Je, huu ni mwendelezo wa Serikali kutudharau Walimu Shule za Msingi?

Je, huu ni mwendelezo wa Serikali kutudharau Walimu Shule za Msingi?

Naipongeza sana serikali kwa uamuzi huu.

Imeona walimu wa s/m wanadanganyika na vitu vidogo,tena kirahisi mno.

Reference: General elections.
 
Pole Sana mwalimu, tatizo wengi wenu walikua washajiwekea ulaji, ukienda kusimamia unapewa lak 3 had 5 af pepa ikianza mnachukua pepa moja kusolve na kurudisha majibu kwa watoto. Matokeo yake secondary wanaenda vilaza hawajui kusoma Wala kuandika.
...
Asante sana.

Mitihani ya NECTA iheshimiwe.
 
Mbele yangu Kuna mzigo mkubwa wa daftari za stadi za kazi darasa la tano ninazopaswa kusahisha

Naangalia nje namuona mwalimu wa sekondari yuko bize kusimamia mtihani wa darasa la Saba
Mkuu mbona kama vile wewe sio mwalimu maana kipindi cha mitihani ya taifa ya darasa la 7 huwa hawaruhusu walimu wengine tifauti na headteacher kuwa maeneo ya shule
 
Kwa swali hili na logic uliyoitumua hapa kweli wewe ni Mwalimu.

By the way hii kazi ilikuwa wito wewe furaha yako ni kufundisha na kuelimisha na sio kupata sifa au ujira, kwahio kama vile akunyimae Kunde anakupunguzia Mashuzi, vilevile aliyekunyima kusimamia basi amekuongezea muda wa kusahihisha na kuwanoa wanafunzi wako.
Nafikiri jibu hili umelenga kumuumiza zaidi mtoa mada.

Huko alipo anasaga meno kwa hasira
 
Nipo shuleni ofisini

Mbele yangu Kuna mzigo mkubwa wa daftari za stadi za kazi darasa la tano ninazopaswa kusahisha...
Ni sawa tu, kwani kwenye uchaguzi kazi yenu uwa ni ipi? Malipo Hapa Hapa, na bado
 
Mleta mada kama ni mwalimu serikali ilikuajiri kimakosa

Hiyo kitu inaitwa segregation of duties

Huwezi kufundisha wewe,utunge mtihani wewe,usimamie wewe na usahihishe wewe!!!
Alitakiwa spangle kwingine, nadhani ndio haja yake
 
Kwa swali hili na logic uliyoitumua hapa kweli wewe ni Mwalimu.

By the way hii kazi ilikuwa wito wewe furaha yako ni kufundisha na kuelimisha na sio kupata sifa au ujira.., Kwahio kama vile akunyimae Kunde anakupunguzia Mashuzi, vilevile aliyekunyima kusimamia basi amekuongezea muda wa kusahihisha na kuwanoa wanafunzi wako.
Ila kumbuka kwenye kusimamia mitihani wasimamizi ulipwa posho. Hivyo kwenye hii mitihani walimu husika wa shule za msingi wamekosa hizo posho.
 
Nimesoma maoni yote hakuna hata mmoja aliyeonyesha mzizi wa tatizo wote tunamlaumu mtoa mada ,lazima kama wadau wa elimu tujiulize kwa nini tatizo hili litokee ?Nani anatakiwa kulaumiwa ni huyu mwalimu au Serikali?
 
Haiwezekani mtambuliwe na na kuheshimiwa na wengine wakati ninyi wenyewe hamjitambui. Jipeni moyo yawezekana nanyi mtakwenda kusimamia mtihani wa kidato cha nne mwezi November.
 
NDIYOOO!! Mna cheat nakupeleka watoto hawajui KKK sekondari, toeni ujinga wenu hko mwaka huu imekula!

Kwanza wengiwenu mlifeli form four so kaeni kiadabu na walimu wasec. wawanoe angalao
 
Nipo shuleni ofisini

Mbele yangu Kuna mzigo mkubwa wa daftari za stadi za kazi darasa la tano ninazopaswa kusahisha

Naangalia nje namuona mwalimu wa sekondari yuko bize kusimamia mtihani wa darasa la Saba

Najiuliza kwanini nisisimamie mwenyewe mwalimu wa shule ya msingi?

Je, Serikali imenichukia sana kiasi cha kuninyang'anya majukumu yangu?

Hili limenisikitisha sana nahisi nakosa furaha yangu ya kawaida hapa shuleni

Ni kawaida yangu asubuhi kuwatia moyo watahiniwa kuwa watulivu kisaikolojia ila ukweli leo nimejikuta nimeshindwa kufanya hivyo

Je, huu ni muendelezo wa serikali yetu kutudharau waalimu shule za msingi?
Nilisikia ati walimu wa primary ni form four failures
 
Nilisikia ati walimu wa primary ni form four failures
Sio failures, serikali inatambua kuwa ufaulu ni division 1 Hadi division 4
Failure ni division 0
Hizi div 4, mambumbu wengi Kama wewe mumeaminishwa kuwa ni failure
Hii div 4 sio ya waalimu tu, ni ya kada zote Kama vile majeshi ya ulinzi na usalama, kada za afya, (manesi na maklinical officers) waandishi wa habari, wanasiasa na wengineo
 
Mleta mada kama ni mwalimu serikali ilikuajiri kimakosa

Hiyo kitu inaitwa segregation of duties

Huwezi kufundisha wewe,utunge mtihani wewe, usimamie wewe na usahihishe wewe!
Mbona toka Uhuru 1961 ilikuwa ulifanyika hivyo? Hiyo segregation mmeiona leo?
 
Mwalimu bora anabidi apate division 1 hadi 3 na sio Division four
 
Back
Top Bottom