Je,ilikuwa mpango wa Mungu Afrika kutawaliwa ili tupate Injili au kujua dini?

Je,ilikuwa mpango wa Mungu Afrika kutawaliwa ili tupate Injili au kujua dini?

Mnyatiaji

JF-Expert Member
Joined
Dec 13, 2018
Posts
3,728
Reaction score
4,817
Nimekuwa nikijiuliza hilo swali apo juu mara kadhaa kama tusingetawaliwa kuanzia waarabu mpka mkoloni mzungu inamaanisha hizi dini zisingekuepo.Je,hayo yalitokea kama mapenzi ya Mungu?
 
Mapenzi ya mungu yupi? jaribu kuwa specific.
 
Kuteswa, kudharirishwa, kufedheheswa, kuuliwa hovyo yaani kunyongwa na kuchinjwa. kufungwa minyororo shingoni na kupigwa mijeredi kama mbwa au punda, wanawake na watoto kubakwa, kufanywa Watumwa.

Hayo ndio mapenzi ya mungu?
 
Alikosa efficient way ?, yaani kama unavyodownload software (akatupa huo uelewa)?...

Au kama ambavyo haufundishwi kula au kusikia njaa...., Hizi imani zinasaidia tu kuvuka matatizo / kuyakubali kwamba yote ni mipango unless otherwise acceptance ingekuwa ngumu
 
Dini ni tool ya kumcontrol mwanadam hasa afrika... elimu ya dini ndio elimu pekee inatolewa bure duniani hasa afrika. Na nielimu ambayo haitaji uwe na alama za juu ili uisome, ni elimu pia hujengwa kwahofu ili usichunguze mambo ila uamini tu kile unachambiwa

watu weupe wamekuwa wakarimu wa kusupport na kuchapisha kila aina tafsiri ya lugha kwa lugha tofauti tofauti kwa masomo ya dini...

lkn wamekuwa wagumu kufanya hvyo kwa elimu ya maendeleo, uvumbuzi, utabibu,falsafa, sheria teknologia nk bali wamekuwa wakizifanya elimu za hz kuwa ghali na za gharama ambazo zmewekewa alama za ufaulu wa juu ili uweze kuzsoma...na km huna hela huwez kuzipata hzo elimu ili uwe mbumbu na waweze kukutawala... #Amka Afrika
 
Hapo waafrika ndo tulipokubali kutawaliwa na kunyanyasika katika dunia hii, maana tuliuza thamani yetu. Hizi dini zipo kwaajili ya kututawala, Mungu wetu tulimuacha ndo maana siku zote tutakuwa nyuma hatutowaweza watu weupe. Kibaya zaidi hizi dini zimewaathiri sana waafrika kuliko huko zilikotoka. Mungu wetu tumemuacha tunaabudu Mungu wa wengine, hata maandiko yameandikwa kwa watu wa huko itakuwaje wew yakusaidie. Ili afrika tuwe vinara inabid turejeshe dini zetu za asili yetu. FOREIGN RELIGIONS SHOULD BE ERASED
 
Mungu naye pia ni mtumwa anayefungwa na mfumo wake mwenyewe.

Hawezi kumuumba mungu mwingine mkubwa kuliko yeye, hawezi kurudi nyuma ya muda arekebishe mambo ambayo hayakwenda atakavyo
 
IMG_20210130_123255.jpg
 
Yaani hizo slavesh religion ndo tuzifuate? Acheni ujinga nyie watu Africa tuna miungu yetu tuliyoitelekeza ndo maana kama tumelaniwa vile,dini za mashariki ya kati ni mizigo mizito tuliyojitwisha waafrika bila sababu za msingi,hivi tangu wazilete hizo dini huyo mungu wa wayahudi ashawahi kutusaidia zaidi ya kuongeza majanga tu?
 
Nimekuwa nikijiuliza hilo swali apo juu mara kadhaa kama tusingetawaliwa kuanzia waarabu mpka mkoloni mzungu inamaanisha hizi dini zisingekuepo.Je,hayo yalitokea kama mapenzi ya Mungu?
Swali fikirishi.
 
Yako mengi sana ya kujifunza kwenye suala la dini
Kwanza kabisa dini zetu za kitamaduni zilikuwa na miiko yake, nzuri na mibaya.
Mfano mauaji ya twins, sadaka za binadamu nk. Lakini licha ya yote hayo dini hizi hazikuwa static, yaan hakuna Mungu mmoja, bali wengi wenye masharti totauti tofauti na ukihamia eneo fulani Basi utalazimika kuabudu Mungu wa huko.
Hivyo basi huu pia ulikuwa mwanya wa Hawa wakoloni kutumia Mungu wao kuturubuni.
Tunachoweza kufanya kwa sasa ni kuendelea kuamini kwa jinsi kila mmoja anavyoona inafaa kwake. Maana zaidi ya miaka 500 ya kutawaliwa unategemea dini zetu tutazikumbuka? Ngumu sana.
Kama kwenye kabila lako au ukoo wako bado mnaendeleza dini za kitamaduni Basi mzi tathmini muone Kama zinafaa. Ila leo Mimi kutoka Singida uniambie kuabudu mila za wachaga kweli siwezi kabisa. Hapa kwenye dini kila mmoja afuate msimamo wake.
Ushauri. Waafrika tuache kurogana na kuoneana wivu wa kijinga. Hii ni shida sana. Baadhi ya maeneo Kuna wachawi hatari na hawapendi maendeleo ya wengine. Tupendane waafrika
 
kama tusingetawaliwa
Maswali kama haya huwa hayana mantiki

Haya maswali ya kama kama kama.

We jiulize tu kama baba na mama yako wasingefanya yao ukapatikana wewe hiyo kazi unayoifanya wewe ingelifanywa na nani ?

Je ni mpango wa Mungu wazazi wako kukuzaa ili leo uje kuwa hapo ulipo ama imekuaje ?

Mkuu kama waafrika tusingetawaliwa na wakolpni basi nina imani Mungu kama lengo ilikuwa dini itufike angekuwa na option zingine za kufanya mpaka sisi dini itufike.

Kuna msingi unaosema hivi. "Lililokupata halikuwa likukose,na lililokukosa halikuwa likupate"

Sio limekupata jambo eti oooh lisingenipata ingekuwaje vile,hakuna ingekuwaje limeshakupata jadili juu ya jambo ambalo limeshakupata tayari usijadili mambo ya lau kama lau kama lau kama..
 
Yako mengi sana ya kujifunza kwenye suala la dini
Kwanza kabisa dini zetu za kitamaduni zilikuwa na miiko yake, nzuri na mibaya.
Mfano mauaji ya twins, sadaka za binadamu nk. Lakini licha ya yote hayo dini hizi hazikuwa static, yaan hakuna Mungu mmoja, bali wengi wenye masharti totauti tofauti na ukihamia eneo fulani Basi utalazimika kuabudu Mungu wa huko.
Hivyo basi huu pia ulikuwa mwanya wa Hawa wakoloni kutumia Mungu wao kuturubuni.
Tunachoweza kufanya kwa sasa ni kuendelea kuamini kwa jinsi kila mmoja anavyoona inafaa kwake. Maana zaidi ya miaka 500 ya kutawaliwa unategemea dini zetu tutazikumbuka? Ngumu sana.
Kama kwenye kabila lako au ukoo wako bado mnaendeleza dini za kitamaduni Basi mzi tathmini muone Kama zinafaa. Ila leo Mimi kutoka Singida uniambie kuabudu mila za wachaga kweli siwezi kabisa. Hapa kwenye dini kila mmoja afuate msimamo wake.
Ushauri. Waafrika tuache kurogana na kuoneana wivu wa kijinga. Hii ni shida sana. Baadhi ya maeneo Kuna wachawi hatari na hawapendi maendeleo ya wengine. Tupendane waafrika
Sahihi kabisa.

Nikitizama dini za tamaduni naona zina mapungufu kibao ambayo mengi hayana mantiki na hayana ukubaliano na akili,bora dini ambayo niko nayo naona inanipa utulivu juu ya imani yangu
 
Back
Top Bottom