Je,hatukuambiwa umeme wa gesi ya Mtwara ukikamilika tatizo la umeme litakuwa historia?

Je,hatukuambiwa umeme wa gesi ya Mtwara ukikamilika tatizo la umeme litakuwa historia?

konda msafi

JF-Expert Member
Joined
Sep 5, 2018
Posts
1,696
Reaction score
8,763
Nakumbuka kila kiongozi mwandamizi wa serikali ya awamu ya 4 akiwa kwenye tv alikuwa anahubiri ukomo wa tatizo la umeme pale mradi wa umeme wa gesi ya Mtwara utakapokamilika.

Kulikuwa na uzinduzi mwingi tu sijui wa Kinyerezi one, sijui terminal two. Tulihakikishiwa mradi ukikamilika hakutakuwa tena na tatizo la umeme.

Hivi watanzania ndio kusema hatukumbuki kama tuliahidiwa hivyo? Na kama tunakumbuka kwa nini tupo kimya tu hata hatuhoji utadhani hatukuwahi kuahidiwa kitu kama hiki na serikali yetu?

Bila aibu tunaletewa mipango mingine mipya na kuahidiwa tatizo la umeme linaenda kuisha ilihali juzi tu tulipewa ahadi kama hiyo na haikutimia.

Natamani watanzania wawe na ujasiri wa kuwahoji viongozi wao vitu kama hivi. Haiwezekani tunaahidiwa kitu flani, gharama kubwa inatumika na pengine maisha ya watu yanapotea (refer vurugu za Mtwara kwenye kusafirisha gesi kuja Dar) lakini Serikali inakuja na mpango mwingine kana kwamba haijawahi kuwa na mpango kama huo kabla.
 
Hiyo ilikuwa kauli ya wanasiasa lakini hukuwahi kusikia mhandisi yoyote anaongea hivyo.

Kauli za kisiasa ni kufurahisha lakini katika hili kama gas ingendelezwa kama ilivyokuwa imepangwa naamini tungekuwa tumetatua tatizo, shida Mwendazake alipiga U-turn kwenda kwenye umeme wa maji.
Nchi inasafari ndefu sana.
 
Ni kweli mradi huu haujakamilika kwani mwendazake alipoingia madarakani aliutupilia mbali akaja na mradi wake wake wa stigler george.

Hii nchi wanasiasa wanaipelekaipeleka jinsi wanavyotaka ndio maana hatuendelei.

Mradi huu ungekamilia kweli tatizo la umeme lisingekuwepo.

Tumetumia umeme wapo maji tokea uhuru tatizo lake ni lilelile UKAME
 
Pia tuliambiwa na Kalemani kwamba bwawa la Nyerere litajazwa maji 15 Novemba 2021. Usisahau hilo
 
Na hata hii stiglers ikikamilika bado story zitakuja kua hizo, utasikia mtawala anasema tunakuja Sasa na umeme wa kutumia Nuclear ndio utamaliza matatizo yote.

Mwendo wa Michongo tu.
 
ndio enz za mkwere [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23],
 
Na hata hii stiglers ikikamilika bado story zitakuja kua hizo, utasikia mtawala anasema tunakuja Sasa na umeme wa kutumia Nuclear ndio utamaliza matatizo yote.

Mwendo wa Michongo tu.
Kwa hiyo wanatuchukuliaje? Kwamba hatuna kumbukumbu? Au hata kama tunakumbuka hatuna cha kuwafanya, si ndio?
 
Basi bhana, ikaingia awamu ya 5! Ikaja na mradi mpya wa Bwawa la Nyerere! Kwa madai kuwa GESI SI YETU NI YA MABEBERU!!
 
Basi bhana, ikaingia awamu ya 5! Ikaja na mradi mpya wa Bwawa la Nyerere! Kwa madai kuwa GESI SI YETU NI YA MABEBERU!!
Kwa hiyo tulishindwa kuuliza kipi kimetokea hadi gesi imekuwa ya mabeberu ghafla?
 
Hiyo mikataba ya gesi iiyoingiwa nafikiri ni pasua kichwa, ndo maana magu akaangukia kwenye stiglaz, tatizo la nchi hii ya wadanganyika lilianzia kipindi cha Nyerere kuipa kipaumbele siasa kuamua mustakabali mpana wa uchumi na maisha ya watu.

Badala ya kujenga taasisi imara ambazo zitaamua mambo yenye mustakabali mpana kwa nchi, wakaingiza ma siasa kwenye kila sekta. Nchi ikawa inaendeshwa kwa slogan za kisiasa, mara azimio la arusha, siasa ni kilimo, azimio la iringa, ahadi za mwanatanu, chama kushika hatamu, ccm ina wenyewe.

Sasa siasa ni mananeno maneno tu ya mdomoni, hayana impact yoyote kwa ustawi wa nchi...........taasisi imara ambazo zimejikita kwenye weledi, ufanisi na uwajibikaji ndo mwarobaini wa maendeleo ya taifa lolote, na siyo siasa.​
 
Ndo tujiulize kama walisema kuwa hakutakuwa na tatizo la umeme tena apa nchini, imekuwaje tatizo limerudi tena?. Watanzania uwezo wa kuongea hatuna wala uwezo wa kuhoji hatuna. Hii nchi imekuwa ni ya watu wachache ambao wanaiendesha vile wanavyojisikia wao tu bila kuangalia maslahi ya wananchi.

Gari likiwa bovu, dereva akiwa mbovu, na abiria wakawa wabovu, kimya tu hawahoji kitu, kuwa jamani eeh tubadilishieni injiniiiii. Dereva yeye haelewi, wala konda hatazami kelele za abiria, wao wanachotazama ni kuwa wamepata nauli zao na zipo mfukoni bs na pesa hairudishwi. Ukitaka shuka kapande gari nyengine. (Tuhamie Burundi tu).
 
Nakumbuka kila kiongozi mwandamizi wa serikali ya awamu ya 4 akiwa kwenye tv alikuwa anahubiri ukomo wa tatizo la umeme pale mradi wa umeme wa gesi ya Mtwara utakapokamilika.

Kulikuwa na uzinduzi mwingi tu sijui wa Kinyerezi one, sijui terminal two. Tulihakikishiwa mradi ukikamilika hakutakuwa tena na tatizo la umeme.

Hivi watanzania ndio kusema hatukumbuki kama tuliahidiwa hivyo? Na kama tunakumbuka kwa nini tupo kimya tu hata hatuhoji utadhani hatukuwahi kuahidiwa kitu kama hiki na serikali yetu?

Bila aibu tunaletewa mipango mingine mipya na kuahidiwa tatizo la umeme linaenda kuisha ilihali juzi tu tulipewa ahadi kama hiyo na haikutimia.

Natamani watanzania wawe na ujasiri wa kuwahoji viongozi wao vitu kama hivi. Haiwezekani tunaahidiwa kitu flani, gharama kubwa inatumika na pengine maisha ya watu yanapotea (refer vurugu za Mtwara kwenye kusafirisha gesi kuja Dar) lakini Serikali inakuja na mpango mwingine kana kwamba haijawahi kuwa na mpango kama huo kabla.

Screenshot_20210505-181554.png
 
Nakumbuka kuhusu gesi tuliahidiwa mengi makubwa zaidi ya hayo.
 
Back
Top Bottom