Je, Hayati Magufuli alikuwa na hirizi ya simba?

Pana mtawala mmoja alitumia uchawi unaitwa dagoo kupitia fimbo yake aliyoibeba nyakati zote mbele za watu ili kuwapumbaza watu wote kimya asiwepo wa kumpinga,Nashangaa kanisa lilitaka kumpa mchakato wa utakatifu.
Dagoo ni uchawi wa kutumia fimbo inayobebwa na watawala mfano machiefu wakimuiga Musa.
Ni mstari mdogo sana kumtenganisha mtawala au boss wa kiafrika na ndumba.
Ofisin Kila boss ana mganga wake.
 
Kwa hii KATIBA tuliyo nayo inampa mamlaka makubwa sana Rais wetu na AKITOKA MUNGU ANAFUATIA RAISI WA NCHI.......

Hata wewe Jemima Mrembo akiukwa U Madam president Kwa katiba yetu unaweza tengeneza strong institution yako na ukafanya utakavyo nakuifanya nchi kua kama ZIMBABWE ya MUGABE 😊😊😊
 
Watumishi wa uma wengi wana karba ya uzembe, ubadhirifu, rushwa na wizi. Hivi vitu ndivyo vilikuwa maadui wa Magu.

Kwa hiyo ilikuwa akikuita na kama kweli una ishu lazima uogope. Hata kama ulizingua mwaka jana lazima ushtuke pengine faili limeshafika mezani.

Ndio naana ilifika mahali watumishi wa uma wakawa wanasema serikali sio mahali salama tena kwa kufanya kazi. Sababu wanajua hawawezi kuishi bila upigaji, rushwa, wizi na dili.

Kwa sasa serikalini ni mahali salama tena..ushindwe wewe tu.
 
Moja ya chanzo cha umasikini ni kuamini huu upuuzi wa ushirikina.
Tembea ujionee Kwa watu wa lake zone tunaelewa ilizi ya Simba 🦁 Kuna mwalimu mmoja alikua nayo aliogopeka mpaka na WALIMU wenzake....

Hata mkiwa mna mjadili na akitokea inakua NANI AMFUNGE PAKA KENGELE 😊😊😊

Ushirikina upo mkuu japo CIVILIZATION ZA WAZUNGU NA SERIKALI HAIAMINI UCHAWI.....

Cc. Kiranga
 
Huwezi ukawa mtawala usiwe mshirikina,thus tangu kuumbwa kwa dunia hakuna mtawala yeyeto Duniani aliyefaulu kuingia mbinguni.
Huwezi tenganisha utawala na kafara ya damu za watu Kama shukrani kwa shetani ili kulinda utawala.
 
Nilipokuwa nafanya kazi TANROADS kuna uzembe fulani ulifanyika ofisini. Mkurugenzi wa idara pamoja na mimi tulipigiwa simu twende ofisini kwake. Yule m'baba hakuwa wa kawaida aisee
Kumbe mlikuwa wazembe, kwa hilo sioni kosa la Magufuli, kwa hili kwangu alikuwa jasiri muongoza njia, leo tunatolewa sadaka na Tanganyika yetu kwasababu ya uzembe wa kutosoma mikataba.
 
Kwakua mlishajiaminisha kua huyu mwalimu sijui ana hirizi ya Simba hivyo inabidi tumuogope,kwani usipomuogopa atabadilika na kua Simba kisha atawala?
 
Nilipokuwa nafanya kazi TANROADS kuna uzembe fulani ulifanyika ofisini. Mkurugenzi wa idara pamoja na mimi tulipigiwa simu twende ofisini kwake. Yule m'baba hakuwa wa kawaida aisee
Wazee wengi wa kisukuma wa kizamani huendesha familia zao kikoloni so haishangazi kuona tabia Ile alio kua nayo 😊😊
 
hiyo ni asili ya mtu na msimamo wa mtu. ni kweli najua kuna watu huwa wanakula hiyo hirizi, ila kuna wengine kama mimi, nimeumbwa hivyo, kutawala. hata nikienda kwa mkubwa namna gani huwa nikifika tu namtawala, naona kabisa ananiogopa, nina kautisho fulani hivi na sina hirizi ya simba wala uchafu wowote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…