Habari ya Mujini
JF-Expert Member
- Dec 22, 2013
- 2,517
- 1,044
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Daaah halafu ukiangalia huu ugonjwa waweza sema unapendelea asee. Kuna ndugu yangu yeye ni mlevi sana na anahakikisha kila akilewa anaondoka na barmaid. yaani kwa siku hata wadada watatu anaondoka nao tena wale hatarishi kabisa na hana rekodi ya kutumia kondom kabisaa. Tangu ujana wake ndio yuko hivohivo na mpaka sasa umri unamtupa mkono lakini bado na wadada kama damu.
Lakini mpaka leo hana vvu wala ukimwi asee na anadunda kama kawa mipombe kama kawa mademu mwendo uleule. Sasa katembee wewe na barmaid mmoja tu uone kama hujafa kwa presha kabla tarehe yako ya kurudia kupima.
Jibu ni kwamba kuna watu hawapati Virusi vya Ukimwi Naturally, wana genetic composition ambayo haifevi virusi kuingia , kwa mfano kuna hii gene inaitwa CCR5-Δ32, wenye gene hii hawaathiriwi na HIV
Google hii information ya CCR5 Delta 32
Kutokana na maelezo yako inaonesha hujui bado.Uliyoeleza hapo juu ni uongo mtupu.Hata huo uongo uliousoma pia umeshindwa kuuelewa.Ngoja nikwambie uongo wenyewe uko vipi kuhusu CCR5-Δ32 receptor halafu nitakwambia kwa nini huo ni uongo.Tuliza akili yako;
Hata huu uongo ulioumeza,hukuumeza kama inavyotakiwa.Uongo huu haukusema kwamba watu hawa hawapati HIV bali HIV hawezi kuathiri targeted cell kwa kuwa hawana receptors kuruhusu HIV kudhuru cell zinazohusika na kinga.Lakini uongo huu unakubali kwamba HIV huweza kuingia kwenye damu ya mtu lakini mtu huyu hawezi kuathirika.Wewe unasema watu hawa hawapati HIV.Umeona tofauti hapo?
Jibu lako lilitakiwa kueleza kwa nini hawa watu niliokuuliza mimi kwenye swali langu hawajapata HIV na si kwa nini hawaathiriwi na HIV.Umeelewa hapo?Mnapenda kuja na materminology ambayo hamyaelewi,ndio maana nakusihi uwe tayari kusikiliza.Kama hata uongo huu umeshindwa kuunasa kama ulivyo Je,utaweza kuelewa ukweli nitakao kwambia?Nikwambie kitu;hawa jamaa wana sababu kubwa sana ya kutuambia hivyo kuhusu CCR5-Δ32 ambayo nitakwambia baadaye,wewe hujui.
Ukweli ni huu hapa chini.Nikikwambi uthibitishe kwamba watu wenye CCR5-Δ32 gene hawaathiriwi na HIV(ambaye kwangu mimi ni feki) nitakuwa nimekuonea bure,maana hata hao waliokuandikia uongo huo hawana scientific paper/proof.Najua utahangaika sana kwenye mitandao ili kurudisha majibu lakini ukweli unabaki palepale kwamba hiyo uliyoisoma sio sayansi ya kweli,yaani ni pseudo-science,au ni sayansi ya kurubuni akili za watu ili wajipatie pesa kupitia mauzo ya ARVs,kwa kuwa wanajua sisi hatuwezi kuingia kwenye damu ya mtu kujithibitishia kwamba HIV hawezi kuingia kwenye cell ambazo hazina coreceptors kwa macho yetu.Sayansi ya kweli ni hii ninayokueleza mimi.
Mimi ninakuwekea scientific paper hapa kuthibitisha kwamba ulichoeleza wewe kuhusu gene mutation ni uongo,na wewe lete scientific paper kupinga ile ninayoleta mimi.
Duuh...mkuu hoja zako kama zina ukweli ndan yake...sasa kwann miaka ya nyuma kabla ya ARVs wagonjwa wa ukimwi walikuwa wakiumwa sana na kukonda au ule nao haukuwa ukimwi?
Daaah halafu ukiangalia huu ugonjwa waweza sema unapendelea asee. Kuna ndugu yangu yeye ni mlevi sana na anahakikisha kila akilewa anaondoka na barmaid. yaani kwa siku hata wadada watatu anaondoka nao tena wale hatarishi kabisa na hana rekodi ya kutumia kondom kabisaa. Tangu ujana wake ndio yuko hivohivo na mpaka sasa umri unamtupa mkono lakini bado na wadada kama damu.
Lakini mpaka leo hana vvu wala ukimwi asee na anadunda kama kawa mipombe kama kawa mademu mwendo uleule. Sasa katembee wewe na barmaid mmoja tu uone kama hujafa kwa presha kabla tarehe yako ya kurudia kupima.
Hauko serious wewe....
..... watu wanakufa tunaona kwa macho yetu ati unasema ni uzushi ....
.... ukapimwe akili, ....
.... kwa maana hii hata mchawi au jini ni imani tu
Unatumia nguvu nyingi kwenye Maconspiracy theories wakati hujui chochote. Lete ushahidi na scientific evidence wa hoja zako muflisi
HIV/AIDS au VVU/UKIMWI hauambukizwi kwa njia ya ngono/sex na HIV hasababishi ukimwi.Jitahidini kidogo ku stretch uwezo wenu,elimu ipo lakini mnairuka kwa makusudi.
HIV/AIDS is a mindset disease.Sijui kama nitaeleweka kwa kusema hivi.Yaani ugonjwa huu haupo kiuhalisia,kinachoua si HIV bali kinachoua ni ARVs kwa wale wanaozitumia.Hata kama mtu hatumii ARVs na amedhoofika wewe mpime tu utagundua kwamba lazima awe na ugonjwa fulani unaofahamika,aidha TB,Pneumonia,Cancer nk.
Watu wanadhani mimi nimekurupuka kwa siku moja tu na kuja kuandika yote haya,la hasha nimefuatilia na kufanya tafiti ya mambo haya kwa zaidi ya miaka 5.Watu wanachukulia kirahisi sana,hawagundui hata kwa nini mimi ninawaeleza haya,hawagundui hata kidogo upendo huu ninaouonesha kwao.
Ndugu. unachojaribu kusema ni kwamba ARVs badala ya kuongeza maisha bali ndio inasababisha vifo. Sijakuelewa vizuri labda.
Unazidi kunisikitisha ndugu yangu.Unachoniomba hapo kwenye nyekundu hukukiona sehemu ya chini kabisa ya maelezo niliyotoa?Au unafanya makusudi?Chini niliweka scientific paper/proof,Je,hukuiona?
Ndio maana nikakushauri kwanza ujiweke tayari kiakili kusikiliza ndio utapata elimu.Wewe hauko tayari bado kusikiliza na ndio maana ume bypass na hukuiona kabisa hiyo scientific paper.Unaendelea kunizidishia majonzi kwa kung'ang'ania kupinga pasipo kuhoji.
Swali langu hukunijibu bado,ok,si tatizo.Nimeleta scientific paper hutaki kuisoma halafu unakuja tena unaniomba scientific evidence.Jitahidi kubadilika ndugu yangu,najua ni ngumu kukubali,lakini jitahidi kidogo.
HIV/AIDS au VVU/UKIMWI hauambukizwi kwa njia ya ngono/sex na HIV hasababishi ukimwi.Jitahidini kidogo ku stretch uwezo wenu,elimu ipo lakini mnairuka kwa makusudi.
HIV/AIDS is a mindset disease.Sijui kama nitaeleweka kwa kusema hivi.Yaani ugonjwa huu haupo kiuhalisia,kinachoua si HIV bali kinachoua ni ARVs kwa wale wanaozitumia.Hata kama mtu hatumii ARVs na amedhoofika wewe mpime tu utagundua kwamba lazima awe na ugonjwa fulani unaofahamika,aidha TB,Pneumonia,Cancer nk.
Watu wanadhani mimi nimekurupuka kwa siku moja tu na kuja kuandika yote haya,la hasha nimefuatilia na kufanya tafiti ya mambo haya kwa zaidi ya miaka 5.Watu wanachukulia kirahisi sana,hawagundui hata kwa nini mimi ninawaeleza haya,hawagundui hata kidogo upendo huu ninaouonesha kwao.
*unataka tuamini linki zako ila wengine wakikuwekea unazikataa.... kwanini tuanini link zako na kuacha zingine!??
*Unaulizwa maswali mengi na mengi unajibu kwa kuuliza maswali na wewe, hapo unazidi kujichanganya
.......... nijibu haya tu na kazi imeisha......
*ukimwi ulianza kugundulika kwa mtu wa kwanza kabla ua arv kuwepo.... aliupata kwa njia gani bila ya kuambukizwa kupitia arv!??
*arv ya kwanza kugundulika ilikua 1988 lakini kwa tabzania zilichelewa kufika mpaka miaka ya mwanzo ya 90, je kwa kipindi chote hicho maambukizi yalikua kwa njia gani!??
*TB unayoisema imeanza zamani sana na wagonjwa walikua wanapata dawa mbalimbali, inakuaje kwa tb hii kuuwa watu wengi namna hiyo na kukondesha kiasi hicho.
*kama ni TB mbona ukimwi unasemekana ulianzia Bukoba miaka hiyo, watu wa mikoa mingine walikua hawaugui TB!?? kwanini na wenyewe wasiishe kama watu wa BK walivyokua wanadhoofika
naomba majibu kwanza na usinijubu kwa maswali tafadhari
Uko sahihi mkuu,watu wengi walishaniambia hivyo.Tatizo mada hii ina mambo mengi sana na watu ni lazima wayasome yote ili wakubaliane na ukweli,haitakiwi kusoma kwa kurukaruka.Kwa navyowajua wana JF wengi hawana tabia hiyo.Nina mifano hai,mimi sio wa kwanza kuanzisha mada kama hii,kuna mwana JF mmoja alishawahi kuanzisha lakini watu waliishia kupinga tu,lakini ukiisoma ile mada jinsi ilivyoandaliwa,utagundua kwamba jamaa alitumia muda wake mwingi sana kuonesha upendo kwa wengine,lakini aliishia kupingwa tu na sijamwona tena akizungumzia au kuchangia kwenye mada kama hizi tena hadi leo,labda pengine hakuwa na hoja na uzoefu wa kutosha kujibu hoja za watu.Hii inakatisha sana tamaa,na ndio maana mimi ninatumia utaratibu huu.Natoa dokezo,watu wanauliza maswali,mimi ninajibu kwa kutoa evidence pale zinapohitajika.
Nashukuru kwa maoni yako.Sasa hivi niko mbioni kuanda kajarida/kakitabu kinachoeleza ukweli kuhusu;
1.HIV/AIDS
2.CANCER
3.MARIJUANA(BANGI)
4.GMO(Genetic Modified Foods)
na mambo mengine kama hayo.Napanga kuweka maandishi na video kwa kiswahili.Watu wengi wanachukulia mambo kirahisi sana,hawajui kwamba karibu mambo yote tunayoyaona na kuyajua sasa ni feki,yapo kwa ajili ya manufaa ya wengine.Na ndio maana ID yangu ni Deception,niko humu kuwajuza watu mambo tuliyodanganywa.
Mkuu vp kuhusu watu waliokua wanakufa miaka ya tisini wakiwa wamedhohofu sans kabla ya kugundulika kwa ARVs?