Je, inawezekana mtu akalala na mwenye UKIMWI tena peku na asipate UKIMWI?

Je, inawezekana mtu akalala na mwenye UKIMWI tena peku na asipate UKIMWI?

Hauko serious wewe watu wanakufa tunaona kwa macho yetu ati unasema ni uzushi ukapimwe akili, kwa maana hii hata mchawi au jini ni imani tu
 
Daaah halafu ukiangalia huu ugonjwa waweza sema unapendelea asee. Kuna ndugu yangu yeye ni mlevi sana na anahakikisha kila akilewa anaondoka na barmaid. yaani kwa siku hata wadada watatu anaondoka nao tena wale hatarishi kabisa na hana rekodi ya kutumia kondom kabisaa. Tangu ujana wake ndio yuko hivohivo na mpaka sasa umri unamtupa mkono lakini bado na wadada kama damu.
Lakini mpaka leo hana vvu wala ukimwi asee na anadunda kama kawa mipombe kama kawa mademu mwendo uleule. Sasa katembee wewe na barmaid mmoja tu uone kama hujafa kwa presha kabla tarehe yako ya kurudia kupima.

Mkuu ndugu yko ni mwalimu dasrama??!! Samahani lakini maana umenikumbusha ticha wangu mmoja hivi!!
 
Jibu ni kwamba kuna watu hawapati Virusi vya Ukimwi Naturally, wana genetic composition ambayo haifevi virusi kuingia , kwa mfano kuna hii gene inaitwa CCR5-Δ32, wenye gene hii hawaathiriwi na HIV

Google hii information ya CCR5 Delta 32

Kutokana na maelezo yako inaonesha hujui bado.Uliyoeleza hapo juu ni uongo mtupu.Hata huo uongo uliousoma pia umeshindwa kuuelewa.Ngoja nikwambie uongo wenyewe uko vipi kuhusu CCR5-Δ32 receptor halafu nitakwambia kwa nini huo ni uongo.Tuliza akili yako;

Hata huu uongo ulioumeza,hukuumeza kama inavyotakiwa.Uongo huu haukusema kwamba watu hawa hawapati HIV bali HIV hawezi kuathiri targeted cell kwa kuwa hawana receptors kuruhusu HIV kudhuru cell zinazohusika na kinga.Lakini uongo huu unakubali kwamba HIV huweza kuingia kwenye damu ya mtu lakini mtu huyu hawezi kuathirika.Wewe unasema watu hawa hawapati HIV.Umeona tofauti hapo?
Jibu lako lilitakiwa kueleza kwa nini hawa watu niliokuuliza mimi kwenye swali langu hawajapata HIV na si kwa nini hawaathiriwi na HIV.Umeelewa hapo?Mnapenda kuja na materminology ambayo hamyaelewi,ndio maana nakusihi uwe tayari kusikiliza.Kama hata uongo huu umeshindwa kuunasa kama ulivyo Je,utaweza kuelewa ukweli nitakao kwambia?Nikwambie kitu;hawa jamaa wana sababu kubwa sana ya kutuambia hivyo kuhusu CCR5-Δ32 ambayo nitakwambia baadaye,wewe hujui.

Ukweli ni huu hapa chini.Nikikwambi uthibitishe kwamba watu wenye CCR5-Δ32 gene hawaathiriwi na HIV(ambaye kwangu mimi ni feki) nitakuwa nimekuonea bure,maana hata hao waliokuandikia uongo huo hawana scientific paper/proof.Najua utahangaika sana kwenye mitandao ili kurudisha majibu lakini ukweli unabaki palepale kwamba hiyo uliyoisoma sio sayansi ya kweli,yaani ni pseudo-science,au ni sayansi ya kurubuni akili za watu ili wajipatie pesa kupitia mauzo ya ARVs,kwa kuwa wanajua sisi hatuwezi kuingia kwenye damu ya mtu kujithibitishia kwamba HIV hawezi kuingia kwenye cell ambazo hazina coreceptors kwa macho yetu.Sayansi ya kweli ni hii ninayokueleza mimi.

Mimi ninakuwekea scientific paper hapa kuthibitisha kwamba ulichoeleza wewe kuhusu gene mutation ni uongo,na wewe lete scientific paper kupinga ile ninayoleta mimi.
 

Attachments

Kutokana na maelezo yako inaonesha hujui bado.Uliyoeleza hapo juu ni uongo mtupu.Hata huo uongo uliousoma pia umeshindwa kuuelewa.Ngoja nikwambie uongo wenyewe uko vipi kuhusu CCR5-Δ32 receptor halafu nitakwambia kwa nini huo ni uongo.Tuliza akili yako;

Hata huu uongo ulioumeza,hukuumeza kama inavyotakiwa.Uongo huu haukusema kwamba watu hawa hawapati HIV bali HIV hawezi kuathiri targeted cell kwa kuwa hawana receptors kuruhusu HIV kudhuru cell zinazohusika na kinga.Lakini uongo huu unakubali kwamba HIV huweza kuingia kwenye damu ya mtu lakini mtu huyu hawezi kuathirika.Wewe unasema watu hawa hawapati HIV.Umeona tofauti hapo?
Jibu lako lilitakiwa kueleza kwa nini hawa watu niliokuuliza mimi kwenye swali langu hawajapata HIV na si kwa nini hawaathiriwi na HIV.Umeelewa hapo?Mnapenda kuja na materminology ambayo hamyaelewi,ndio maana nakusihi uwe tayari kusikiliza.Kama hata uongo huu umeshindwa kuunasa kama ulivyo Je,utaweza kuelewa ukweli nitakao kwambia?Nikwambie kitu;hawa jamaa wana sababu kubwa sana ya kutuambia hivyo kuhusu CCR5-Δ32 ambayo nitakwambia baadaye,wewe hujui.

Ukweli ni huu hapa chini.Nikikwambi uthibitishe kwamba watu wenye CCR5-Δ32 gene hawaathiriwi na HIV(ambaye kwangu mimi ni feki) nitakuwa nimekuonea bure,maana hata hao waliokuandikia uongo huo hawana scientific paper/proof.Najua utahangaika sana kwenye mitandao ili kurudisha majibu lakini ukweli unabaki palepale kwamba hiyo uliyoisoma sio sayansi ya kweli,yaani ni pseudo-science,au ni sayansi ya kurubuni akili za watu ili wajipatie pesa kupitia mauzo ya ARVs,kwa kuwa wanajua sisi hatuwezi kuingia kwenye damu ya mtu kujithibitishia kwamba HIV hawezi kuingia kwenye cell ambazo hazina coreceptors kwa macho yetu.Sayansi ya kweli ni hii ninayokueleza mimi.

Mimi ninakuwekea scientific paper hapa kuthibitisha kwamba ulichoeleza wewe kuhusu gene mutation ni uongo,na wewe lete scientific paper kupinga ile ninayoleta mimi.

Unatumia nguvu nyingi kwenye Maconspiracy theories wakati hujui chochote. Lete ushahidi na scientific evidence wa hoja zako muflisi
 
Kuna MTU alimtafutia jamaa mwenzie demu mwenye ukimwi makusudi jamaa alipogundua kaletewa demi wa ukimwi yule aliemletea akafariki ktk mazingira ya kutatanisha cjui ilikuwaje
 
Duuh...mkuu hoja zako kama zina ukweli ndan yake...sasa kwann miaka ya nyuma kabla ya ARVs wagonjwa wa ukimwi walikuwa wakiumwa sana na kukonda au ule nao haukuwa ukimwi?

Ukisoma post zangu zote utaelewa,cha msingi kuwa na free mind.Kuwa na moyo wa kudadisi zaidi na si kupinga.Uongo uliorudiwa mara nyingi kuhusu neno ukimwi(yaani ukimwi ukimwi ukimwi ukimwi ukimwi ukimwi...) umefanya akili zetu usahau magonjwa mengine ambayo yana dalili zinazofanana na huo ugonjwa feki wa VVU/Ukimwi.Chukulia kwa mfano TB.TB ilikuwapo hata kabla ya huu ugonjwa feki wa VVU/Ukimwi.Baadhi ya dalili za TB ni;
1.Kukohoa sana
2.Kukonda sana
3.Kupungua uzito
4.Kukosa hamu ya kula
5.Kuishiwa nguvu
6.Homa za mara kwa mara
7.Kuharisha au kutapika kama ni GI TB nk.

Hizi dalili zinafanana kabisa na zile za ukimwi feki.Watu wanajifanya wamezifumbia macho dalili hizi za TB ili kuhalalisha uongo wao,ina maana hata wewe huzijui hizi?Kama hizi ni kweli dalili za TB,Je,ukimwi ni nini hasa?
Lakini leo akija Obama akisema mtu akiwa na dalili hizi lazima utakuwa ukimwi,watu watakubali kama mazuzu huku wakisahau kwamba hata TB ina dalili hizo.
 
Daaah halafu ukiangalia huu ugonjwa waweza sema unapendelea asee. Kuna ndugu yangu yeye ni mlevi sana na anahakikisha kila akilewa anaondoka na barmaid. yaani kwa siku hata wadada watatu anaondoka nao tena wale hatarishi kabisa na hana rekodi ya kutumia kondom kabisaa. Tangu ujana wake ndio yuko hivohivo na mpaka sasa umri unamtupa mkono lakini bado na wadada kama damu.
Lakini mpaka leo hana vvu wala ukimwi asee na anadunda kama kawa mipombe kama kawa mademu mwendo uleule. Sasa katembee wewe na barmaid mmoja tu uone kama hujafa kwa presha kabla tarehe yako ya kurudia kupima.

HIV/AIDS au VVU/UKIMWI hauambukizwi kwa njia ya ngono/sex na HIV hasababishi ukimwi.Jitahidini kidogo ku stretch uwezo wenu,elimu ipo lakini mnairuka kwa makusudi.

HIV/AIDS is a mindset disease.Sijui kama nitaeleweka kwa kusema hivi.Yaani ugonjwa huu haupo kiuhalisia,kinachoua si HIV bali kinachoua ni ARVs kwa wale wanaozitumia.Hata kama mtu hatumii ARVs na amedhoofika wewe mpime tu utagundua kwamba lazima awe na ugonjwa fulani unaofahamika,aidha TB,Pneumonia,Cancer nk.

Watu wanadhani mimi nimekurupuka kwa siku moja tu na kuja kuandika yote haya,la hasha nimefuatilia na kufanya tafiti ya mambo haya kwa zaidi ya miaka 5.Watu wanachukulia kirahisi sana,hawagundui hata kwa nini mimi ninawaeleza haya,hawagundui hata kidogo upendo huu ninaouonesha kwao.
 
Hauko serious wewe....

Unaweza kuthibitisha kwamba siko serious?

..... watu wanakufa tunaona kwa macho yetu ati unasema ni uzushi ....

Unaweza kuthibitisha pia kwamba uliowaona wewe walikufa kwa HIV/AIDS?

.... ukapimwe akili, ....

Nilijua kwamba mwishowe ungenitukana.Usihofu,hayo ni madhaifu tu kila mtu anayo ya kwake.Nipo kwa ajili ya kukuelewesha kama utakuwa na utayari huo wa kusikiliza kwa kuwa najua itakuwaje kama wewe au ndugu yako mtakutwa na janga hili endapo mtapimwa HIV+.Niko tayari kukuokoa kama una nia hiyo.

.... kwa maana hii hata mchawi au jini ni imani tu

Hii sio imani ndugu yangu,hii ni sayansi.Mimi si kwamba siami kwamba HIV hasababishi ukimwi,bali najua kwamba HIV hasababishi ukimwi.
Labda wewe unayepinga,Je, unaweza kuthibitisha kwamba HIV anasababisha ukimwi?Na wale wanaokufa wanakufa kwa ukimwi uliosababishwa na HIV?

Karibu.
 
Unatumia nguvu nyingi kwenye Maconspiracy theories wakati hujui chochote. Lete ushahidi na scientific evidence wa hoja zako muflisi

Unazidi kunisikitisha ndugu yangu.Unachoniomba hapo kwenye nyekundu hukukiona sehemu ya chini kabisa ya maelezo niliyotoa?Au unafanya makusudi?Chini niliweka scientific paper/proof,Je,hukuiona?
Ndio maana nikakushauri kwanza ujiweke tayari kiakili kusikiliza ndio utapata elimu.Wewe hauko tayari bado kusikiliza na ndio maana ume bypass na hukuiona kabisa hiyo scientific paper.Unaendelea kunizidishia majonzi kwa kung'ang'ania kupinga pasipo kuhoji.

Swali langu hukunijibu bado,ok,si tatizo.Nimeleta scientific paper hutaki kuisoma halafu unakuja tena unaniomba scientific evidence.Jitahidi kubadilika ndugu yangu,najua ni ngumu kukubali,lakini jitahidi kidogo.
 
HIV/AIDS au VVU/UKIMWI hauambukizwi kwa njia ya ngono/sex na HIV hasababishi ukimwi.Jitahidini kidogo ku stretch uwezo wenu,elimu ipo lakini mnairuka kwa makusudi.

HIV/AIDS is a mindset disease.Sijui kama nitaeleweka kwa kusema hivi.Yaani ugonjwa huu haupo kiuhalisia,kinachoua si HIV bali kinachoua ni ARVs kwa wale wanaozitumia.Hata kama mtu hatumii ARVs na amedhoofika wewe mpime tu utagundua kwamba lazima awe na ugonjwa fulani unaofahamika,aidha TB,Pneumonia,Cancer nk.

Watu wanadhani mimi nimekurupuka kwa siku moja tu na kuja kuandika yote haya,la hasha nimefuatilia na kufanya tafiti ya mambo haya kwa zaidi ya miaka 5.Watu wanachukulia kirahisi sana,hawagundui hata kwa nini mimi ninawaeleza haya,hawagundui hata kidogo upendo huu ninaouonesha kwao.

Ndugu. unachojaribu kusema ni kwamba ARVs badala ya kuongeza maisha bali ndio inasababisha vifo. Sijakuelewa vizuri labda.
 
Ndugu. unachojaribu kusema ni kwamba ARVs badala ya kuongeza maisha bali ndio inasababisha vifo. Sijakuelewa vizuri labda.

Ukisoma post zangu vizuri utanielewa tu.Nina maana hiyohiyo kwamba ARVs ndio husababisha vifo kwa wale wanaozitumia.Nifuatilie kwenye post zangu utanielewa tu mkuu.Watu husema,"mbona mtu anaumwa kabisa lakini akianza kutumia ARVs anakuwa safi".Wanaosema hivi bado hawajui ukweli,ngoja nikupe mfano;

Mara nyingi mtu aliyedhoofika halafu akakutwa na huyu HIV feki lazima atakuwa na ugonjwa maalum unaofahamika mfano TB.Mgonjwa huyu watampa ARVs pamoja na dawa za TB.Bila shaka atapona TB ataanza kunenepa huku watu wakijua kwamba ARVs ndizo zimemponya.Baada ya muda mrefu sana mtu huyu ataanza kuonesha dalili nyingine hata kama hana TB,kama vile nywele kuwa dhaifu,kupungua kilo/uzito,ngozi kuwa dhaifu au kutoka vipele,cancer,upungufu wa damu,ugonjwa wa ini,figo kushindwa kufanya kazi vizuri na hatimaye miguu kuvimba sehemu ya chini,tumbo kujaa,matatizo ya moyo nk.
Je,ushawahi kujiuliza kama mtu hana TB,hana malaria,hana typhoid nk,Je,magonjwa niliyotaja hapo juu yanasababishwa na nini?Kama yanasababishwa na HIV,Je,anasababishaje magonjwa haya?

1.HIV anasababishaje ugonjwa wa moyo?
2.HIV anasababishaje nywele kuwa dhaifu?
3.HIV anasababishaje kupungua kwa uzito?
4.HIV anasababishaje udhaifu wa ngozi na vipele/vidonda?
5.HIV anasababishaje cancer?
6.HIV anasababishaje upungufu wa damu?
7.HIV anasababishaje ini kushindwa kufanya kazi?
8.HIV anasababishaje figo kushindwa kufanya kazi?

Waliotudanganya hawawezi kuelezea ni kwa vipi HIV anaweza kusababisha matatizo ya hapo juu.Mimi nitakuelezea;

ARVs zinasababisha lactic acidosis kwenye damu hivyo damu inakuwa na tindikali/acid nyingi.Daktari yeyote yule hawezi kupinga maelezo haya,kama yupo aje hapa kupinga.

Sasa basi,damu inapokuwa na acid mwili unakumbwa na kila aina ya tatizo kwa kuwa damu haikuumbwa iwe na acid bali imeumbwa iwe na alkali/nyongo na kiwango thabiti cha nyongo kwenye damu kinatakiwa kiwe ni pH=7.365,kikiwa chini ya 7.3 tu matatizo yanaanza.

Nakupa faida hapa;Fuatilia wagonjwa wote wa cancer iwe ocean road au kokote kule,lazima pH ya damu zao iwe chini ya 7.365,lazima.Fahamu pia sumu yoyote ni acid by nature,hivyo acid kwenye damu maana yake ni sumu kwenye damu.Seli zote za damu zinazungukwa na acid,seli zikizungukwa na acid haziwezi kupumua kwa kuwa kwenye acid hamna oxygen ya kutosha,Je,unafahamu kitu kinachoitwa oxygen debt kwenye biology kinatokeaje?

Rahisi sana,ni muscles zinajaa lactic acid baada ya kufanya mazoezi kwa muda na hizo mtu hujisikia maumivu kesho yake anapoamka.Hii inatokea kwa kuwa seli zinakosa oxygen ya kutosha,baada ya muda damu inajibalance yenyewe na maumivu huondoka yenyewe.

Kama damu ina pH chini ya 7.365,ini,figo,moyo vyote haviwezi kufanya kazi vizuri.Mwili unapoteza madini kama vile calcium na magnesium ambayo ndio muhimu kwa contraction na relaxation ya heart muscles.Pia kupotea kwa calcium kunafanya mifupa iwe dhaifu na kuvunjika kwa urahisi.

Seli ni rahisi kuwa mutated au kufa na hii husababisha cancer na matatizo kama vile vipele kwenye ngozi au ngozi kuwa dhaifu.Kisukari pia hapa ni mahali pake.Bone marrow pia huathirika sana na acid hii hivyo hushindwa kuzalisha damu vizuri,na ndio maana huwa unasikia wagonjwa waliobobea kwenye matumizi ya ARVs huwa wanabadilisha damu mara kwa mara.

Ndugu yangu sayansi hii ni pana naweza kuandika kitabu,niishie hapa.Ili kuthibitisha kwamba ARVs zinasababisha lactic acidosis hebu ingia kwenye website hii ya wamarekani wenyewe ujisomee,sio mimi,hii ni ya wamarekani wenyewe,unaweza kujionea picha ya mwewe chini ya hiyo web ni ishara kwamba hiyo ni ya wamarekani.

Ingia kwenye web,soma sehemu ya WARNING;Wenyewe wanakwambia husababisha serious LIFE THREATENING side effects.

Tenofovir Disoproxil Fumarate (Viread) | Patient Version | AIDSinfo
 
Unazidi kunisikitisha ndugu yangu.Unachoniomba hapo kwenye nyekundu hukukiona sehemu ya chini kabisa ya maelezo niliyotoa?Au unafanya makusudi?Chini niliweka scientific paper/proof,Je,hukuiona?
Ndio maana nikakushauri kwanza ujiweke tayari kiakili kusikiliza ndio utapata elimu.Wewe hauko tayari bado kusikiliza na ndio maana ume bypass na hukuiona kabisa hiyo scientific paper.Unaendelea kunizidishia majonzi kwa kung'ang'ania kupinga pasipo kuhoji.

Swali langu hukunijibu bado,ok,si tatizo.Nimeleta scientific paper hutaki kuisoma halafu unakuja tena unaniomba scientific evidence.Jitahidi kubadilika ndugu yangu,najua ni ngumu kukubali,lakini jitahidi kidogo.


*unataka tuamini linki zako ila wengine wakikuwekea unazikataa.... kwanini tuanini link zako na kuacha zingine!??

*Unaulizwa maswali mengi na mengi unajibu kwa kuuliza maswali na wewe, hapo unazidi kujichanganya


.......... nijibu haya tu na kazi imeisha......

*ukimwi ulianza kugundulika kwa mtu wa kwanza kabla ua arv kuwepo.... aliupata kwa njia gani bila ya kuambukizwa kupitia arv!??

*arv ya kwanza kugundulika ilikua 1988 lakini kwa tabzania zilichelewa kufika mpaka miaka ya mwanzo ya 90, je kwa kipindi chote hicho maambukizi yalikua kwa njia gani!??

*TB unayoisema imeanza zamani sana na wagonjwa walikua wanapata dawa mbalimbali, inakuaje kwa tb hii kuuwa watu wengi namna hiyo na kukondesha kiasi hicho.

*kama ni TB mbona ukimwi unasemekana ulianzia Bukoba miaka hiyo, watu wa mikoa mingine walikua hawaugui TB!?? kwanini na wenyewe wasiishe kama watu wa BK walivyokua wanadhoofika



naomba majibu kwanza na usinijubu kwa maswali tafadhari
 
HIV/AIDS au VVU/UKIMWI hauambukizwi kwa njia ya ngono/sex na HIV hasababishi ukimwi.Jitahidini kidogo ku stretch uwezo wenu,elimu ipo lakini mnairuka kwa makusudi.

HIV/AIDS is a mindset disease.Sijui kama nitaeleweka kwa kusema hivi.Yaani ugonjwa huu haupo kiuhalisia,kinachoua si HIV bali kinachoua ni ARVs kwa wale wanaozitumia.Hata kama mtu hatumii ARVs na amedhoofika wewe mpime tu utagundua kwamba lazima awe na ugonjwa fulani unaofahamika,aidha TB,Pneumonia,Cancer nk.

Watu wanadhani mimi nimekurupuka kwa siku moja tu na kuja kuandika yote haya,la hasha nimefuatilia na kufanya tafiti ya mambo haya kwa zaidi ya miaka 5.Watu wanachukulia kirahisi sana,hawagundui hata kwa nini mimi ninawaeleza haya,hawagundui hata kidogo upendo huu ninaouonesha kwao.

Mkuu vp kuhusu watu waliokua wanakufa miaka ya tisini wakiwa wamedhohofu sans kabla ya kugundulika kwa ARVs?
 
So unataka kutuambia tusiangaike na kondom wala nini tuamini tu hakuna kitu kinaitwa ngoma ni uzushi tu afu kesho uanze kunyauka kama jani la kondeni kama ni swala la wengine kutopata ni kadiri ya majaliwa ya Mungu maana neema sio ya wote ila mmoja mmoja kozi hata ebira kuna waliopona bila hata kutumia dawa, malaria yenyewe kuna wale inawaendesha hatua tu za mwanzo, wakati mwingine mpaka dalili zitokee yuko highest stage ya makaria
 
*unataka tuamini linki zako ila wengine wakikuwekea unazikataa.... kwanini tuanini link zako na kuacha zingine!??

*Unaulizwa maswali mengi na mengi unajibu kwa kuuliza maswali na wewe, hapo unazidi kujichanganya


.......... nijibu haya tu na kazi imeisha......

*ukimwi ulianza kugundulika kwa mtu wa kwanza kabla ua arv kuwepo.... aliupata kwa njia gani bila ya kuambukizwa kupitia arv!??

*arv ya kwanza kugundulika ilikua 1988 lakini kwa tabzania zilichelewa kufika mpaka miaka ya mwanzo ya 90, je kwa kipindi chote hicho maambukizi yalikua kwa njia gani!??

*TB unayoisema imeanza zamani sana na wagonjwa walikua wanapata dawa mbalimbali, inakuaje kwa tb hii kuuwa watu wengi namna hiyo na kukondesha kiasi hicho.

*kama ni TB mbona ukimwi unasemekana ulianzia Bukoba miaka hiyo, watu wa mikoa mingine walikua hawaugui TB!?? kwanini na wenyewe wasiishe kama watu wa BK walivyokua wanadhoofika



naomba majibu kwanza na usinijubu kwa maswali tafadhari

The so called HIV was laboratorily engineered. The whole concept was relating to cancer cells at initial stage. So all the research were targeting how to evade the new type of cancer.

Jina la HIV/AIDS lilianza tumika after sometimes (sikumbuki mwaka) ila in 1980's hivi. Na first drug to be used was the AZT ambazo baadae zikaja kuzuiwa. Kama ulifuatilia documentary ya madaktari wanao mponda huyo alianzisha jina la HIV/AIDS utaona jinsi hali ilivyokuwa.

Wametuaminisha how the virus inafanya kazi na kuangamiza... lakini in most cases watu wanaenda fasta sana kwa kuanza kutumia ARV kwani zinakuwa na magonjwa sababishi yanayotokana na matumizi ya hizo dawa. Kama ilivyo kwa AZT . Itafika kipindi watu watajua shida zake na wataachana nazo wataamia kwenye dawa zingine.

At the end hii imekaa ki conspiracy sana
 
Uko sahihi mkuu,watu wengi walishaniambia hivyo.Tatizo mada hii ina mambo mengi sana na watu ni lazima wayasome yote ili wakubaliane na ukweli,haitakiwi kusoma kwa kurukaruka.Kwa navyowajua wana JF wengi hawana tabia hiyo.Nina mifano hai,mimi sio wa kwanza kuanzisha mada kama hii,kuna mwana JF mmoja alishawahi kuanzisha lakini watu waliishia kupinga tu,lakini ukiisoma ile mada jinsi ilivyoandaliwa,utagundua kwamba jamaa alitumia muda wake mwingi sana kuonesha upendo kwa wengine,lakini aliishia kupingwa tu na sijamwona tena akizungumzia au kuchangia kwenye mada kama hizi tena hadi leo,labda pengine hakuwa na hoja na uzoefu wa kutosha kujibu hoja za watu.Hii inakatisha sana tamaa,na ndio maana mimi ninatumia utaratibu huu.Natoa dokezo,watu wanauliza maswali,mimi ninajibu kwa kutoa evidence pale zinapohitajika.
Nashukuru kwa maoni yako.Sasa hivi niko mbioni kuanda kajarida/kakitabu kinachoeleza ukweli kuhusu;
1.HIV/AIDS
2.CANCER
3.MARIJUANA(BANGI)
4.GMO(Genetic Modified Foods)

na mambo mengine kama hayo.Napanga kuweka maandishi na video kwa kiswahili.Watu wengi wanachukulia mambo kirahisi sana,hawajui kwamba karibu mambo yote tunayoyaona na kuyajua sasa ni feki,yapo kwa ajili ya manufaa ya wengine.Na ndio maana ID yangu ni Deception,niko humu kuwajuza watu mambo tuliyodanganywa.

Itakuwa vyema mkuu Deception ukifanya hivyo ,pia katika pitapita zangu kwenye harakati za kuutafuta ukweli nilikutana na issue fulan ambayo ilinistua kidogo kwamba hiki tunachoambiwa kuwa GLOBAL WARMING ndani yake kuna uongo mwingi sana. Sijalifuatilia sana lakini kuna dalili ambazo naanza kuona kwamba kuna mambo mengi sana ambayo ni uongo ila tunakaririshwa tu kwa manufaa ya kikundi Fulani cha watu
 
Mkuu vp kuhusu watu waliokua wanakufa miaka ya tisini wakiwa wamedhohofu sans kabla ya kugundulika kwa ARVs?

Ngoja nikwambie kitu hapa mkuu;Kuna vitu vya kusikia na vya kuona mwenyewe.Halafu vile vya kuona mwenyewe pia unaweza kuvielewa au usivielewe kulingana na upeo au elimu aliyonayo mtu.Watu wengi wanazungumza vitu vya kusikia zaidi,na wale walioona hawakuwa na uelewa au elimu ya kutosha kipindi ambacho wanaona hivyo vitu.

Mimi ninayezungumza hapa nimefanya tafiti nyingi za kisayansi.Siko hapa JF kuleta porojo kama wengine wanavyodhani,watu wamejikita zaidi kwenye upingaji lakini hawakujiandaa kuelewa.Kama mtu hakujiandaa kuelewa utamjua tu,na kamwe hawezi kuelewa hata ukimpatia evidence ya aina gani,mtu huyu atalazimisha umpe evidence si kwamba anataka kuelewa la hasha bali anataka ukwame,ukimpa evidence haisomi/haifuatilii na badala yake anatafuta mtego mwingine ili ukwame.Hii ndio tabia ya watu wengi humu JF,wamejiandaa kupinga na kuleta porojo zaidi badala ya kutoa hoja za kisayansi ili kupinga zile ninazotoa mimi.

Jibu lako hili hapa chini;
Miaka ya 1990 ARVs zilikuwa zimeshagundulika ila zilikuwa bado hazijafika kwa wingi Tanzania.ARVs(AZT) zilianza kutumika kwa mara ya kwanza Marekani mwaka 1987,hivyo nakubaliana na wewe kwamba wengi walikuwa hawatumii ARVs Tanzania lakini walikuwa wanakufa kwa magonjwa.Swali linakuja,Je,walikuwa wanakufa kwa magonjwa gani?

Kumbuka kwamba(kama ulikuwa na akili timamu miaka ya 1990) hali ya uchumi kwa upande wa huduma za kijamii ilikuwa mbaya sana kipindi kile hasa huduma za kiafya.

Magonjwa yaliyoongoza kwa kuuwa watu yalikuwa ni malaria na TB,malaria ikishika namba moja.Vipimo vilikuwa duni na madawa pia yalikuwa adimu.Na ndio maana hata ukiangalia takwimu za wagonjwa wa TB zilikuwa zinashuka kuanzia mwaka 1990 kuja juu kwa kadri huduma za kiafya zilivyoboreshwa.Watu walikufa kwa TB na malaria na si HIV.Kama mtu ana uthibitisho kuonesha kwamba HIV/AIDS ndio iliua watu wengi kipindi kile basi alete hapa jukwaani.Maana kuna mambo ya kusikia bila kuona na ukweli.

Kuhusu malaria,unaweza usiamini kwa kuwa haikudhoofisha watu.Lakini TB ilikuwa inatisha ndugu yangu.Si unajua TB iliyokomaa ikoje?Sasa changanya na tatizo la upatikanaji wa huduma za kiafya kipindi kile yaani madawa na vipimo.Hivyo wagonjwa wengi wa TB walishindwa kupata huduma za vipimo na dawa kwa sababu mbalimbali zikiwemo uelewa,umbali wa kufika vituo vya afya vipimo duni na madawa.

Mgonjwa wa TB aliyekosa kabisa huduma huwezi kumuangalia mara mbili.Sasa ukichanganya na kasumba tuliyomezeshwa ya HIV/AIDS jinsi tulivyotangaziwa na vyombo vya habari kipindi hicho redio ni moja,basi kila kitu kinachotangazwa tunakiamini,hivyo tukasahau kabisa kama dalili za TB ndio zilezile dalili za HIV/AIDS tulizoambiwa;
-Kukonda sana
-kupungua uzito
-kuishiwa nguvu
-homa za mara kwa mara
-Kutapika au kuharisha kutegemeana na aina ya TB(GI TB)
-Kukohoa mara kwa mara nk.

Lakini watu bado wanafunga milango yao ya fahamu kujifanya hawajui kama hizi dalili mtu mwenye TB pia anakuwa nazo eti kwa sababu redio imetangaza kwamba hizi ni dalili za VVU/Ukimwi.Silaumu sana kwa maana elimu na uelewa pia kipindi kile vilikuwa chini sana.

Hakuna mgonjwa yeyote wa TB ambaye nywele zake zilinyonyoka kipindi kile kabla ya ARVs hazijaanza kutumika.Kama mtu ana evidence alete hapa.Baada ya ARVs kuanza kutumika ndio ikaongezeka dalili nyingine ya kunyonyoka nywele au nywele kuwa dhaifu.Pia baada ya ARVs kuanza kutumika,zikaongezeka dalili nyingine kama vile;
-Ugonjwa wa moyo
-Matatizo ya figo
-matatizo ya ini
-tumbo kujaa
-miguu kuvimba
-Upungufu wa damu
-Cancer/saratani

Hayo matatizo niliyotaja hapo juu,hamna hata tatizo moja linalosababishwa na HIV.Kama mtu anapinga alete ushahidi.

Nywele kunyonyoka ni dalili mojawapo ya mtu anayetumia ARVs.ARVs na dawa za chemotherapy zinafanana kwa kuwa na common component.Mgonjwa wa cancer pia akitumia chemotherapy hunyonyoka nywele.Kama mtu anapinga hili pia,aje na evidence.

Watu walikuwa wanadhoofika kabla hata kutangazwa kwa HIV mwaka 1984,yaani miaka ya 1970 na kabla ya hapo,walikuwa wana dalili zote za TB nilizozitaja na watu wa kipindi hicho walikuwa wanaona kwa macho yao.Lakini baada ya kutangazwa kwa HIV,watu wamesahau kabisa kama kuna ugonjwa unaitwa TB na una dalili kama za HIV/AIDS tulizoambiwa/kudanganywa,ama kweli ujinga ni mbaya sana.

Angalizo;
Watu wanaangalia tu upande mmoja,lakini hawajui pia kwamba asilimia ya 97%(WHO data) ya watu waliopimwa wakakutwa na huyu HIV feki katika bara la Afrika hawana AIDS.Asilimia 3% ya walio na huyu HIV feki ndio wana AIDS.Na AIDS waliyonayo inalezeka kisayansi wameipataje,lakini haikusababishwa na huyu HIV feki.

Nikianza kutoa list ya maswali ya kutatanisha kuhusu HIV/AIDS sitamaliza,lakini siko hapa kwa ajili hiyo bali nipo hapa ili kuwaelewesha watu.Lakini kuna watu wamejikita kupinga tu na kuuliza maswali ya mitego ambayo wao wanadhani hayajibiki,kumbe yana majibu rahisi sana.Wanataka wajibiwe,lakini wakijibiwa hawasomi,na wakisoma wanasoma kwa bias,yaani wanasoma huku wakiwa na mlengo wa kupinga.Siwezi kupoteza muda wangu kujadiliana na watu kama hao.

Fahamu pia sasa hivi katika NGO zinazoshughulikia masuala ya HIV/AIDS kuna kitengo kinachohusiana na cervical cancer kwa wanawake.Sasa umeshawahi kujiuliza kwa nini wameweka kitengo hicho ndani ya NGO hizo?

Jibu ni rahisi sana;Ni kwa sababu wanawake wengi wanaotumia ARVs kwa muda mrefu mwishowe hupata cervical cancer,cancer hii haisababishwi na HIV la hasha,husababishwa na matumizi ya ARVs.Dawa za uzazi wa mpango pia husababisha cancer,lakini hapa nazungumzia specifically ARVs.
Je,unajua pia kwa nini mama wajawazito sasa hivi kuna sheria lazima wapimwe HIV?Jibu ni rahisi sana;Hawa jamaa si kwamba wanatupenda saaaana la hasha,bali wanatafuta wateja kinguvu,wanajua kwamba mama wajawazito ni rahisi sana kukutwa HIV+ kutokana na trick waliyoiweka kwenye vipimo vya HIV.Mama wajawazito wana uwezekano mkubwa wa kutoa protein ambazo zinafanana kabisa na zile zinazokuwa targeted na vipimo vyao ambazo hufanya mwili wa mama mjamzito ku generate antibodies dhidi ya hizo protein.Antibodies hizi zikionekana ndizo zinazofanya vipimo vioneshe kwamba mtu ni HIV+.Lakini kuna muda protein hizi zinatoweka kama hali iliyosababisha zitokee ikitoweka.Na ndio maana mtu anaweza kuwa HIV+ leo halafu siku nyingine akapima akawa HIV-.

Hivyo basi,mtu kuwa HIV+ is not a big deal,ni usanii tu wa vipimo.Ila mtu anayetumia ARVs kwa muda mrefu huwa mara nyingi anaonekana HIV+ kutokana na sayansi ya dawa zilivyo.Yaani ndugu yangu haya mambo ni mengi sana na ni mazito,inahitaji utulie sana,huwezi kutulia kama una attitude ya kupinga.

Mtu mwenye attitude ya kupinga hawezi kupata kitu hapa,atarukaruka tu huku na kule.Na ndio maana hawa jamaa pamoja na kwamba nawachukia,lakini hapa wametumia sayansi kubwa sana kudanganya watu.Na kwa jamii hii ya watu ninayoiona humu JF,wataishia kuongozwa kama ng'ombe malishoni,waombe tu wasipimwe HIV+,watajuta,kwa kuwa hawatajua la kufanya ili kujitetea.Na lazima ARVs ziwaue watu kama hawa.
 
Back
Top Bottom