Je, Israel ya sasa ni Taifa teule la Mungu au ni propaganda tu za kanisa?

Hahaa...Taifa Teule, sasa iweje Mungu ambaye hana upendeleo awe na taifa teule tena? Ina maana kuna watu wengine wanakuwa na maana zaidi kwake kisa wamezaliwa sehemu fulani ya Dunia tu na sio matendo yao?
Hapana hakuchagua kwa sababu wao ni bora zaidi au walizaliwa sehemu fulani tu ya dunia soma hapa

Kumb. Torati 7:7-8
7 BWANA hakuwapenda ninyi, wala hakuwachagua ninyi, kwa sababu mlikuwa wengi kuliko mataifa yote, maana mlikuwa wachache kuliko watu wote;
8 bali kwa sababu BWANA anawapenda, na kwa sababu alitaka kuutimiza uapo wake aliowaapia baba zenu.

Ukisoma hapa utaona Mungu hakuona wana maana yeyote bali aliwachagua sababu ya agano lake na Abraham maana kipindi cha Abraham dunia ilikuwa imegeukia upagani na miungu ya babeli chini ya Nimrod ila Abraham pekee ndio alikuwa ameshikilia imani ya huyo MUNGU.

Ni sawa na wewe ukiwa bado hujachagua chama cha siasa lakini ukaona CCM inakuletea maendeleo,inakujali shida zako,inasikiliza maoni yako je ukifika wakati wa uchaguzi 2020 utachagua chama gani?? Si utaenda CCM?? same to God naye aliwachagua sababu walikuwa waaminifu kwake.

Tena ukitaka kujua Mungu hachagui watu sababu ni wa maana kuliko wengine pitia hapa

1 wakorintho 1:27
27 bali Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu;
28 tena Mungu alivichagua vitu vinyonge vya dunia na vilivyodharauliwa, naam, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko
 
mkuu leo umenibariki sana.
 
Hakuna taifa TEULE LA WAYAHUDI KWA SASA HIZO NI NDOTO ZA JIONI KAMA WALIKUWA KWELI NDIO WATEULE WASINGE COMWA MOTO MILIONI 6 MUNGU ANAWATAZAMA WATEULE WAKE.... kwanza wakristo wanasema AGANO LA KALE HALIFAI NA LIMEPITWA NA WAKATI KWA HIO WAYAHUDI WALIPITWA NA WAKATI UTUKUFU WAO ILIISHIA HAPO sasa hoja inakuja jee WAYAHUDI HAWA NI KWELI UZAO WA ABRAHAM KWA ISAAC ? historia inatumbia siyo hawa hao wanaojiita sasa wayahudi ni WASHKANAZI KABILA LA KHAZARIAN. UZAO WA JAPHET MTOTO WA NUHU SIO ULE WA ASILI UZAO WA SHEM AU SEM walijipachika uyahudi kukimbia vita kwao walikuwa wapagani kwa hio wakakimbilia mataifa ya ULAYA KUELEKEA UYUNANI NA MACEDONIA NDIO WAKAJIPACHIKA UYAHUDI KWA KUJILAZIMISHA BUT DNA PIA IMEONESHA SIO WAYAHUDI WA UKOO WA ABRAHAM .. pia kumbukeni WAYAHUDI BADO WANAMSUBIRI MASIHA YESU KWAO SIO MASIHA NA HAWAMKUBALI MPKA LEO HII
 
Israel aliyo iacha yesu sio hi ambayo ipo sasa na pia sio ile ambayo mungu alileta ufunuo aliposema
Ewe bethrehemu katika nchi ya Yuda hu mdogo kamwe kitika majumbe wa Yuda kwa kuwa kwako atatoka mtawala atakae wachunga watu wangu Israel
Pia yesu akathibitisha ufunuo huu alipo
Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea kwa wana wa Israel
Hi Israel ya sasa ni Israel iliyotengenezwa na Marekani
Israel aliyo iacha Yesu ndani yake mlikuwa mna mji wa Jerusalem
Kwa hiyo iliuipate Israel ile inabidi ukusanye pamoja yani hiyo inayojiita Israel pamoja na Palestrina
Ila haziwezi kuchanganyika kwa sababu tayari kuna mgawanyiko wa kiimani
Na huu ugomvi upo kwa sababu walitaka kuifanya Israel kuwa ionekane kuwa ndio chimbuko la ukristo ila ikashindikana wakaona wazitenganishe iwepo Israel na Palestine
Wakaja kustuka kuwa Palestine ambako hakuna kabisa ukiristo wakati Palestine ndiko inapatikana Jerusalem ambapo ndio mji aliozaliwa Yesu
Na ndio maana sasa wazungu wenye dini yao wanataka kuirudisha tena Palestine ndani ya Israel ya sasa walioitengeneza wazungu na dini yao
Laki mwisho wa siku ile nchi haitakuwa Salama hadi dunia inaisha kwa sababu Yesu aliwani na Mungu pia aliwani kwa sababu ya jeuli yao kama mungu anavyosema katika Qurani kuwa

Kwa sababu ya jeuri yao wana wa Israel nimetia chuki na uadui ndani yao mpaka siku ya kiama
 
Maana ya Paulo ni ktk kifungu hiki cha kuhitimisha Roman 11:28~32

""Basi kwa Habari ya injili wamekuwa adui kwa ajili yenu; bali kwa Habari ya kule kuchaguliwa wamekuwa wapenzi kwa ajili ya baba zetu 29.Kwa sababu karama za Mungu hazina majuto,wala mwito wake.30 Kwa maana ninyi zamani mlimwasi Mungu, lakini sasa mmepata rehema kwa kuasi kwao;31.Kadhalilika na hao wameasi sasa,ili kwa kupata rehema kwenu wao nao wapate rehema 32 Maana Mungu amewafunga wote pamoja katika KUASI ili awarehemu wote.
 
Isaya 1:9 ""Kama Bwana wa majeshi asingalituachia mabaki machache sana,tungalikuwa kama sodoma, tungalifanana na Gomora.

Maswali yangu
#Haya mabaki huoni ndio hao wayahudi waliobakia?
#Je! Unadhani walibaki kwa bahati mbaya?Maana wanazidi kuongezeka tu na kuujenga Yerusalem.
#Haudhani kwamba lipo kusudio wameachwa walitekeleze.?
 
Mkuu bado hujathibitisha kwamba Israel ya mashariki ya kati ndio taifa teule kwa mujibu wa agano jipya..... Kma unao uthibitisho leta hapa tuujadili

Pia nlikuomba unipe tafsiri ya hivo vifungu vya wagalatia ili twende pamoja kwamba paulo aliposema warithi wa ahadi za Abraham ni wakristo (wayahudi wa kiroho) je alimaanisha nini??
 
Kwanni uwaze kuwa hayo mabaki ni Israel ilihali hawamfuati Yesu je watasaidia vp dunia isiwe Sodoma???

2. Nani alibaki?? Wameongezekaje?? Unaweza leta takwimu?? Hivi unafahamu wayahudi zaidi ya makabila 8 hayajulikani yalipo ila 90% ya Israel ya sasa ni Ashkenazi jews?? Je hayo makabila yaliyosalia yakwapi?? Unaweza leta ushahidi kuwa bado yapo??

3. Kusudi lazima liwepo kma ambavyo hta waafrika tumesalia hadi leo na kusudi ni wote tumuamini Yesu.... Hilo ndio kusudi kibiblia.... Sasa unaweza nipa kusudi la Israel ya kina Netanyahu ambalo ni tofauti na hili?? Na kama kusudi ni moja kwa dunia nzima je nini special kuhusu Israel??
 
Je Israel ya sasa ni Taifa teule la Mungu au ni propaganda tu za kanisa?
HAPANA KWA HERUFI KUBWA HAPANA WALA SIO
BE IN TOUCH KESHO NAWEKA HAPA FACT ZA BIBLIA KWANINI SIO TAIFA TEULE LA MUNGU
PIA HADI SASA ISRAELI WAPO UTUMWANI HAKUNA MWANA WA ISRAEL AMBAYE YUPO NCHINI KWAKE HADI SASA
 
HakunaTaifa teule fulani ...Isreal ilikuwa Pilot state tu kwa ajili ya wokovu..

Uteule gani angali jews hao ndio nambari moja kuharibu dunia,... Media zote kubwa marekani zinamilikiwa na wao...porn industry zote ni za Jews....Holy woody yote ni myahudi...maadili yote yanaharibiwa na Jews...

Kwakifupi ni baadhi ya makanisa hasa ya kipentekoste ndio yanadai kuwa israeli ni Taifa Teule
 
Essau alikuwa na hairy skin.. Jacob ili kumlaghai baba yao, akajivika ngozi ya mbuzi ili mzee Isaka akimwekea mikono asigundue tofauti. Inasemekana mchongo huu uliratibiwa vizuri na mama yao Rebeka ambaye alikuwa akimpenda zaidi Jacob..

Hii baraka inaonesha kama Mungu alichezwa shere coz inaonekana laiti Isaka angejua kilichofanyika asingeridhia.. Mzee wa watu katoa baraka kwa mtu pasiokujua sie mlengwa. Huu bado nauita ni utapeli.

Anyway, hii sio mada kuu. Acha nikaushe!
 
Nakubaliana na wewe kwa sehemu kwamba kanisa ndio warithi wa ahadi maana haki inahesabiwa kwa imani na sio tena kwa matendo ya sheria,,lakini pia kanisa sio exclusive kwa wayahudi maana wapo wayahudi pia walio wakristo.

Hawa wayahudi unaowaita Ashkenazi ni kabila moja la yuda ambalo toka awali sehemu yao ya urithi ilijumuisha pia Yerusalem.Kuna ramani uliiweka hapa jukwaani kuonyesha mipaka ya Israel.Utaona Israel ilikuwa na mpaka mto Euphrates ulioko iraq,,maana yake ilikuwa nchi pana sana wakati ikiwa na kabila 12.

Sasa Unakumbuka mgawanyiko ulitokea baada ya kifo cha Suleiman.Kukawa na Israel na yuda.Baadae makabila 11 yaliojiita Israel yakapotea likabaki kabila moja la yuda..Nchi Imekuwa ndogo kwa sababu sio ya makabila 12 tena.

Bado upo wokovu kwa Israel kwa sababu wapo pale kimkakati.kitabu cha Daniel kina majira yalioko hapa duniani na kama ukapata tafsiri yake utaona kwamba bado kuna wakati unasubiriwa kwa ajili ya makusudi muhimu pale mashariki ya kati na hasa Jerusalem.

Kuongezea kuhusu kanisa ni kwamba hili kanisa misingi yake ipo katika sheria,,taratibu na ibada ya wayahudi ndio maana kwenye hio mistari ya Roman 11: inasema kuasi kwa wayahudi kulitupa sisi mataifa nafasi ya kuwa na hio imani...na kuasi kwa wayahudi ni kule kutoona haja ya kuacha sheria ambao ulikuwa msingi wao tokea Musa,,na waifuate imani isiohitaji matendo ya sheria.Lakini kwenye ule mstari wa 32.unakuonyesha kwamba bado nao kwa kule kuwepo kwa kanisa kuna maana kwamba na wao wana time yao ya kufikia toba. Mwisho kabisa status ya Israel haijawahi kubadilika kutoka kuwa taifa teule.Na sio taifa teule kwa faida ya Israel ila kwa faida ya dunia.
Mambo mengi yenye kuiathiri dunia kwa njia hasi au chanya ili kufikia malengo ya Mungu hupitia pale.

Kumbuka bado hajaja ant christ,,bado dunia haijarudi tena kuwa nchi moja yenye sarafu moja na kiongozi mmoja. Haya yote yanatakiwa yaanzie kwenye hilo taifa teule. Uteule wake utaisha wakati utawala wa kristo utakapoanza ambao utakuwa hauna kikomo.
 
Mkuu hayo ulioyataja kwamba ni wayahudi wamayafanya kuharibu dunia kwani yako kikatiba kwamba ni lazima kuyafuata!! Mtu mzima akifanya jambo ni sahihi kwake maana anajua mema na mabaya,,na kwa akili yake amechagua lile alilolipenda.Hata wewe ukaenda hizo nchi zilizoendelea hukatazwi kuwa na studio ya kurekodi porn za aina zote,,au kasino au kiwanda cha mabomu,,au kiwanda cha sumu.
 
Watu walipojichanganya ni kwenye uelewa wa Agano la mungu(kama yupo),na abraham,

ukisoma neno kwa neno kama ni mzito,utakubaliana na hoja ya israel kama taifa teule,
lakini agano lilihusu UZAO WA ABRAHAM,

na akaambiwa watakuwa wengi kama mchanga,kuanzia mto frat huko iraq mpaka bonde la mto nile kule misri kama sikosei,
Keyword hapa ni UZAO WA ABRAHAM,

Agano halikuspesfy kwamba UZAO uliosemwa hapo ni waisrael,

then hii concept ya Taifa teule ni wazi kuwa ni ilikuja baadae mno,

ni kama ulifanyika usanii fulani ndo maana tunapata habari za yakobo mara kadhulumu haki ya Esau,mara kapigana mieleka na mungu etc,

lakini ukistick kwenye Agano la abraham na huyo mungu wake,maneno mbona yako wazi.

Pia concept ya uwepo wa kitu kinaitwa israel,bado ni ya kubuni,
ukichukulia mamake jacobo ni mtu mwenye asili ya syria,yakobo mwenyewe ni msyria,
watoto wa yakobo wote wanatokana na wamama wa syria,kwani yakobo alikwenda kwa mjomba wake Laban kule syria na ndiko akaoa mtu na dadake pamoja na mahousegal wa kisyria,
el alikuwa mungu wa kipagani kule caanan,sioni logic ya israel kutumia jina la miungu wa kale kama jina la taifa ama nchi,

jehova angevumilia vipi taifa lake teule liitwe kwa jina la mungu wa kicaanan,
so hivi vitu ni vya kubuni tu,tunapoteza mda mwingi sana kuvifikiria,

waisrael wao ni wajanja mno,wanajijua kuwa imani yao ni fake,hata ule ukuta pale jerusalem wanaendaga kugusa wanajua sio ukuta wa hekalu la solomoni LAKINI sasa wabafanya maigizo hayo kwa faida yao,
na hii ndo maana asilimia 70 ya waisrael,hawasali
 
Concept ya taifa teule,ilianza wakati wa moses(kama aliwahi kuishi),ni wakati wa moses ndipo jina la mungu jehova lilipojitokeza,
wakati huyu mungu akijitambulisha kwa moses,alisema kuwa kina Abraham,isaka na yakobo hawakumtambua huyo mungu kwa jina la jehova,

hapa unapata kujua wazi kuwa abraham,isaaka na yakobo waliabudu mungu yuleyule alieabudiwa na watu wa caanan,mungu huyo ni El,
na hata abraham kipindi akiwa mgeni pale kaanan,alimtambua Melkizedeki kama kuhani mkuu wa mungu El,

huyo el alikuwa mungu mkuu wa jamii zote za caanan,

sasa unajiuliza kwani jehova aendelea kukubali taifa lake teule litumie jina la mungu wa kipagani?

Jehova anajitetea kwa moses kuwa ,hapo mwanzo kina abraham,isaac na yakobo walinjua kwa jina jingine lakini jina lake halisi ni jehova,

lakini tena ukirudi kuchimba story ya jehova,inaonekana jehova alikuwa ni miongoni wa miungu iliyoabudiwa na kabila la wamedian,Yahwew ama jehova kwa kiswahili alikuwa ni mungu wa vita wa median,kwahiyo inshort alikuwa mungu wakipagani pia,

baada ya moses kumuua mtumishi wa farao alikimbilia nchi ya midian,akakaa kwa miaka mingi,na huko ndiko alipomuoa mkewe zilipa,
baba mkwe wa moses alikuwa ni kuhani wa mungu yahwew ama jehova kwa kiswahili,

so huko median ndiko hasa concept ya mungu jehova alipoitoa moses,


na ni hapo ndipo concept ya taifa la mungu ilipoanza
 
Nje ya kujadili na kukosoa imani za watu wengine huwa huna kazi ya kufanya?Au ndivyo mnafundishwa pale kwenye chuo cha Ahsante Nkapa pale Morogoro?Why don't you invest more of your time trying to solve the problems facing your religious community in which ignorance and poverty are persistent?Ukiyafanya hayo hakika utapata thawabu kwa Mnyazi Mungu na jamii yako itapunguza chuki kwa jamii zilizo busy kujishughulisha na maendeleo yao kiuchumi,kiroho na kijamii.
Ni ushauri tu ndugu yangu!
 
Povu la nini ndugu?
Umepewa mistari,jibu nawe kwa mistari.
After all katika siku ambayo mleta mada kawabariki wakristo wasioweza kujitetea kwa mistari ni leo.
sioni haja ya povu hata kama wewe ni mlokole uliyekaririshwa kuwa pale Tel Aviv ndio taifa teule.
mleta mada ameleta mada nzuri inayokutaka wewe umuonyeshe kweli eneo lile lilipo Israel kwa sasa ndipo taifa Taifa teule lilipo.
je utaifa teule ni ukiristo ama ni eneo?
 
Sijatoa povu ila nimemshauri.
Nguvu anayoitumia kwa chambuzi hizi za dini asiyoiamini akiitumia kama ninavyomshauri hakika hata MUM itastawi kuliko Jordan University katika mji huo huo.
Na akiwekeza angalau kuandika andiko lenye kuwasaidia yatima na wenye njaa ingekuwa ni heri.Mimi naona elimu ya MUM haiko kumsaidia mwananchi wa kawaida rather than kueneza chuki na kujihesabia haki.No wonder mnataka serikali igharamie makadhi ili muajiriwe maskini!
 
undefinedkwani mkuu unaogopa nini?,undefinedhapa dunia kila mtu ana chaguo lake,huyo @zitojunior pengine hapa duniani kachagua kuwa analyst wa haya mambo,undefinedwengine wanabobea kwenye kilimo,sayansi,biashara,wizi ,ukabaji etc,undefinedkila mtu anataka aache legacy fulani hapa duniani,undefinedwe mwache tu usimpangie,undefinedwala huna haja ya kumnunia mtu kwa hizi dini za kuja na merikebu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…