hatujui mbunge kazi yake ni nini? Hoja hizi zinawafaa sana wale waumini wake ambao nadhani wengi hawatokei huku.

Katika viu ambavyo kama mtanzania nitavipiga sana vita ni ukabila na udini. Na kama Gwajima sio tafsiri sahihi ya mdini na mkabila basi vitu hivyo havipo duniani. Hata huko Rwanda na kwingineko mambo hayakuanza siku moja tu kuwa mabaya bali yalianza kidogo kidogo kama hivi watu kufumbia macho wenye udini na ukabila kama gwaji boy kwa kisingizio cha uchama au unyinyiemu
 
Hahaha yani hata wewe unaweza kuuliza swali hili, kwamba Halima Mdee kaifanyia nini kawe kwa miaka 10?

Haya maswali tuachie sisi siyo wewe.

Unazijua kazi na majukumu ya mbunge?!

Au nawe ndio wale kwamba Mbunge
ajenge madaraja, au alete maendeleo?!

Bandika hapa kazi na majukumu ya mbunge kisha utaelewa logic yangu.
 
Wanabodi,

Mimi ni mkazi wa Kawe, kwa vile sasa tuko kwenye kampeni za uchaguzi, ili tumtendee haki Mbunge wetu, kama kuna mtu anaweza kutueleza humu, Jee Mbunge wetu Mhe. Halima Mdee, ameufanyia nini Kawe Kawe katika kipindi chake chote cha miaka 10, ili tumfanyie assessment kama anastahili kuongezewa miaka mitano mingine, au apumzishwe?.

Declaration of Interest
Japo mimi Paskali Mayalla kwa sasa ni kada wa Chama Cha Mapinduzi, CCM, lakini bandiko hili sio la ukada au propaganda za kampeni za uchaguzi, bali ni bandiko hojaji la kweli kuuliza Mhe. Halima Mdee ameifanyia nini Kawe in the past 10 years kustahili kuendelea?.

Rais John Kennedy wa Marekani aliwahi kusema, " usijiulize Marekani ikufanyie nini, bali ujiulize, utaifanyia nini Marekani. Mhe. Halima Mdee ndie Mbunge wetu Kawe kwa kipindi cha miaka 10, naomba kuuliza kwa anayejua, Jee Halima Mdee ameifanyia nini Kawe?.

Leo nilikuwa mahali nikamsikia Askofu Gwajima, kumbe ni mdau wa maendeleo ya Kawe kwa kipindi kirefu na ameisha fanya makubwa kwa Kawe kama Mwananchi tuu wa kawaida!.

Kumbe Askofu Gwajima baada ya kuhamia Kunduchi Salasala, alikuta kuna tatizo la maji. Kwanza alichimba visima virefu 12 kwenye misikiti ya Salasala na kuwapatia maji Waislamu, kisha akanunua pump ya mamilioni kutoka Ujerumani, akanunua mabomba na mita za maji na kusambaza maji kwa kaya 250 za majirani wake wanaomzunguka, sasa wanapata maji safi na salama!.

Askofu Gwajima tayari ameisha saidia magari 7 ya ambulance za wagonjwa kwa hospitali mbalimbali, na kuahidi atazipatia magari ya wagonjwa hospitali za Kawe na Kinondoni.

Gwajima amesema, kazi ya kuwaletea maendeleo Watanzania sio kazi ya serikali pekee, ni kazi ya wananchi kwa kushirikiana na serikali, hivyo hapo alipo, tayari ameagiza tinga tinga la kuchonga barabara na malori mawili ya tipper, ambapo barabara zote za Kawe na Kinondoni zitachongwa, vijana wa Kawe watapatiwa ajira za kuchimba mitaro ya maji, hivyo kama ni serikali, itabaki kazi ya kuziwekea tuu lami!.

Mwana Kawe yoyote akiyasikia haya Askofu Gwajima aliyoyafanya Kawe, kabla hata hajawa Mbunge, ukilinganisha na alichofanya Halima Mdee kipindi chake chote cha miaka yake 10!, Utakubaliana na mimi, Jee is it, it's high time, tumshukuru Mhe Halima Mdee kwa utumishi wake wa miaka 10 Kawe?, na tumuage kwa heshima na upendo na taadhima kwa kumwambia, Bye Bye Mhe. Halima Mdee Kawe, asante sana kwa utumishi wako Kawe?, na Jee tumkaribishe Askofu Dr. Josephat Gwajima kwa kunwambia, "karibu, Kawe Askofu Gwajima?.

Nauliza tuu!.

Paskali
Anayezuia maendeleo ya Kawe ni nani?!
Watawala hawapeleki pesa kwenye majimbo ya upinzani ulitaka Halima alitoe wapi pesa
Acha kufurahia shida za watu
Mnamtaka huyo mwingine asiye na hofu ya Mungu

Acha hizo
Mnaelewa fika maendeleo ya sehemu na sehemu yanakwamishwa na nani
Barabara za kuelekea Chuo cha Ardhi Maeneo ja Jeshini Kuelekea Bwalo la Jeshi kote kule Kawe sokoni bondeni upande mpaka changanyikeni barabara mbovu watu wanaishi kama wakimbizi pesa mmenunua nini tena?!

So punguza kumnanga Halima
 
Wanabodi,

Mimi ni mkazi wa Kawe, kwa vile sasa tuko kwenye kampeni za uchaguzi, ili tumtendee haki Mbunge wetu, kama kuna mtu anaweza kutueleza humu, Jee Mbunge wetu Mhe. Halima Mdee, ameufanyia nini Kawe Kawe katika kipindi chake chote cha miaka 10, ili tumfanyie assessment kama anastahili kuongezewa miaka mitano mingine, au apumzishwe?.

Declaration of Interest
Japo mimi Paskali Mayalla kwa sasa ni kada wa Chama Cha Mapinduzi, CCM, lakini bandiko hili sio la ukada au propaganda za kampeni za uchaguzi, bali ni bandiko hojaji la kweli kuuliza Mhe. Halima Mdee ameifanyia nini Kawe in the past 10 years kustahili kuendelea?.

Rais John Kennedy wa Marekani aliwahi kusema, " usijiulize Marekani ikufanyie nini, bali ujiulize, utaifanyia nini Marekani. Mhe. Halima Mdee ndie Mbunge wetu Kawe kwa kipindi cha miaka 10, naomba kuuliza kwa anayejua, Jee Halima Mdee ameifanyia nini Kawe?.

Leo nilikuwa mahali nikamsikia Askofu Gwajima, kumbe ni mdau wa maendeleo ya Kawe kwa kipindi kirefu na ameisha fanya makubwa kwa Kawe kama Mwananchi tuu wa kawaida!.

Kumbe Askofu Gwajima baada ya kuhamia Kunduchi Salasala, alikuta kuna tatizo la maji. Kwanza alichimba visima virefu 12 kwenye misikiti ya Salasala na kuwapatia maji Waislamu, kisha akanunua pump ya mamilioni kutoka Ujerumani, akanunua mabomba na mita za maji na kusambaza maji kwa kaya 250 za majirani wake wanaomzunguka, sasa wanapata maji safi na salama!.

Askofu Gwajima tayari ameisha saidia magari 7 ya ambulance za wagonjwa kwa hospitali mbalimbali, na kuahidi atazipatia magari ya wagonjwa hospitali za Kawe na Kinondoni.

Gwajima amesema, kazi ya kuwaletea maendeleo Watanzania sio kazi ya serikali pekee, ni kazi ya wananchi kwa kushirikiana na serikali, hivyo hapo alipo, tayari ameagiza tinga tinga la kuchonga barabara na malori mawili ya tipper, ambapo barabara zote za Kawe na Kinondoni zitachongwa, vijana wa Kawe watapatiwa ajira za kuchimba mitaro ya maji, hivyo kama ni serikali, itabaki kazi ya kuziwekea tuu lami!.

Mwana Kawe yoyote akiyasikia haya Askofu Gwajima aliyoyafanya Kawe, kabla hata hajawa Mbunge, ukilinganisha na alichofanya Halima Mdee kipindi chake chote cha miaka yake 10!, Utakubaliana na mimi, Jee is it, it's high time, tumshukuru Mhe Halima Mdee kwa utumishi wake wa miaka 10 Kawe?, na tumuage kwa heshima na upendo na taadhima kwa kumwambia, Bye Bye Mhe. Halima Mdee Kawe, asante sana kwa utumishi wako Kawe?, na Jee tumkaribishe Askofu Dr. Josephat Gwajima kwa kunwambia, "karibu, Kawe Askofu Gwajima?.

Nauliza tuu!.

Paskali
Njaa yako mbaya sana Paskali. Kujifanya hujui kazi na wajibu wa mbunge ili kuwalaghI watu na kuwasingizia wengine ama umefanya kile shetani anapenda na anakiendeleza. Sasa kama hakukuta maji ttizo ni Halima au CCM hawajafanya wajibu wao? Huyu aliyechimba visima kachimba kwavile ni mbunge auili aachiwe kesi zilizomkabili? Je, tukienda kwa majimbo yote ya CCM tutakuta flyover kama ubungo kwa kubenea au kongwa kwa mtemi wako? Jaribuvkwa mwandishi fair, na mahaba yako na ccm au wafaidika wake yasikufanye ufukuzwe ka tb-.
 
Ulipata vip kura moja kwenye kura za maoni kwa nini ulipata kura moja tu!?
Kwa kura yako moja unapata wapi ujasiri wa Kuhoji mwanamke aliye shinda kwa zaidi ya kura laki !
Wewe Ulishindwa vipi kuwa shawishi wajumbe ambao hawaja zidi ata 500!
Leo una hoji jambo ambalo ni zito kuliko kuwashawishi watu ambao hawazidi ata 500 wakupatie kura ata 60 pengine na ni watu ambao mnajuwana maana mjomba wewe ni Mhenga!!!!
Tuna safari ndefu sana kama taifa watu wake ndio wa aina yako 🤔
 
Back
Top Bottom