Diplomatic Imunnity
JF-Expert Member
- Apr 2, 2012
- 1,179
- 320
Najaribu kukuelewa sana hasa kwenye hoja ya ugonjwa na arvs nani wa kwanza kusambaa.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
yani imenibidi nikashee na rafiki zangu hii elimu. ahsante sana DECEPTION
Kwa elimu ya deception juz jioni nimekaa na familia yangu tulijadili sana hii issue na sasa naanza kuona mwanga uliojificha
Fuatilia hapa mkuu kwa elimu zaidi
www.fadhilipaulo.com
Ukweli kuhusu AIDS/HIV
Mi nadhani inawezekana. Kuna jirani yangu mmoja jina(), kabla ya kuoa alikwisha lala na wanawake wasiopungua 60, na wengine alikuwa anaambiwa wana ukimwi na kwa kudhibitisha kabisa ni kweli wanao na wengine washafariki kwa hali zao kuwa mbaya ila yeye mpaka leo kila anapopima ukimwi anakutwa hana.
ey try to get serious.... mi naona unapotosha watu tu na theory zako!!!
* HIV/AIDS Imeanza kuingia kabla hata ya ARVs kuuzwa, unavosema kuwa HIV/AIDS ni mradi wa kuuza ARVs unakosea sana.... ingeku hivyo basi ARVs zingekuja zamani sana pamoja na ugonjwa huo
* HIV/AIDS inasababishwa na ARVs.... seriously!???
...wangapi ambao hawajaanza hata kutumia hizo dawa na tiari wanaugua ukimwi...
... ni ugonjwa gani unaowadhoofisha mpaka kufa ambao bado hauna jina na ni nini dawa ya huo ugonjwa...
....ukimwi upo jamani, acheni siasa kwenye mambo ya msingi
Kama HIV haisababishi ukimwi je ni ugonjwa gani huo unaowafanya watu Kukonda sana mpaka wabaki na kilo mbili, na kunyonyoka nywele?
...nini kinasababisha mkanda wa jeshi na nini tiba yake?...
...kama ARVs ndiyo inasababisha ukimwi iweje mtu ambaye hakuwahi kutumia ARV apungukiwe na nguvu kiasi cha kumuacha na kilo 2 na maradhi yasiyo na idadi.
....Bado napata utata na kivipi ARV ndie msababishi wa AIDS
Mkuu deception naomba ufafanuz
HIV virus inapenya kwa Urahisi kwenye epithelium tissues/cells, mfano wa Epithelium cells ni zile cells ambazo kiasili zina unyevunyevu na blood capillaries zipo karibu karibu, mfano wa cells hizo ni Kichwa cha uume ambao haujatahirwa, au kama umetahiriwa basi ni pale kwenye kitundu cha kutolea mkojo, ukibinya uume na kuangalia kile kitundu utaona kale ka ngozi kekundu.
Uke wa mwanamke kwa ndani ndo kuna aina hii ya tissue sana.
Tissue zenye ngozi ngumu mfano mikono, vidole siyo rahisi vidudu kupenya kwa sababu tissue za viungo hivi hazina receptors za HIV.
Ndiyo maana inashauriwa kutahiriwa wanaume, ili ngozi ngumu iote ambayo haina receptors kwa HIV
Unaweza Ukamtia kidole mwanamke mwenye Ukimwi, usipate Ukimwi, kwa sababu kidole hakina receptors hizi unless uwe una jeraha/ mchubuko haswa unaokuexpose kwa receptors wa virusi hivi
Au Shahawa za mwanaume zinaweza kudondokea let say kwenye ngozi ya nje ya mwili, kama tumbo, kifua, mapaja lakini Mhusika asipate Ukimwi, mpaka iwepo jeraha lenye kuexpose inner epithelium cells.
Sehemu nyingine zenye epithelium cells kwa wingi ni ukibinua jicho ngozi ile nyekundu, ukibinua mdomo, Mkunduni.
NA LIQUIDS ZENYE HIV LOAD KWA WINGI ZAIDI NI 1. DAMU, 2. SHAHAWA, 3. MAJI YA UKENI
Nakupongeza sana kwa elimu nzuri unayoitoa mwanzoni nilipoanza kusoma huu uzi nilibaki 50/50 ,nilitaka kupinga kama watu wengine wanavyokupinga lakini niliona kwamba kabla ya kukupinga niliona ni vyema nikatafuta facts kwanza. Kizuri ni kwamba ulimwengu wa teknolojia umekua, niliingia Google kuutafuta ukweli ulipo. Niliyokutana nayo ndiyo yamenifanya nije hapa leo nikupongeze ingawa bado naendelea ku-speculate zaidi na zaidi. Facts nilizokutana nazo ni kwamba HIV ni retrovirus kama ulivyoeleza hapo mwanzo na amesingiziwa tu kuwa anasababisha AIDS. But purposely walitengeneza Antiretrovirus drugs ili kurasmisha walichokisema kumbe ARV ndizo zinazoharibu kinga ya mwili halafu wanamsingizia HIV.
Pamoja sana mkuu nashukuru kwa kunifumbua macho juu ya hilo , ushauri wangu kwa wengine ni kwamba kwamba mtu anapokuja na hoja aliyoiwekea evidences tusikimbilie kupinga tu. Be ready to learn something kutoka kwake,penye doubt muulize, hujaridhika na majibu tafuta ukweli kwenye mitandao. NA KWA TAARIFA YAKO UKIMWI HAUJAANZIA AFRIKA KAMA TULIVYOKARIRISHWA
Watanzania wengi hawajakomaa katika kufanya mijadala,na ndio maana tunabaki nyuma kiuelewa kwa kuwa tunapoona au kusikia kitu kipya tunaanza na kupinga kwanza kabla ya kuruhusu akili kudadisi au kujiuliza,hii ni mbaya sana.
1.Kuwa makini sana, usije wewe ndio ukawa hauko serious.
2.Unathibitisha vipi kwamba mimi napotosha watu?
3.Una uhakika gani kwamba haya ninayoeleza ni theory zangu?
Wewe umeshajikita kwenye upingaji na umefunga kabisa milango yako ya fahamu kuelewa chochote nitakachoeleza,hivyo nakusikitikia sana kwa kukosa kuujua ukweli huu wa karne,na kuikosa elimu hii kunaweza kukusababishia matatizo makubwa aidha wewe au ndugu zako wa karibu endapo utafikwa na janga hili.
Unachokiongea hapo juu hukielewi kabisa;
1.Hufahamu hata historia ya HIV/AIDS hata kwa tanzania pekee.
2.Hujawahi hata kuhudhuria clinic za watu wanaotumia ARVs na kufanya utafiti.
3.Unaweza kunijibu nimekosea vipi kusema kwamba HIV/AIDS ni mradi wa kuuza ARVs?
4.Una uhakika unajua ni lini ARVs zilianza kutumika?na ni aina gani za ARVs zalianza kutumika?
Seriously!
Ugonjwa wa AIDS kwa watu wanaotumia ARVs unasababishwa na ARVs na si HIV.Una hoja ya kupinga hilo ninalosema mimi ili tuwape wengine faida?
1.Nikikuuliza ukimwi ni nini utajibu vipi?
2.Unajua ukimwi unasababishwa na nini?
3.Je,unajua kama ukimwi ulikuwepo karne nyingi kabla ya kutangazwa kwa HIV mwaka 1984?
1.Kuna magonjwa mengi yanadhoofisha watu mpaka kufa zaidi ya huu ugonjwa feki wa HIV/AIDS,ni kweli wewe hujui hili?
Mfano mmojawapo wa ugonjwa huo ni TB.Je,unajua kwamba ukiwa na TB muda mrefu utakonda sana,utaishiwa nguvu,unaweza kutapika,unaweza kuharisha kutegemea na aina ya TB,utakosa hamu ya kula,utakuwa na homa mara kwa mara,na ajabu zaidi unaweza ukapimwa HIV na vipimo vikatoa majibu Negative/huna HIV.Je,hizi nilizotaja sio dalili za ugonjwa feki wa HIV/AIDS ulizoambiwa wewe zamani?Huoni kwamba dalili hizo zinafanana?
Kama hayo maelezo ni sahihi,Je,ukimwi ni nini basi?
2.Dawa ya ugonjwa hutegemea na aina ya ugonjwa.Kama ugonjwa ni TB utapewa tiba ya TB na utapona kabisa.
Wewe ndio unaleta siasa kwenye mambo ya msingi.Watu wameshaanza kuelewa,wewe unaleta siasa,hujaleta hata hoja moja ya kisayansi kuthibitisha unachokisema,sasa nani kati ya mimi na wewe analeta siasa?
Ndugu yangu ninakushauri tu.Hata kama umegundua umeingia vibaya kwenye mada hii,usijali kuonekana mdhaifu,hivyo ndivyo mijadala ilivyo,jitahidi kuwa na free mind katika maisha yako ili uwe mwepesi wa kuhoji/kudadisi au kuuliza endapo utakumbana na kitu kipya akilini mwako,usiwe mwepesi wa kupinga tu kila jambo jipya.Utakosa mengi na hasa yale ya muhimu katika maisha yako.
1.Ukimwi hauambukizwi
2.Ukimwi hauambukizwi kwa njia ya ngono
3.HIV hawezi kusababisha ukimwi na hasababishi ukimwi kwa kuwa hana sifa ya kusababisha ukimwi.Nashauri tujitahidi kwenda nje ya mainstream kutafuta habari,mambo mengi tunayoyafahamu kwenye dunia hii hayapo kama tunavyoyaona au kuyasikia,na mambo yamewekwa hivyo kwa sababu maalum kabisa.Anayesikia haya kwa mara ya kwanza atadharau au kufunga milango yake ya fahamu,kufunga milango ya fahamu hakubadilishi ukweli kuwa uongo,ukweli utabaki palepale.
Ukielewa ukweli kuhusu jambo hili utakubaliana na mimi kwamba mtu yeyote anayeogopa HIV ni sawa na kuogopa kivuli chake mwenyewe.Kama una swali lolote ambalo unadhani lina utata kuwa huru kuuliza.Nimetimiza wajibu wangu kutoa dokezo,kama mtu ana dukuduku/swali awe huru kuniuliza.
Hebu gusa link hapo chini kwa kuanzia;
https://www.youtube.com/watch?v=pB8g0b-FkW0
Ni kwel kabla hujatumia unakua vizuri kosa utumie na ukaacha ndo unaanza kuumwa....
...Na inakuaje mtu anakonda unakohoa kama ukimwi haupo nifundishe tafadhali.....
....Na kwa nn wanasema ukitumia hzo dawa hutakiwi kuacha....
Mkuu inaonekana unajua mengi tuwekee taarifa kwa kina zaidi au anzisha uzi nasi tupate uelewa wa kina
Hao wanaopinga kuwa HIV hasababishi AIDS hivi mko serious?.
Kama hoja ni kama ya Thabo Mbeki kwamba Umasikini na lishe duni ndo inasababisha Ukimwi, vipi kuhusu matajiri kama Lwambo Makiadi, Vipi kuhusu Mashoga wa Marekani wenye pesa walioambukizwa, Vipi Matajiri Lukuki ambao wanaafford Misosi ya maana?.
Jamani Tumeuguza mama zetu, kaka zetu, ndugu zetu n.k Tumeona hali ilivyo, msifanye masikhara
Na kama HIV hasababishi AIDS kwa nini hutokea mpenzi mmoja aliyefiwa na mwenziwe kwa AIDS naye baada ya muda fulani huanza kudevelop Dalili za AIDS?
Hao wanaopinga kuwa HIV hasababishi AIDS hivi mko serious?.
Kama hoja ni kama ya Thabo Mbeki kwamba Umasikini na lishe duni ndo inasababisha Ukimwi, vipi kuhusu matajiri kama Lwambo Makiadi, Vipi kuhusu Mashoga wa Marekani wenye pesa walioambukizwa, Vipi Matajiri Lukuki ambao wanaafford Misosi ya maana?.
Jamani Tumeuguza mama zetu, kaka zetu, ndugu zetu n.k Tumeona hali ilivyo, msifanye masikhara
Na kama HIV hasababishi AIDS kwa nini hutokea mpenzi mmoja aliyefiwa na mwenziwe kwa AIDS naye baada ya muda fulani huanza kudevelop Dalili za AIDS?
Unaelezeaje kuhusu wanaume ambao wamepimwa wakakutwa HIV+ wanaishi na wanawake na kuwapa mimba lakini wanawake hao wanapimwa ila hawakutwi na HIV?
Unakumbuka swali hilo hapo chini?Kama ulikuwa hujaliona basi nimekuwekea tena hapo chini.
Ndio maana nikasema kwamba kutokana na ufeki wa ugonjwa huu kuna mikanganyiko mingi sana,we mwenyewe umejionea au kusikia kama ulivyoeleza hapo juu.Maneno yako hapo juu hata wenyewe wanakubali kwamba si rahisi mtoto kuambukizwa na wametoa asilimia 98% kama mama atakula ARVs na 75% kama mama hatakula ARVs kuonesha uwezekano wa mtoto kuepuka maambukizi haya ambayo mimi kwangu ni feki.Hongera kwa kuhoji hilo,maana kujihoji ni mwanzo wa kuelewa ukweli.
Unajua mkuu,hawa jamaa wanajua hii ndio starehe ya watu wengi,na ndio maana wameng'angania kwamba unaambukizwa kwa njia hii kwa kuwa kila mtu akiambiwa anao atakuwa na uwezekano mkubwa kwamba alishawahi kufanya ngono hivyo hata mtu mwenyewe hatapinga akiambiwa kwamba anao.Mkuu wewe furahia maisha tu,wasitufanye tuwe watumwa wa asili yetu.Wanajifanya hao ndio miungu,tumeshabaini ukweli na tuko huru.
Hata ukiwa na manjonjo ya aina gani,fanya mbwembwe zote unazozijua duniani kwenye ngono,huwezi kupata ukimwi/VVU.Kuonekana kwamba una VVU ni matokeo ya vipimo feki na si kwamba kweli una VVU.VVU hayupo kiuhalisia hivyo basi ukimwi hausababishwi na VVU.Fuatilia vizuri post zangu utaelewa au watu kama mavado wanaweza kukusaidia pia.Ukijua sayansi inayotumika katika vipimo vya VVU utajua ukweli uko wapi.Na ndio maana niliwahi kusema kwamba,ukitaka ukimwi uishe,basi watu wasijitokeze kupima VVU,au wagome kabisa kupima VVU na badala yake mtu akiumwa apimwe ugonjwa wake halisi tu na kupewa tiba halisi kama zamani,hapo ukimwi utakuwa umeisha.Lakini kwa kampeni hizi feki za kutuonesha kama vile wanatupenda saaaana na wanajali saaaana maisha yetu,watu watapimwa VVU na vipimo feki,wataonekana VVU+ na hatimaye watapewa dawa za ARVs ambazo ndio hasa zinazosababisha ukimwi kwa wanaozitumia halafu tunamsingizia VVU.Ukijua mtego huu basi utakuwa umejikomboa na janga hili.Njombe wanaongoza kitakwimu kwa VVU/Ukimwi kwa sababu wanajitokeza sana kupima VVU,hawaogopi kupima na kuchukua majibu,hii ndio sababu kubwa na hamna sababu nyingine,lakini kwa mtu anayechukulia mambo kiurahisi hataelewa ninachosema,labda watu kutoka njombe waje kuthibitisha wenyewe hapa.